KIjana mmoja raia wa Sweden amegeuka na kuwa kijana wa kimasai
Max pia alikuwa miongoni mwa vijana 5,000 wa Ilchamus katika kaunti ya Baringo waliotawazwa kuwa wanaume kamili baada ya kupashwa tohara.
Kwa sasa anafuata mila yake mpya inayoshirikisha mavazi yanayovaliwa pamoja na shuka nyeusi,simi iliofungwa katika ukanda wake wa rangi ya hudhurungi,viatu vyeusi na nguo iliorembeshwa kwa shanga.
Hafla hiyo ya kuhitimu imemfanya kuingia katika umri wa Ilmeng'ati.
''Mimi ni Max Lemeyan Le Kachuma kutoka kabila la Ilchamus na ukoo unaojiita Iltoimai''alisema jina lake huku akinywa maziwa yalio chungu katika kikombe.
No comments:
Post a Comment