TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, January 21, 2012

Premier League table-Saturday, 21 January 2012 19:26 UK


Bolton   3 - 1   Liverpool

Position Team P GD PTS
Full Premier League table     
1 Man City 21 41 51
2 Man Utd 21 32 48
3 Tottenham 21 18 46
4 Chelsea 22 15 41
5 Arsenal 21 7 36
6 Newcastle 22 2 36
7 Liverpool 22 4 35
8 Stoke 22 -10 30
9 Norwich 22 -4 29
10 Sunderland 22 5 27
11 Aston Villa 22 -3 27
12 Fulham 22 -3 26
13 Swansea 22 -4 26
14 Everton 22 -4 26
15 West Brom 22 -9 25
16 QPR 22 -15 20
17 Bolton 22 -19 19
18 Blackburn 22 -12 18
19 Wolves 22 -15 18
20 Wigan 22 -26 15

Norwich   0 - 0   Chelsea

Fernando Torres endured another miserable day as Norwich frustrated Chelsea to earn a point and further hit the London side's slim title hopes.

Fulham   5 - 2   Newcastle

Dempsey is the first American player to score a Premier League hat-trick 

QPR   3 - 1   Wigan

Helguson scores his second penalty of the season 
Goals from Heidar Helguson, Akos Buzsaky and Tommy Smith lifted Mark Hughes' QPR out of the Premier League relegation zone and left Wigan rooted to the bottom of the table.

Everton   1 - 1   Blackburn

Tim Cahill's clearances crashes off David Goodwillie and into the net
 Everton1-1BlackburnFT 

  •  

MASIKINI , R.I.P Hon. Jeremiah Sumari!5 TUTAMKUMBUKA


Much thanks to the The World Race Group that came to visit us at Ruaha University College in Iringa today. May God bless you abundantly. Frankly speaking we have learned a lot from you guys. Special thanks to Brittany Gray, Gary Lee, Ashley Holcomb, Katie Bury and others, be blessed! - Mbarikiwa PSA Chairperson.
 
 
 
 
By: correspondent
 


R.I.P Hon. Jeremiah Sumari!5 hours ago ·
while giving honor to farewell the body of the deceased, an act held in Dar es Salaam Karimjee today, God can be placed a safe part of his parish










MAJI MACHAFU YAKWAKERA WAKAZI WA JIJINI- NI BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI

 Maji ambayo yametwama tangu juzi, baada ya manyunyu kidogo, yamezidi kuwa kuro kwa wapita njia pamoja na vyombo vya usafiri ambvyo ukwepa maji na hivyo kusababisha msongamano wa magari
 Mwendesha Pikipiki akivuka Eneo hilo kwa tabu
 Mwendesha Pikipiki, na Abiria wake wakivuka kwa taabu
Mkazi wa jiji ambaye akutambuliika jina lake akijaribu kuzibua Mitaro , kwenye maungio ya Barabara ya Uhuru na Msimbazi  leo, maji hayo yamesababishwa na mvua kidogo zilizonyesha juzi( Picha Zote na Shaaban Mpalule).

MWIZI AGEUKA NINJA KARIAKOO, ARUKA MAGOROFA NA KUWAACHA WANANCHI WALIOKUWA NA ASIRA KALI ZA KUUA.


