TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, February 27, 2016

WAZIRI Nape awapongeza Efm

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza wakati wa hafla ya kutimiza mwaka mmoja kwa kipindi cha Makao Makuu ya Michezo (Sports Head Quarter) kinachorushwa hewani kupitia 93.1 Efm Radio jana jijini Dar es Salaam.
 Mtendaji wa EfmRadio Frances Ciza akizungumza wakati wa hafla ya kutimiza mwaka mmoja kwa kipindi cha Makao Makuu ya Michezo (Sports Head Quarter) kinachorushwa hewani kupitia 93.1 Efm Radio jana jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akikata keki ya birthday ya kipindi cha Makao Makuu ya Michezo (Sports Head Quarter) kinachorushwa hewani kupitia 93.1 Efm Radio jana jijini Dar es Salaam.Kipindi hicho kimetimiza mwaka mmoja tokea kuanzishwa kwake.Kulia nim Mkurugenzi Mtendaji wa EFM Radio Francis Ciza.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (wapili kulia) pamoja na mashabiki wa Timu za Taifa wakiwa wameshika  keki ya birthday ya kipindi cha Makao Makuu ya Michezo (Sports Head Quarter) iliyotolewa na mashabiki hao wakati wa hafla kutimiza mwaka mmoja tokea kuanzishwa kwa kipindi hicho jana jijini Dar es Salaam.Picha Frank Shija, WHUSM

MKUU WA WILAYA YA SIMANJIRO AZANGUMZA NA WAZEE NA KUWAPA MSAADA WA MAGUNIA 100 YA MAHINDI

 Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Mahmoud Kambona, (kulia) akiwazawadia wazee wa Mji mdogo wa Mirerani sh 50,000  baada ya kuzungumza nao na kuwakabidhi msaada wa magunia 100 ya mahindi yaliyotolewa na Mkurugenzi wa kampuni ya TanzaniteOne Hussein Gonga.
 Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Mahmoud Kambona, (kulia) akiwazawadia wazee wa Mji mdogo wa Mirerani sh50,000  baada ya kuzungumza na wazee wa mji huo na kuwakabidhi msaada wa magunia 100 ya mahindi yaliyotolewa na Mkurugenzi wa kampuni ya TanzaniteOne Hussein Gonga.
Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Mahmoud Kambona, akigawa kwa wazee wa mji mdogo wa Mirerani, moja kati ya magunia 100 ya mahindi ya msaada yaliyotolewa na Mkurugenzi wa kampuni ya TanzaniteOne Hussein Gonga, kwenye ofisi za Sawata.
 Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Mahmoud Kambona, akizungumza na wazee wa mji mdogo wa Mirerani na kuwagawia msaada wa magunia 100 ya mahindi ya msaada yaliyotolewa na Mkurugenzi wa kampuni ya TanzaniteOne Hussein Gonga, kwenye ofisi za Sawata.

ZIARA YA WAZIRI MKUU MAJALIWA – MTWARA

Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akitembelea bandari ya Mtwara Februari 27, 2016.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego.
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akitembelea bandari ya Mtwara Februari 27, 2016.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wafanyakazi wa kampuni ya TPDC baada ya kuwasili kwenye mtambo wa kuchakata gesi wa Madimba, Mtwara Vijijini kukagua shughuli za gesi Februari 27, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mtambo wa kuchakata gesi wakati alipoutembelea Februari 27, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TPDC baada ya kutembelea mtambo wa kuchakata gesi wa Madimba, Mtwara Vijijini Februari 27, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mtambo wa kuchakata gesi wakati alipoutembelea Februari 27, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na walimu na wakufunzi wa Chuo cha Elimu cha Mtwara baada ya kuzungumza nao chuoni hapo , Februari 27, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na walimu na wakufunzi wa Chuo cha Elimu cha Mtwara baada ya kuzungumza nao chuoni hapo , Februari 27, 2016. 

MAJALIWA AWASILI MTWARA KWA ZIARA YA SIKU MOJA

Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akisalimiana na viongozi wa mkoa wa Mtwara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege ea Mtwara kwa ziara ya siku moja mkoani humoFebruari 27, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

magonjwa ya mifugo ,majanga ya moto ni tatizo katika hifadhi ya mkomazi

Waandishi wa habari wakiwa wanamuangalia mnyama aina ya kobe aliopo ndani ya hifadhi ya mkomazi

Na Woinde Shizza,Same

Vita dhidi ya magonjwa ya mifugo ,majanga ya moto ,ongezeko la watu pamoja na ukame  ni changamoto kubwa inayoikabili hifadhi ya taifa ya Mkomazi ilipo wilayani same Mkoani Kilimanjaro ambapo imesababisha baadhi ya wanyama ambao ni vivutio vikubwa katika hifadhi hiyo kutoweka  .

