TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, April 12, 2012

Mukama ang'aka

 *Awashukia wanaotakiwa kujivua gamba
*Adai wanatumika kumuhusisha na ufisadi
*Asema ndani ya CCM wote si Richmond


 Katibu Mkuu wa CCM Bw.Wilson Mukama.

Agnes Mwaijega na David John

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Wilson Mukama, amedai kukerwa na baadhi ya watu wanaomuhusisha na ufisadi uliofanyika kwenye miradi ya machinjio, maji na kusisitiza yeye ni msafi.

Bw. Mukama aliyasema hayo Dar es Salaam  wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya tuhuma dhidi yake ambazo zimetolewa katika vyombo vya habari vikimuhusisha na ubadhirifu wa fedha za miradi hiyo.

Alisema si kweli kwamba viongozi wote ndani ya CCM wanahusika na ubadhirifu katika miradi mbalimbali bali inawezekana tuhuma hizo zimeelekezwa kwake kwa sababu anahusika katika mapambano ya kuwavua magamba watu wanaokiuka maadili ndani ya CCM.

“Ndani ya CCM, si watendaji wote ni Richmond, inaonekana wengine wanatumia fursa hiyo kutaka kunichafua ili nionekane nashiriki ufisadi, mimi ni msafi nafanya kazi kwa kuzingatia maadili na nina wito ndiyo maana pamoja na kuwa mstaafu, bado nilionekana nafaa kuwa na wadhifa ndani chama,” alisema.

Aliongeza kuwa, taratibu za kisheria zipo hivyo kama kuna mtu ambaye mwenye hatia kwa tuhuma kama hizo kuna vyombo ambavyo vinaweza kushughulikia.

“Nashangazwa na baadhi ya watu kusema vitu ambavyo hawavijui undani wake, ni vema akaonesha uhalisia wa kitu anachokisema, miradi mingi ya maendeleo nchini inakufa kutokana na mabadiliko ya uongozi si ulaji wa fedha kama wengi wanavyodhani.

“Ieleweke wazi kuwa, miradi inakufa inapotokea yule aliyepewa nafasi ya kusimamia anapoondolewa na kuwekwa mwingine ambaye anashindwa kuuendeleza,” alisema Bw. Mukama.

Alisema kuna watu ambao hujitahidi kuonesha juhudi zao ili kuiwezesha nchi kupiga hatua lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kuandamwa, kusakamwa na kusemwa vibaya bila wahusika kufanya uchunguzi yakinifu.

“Katika nchi hii wanaofikiri kwa kina na kuumiza vichwa kwa ajili ya mafanikio wanaandamwa kila kukicha lakini waliokaa tu, wanaachwa na kuonekana wa maana.

“Tatizo kubwa la nchi hii wajinga ni wengi kuliko waelevu lakini haiwezekani nchi ikawa chini ya uongozi wa wajinga na wahuni ambao hawawezi kuliletea taifa manufaa.

“Watu wanaleta siasa magazetini badala ya kujikita katika kazi za msingi lakini mimi najua ninachokifanya, siwezi kuendelea kuona nchi haina mabadiliko,” alisistiza Bw. Mukama.

Aliongeza kuwa, suala la kujivua gamba katika chama litaendelea kwa wananchama wote ambao wataonekana kwenda kinyume na maadili na taratibu za chama.

Akizungumzia utendaji wa kamati za bunge, Bw. Mukama alisema kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni masuala yanayojadiliwa katika kamati hizo hayakupaswa kuwafikia wananchi kabla ya kumfikia spika na kujadiliwa bungeni.

Alisema kazi ya kamati mbalimbali si kutoa taarifa zilizojadiliwa na wabunge kwenye kamati husika bali zipo kwa kurahisisha utendaji wa wabunge.

“Mimi sioni kama ni sahihi masuala ya kamati mbalimbali za bunge kujulikana kabla ya kufika bungeni ambako ndiko yanapaswa kutolewa maamuzi,” alisema.
*Polisi kuimarisha ulinzi maeneo mengi
Na Waandishi Wetu, Arusha
MACHO na masikio ya wafuasi na wakereketwa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), leo yanaelekezwa jijini Arusha ambapo Mahakama Kanda ya Arusha, itatoa hukumu ya kesi ya kupinga matokeo ya ubunge Jimbo la Arusha Mjini.