 Jamaa huyo baada ya kula kichapo, aliingia humu ndani wanapochezea michezo ya Bahati na Sibu
 Wananchi waliendelea kujazana na kudai wanahitaji roho yake
 Baada ya ukosefu wa Amani eneo hilo, na Ibilisi kuzingira, ghafla alitokea Askari, na kuanza kuwatuliza wananchi waliokuwa hawashikiki, tulieni basi nimpeleke Polisi "alisema Askari
 Raia wengine walinyoosha mikono juu kulalamika, "we askari vipi toka tuachie huyo bhana, roho yake tunywe Damu, la sivyo na wewe tutakudungua mawe"walisema wananchi
 Afande naye" Mimi ni Askari sawa eh, kazi yenu imeisha umebaki wakati wangu, huyu anakwenda kunyea Debe, saawa jamani, Amri ni moja sasa natoka naye"alisema Afande
 Naingia Ndani kumtoa, ila msimguse tena,
 Afande, Wataniua hao Mzee, nikitoka humu ndani, si unaona walivyokasirika, na wewe upo pekee sasa utanisaidiaje, au ndo unataka kunitoa kafara, najuta kuiba hii Simu, Nikipona Leo Siibi tena, EH-Mungu Nisaidie, nimekosa kwako na Kwa Raia Pia, YESUUUUUU Niokoe
 We, Pumbavu zako, Yesu ndiyo kakutuma kuiba Simu ya Watu, sasa leo utaona , lazima tunywe Damu yako na Huyu afande hatokusaidia hapa, hata uniangalie roho hiyo tunaitoa sawa, hakuna huruma Tena,
 Kizaa zaa kilianza baada ya Afande kutoka naye nje, Raia tuachie huyooooooooo tumsulubu, Polisi -Hapana jamani mwacheni tumpeleke akatumikie Serikali, Raia Serikali ya nini huyo Izraeli anamuitaji, Mbona wetu huyo, Kelele za Mabishano zilipozidi, Afande alijinasua na kumwacha
 Haya sasa tunakupeleka Kukutoa Roho, Twende Mwizi wewe,"Jamani nioneeni huruma, basi, Duh, nikiponyoka Mikononi mwao hapa ni mbio na wataona wenyewe mchezo, ngoja niwalie taiming
 Gafla alidandia gari lililokuwa mwendo kasi kidogo, Dereva aliamuli kusiamama hadi alipotelemshwa kwa virungu, matofari, mawe, hadi gari hilo kuvunjwa Vioo, Telemka wewe hapa kipigo tu
 Raia waliendelea kukamua kisawasawa, kipigo kilizidi, Damu ilizidi kumwagika, na hapo ndipo walipobugi, baada ya kupata Upenyo tu, alinyoropoka na kuingia kwenye Majengo ya Serikali(NHC) yanayokaliwa na Wahindi, na kupanda Juu kabisa ya Gorofa tano, mchezo uliofuata mazee
 Hawa watu hawajui kwamba mimi na Osama Bin Laden Tulisoma Shule Moja nini, nilikuwa nawapigia Heaabu tu, na hapa wamekosea tayari Siku ingine wanitafute siyo leo tena, kama wanaweza kufuata jeshi la Mtu Mmoja kazi kwao, Jamaa aliomndoka kwa mfumo huo na kuwashinda watu wote Kariakoo leo. gorofa kwenda gorofa na zaidi ya gorofa tano karuka kama ninja

Wananchi waliokuwa na Asira kali walibaki kumtafuta bila mafanikio,(Duh huyu jamaa ni kiboko, katuacha hivoi hivi, hapana siamini , ila lazima tumkamate" alisema jamaa hapo juu aliyesimama lakini  hadi mwisho wa mchezo kama za OSAMA, NA MULLA OMARY(Picha Zote na Shaaban Mpalule).