Hayo yamebainishwa na afisa utalii mwandamizi  wa hifadhi ya mkomazi   Pellagy Marandu wakati akiongea na waandishi wa habari waliotembelea hifadhi hiyo kujionea vivutio ambavyo vinapatikana ndani ya hifadhi hiyo.

Alisema changamoto hizo zimekuwa zinaletwa na wafugaji ,wakulima ambao wamekuwa wanaleta wanyama ndani ya hifadhi ambapo alibainisha kuwa wanyama wengine wanaweza wakawa na magonjwa ya kuambukiza hivyo wanapoingia ndani ya hifadhi wanaweza kuambukiza wanyama walioko hifadhini hali ambayo inaweza kusababisha janga kubwa kwa hifadhi.

“kwa upande wakulima wamekuwa wakileta madhara wakati wa kuandaa mashamba yao kwa ajili ya kilimo ambapo wamekuwa wakiaribu mazingira kwa kuchoma moto mabaki ya mazao ambayo walipanda msimu uliopita “alisema Marandu

Aidha ilikukabiliana na changamoto hizo wamekuwa wakifanya doria kwa kushirikiana na wananchi wanaozunguka hifadhi ambao ni ujirani mwema ambapo wamekuwa wakiweza kufichua wale wote ambao wanaingiza mifugo ndani ya hifadhi kinyume cha sheria ambao wamekuwa wakipigwa faini huku wengine wakifikishwa mahakamani .

Kwa upande wake mkuu  wa hifadhi ya Mkomazi Donat Simon Mnyagatwa Alisema kuwa mbali na kuwepo na changamoto hiyo ya kuingiza mifugo ndani ya hifadhi pia wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji ambapo alibainisha  kuwa  hili ni tatizo kubwa  linaloikabili hifadhi hiyo kwani maji ni uhai ,kuanzia kwa binadamu na hata kwa wanyama .

“Ni kweli ili nitatizo kubwa lakini pia tumeanza kuandaa mipango mathubuti  kwa ajili ya kutatua tatizo hili ambapo kwa upande wa binadamu tupo kwenye mkakati wa kuanza kuchimba visima virefu ili kuweza kupa maji mengi ambayo pia maji hayo yataweza kukusanywa kwa pamoja kwa ajili pia ya wanyama wetu,pia tunampango wa kuongeza mabwawa yaliyopo ndani ya hifadhi ili kuakikisha pia tunaondokana na changamoto hiyo”alisema Mnyagatwa

Aidha alibainisha kuwa mbali na changamoto hiyo pia wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa miundo mbinu ya barabara pamoja na nyumba za kuishi watumishi ambapo alisema kuwa mpaka sasa zaidi ya familia tisa zinaishi ndani ya hifadhi  huku familia zingine zikiishi nje ya hifadhi ,pamoja changamoto hizo ameiomba Halmashauri ya same kupitia Tanroad kurekebisha barabara ya kuelekea hifadhini ili iweze kupitika kwa urahisi kwa kipindi chote.

Mnyagatwa alibainisha kuwa kwa lengo la ujirani mwema wananchi ambao wamekuwa wakizunguka hifadhi wamekuwa wakipatiwa mafunzo maalumu ya kutambua umuimu wa utunzaji wa hifadhi pamoja na kutambua mipaka ya hifadhi na athari za kuingiza wanyama hifadhini ,mathara ya uaribifu wa mazingira ambapo alisema wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwaelimisha na elimu hii imesaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa uhalifu ndani ya hifadhi.

HAYA NDIYO YALIYOSABABISHA UCHAGUZI ZANZIBAR UFUTWE

Baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha kuwataka waandishi wote wa habari za kiuchunguzi pamoja na watafiti kuweka hadharani na kuueleza umma kile kilichotokea Zanzibar, Waandishi na watafiti mabalimbalai wamejitokeza na vielelezo vinavyoeleza jinsi uchaguzi huo ulivyoharibika

Vielelezo hivyo ni Nakala za fomu namba MUR. 12A za matokeo zilizotoka katika vituo vya kujumuisha kura ambazo zilikuwa zimejazwa kimakosa.
Hii ni fomu kutoka Kituo cha Skuli ya Mabaoni namba 23801, Jimbo la Chonga namba 2909 fomu hii siyo halali kutokana na kukosa mhuri wa tume ya uchaguzi Zanzibar. Msimamizi wa kituo ni Khamis mkungwa Zaid.