Kesi hiyo ambayo ilifunguliwa na wapiga kura watatu ni ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi mbunge wa jimbo hilo Bw. Godbless Lema (CHADEMA),  dhidi ya mpinzania wake, Dkt. Batlida Burian (CCM).

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa waliozungumza na Majira, walisema hukumu hiyo itatikisa jiji hilo ambapo taarifa za kuaminika kutoka vyanzo mbalimbali, zinadai ulinzi katika maeneo mbalimbali utaimarishwa ili kuhakikisha hakuna uvunjifu wa amani.

Hukumu hiyo inatolewa katika kipindi ambacho wafuasi na wapenzi wa CHADEMA wakisherehekea matokeo ya kura yaliyompa ushindi mbunge mteule wa Arumeru Mashariki, Bw. Joshua Nassari, huku CCM ikiwa inatafakari ni wapi ilijikwaa hadi mgombea wake, Bw. Sioi Sumari akabwagwa chini.

Siku ya jana katika baadhi ya maeneo, gumzo kubwa lilikuwa hukumu hiyo ambapo baadhi ya watu walisikika wakisema hukumu itakayotolewa iwe ushindi wa Bw. Lema au kutenguliwa, utatikisa jiji hilo.

Jaji ambaye atatengua kitandawili hicho ni Gabriel Rwakibarila wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga baada ya upande wa walalamikiwa kumkataa Jaji Joyce Mujulizi ambaye awali alipangiwa kusikiliza kesi hiyo kwa madai ya kutokuwa na imani naye.

Wakati wa kusikilizwa kesi hiyo, upande wa Bw. Lema uliwasilisha mashahidi wanne. Katika uchaguzi huo uliofanyika 2010, Bw. Lema aliibuka mshindi kwa kura 56,169, wakati mpinzani wake Dkt. Burian akipata 37,460.
Askari wa kikosi cha zimamoto na Uokoaji cha Halimashauri ya Jiji la Dar es salaam wakipambana kuzima moto uliolipuka na kuteketeza majiko ya soko la Samaki la kimataifa la feli jana chanzo cha moto huo ni mlipuko wa mafuta katika moja ya majiko ya kukaangia samaki.
Na Bahati Mohamed

WANACHAMA wa Chama cha Tanzanian Labour Party (TLP), wamempa Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Bw. Augustino Mrema muda wa siku 40 awe amejiuzulu wadhifa wake kwa madai ya kuchangia chama hicho kishindwe katika uchaguzi wa mdogo wa ubunge Jimbo Arumeru Mashariki, mkoani Arusha.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Hamad Tao, aliyasema hayo Dar es Salaam  wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema tamko la kumtaka Bw. Mrema kujiuzulu analitoa kwa niaba ya wanachama wa chama hicho kutokana na matokeo mabaya ya kura 18 walizopata katika kata zote za jimbo hilo na kusisitiza kama atashindwa kujiuzulu ndani ya muda huo, wataitisha  maandamano nchi nzima ili kushinikiza aondoke.

“Bw. Mrema alipewa fedha za kutosha kwa ajili ya kampeni lakini hatukuona alichofanya zaidi ya kuzitumia kwa matumizi binafsi,” alisema Bw. Tao.

Aliongeza kuwa, wanachama wa TLP hawakuridhishwa na uchaguzi uliofanyika katika chama chao juu kumpata mtu ambaye atawania nafasi ya ubunge wa Afrika Mashariki.

Alisema aliyechaguliwa kugombea nafasi hiyo kwa tiketi ya TLP si mwanachama wa muda mrefu bali alipewa kadi ya uanachama akitokea CCM ili aweze kuwania nafasi hiyo.

Bw. Tao aliipongeza CHADEMA kwa kupata ushindi katika uchaguzi uliofanyika Arumeru Mashariki.
TATIZO la rushwa nchini lipo katika sekta mbalimbali lakini hali hiyo haina maana kuwa inakubalika katika jamii.
Ukweli ni kwamba, rushwa haikubaliki kutokana na madhara yake ndio maana Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha vitendo hivyo vinatokomezwa.

