Pages

Monday, January 30, 2012

DAR LIVE KWAWAKA MOTO, MAPACHA WATATU, TID, SUPER SHINE, MR BLU WAFANYA KUFURU

WASANII wa muziki wa kizazi kipya na dansi Bongo, Khaleed Mohamed ‘TID’, Herry Samir ‘Mr Blu’, wakiwa na kundi la Mapacha Watatu ambalo linaongozwa na Khaleed Chuma ‘Chokoraa’, Junior Kalala ‘Kalala Junior’, na Joseph Michael ‘Jose Mara’, na kundi la muziki wa mwambao la Super Shine, usiku wa kuamkia leo wamefanya kufuru ndani ya ukumbi wa kisasa wa Dar Live uliopo Mbagala jijini Dar es Salaam. Wanamuziki hao walivunja rekodi ya mashabiki wengi waliowahi kushuhudia makamuzi kama hayo katika kituo hicho cha burudani nchini.
Shoo hiyo pia ilisindikizwa na makundi mengine kama Wakali Dancers, na wasaniii wengine wa Bongo Fleva wakiwemo Zuhura na Dogo Mfaume na Hejos Band. Watoto wakiserebuka ukumbini.
Msanii wa kucheza na kuigiza, Mpella Shaa ‘Kidevu cha Kuku’ akiwa amekaa juu ya chupa jukwaani hapo.
Mr Blue akitoa burudani kwa kila mtu.
Bosi wa TOP Bandi, mwanamuziki TID, akiwajibika.
Kundi la Wakali Dancers likitesa jukwaani.(Na: Mwandishi Wetu)

No comments:

Post a Comment