Fomu nyingine inatoka katika kituo cha Urusi chenye namba 26503, katika jimbo la Jang’ombe namba 1940

A. Hii ni fomu kutoka kituo cha Gamba namba 2008
Hii ni fomu kutoka kituo cha Gamba namba 2008, Jimbo la Mkwajuni namba 1926, fomu hii imepoteza uhalali kwasababu imefutwafutwa na haina mhuri wala jina la msimamizi wa kituo.

B. Kituo cha Skuli ya Mwembe Makumbi
Hii ni fomu kutoka katika kituo cha Skuli ya Mwembe Makumbi namba 21618, Katika jimbo la Chumbuni namba 1931, fomu hii imekosa uhalali kwasababu imefutwa majina ya mawakala na kupandikizwa majina mengine juu ya maandishi ya kivuli.

C. Jimbo la Chumbuni namba 1937
Hizi mbili, fomu kutoka kiwanja cha mpira Masumbani namba 29304 kutoka jimbo la Chumbuni namba 1937, fomu hii inakosa uhalali kwa sababu haina mhuri , maandishi ya meandikwa tena kwa kalamu juu ya maandishi ya kivuli na saini imewekwa zaidi uya mara moja. Fomu ya pili ni kutoka jimbo la Chakechake jina la kituo na namba haisomeki, fomu hii inakosa uhalali kwasababu inamhuri ambao siyo wa Tume ya uchaguzi anzibar ni mhuri wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar ambao haupaswa kutumika katika fomu hii.

D. Mihuri ya kughushi
Fomu ya pili ni kutoka jimbo la Chakechake jina la kituo na namba haisomeki, fomu hii inakosa uhalali kwasababu ina mhuri ambao siyo wa Tume ya uchaguzi anzibar ni mhuri wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar ambao haupaswa kutumika katika fomu hii.

Matumizi ya Mihuri Bandia katika karatasi za kujumuishia matokeo ya wagombea nafasi ya Rasi wa Zanzibar.

E. Fomu zimejirudia zaidi ya mara moja
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa ZEC alisema utata wa matokeo ulianza pale wajumbe waliopelekwa Pemba kurudi na kuiarifu Tume dhidi ya matendo yaliyofanywa na wasimamizi wa ZEC Pemba hata hivyo wakati uchunguzi na mabishano yakiendelea Mmoja wa wagombea akaitisha wanahabari na kujitangaza ameshinda kwa matokeo ambayo kila mmoja wetu alishangaa sana,

Ni kitendo cha aibu na Fedheha kubwa wanaoshabikia hawakuona madhara yake,sijui alitoa wapi Takwimu ambazo zilitoa ushindi kwa wagombea wawili tu,tena ukijumlisha asilimia ni 100 inasikitisha sana,Shinikizo la kunitaka nimtangaze mshindi kinyume na taratibu lilinifanya niubebe msalaba kusimamisha na kufuta matokeo baada tu ya kuitisha fomu chache za uthibitisho mwandishi haya ndio tuliyakuta,Ni nusu ya uchaguzi wote kila jimbo ulichezewa

Tumejiridhisha watu wetu watendaji wa ZEC walio apa walifanya haya,kutumia mihuri ya Bandia kujaza hizi fomu kinyume na taratibu kama mnavyo ona alisisitiza Mzee Jecha kwa masikitiko akiwaonyesha waanndishi waliofika kuhoji nini kilitokea hasa.BLOG http://zanzibariamani.blogspot.com/

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKUTANA NA VIONGOZI WA DINI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa dini kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salam Februari 26, 2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya viongozi wa dini wanaunda kamati ya amani ya Dar es salam na baadhi ya mikoa nchini wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. 
Baadhi ya viongozi wa dini wanaunda kamati ya amani ya Dar es salam na baadhi ya mikoa nchini wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mkuu wa KKKT Mstaafu, Elinaza Sendoro baada ya kuzungumza na Viongozi wa Dini kwenye Kituo cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mkuu wa KKKT Mstaafu, Alex Molasses baada ya kuzungumza na Viongozi wa Dini kwenye Kituo cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini baada ya kuzungumza nao kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyererejijini Dar es salaam Februari 26, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini baada ya kuzungumza nao kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyererejijini Dar es salaam Februari 26, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini baada ya kuzungumza nao kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyererejijini Dar es salaam Februari 26, 2016.