Rushwa inaathiri maendeleo ya mtu binafsi, familia, Taifa na kushusha hadhi ya mtoaji na mpokeaji. Rushwa inachangia kupindisha kanuni za maadili wakati wa kutekeleza majukumu kwa maslahi ya umma, mtu au kikundi fulani.

Vitendo hivyo vinajumuisha matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha baadhi ya viongozi wa umma na sekta binafsi, kutumia madaraka waliyonayo kinyume cha sheria ili kujinufaisha.

Rushwa 'imebatizwa' majina mengi, wengine huiita mlungula, kitu kidogo, shati la mikono mirefu au zawadi.

Watu wanaojihusisha na vitendo hivyo, wanawanyima wananchi mategemeo ya kuwa na maisha bora, kuwakosesha elimu, huduma bora za afya, chakula, maji na mahitaji mengine ya kibinadamu.

Sisi tunasema kuwa, rushwa ni wizi dhidi ya Taifa na wananchi ambao wanategemea maisha bora, inachochea makosa ya jinai yanayovuka mipaka, kuvunja amani na utulivu.

Rushwa ina madhara makubwa kiuchumi kwa lugha nyepesi ni uovu unaowavunja moyo Watanzania na wafanyabiashara ambao wangependa kuwekeza nchini.

Inaongeza ugumu wa maisha kwa wananchi wakati mwingine husababisha kupungua ubora wa bidhaa ambazo huzalishwa viwandani.

Imani yetu ni kwamba, rushwa husababisha mapato ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kupungua hivyo kupuguza uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi kutekeleza malengo ya kuboresha maisha yao na miundombinu ya nchi.

Uovu wa rushwa unachangia kuongeza umaskini katika jamii, kuathiri ubora wa elimu na sekta nyingine nchini. Rushwa inaweza kusababisha mgonjwa asipone haraka au kupoteza maisha kama atakataa au kukosa kile alichodaiwa kukitoa.

Tukifikia kiwango cha kuibubali rushwa kama sehemu ya utamaduni wetu katika vyombo vya sheria, waathiriwa wataamua kujilinda wenyewe kwa kuchukua sheria mkononi hivyo kuharibu sifa ya amani na utulivu tulionao.
Na Godwin Msalichuma, Kilwa
WAKULIMA wa korosho wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi, wamekitaka chama
kikuu cha ushirika mkoani humo, Ilulu kutenga korosho kwa ajili ya
kubangulia  ili kuziongezea thamani ya zao hilo na zingine kuzitafutia soko nje ya nchi.
Hali hiyo itasaidia kuacha  kutegemea wanunuzi wa kati ambao wengi wao ni wababaishaji  na wanachangia soko la zao hilo na hivyo kusababisha mkulima kukosa malipo kwa wakati na kuendelea kulima kilimo kisicho na tija.

Mwito huo ulitolewa hivi karibuni na wakulima hao waliokutana katika
mkutano wa wadau wa kilimo ulioitishwa na shirika lisilo la kiserikali
la kimataifa la Action Aid Internainal Tanzania (AAIT) ikiwa ni sehemu
ya utekelezaji wa mradi wa kuimarisha na kukuza kilimo cha zao hilo
wilayani humo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha
maendeleo ya wananchi mjini Kilwa masoko.

Walisema ili kuondokana na ubabaishaji unaofanywa na wanunuzi wa kati
ni vyema Ilulu ikatafuta soko la zao hilo nje ya nchi na kuuza ,moja
kwa moja kwa wanunuzi wakubwa mara baada ya kukusanya korosho kutoka
kwa wakulima na kuachana na utaratibu wa sasa ambapo chama hicho
kinawauzia wanunuzi wa kati ambao nao wanaenda kuuza kwa wanunuzi
wakubwa wanauza nje ya nchi.
“Mfumo wa ununuzi unaotumika ni mzuri lakini linapokuja suala la soko
ndio tatizo linapoanzia hapo…tunadhani ili kuondokana na tatizo hili
ni vyema chama chetu kikuu kikatafuta soko nje ya nchi…lakini pia kiwe
na mipango madhubuti ya kubangua angalau kiasi kidogo ili kuongeza
thamani korosho zetu”, alisema Bw.Yusufu Mcheni Mwenyekiti wa Chama
cha Msingi cha TAPWA.

