TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, October 10, 2011

PERUGINA INVESTMENT , SIDE WAY WAJITOKEZA KUDHAMINI MISS UTALII DODOMA

washiriki Miss Utalii Dodoma, wakigonganisha Glass na Mkurugenzi wa Side Way Lodge, Valley Marandu. Muda Mfupi baada ya Kutangaza Udhamini wake ambapo warembo watalala kwa Kipindi chote cha Kambi.
Fainal za Miss Utalii Mkoa wa Dodoma zimepangwa kufanyika kwenye ukumbi Mpya wa Kisasa wa CLUB LA AZIZI,  ikiwa ni mabadiliko ambayo yamefanywa baada ya Mkoa wa Dodoma kutaka kufanyika kwenye ukumbi kutokana na kuwa bora kwa sasa ikilinganishwa na kumbi zingine za mkoa huo.
katika onyesho hilo ambalo awali lilipangwa kufanyika ukumbi wa new Dodoma hotel,  maandalizi yanaendelea kwenye ukumbi wa New Dodoma Hotel na warembo wote wako katika hali ya ushindani ambapo baadhi ya wadhamini wanazidi kujitokeza kusaidia fainal hizo.
Baadhi ya wadhamini walijitokeza ni PERUGINA INVESTMENT CO. LTD, SIDE WAY LODGE, Warembo  wanaoendelea na mazoezi ni pamoja na Jackline Leshange,Bahati Mwinyi,Martha Simon,Elizabeth Ayoub,Magreth Kapelle, Jazila Maulid, Agnes Stephan, Lucy Charlecy, Khadija Ally, Kija Masanja, Tausi Shaaban,Kibibi Aman, Nyabitage King'ala, Joyce Mwakibinga, Axer Peter, Nelly  Fabian Angelo,Anna Gisbert, Janet John, Julieth Katunzi, Ester George, Mary Wilson, Jenifer Kayanda, Bety Magawa,  na  Jackline John , chini ya jopo la wakufunzi(Walimu), ambao ni Miss Utalii Njombe na Balozi wa Hifadhi ya Taifa  ya Kitulo 2010/2011, Neema Isdory, Miss Utalii Tabora na Balozi wa Utalii wa Ndani, Sweet Maliwa,  Miss Utalii Vyuo Vikuu Kanda ya Kati, Tabia Msuta.

Washindi katika Fainal hizo wataungana na Washindi wa wenzao wa Mikoa ya Singida, Tabora, pamoja na Katavi kuunda Kanda ya Kati iliyopangwa kufanyika mwezi wa kumi na mbili kati ya Mkoa wa Dodoma na Tabora.
Katika Onyesho hilo Mgeni Rasmi anatazamiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma pamoja na Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa huo ambao ni Wageni waalikwa, Afisa Utamaduni Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Mkuu wa jeshi la Polisi Dodoma, pamoja na Maraisi wa Vyuo vya Wanafunzi vilivyopo Dodoma.
Wengine  waliojitokeza kudhamini Fainal hizo  Mpaka sasa ni Pamoja na, Kifimbo FM Radio kwa Upande wa (Matangazo), CLUB LA AZIZI,  Asante Water(Maji ya kunywa Washiriki),Ngoto Feniture, Royal Village, Clouds Fm Radio, TANAPA, Ngorongoro Creater, VETA Hotel, Shabibi Bus Service.
wengine ni Tanzania Daima & Sayari News Paper, Image Masters, Papaa Msofe, Zoizzuu Fashion, Dar City College, Kumekucha Action Mart, Viovena & Co LTD, Haji  Mapoda cosmetics pamoja na waheshimiwa Wabunge wa Dodoma.

Fainal za Miss Utalii Tanzania 2011/2012 Maanadalizi yake yanaendelea katika mikoa yote ya Tanzania ambapo Fainal za Taifa zimepangwa kufanyika pia Katika Mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya washiriki Miss utalii Dodoma 2011,wakiwa katika Pozi kwenye kambi yao SIDE WAY LODGE.