MABADILIKO KWA BAADHI YA MAKAMANDA WA POLISI WA MIKOA.

 Mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Leonard Paul amehamishwa kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Ulrich Matei aliyekuwa Mkuu wa Utawala Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mihayo Msikhela aliyekuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga amehamishwa kwenda kuwa Mkuu wa Kikosi cha Kuzuia dawa za kulevya. Aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Ramadhani Mungi anaenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Bandari na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Wilbrod Mtafungwa ambaye alikuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe. 

Aliyekuwa Afisa mnadhimu Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Prudenciana Protas anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe. Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Philipo Kalangi amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi na nafasi inachukuliwa na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Shinyanga ACP Ramadhan Ng’azi. 

Aidha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Camilius Wambura anakwenda kuwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Francis Massawe kutoka Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam.

Aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Gilles Mroto anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya kuchukua nafasi ya Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Gemini Mushi aliyehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi Dar es Salaam.

Wengine ni pamoja na Naibu Kamishna wa Polisi DCP Hezron Gimbi anayetoka Upelelezi Makao Makuu Dar es Salaam kwenda kuwa Mkuu wa Utawala Kanda Maalumu Dar es Salaam pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Costantine Massawe anakwenda kuwa Mkuu wa Oparesheni wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Mabadiliko hayo ni ya kawaida kwa mujibu wa Sheria, kanuni na taratibu za Jeshi la Polisi.
Imetolewa na:
Advera Bulimba-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi (T)
Makao Makuu ya Polisi.

Friday, February 26, 2016

T.M.F NI NINI?

Wakfu wa Tasnia ya habari Tanzania(Tanzania Media Foundation-TMF), imerithi kazi za mradi wa mfuko wa vyombo vya habari tanzania, (Tanzania Media Fund Project), uliofanya kazi kutoka juni 2008 hadi septemba 2015, TMF mpya ambayo ilianza shughuli zake octoba 2015, ina maono ya kuimarisha tasnia ya habari na kuifanya kuwa huru ili kukuza uwajibikaji.

TMF imedhamilia kubadili sekta ya habari kwa kutoa Ruzuku na mafunzo ya kivitendo ili sekta hii iwe huru na endelevu na inayowajibika kikamilifu kuibua masuala yenye maslai mapana kwa umma, TMF inafanya kazi zake kwa misingi ya uwazi bila upendeleo, kwa fikra tofauti na mpya, kwa ubora kwa kujifunza na kufikirisha, kwa ari ya kupata matokeo na utendaji kazi wa pamoja.

TMF kwa sasa inatekeleza mpango mkakati wa mwaka 2015-2018, Kuimarisha Tasnia ya Habari ili kuleta Uwajibikaji. kwa kutekeleza mkakati huo, TMF inatarajia kupata matokeo matatu ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha kuridhika kwa watumiaji habari wa vyombo vya habari vilivyojengewa uwezo na TMF kufuatia upatikanaji zaidi wa habari za uchunguzi na zenye maslahi mapana kwa umma.

2. kuongezeka kwa uimara na uendelevu wa taasisi za habari zinazojengewa uwezo na TMF, lakini pia kuwepo kwa TMF imara na Endelevu.

Wakati sehemu moja ya matokeo inahusu uimara na uendelevu wa TMF kama taasisi, matokeo mawili ya mwanzo yanahusu kuongeza uwezo wa weledi kwa vyombo vya habari na wadau wa habari sambamba na kuongeza ubora, wingi na habari tofautitofauti za uandishi wa kiuchunguzi na wenye maslahi ya umma katika sekta ya habari.

Matokeo haya mawili yanahusu moja kwa moja aina ya ruzuku tano ambazo TMF itatoa kuanzia 2016. Ruzuku zinazowalenga waandishi binafsi ni Ruzuku ya habari za vijijini, Ruzuku ya Ushirika wa Kubobea na Ruzuku ya masuala ya Kimkakati, Ruzuku zinazolenga taasisi ni Ruzuku ya Maudhui Maalum na Ruzuku ya Mabadiliko kwa Maudhui Endelevu.

