CHAMA cha Michezo ya Jadi Tanzania
 (Chamijata) kimesema kimepata mwaliko kushiriki mashindano ya kurusha 
mishale ambayo yatafanyika nchini China kuanzia Machi 28 hadi 20 mwaka 
huu.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa 
Chamijata Tanzania Mohammed Kazingumbe wakati akizungumza na Fullshangwe
 katika ofisi za chama hicho jijini Dar es Salaam.
Alisema Chamijata imekuwaikipata 
mialiko mara kwa mara katika nchi za China na Korea Kusini hivyo kwa 
mwaka huu mwaliko wa kwanza ni kutoka China na mialiko mingine ipo 
ambayo ni kwenda Korea Kusini mwezi Septemba.
Mwenyekiti huyo alisema kwa sasa 
wanahangaika kutafuta wafadhili ili waweze kupeleka timu na viongozi wa 
Chamijata wakati huo ukifika.
“Tumepata mwaliko wa kwenda China 
katika mashindano ya kurusha mishale ambayo yatafanyika Machi 28 hadi 30
 hivyo jithada na mikakati yetu ni kuhakikisha kuwa tunashiriki,” 
alisema Kazingumbe.
Kazingumbe alisema Chamijata ina 
imejipanga vilivyo ili kuhakikisha kuwa michezo ya jadi inarejea katika 
hadhi yake ya awali ambapo amewaomba wadau kuwasaidia kufanikisha hilo.
Mwenyekiti huyo alisema Chamijata 
katika kuhakikisha kuwa inakuza mchezo huo itatumia kitabu ambacho 
wamekiandika chenye maelezo kwakina kuhusu mchezo wa bao.
 
No comments:
Post a Comment