UZINDUZI WA ZUKU TV WAFANA DAR-YAFANYA UZINDUZI RASMI

Mkurugenzi wa TCRA,Profesa John Mkoma akibonyeza kitufe ikiwa ni ishara ya kuzindua Televisheni ya Zuku Africa kupitia kampuni ya Wananchi Satelite Tanzania inayotoa matangazo yake kwa kutumia ving'amuzi nchini Tanzania , Hafla ya uzinduzi iliyofanyika kwenye hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam jana jioni ikihudhuriwa na wadaum mbalimbali na wageni waalikwa. Katika picha kulia ni Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa makampuni ya Wananchi Group na kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Wananchi Group Bw. Ali Mufuruki wakishuhudia tukio hilo.
Mkurugenzi wa TCRA,Profesa John Mkoma mbele ya wageni waalikwa mbalimbali kabla ya kuzindua kampuni ya Wananchi Satelite jana katika hafla iliyofanyika jana kwenye hoteli ya Golden Tulip kulia ni Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa makampuni ya Wananchi Group na kulia ni Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi Group Bw. Ali Mufuruki
Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi Group Bw. Ali Mufuruki akizungumza katika uzinduzi huo na kumkaribisha Mkurugenzi wa TCRA Profesa John Mkoma. Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa makampuni ya Wananchi Group akimkaribisha Mwenyekitiwa Makampuni ya Wananchi Group Ali Mufuruki.
Kundi la TMK wanaume Family likitumbuiza katika uzinduzi huo jana.
Bendi ya Tanzanite ikiongozwa na mwanamzuiki nguli John Mhina ilitoa burudani ya kutosha katika uzinduzi huo jana.
Wageni waalikwa mbalimbali wakifuatilia matukio yaliyokuwa yakiendelea katika uzinduzi huo.
Wadau hawa nao walikuwepo ndani ya nyumba kama unavyowaona wengi wanaipenda ZUKU TV.
Waimbaji wa muziki wa injili pamoja na waigizaji wa filamu hawakukosa uzinduzi huop kutoka kulia ni Mwigizaji Natasha, Monalisa , Mwimbaji Alice na mumewe ambaye pia ni mwimbaji Bw. Robert David wakipozi kwa picha.
Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa makampuni ya Wananchi Group katikati na Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi Group Bw. Ali Mufuruki kulia wakimsikiliza Meneja mkuu wa Wananchi Satelite Bw Mohamed Jeneby akiwaelezea jambo.
Richard Bell Afisa Mtendaji Mkuu wa makampuni ya Wananchi Group kulia i na Mwenyekiti wa makampuni ya Wananchi Group Bw. Ali Mufuruki wakijadili jambo katika uzinduzi huo.
Wadau kutoka ZUKU TV wakipozi kwa picha jana katika uzinduzi huo.
Mwanamuziki AY na wenzake walihudhuria pia uzinduzi huo.
Jaquiline Karanja kulia na Moureen walikuwepo pia hebu wacheki na pozi yao.
Kutoka kulia ni wadau ZIZZOU wa ZIZZOU Fashion, Suzy wa Clouds na mdau Godliver wa Prime Time wakipozi kwa picha.

Friday, January 20, 2012

MECHI YA TWIGA STARS KUONESHWA ‘LIVE’

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekipa Kituo cha Televisheni cha ITV haki ya kipekee (exclusive rights) kuonesha moja kwa moja (live) mechi kati ya Twiga Stars na Namibia itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Twiga Stars ambayo tayari imeingia kambini Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Ruvu iliyoko Mlandizi mkoani Pwani iwapo itafanikiwa kuitoa Namibia itafuzu kucheza raundi ya kwanza na mshindi kati ya Misri na Ethiopia. Twiga Stars ilishinda mechi ya kwanza ugenini mabao 2-0.

Kampuni ya ZH Poppe Limited imegharamia tiketi za waamuzi na kamishna atakayesimamia mechi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya Tanzania (Twiga Stars) na Namibia itakayofanyika Januari 29 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Mbali ya tiketi hizo za ndege, pia kampuni hiyo itagharamia hoteli (malazi na chakula) kwa kamishna na waamuzi hao wanne kwa muda wote watakaokuwepo nchini kwa ajili ya mechi hiyo.
Gharama za tiketi na hoteli kwa kamishna wa mechi hiyo na waamuzi hao watakapokuwa hapa nchini ni sh. 11,856,000.
Bajeti nzima ya mechi hiyo ni sh. 74,660,000. Hiyo inajumuisha usafiri, posho kwa wachezaji, posho kwa benchi la ufundi, gharama za kambi, dawa na maji ya kunywa wakati wa mazoezi na mechi kwa Twiga Stars. Maeneo mengine usafiri wa ndege, usafiri wa ndani (magari mawili), posho na hoteli kwa kamishna na waamuzi.
Gharama nyingine za timu ya Namibia itakayokuwa na watu 25 ambazo ni usafiri wa ndani (magari matatu), hoteli (malazi na chakula) na maji ya kunywa wakati wa mazoezi na mechi.