Sharti la Msingi kwa kila aina ya ruzuku inayotolewa ni kwa kumshirikisha kila mnufaika katika mpamgo wa jifunze wa TMF inayofuata misingi ya kujifunza kwa vitendo kwa maelekezo na ushauri kutoka kwa gwiji wa habari.

KWA NINI RUZUKU KWA WAANDISHI WA HABARI?

Wahitimu wa uandishi wa habari nchini, mara nyingi wanaanza kazi wakiwa na ujuzi mdogo wa vitendo. Tafiti za TMF za miaka ya 2013,2014 na 2015 ziliangalia kwa kina ubora wa mahudhui ya habari. Tafiti hizi zinaweza kupatikana kwa maombi au katika tovuti ya TMF. hali inayoonekana katika vyombo vya habari vya Tanzania ni uandishi uliojikita katika habari za mjini na masuala ya kisiasa ambapo raia wanapewa fursa ndogo ya kutoa maoni yao ikilinganishwa na wataalamu na maafisa wa Serikali. Matumizi ya vyanzo vya habari na anuani zake yako chini, jambo hili linaweka ukomo wa uwezo wa vyombo vya habari kufanya wajibu wake kama mdhibiti.

kuanzia 2016  TMF inatumia mbinu ya kile inachiita mnyororo wa ruzuku, kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali kwa mbinu hii, TMF  itawekeza zaidi katika kuthamini namna ambavyo uwezo wa mwandishi aliyenufaika na ruzuku za TMF amekua katika taaluma na weledi.
inaendelea............

Thursday, February 25, 2016

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI, KATIBU MKUU WALA VIAPO KUIONGOZA TUME YA UTUMISHI YA JESHI LA POLISI NA MAGEREZA

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akila kiapo cha kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi na Magereza mbele ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu, Shabani Lila (kushoto) jijini Dar es Salaam leo. Tume hiyo inashughulikia masuala ya kiutumishi kwa askari Polisi na Magereza. Katikati ni Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugeta. 
 Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu, Shabani Lila (kushoto) akimpongeza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni  mara baada ya kumuapisha kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi na Magereza, katika tukio lililofanyika katika Mahakama hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Tume hiyo inashughulikia masuala ya kiutumishi kwa askari Polisi na Magereza.
 Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu, Shabani Lila (kushoto) akimkaribisha ofisini kwake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni kabla ya kumuapisha kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi na Magereza, katika tukio lililofanyika katika Mahakama hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Tume hiyo inashughulikia masuala ya kiutumishi kwa askari Polisi na Magereza.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akila kiapo cha kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi na Magereza mbele ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu, Shabani Lila (kushoto) jijini Dar es Salaam leo. Tume hiyo inashughulikia masuala ya kiutumishi kwa askari Polisi na Magereza. Katikati ni Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugeta. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni (kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu, mara baada ya Jaji huyo kuwaapisha kuwa viongozi wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi na Magereza katika tukio lililofanyika Mahakamani hapo, jijini Dar es Salaam leo. Injinia Masauni katika Tume hiyo amekuwa Makamu Mwenyekiti, na Meja Jenerali Rwegasira amekuwa Katibu. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

WAZIRI KITWANGA, MASAUNI NA WATENDAJI WAKUU JESHI LA MAGEREZA WAPANGA MIKAKATI KULIBORESHA JESHI HILO

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akizungumza na Watendaji Wakuu wa Jeshi la Magereza nchini pamoja na Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji wa kazi ndani ya Jeshi hilo na Wizara kiujumla. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Wakwanza upande wa kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP), John Minja.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto meza kuu) akizungumza na Watendaji Wakuu wa Jeshi la Magereza nchini pamoja na Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji wa kazi ndani ya Jeshi hilo na Wizara kiujumla. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kulia meza kuu ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Injinia Hamad Masauni. Wapili upande wa kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya. Wapili kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini (CGP), John Minja akifuatiwa na Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Jeshi hilo, Dk. Juma Malewa. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini (CGP), John Minja (kushoto) akijitambulisha kabla ya kuanza kikao cha Watendaji Wakuu wa Jeshi la Magereza pamoja na Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Kikao hicho kilichoitishwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto meza kuu) na kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kulia meza kuu ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Injinia Hamad Masauni. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.