Naye Bw. Athumani Kingolopi wa Chama cha  Msingi Ujirani Mwema ,
alisema kuwa ununuzi  ulikwenda  vizuri mwaka jana chini ya mfumo wa
stakabadhi ghalani na kuwa  mfamo mzuri wa kuigwa, lakini mwaka huu
wanunuzi waligoma kununua kwa bei nzuri mnadani na hivyo kuyumbisha
wakulima ambao wengi wao hadi leo hawajalipwa malipo yao ya pili.

“Kwa maoni yangu naona ni bora tutenge kiasi fulani kwaajili ya
kubangua na zinazobaki zikuzanywe na kuuzwa moja kwa moja nje ya nchi
ili kuondokana na tatizo hili na kumuongezea mkulima kipato…hawa
wanunuzi wa kati wanatuyumbisha”, alisema Bw. Kingolopi.

Awali Mkuu wa Idara ya Kilimo na Usalama wa Chakula kutoka Action aid
Makao Makuu, Bw. Elias Mtinda, alisema kuwa shirika hilo lipo tayari
kuwadhamini wakulima hao ili kupata mkopo kutoka vyombo vya fedha
kwa ajili ya kununulia mashine za kubangulia korosho zao.
Na Said Hauni, Lindi

WATU wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamevamia makazi ya viongozi wa dini ya Kikristo Parokia ya Nyangao Wilaya na Mkoa wa Lindi huku wakipora fedha taslimu sh. milioni tano.

Pia inadaiwa licha ya kupora fedha hizo viongozi hao, ilidaiwa walijeruhiwa watu wanne wakiwemo viongozi wawili na walinzi wao wawili kwa kuwacharanga mapanga sehemu mbalimbali ya miili yao.

Habari kutoka Kata ya Nyangao ambazo zilithibitishwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa zilieleza kuwa tukio hilo lilifanyika Machi 30, mwaka huu majira ya saa 6:45 za usiku.

Kaimu Kamanda wa Polisi, Bw. George Mwakajinga alisema katika tukio hilo watu watatu kati ya hao walishambuliwa kwa kupigwa mapanga sehemu mbalimbali za miili yao wakati mmoja alifungwa kamba na kutupiwa kwenye shimo la taka.

Bw. Mwakajinga aliwataja walioshambuliwa kuwa ni ni, Paroko Housiager Hugo (74) na Padri Michael Mrope (75), Bw. Victor Hanga (58) na Joseph Mathias (45) ambao ni walinzi wa nyumba za viongozi hao.

Alisema, Bw.Hugo ambaye kwa sasa amelazwa Hospitali ya Mision ya Ndanda iliyopo Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara alipigwa mapanga kichwani na mbavuni ambapo, Bw. Hanga ambaye ni mlinzi pia alijeruhiwa na panga kichwani na kulazwa Hospitali Teule ya Nyangao.

Pia aliongeza kuwa Padri Mrope alishambuliwa kwa kupigwa huku mlinzi wake, Bw. Michael akifungwa kamba na kutupiwa kwenye shimo la taka hadi majambazi hayo yalipoondoka na kuokolewa na askari polisi waliofika kwenye eneo hilo.

Alisema, majambazi hayo ambayo yanasadikiwa kufikia zaidi ya 10 walikuwa na silaa mbalimbali yakiwemo mapanga, marungu na bunduki na walivamia makazi ya viongozi hao na kufanikiwa kupora fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni tano na kutokomea nazo kusikojulikana.

“Kabla hawajazichukuwa fedha hizo walipambana na walinzi waliokuwa wakiwalinda, lakini walizidiwa nguvu na ndipo majambazi hayo yalimfunga kamba mlinzi mmoja na mwingine kumjeruhi kwa panga kichwani,” alisema Bw. Mwakajinga.

Kaimu Kamanda huyo alisema katika tukio hilo hakuna mtu ambaye amekamatwa hadi sasa na kwamba askari wanaendelea na kazi ya kuyasaka majambazi hayo ili yaweze kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamani.