WAFANYABIASHA WAONYWA KUACHA KUSAFIRISHA FEDHA BILA YA ULINZI WA POLISI

Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi Zanzibar Wafanyabiashara wakiwemo wawekezaji wa kigeni waliopo hapa nchini, wameonywa kuacha mtindo wa kusafirisha fedha nyingi kutoka eneo moja hadi lingine pasipo na ulinzi wa Polisi.
Onyo hilo limetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Shamsi Vuai Nahodha, wakati akizungumza na wawekezaji wenye Mahoteli katika Fukwe za Bahari ya Hindi na Hifadhi ya Mjini Mkongwe mjini Zanzibar.
Waziri Nahodha amesema kuwa pamoja na kuwapo kwa usalama na amani hapa nchini, lakini hali hiyo isiwafanye watu wakajiamini na kusafirisha fedha nyingi pasipo na ulinzi wa kutosha ili kuepuka kuporwa na majambazi.
Akizungumzia Utalii Mh. Nahodha amesema kuwa kwa kutambua kuwa utalii ndio chanzo kikubwa cha uchumi wa Zanzibar na taifa kwa ujumla, Serikali itahakikisha kuwa inaweka miundombinu ya kutosha kiusalama ili kuondoa matishio yoyote kwa wageni wanaoitembelea nchi yetu kwa shughuli mbalimbali zikiwemo za kitalii.
Aidha amesema ili kuhakikisha usalama zaidi, wawekezaji hao hawanabudi kulitumia Jeshi la Polisi katika kufanya uchunguzi kwa watu wanaotaka kazi kwenye maeneo yao ili kuepuka kuajiri watumishi wasio waaminifu.
“Mnapotaka kuwaajiri wafanyakazi, wakiwemo walinzi kwenye maeneo yenu, hakikisheni kuwa mnaowapa nafasi hizo ni vijana wa maeneo jirani ambao wengi wao wanafahamika kwa sura na tabia kulikoni kutoa watumishi mbali ambao hata kama wakifanya uhalifu na kukimbia ni vigumu kumpata”. Alisema Mh. Nahodha.
Mh. Nahodha ameongeza kuwa athari za kumuajiri mtu wa mbali ni kuwa hata pale atakapofanya uhalifu na kukimbi haitakuwa rahiisi kwa Polisi kumpata mtuhumiwa huyo kwa urahisi.
Awali Mwenyekiti wa Umoja wa Wawekezaji wa Mahoteli Visiwani Zanzibar (ZATI) Zanzibar Association Tourism Industrial Bw. Abullsamad Saidi, alisema kuwa ipo haja kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kusaidia kuongeza kasma ya Jeshi la Polisi Visiwani humo ili waweze kumudu vema kazi zao zikiwemo za ulinzi wa vivutio vya kitelii kwa wageni.
Amesema kuwa pamoja na Jeshi la Polisi kufanya kazi zao vizuri, lakini askari wamekuwa wakipata vikwazo kutokana na uduni na ukosefu wa vitendea kazi kama vile usafiri na radio za mawasiliano.
Hoja hiyo pia imeungwa mkono na Mshauri wa Rais katika Masuala ya Utalii Bw. Issa Ahmed Othman, ambaye amesema kusipokuwa na usalama wa kutosha kwenye maeneo ya fukwe na kuna hatari ya kukosa watalii na hivyo kudhoofisha na kupunguza pato la taifa linalotokana na utalii.
Wakichangia hoja kwenye mkutano huo, baadhi ya wawekezaji waliiomba Serikali kuwa na bajeti ya kutosha katika kulinda maeneo ya vivutio vya kitalii.

