Pages

Tuesday, December 16, 2014

DIAMOND AVUNJA REKODI MAENEO MENGI

WIKI iliyopita katika simulizi hii ya Diamond tuliishia pale ambapo staa huyo aliongelea namna wimbo wake wa Mbagala ulivyopendwa kiasi cha kumfanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete ‘JK’ kumteua kuwa mburudishaji kwenye ziara za kampeni ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, mwaka 2010.Wiki hii tunaendelea

Oktoba 2, mwaka 2010, Diamond alipata safari yake ya kwanza kabisa ambapo alikwenda jijini London, Uingereza na kufanya shoo.Mwaka 2011, Diamond alishinda Tuzo ya

Nzumari iliyotolea nchini Kenya akiwa Msanii Bora wa Kiume toka Tanzania.
Diamond aliweka rekodi ya msanii wa kwanza Bongo kufanya shoo kwenye Ukumbi wa Maisha Club jijini Dar na kujaza mashabiki wengi kiasi kwamba wengine walishindwa kuingia ndani ya ukumbi huo.

No comments:

Post a Comment