Baadhi ya wananchi wanaodai waliweza kushuhudia sakata hilo lakini walishindwa kujitokeza kutoa msaada kutokana na majambazi hayo kufyatua risasi mbili hewani ambapo yalielekea kwenye makazi ya viongozi hao wakiwa kwenye gari moja aina ya Toyota 'Pick Up'.
Radhia Ramadhani na Joyce Kambota

WATU wanne raia wa Nigeria wamekamatwa na madawa ya kulevya aina ya HEROINE yenye thamani ya shilingi bilioni 1 .4 za kitanzania jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar e Salaam, Kamanda wa Polisi  kanda maalum mkoa wa Dar es Salaam Bw. Suleiman Kova alisema watuhumiwa wa kesi hiyo sio watanzania ni  wanaigeria waishio maeneo ya Tabata kinyerezi kibaga.

" Tukio hilo limekuwa la ajabu sana kwani hatujawahi kukamata dawa za aina hiyo zilizokuja kwa dizaini ya pakti za chumvi tena zimekaushwa" alisema Kamanda Kova.

Watuhumiwa hao waliotambulika kama Bw.Ifeanyi     Oko(33),Bw.Uchendu Jerry(35),Bw.Ugwu Valentine(31) na Bi. Ani Lawretta(27)mbali na kukamatwa na paketi nne pia wamekutwa na kete 12 za madawa zilizokuwa tayari kwa kumezwa.

Kamanda Kova aliongeza kuwa hadi sasa nchini kumekuwa na mtandao wa madawa ya kulevya kutoka nchi za nje hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuwafichua watu ambao wana mashaka nao.

Wakati huohuo Kamanda Kova alisema walifanikiwa kuwakamata waalifu Sugu (84) kwa tuhuma mbalimbali kufuatia misako inayoendelea ili kuhakikisha hali ya jiji la Dar es Salaam ni tulivu.

"Miongoni mwa vitu ambavyo tunaweza kujivunia jeshi la polisi ni pamoja na juhudi zilizofanywa na kikosi maalum wakishirikiana na ulinzi shirikishi kwa kufanya dolia na kuwakamata waarifu hao"alisema Kova.

Baadhi ya watuhumiwa hao ni Bw.Rashid Seif(25),Bi.Habiba Juma(22),Bw.Ramadhan Suleiman(30),Bw.Shaban Adam(33),Bw.Salehe Omary(17)na wengine79.
MA D I WA N I w a Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya wamesema kupungua kwa ukusanyaji wa mapato ya halmashauri hiyo ni dalili inayotokana na uvujaji wa fedha unaofanywa na baadhi ya watumishi.Pia walidai hali hiyo imekuwa ikichangia baadhi ya watumishi  kuvujisha na hata kughushi stakabadhi za kukusanyia mapato.
Imeelezwa kuwa watumishi hao wamekuwa wakiigeuza halmashauri hiyo kama shamba la bibi kwa kuchota fedha watakavyo na hivyo kusababisha kushuka kwa mapato kutoka sh. milioni 600 zilizokusanywa mwaka jana hadi kufikia sh. milioni 300 mwaka huu.
Hayo yalisemwa juzi wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani  kilichofanyika katika Ukumbi wa John Mwankenja ambapo walisema kama vitendo vya ufujaji fedha vinavyofanywa na baadhi ya watendaji vitaendelea itabidi Mkurugenzi wa wilaya hiyo Bw. Noel Mahyenga pamoja na Mweka  Hazina wa halmashauri Bw. John Shirima wawajibike.
Akizungumza katika kikao hicho Diwani wa Kata ya Masukulu, Bw. Rephson Mwaisupule alisema,  miezi mitatu iliyopita katika  kipindi cha mwaka jana fedha  zilizokuwa zimekusanywa katika  vyanzo vya ndani vya mapato  zilikuwa sh. milioni 600 lakini  katika hali ya kushangaza mwaka  huu zilizokusanywa ni sh. milioni  300 tu.
Naye Diwani wa Kata ya Kawetele  Bw. Anyimike Mwasakilali alisema tatizo la ufujaji wa fedha za mapato katika halmasahauri hiyo  ni aibu hivyo inatakiwa watendaji wote waliofanya ubadhirifu huo kuchukuliwa hatua za kisheria wakiwemo watendaji wa kata na vijiji wanakusanya fedha katika  kata zao na vijiji.
Naye Diwani wa Kata ya  Lwangwa Bw. Robart Mwaibata alisema baadhi ya watumishi wamekuwa   wakiandika ushuru ma l i p o ma k u bwa ka t i k a stakabadhi za malipo lakini fedha zinazofikishwa halmashauri ni kidogo hali ambayo imekuwa ikisababisha halmashauri kujikuta haina mapato ya  kutosha.
Akizungumzia malalamiko hayo ya madiwani Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bw. Meckison Mwakipunga alisemna kuwa halmashauri tayari imeanza kuchukua hatua dhidi ya watendaji
wanaofuja fedha ambapo hadi sasa watumishi 11 wa halmashauri hiyo wamesimamishwa kazi.
Alisema kuwa, tayari watumishi hao hawapo kazini baada ya kubainika kufuja fedha hizo na uchunguzi zaidi unaendelea  kuhusiana na ufujaji huo ili kujua kama kuna watumishi wengine waliofanya ubadhirifu huo nao waweze kuchukuliwa hatua kama walivyochukuliwa hawa wengine.
Tunachoomba ni ushirikiano kwa nyie madiwani kwenye kamati ya fedha ambayo tayari ipo, kazini
kushughulikia ubadhirifu huo, tunajua tutawabaini wengine ambao wamejificha kwani fedha hizo zimefunjwa na wengi, alisema Mwenyekiti huyo.

Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. JakayaKikwete ajuwa na mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa kamuni ya UnileverGlobal, Bw. Paul Polman, Ikulu jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Ikulu)
Anneth Kagenda na Flora Amon

HALMASHAURI y a Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara imepewa siku 14 kuwa imepeleka mchanganuo mpya ambao pamoja na mambo mengine uwe unaainisha vizuri matumizi ya sh. milioni 77 ambazo inadaiwa kuwalipa wafanyakazi hewa. Agizo hili lilitolewa Dar es Salaam jana na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Bw. Idd Azzan.
Alisema  halmashauri hiyo imetumia fedha hizo kuwalipa wafanyakazi hewa  na watu waliostaafu, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Alisema watu waliolipwa fedha hizo watatakiwa kuzirudisha na ikiwa watakaidi sheria itachukua
mkondo wake. Alisema kuwa halmashauri hiyo inatakiwa kuwabana ili wazirudishe pamoja  na kutoa mchanganuo unaoeleweka juu ya fedha sh. milioni 119 ambazo zilikuwa ni za ujenzi wa zahanati.
"Tunaomba maagizo yote tuliyotoa yatekelezwe kwa muda muafaka, lakini pia ikumbukwe kwamba kamati imesikitishwa kuona hoja zingine zimeshindwa kupatiwa majibu yanayoeleweka," alisema.
Mwenyekiti huyo aliitaka halmashauri hiyo kuwa makini mara tu zinapotakiwa kuwasilisha michanganuo inayoonesha utendaji wao, kutoa ushirikiano kati ya halmashauri ya Babati Mjini na Vijijini.
Naye Mwenyekiti wa LAAT Bw. Augustino Mrema, alitoa onyo kali kwa halmashauri hiyo na kusema;
"Lazima makosa yao yatafutiwe adhabu ya onyo la mdomo ili kuleta tija" alisema.
Wakati huo huo,Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imetakiwa kupunguza matumizi ya fedha kwenye semina, maonsho.
Hayo yalibainisha Dar es Salaam  na Makamu Mwenyekiti wa Hesabu za Serikali Bi.Zainabu Vullu,wakati wakupitia hesabu za wizara hiyo. Bi.Vullu alisema, sh. Bilion 1.9 zimetumika kinyume na bajeti ikiwemo sh. milion 729 kutumika kwenye sherehe za nane nane mjini Dodoma. Alisema mbali na fedha hizo pia Wizara ilichangisha kwa Taasis mabalimbali sh. miloni 86.kwa ajili ya sherehe ya nane                          
Watoto wakicheza kwa kuning'inia katika gari lilokuwa Mtaa wa Braziri eneo la Kinondoni,Dar es salaam.bila kujua kuwa wanahatarisha usalama wao.