Bibi Gonsaga Mwingira Shawa a.k.a Bibi Malaika akiwalisha kieki wajukuu zake katika hafla yake iliyofanyika jijini Dar es Salaam wakati al,ipotimiza miaka 75 ya kuzaliwa kwake
Bibi Gonsaga Mwingira Shawa a.k.a Bibi Malaika akifurahia na kushangiliwa na marafiki, watoto na wajukuu zake kwa kutimiza miaka 75 iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Keki ya kumpongeza bibi Malaika kufikisha miaka 75.
Bibi Malaika akisalimia na Balozi mstaafu wa Ufaransa Mhando katika sherehe ya kumpongeza Bibi Malaika kufikisha miaka 75..
Ndugu jamana na marafiki wakimpatia bibi Malaika zawadi.

Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) na Chuo cha Polisi cha Kimataifa cha Moshi (CCP) wameingia makubaliano ya kukuza na kuendeleza vipaji vya michezo vya vijana. Katika Makubaliano hayo yaliyofikiwa mwezi August, 2011, TPBC na CCP watashirikiana kuchagua vijana wenye vipaji vya mchezo wa ngumi na kuwaendeleza ili waweze kucheza michezo ya majeshi pamoja na mashindano mengine ndani na nje ya Tanzania. Makubaliano haya yamekuja wakati ambapo Tanzania inahitaji msukumo mkubwa kwenye medani ya michezo ili kuweza kufufua ari na moyo wa michezo kama ilivyokuwa katika miaka ya 70 na 80. Aidha, Makubaliano haya yana lengo la kuandaa jeshi zuri la wanamichezo hodari watakaoleta sifa jeshi la Polisi pamoja na Tanzania kwa ujumla. Tayari vijana wengi wanafanya mazoezi katika kambi (Gym) ya ngumi ambayo imewekwa katika viwanja vya michezo vya CCP. Kambi hiyo inawashirikisha pia vijana kutoka maeneo mengine mkoani Kilimanjaro ambao sio Polisi. Katika kusimamia hili, Rais wa TPBC Onesmo Ngowi akishirikiana na Afisa Mipango na Utawala wa CCP Superintendent of Police, Lutusyo Mwakyusa watahakikisha kuwa vifaa muhimu vinapatikana pamoja na mazingira ya kufanyika mazoezi na upatikanaji wa wataalam wanaotakiwa wanapatikana. Naye Superintendent of Police, Yahya Mdogo ambaye ni Afisa wa Michezo katika Chuo cha Polisi cha Kimataifa Moshi ataangalia kwa karibu mwenendo mzima wa mahitaji ya kila siku ya mazoezi. Tayari TPBC imeshatoa vifaa muhimu vya mazoezi pamoja na wataalam (Makocha) wa kuwafundisha mabondia hao wako katika sehemu ya mazoezi. Vijana wengi ambao walikuwa hawana kazi au mahala pa kwenda wakati wa saa za jioni kwa sasa wanafanya mazoezi na wenzao katika uwanja wa CCP. Aidha, baadhi ya mabondia kutoka katika mkoa wa Kilimanjaro ambao walikuwa wameweka kambi katika jiji la Nairobi nchini Kenya na Arusha wamejumuika katika kambi hii mpya. Mabondia hao ni pamoja na Pascal Bruno anayejulikana na wengi kama "Price Kilimanjaro", Emilio Norfat, Charles Damas, Alibaba Ramadhani, Robert Mrosso, Bernard Simon na wengine wengi Baadhi ya wataalam waliojitokeza kuwafundisha vijana hawa ni pamoja na Felix Joseph na Pius Msele ambao kwa nyakati tofauti wamewahi kuwa wachezaji na makocha wa timu ya ngumi ya taifa. Makubaliano haya ni baadhi tu ya mikakati mipya za TPBC za kuamsha ari ya mchezo wa ngumi kwa kuzisambaza mikoani kuliko ilivyozoeleka ngumi kufanyika katika mkoa wa Dar -Es-Salaam peke yake. "Kwa sasa kazi kubwa tulivyo nayo ni kuzipeleka ngumi mikoani ambako tunaamini kuna vijana wengi sana wenye moyo pamoja na vipaji vikubwa" alisema Ngowi.