Anneth Kagenda na Frola Amon

ADHA y a k u k a t i k a umeme mara kwa mara imewawakumba wabunge  waliokuwa wakihudhuria vikao vya kamati za bunge kwenye Ofisi Ndogo ya Bunge, hatua iliyowalazimu kuahirisha vikao hivyo. Akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) Mwenyekiti wake, Bw. John Cheyo, alisema kutokana na adha hiyo, walilazimika kusitisha vikao vyao baada ya kusubiri umeme urudi bila
mafanikio.
"Waheshimiwa wajumbe naahirisha kamati hadi (kesho) kwani leo, hatuwezi kuendelea bila umeme," alisema Bw. Cheyo. Wakati akiahirisha kikao hicho tayari watendaji wa Idara ya Mwasibu Mkuu wa serikali walikuwa wamefika ofisi za bunge kuwasilisha taarifa za matumizi ya fedha. Kwa upande wak e
Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) Bw. Augustino Mrema, yeye alisitisha
kusikiliza mchanganuo wa ripoti ya mkoa wa Singida kutokana na matatizo hayo ya umeme. Wa k i z u n g u m z a n a waandishi wa habari baadhi ya wabunge walisema kukatika kwa umeme kunaathiri shughuli nyingi nchini.
Mbunge wa Mufindi Kusini Bw. Mendrad Kigola alisema "Kukatika kwa umeme kumetuadhiri kwani mambo mengi yameshindwa

Na Charles Mwakipesile, Mbeya

MKUU wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro, amesema mafisadi wanaoiba dawa za Serikali, kuzipeleka kwenye maduka ya watu binafsi na kusababisha uhaba mkubwa wa dawa katika Bohari Kuu (MSD), hawawezi kuvumiliwa.
Bw. Kandoro aliyasema hayo jana mjini Mbeya wakati akifungua warsha ya siku moja iliyoshirikisha wadau wa MSD kutoka mikoa ya Singida, Dodoma, Iringa na Njombe.

Alisema Serikali imekuwa ikishuhudia uhaba mkubwa wa dawa uliopo MSD wakati maduka binafsi yanauza dawa za Serikali ambazo haziruhusiwi kuuzwa katika maduka hayo.

“Kimsingi Serikali inatumia mabilioni ya fedha kuhakikisha MSD inakuwa na dawa za kutosha ambazo zitasambazwa katika hospitali ili ziweze kuwasaidia Watanzania,” alisema.

Aliongeza kuwa, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapaswa kufanya uchunguzi katika maduka binafsi kubaini mafisadi wa dawa ili wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia hiyo.

Bw. Kandoro alisema tabia ya wizi wa dawa unafanywa na watu wasio na nia njema na uchumi wa nchi ambao unategemea watu wenye nguvu na afya bora hivyo kinachotakiwa kufanya uchunguzi ili kuwabaini watu wanaofanya ufisadi wa kuiba dawa MSD.

“Nawaonya wauzaji dawa katika maduka binafsi kuacha tabia ya kuuza dawa zilizopita muda wake, kitendo hiki ni sawa na uuaji kwani matumizi yake ni sawa na sumu mwilini hivyo kusababisha madhara makubwa kwa mtumiaji kiafya,” alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Kanda, Bw. Cosmas Mwaifwani, alisema MSD imejipanga kuhakikisha inawahudumia Watanzania kwa kiwango stahiki na kukidhi mahitaji yao.

Alisema katika mpango wa muda mfupi, wamejipanga kuhakikisha wanakuwa na utaratibu wa kufikisha dawa hadi vituo vya afya kwa ajili ya kumaliza tatizo la upungufu na upatikanaji wa dawa.

Aliongeza kuwa, mawakala wamekuwa wakichelewa kupeleka maombi ya dawa MSD hivyo kusababisha zisipatikane kwa wakati.
Na Zahoro Mlanzi

KIKAO cha Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kimeshindwa kumalizika juzi kama ilivyotarajiwa kutokana na wajumbe waliohudhuria kikao hicho, baada ya kutokea mvutano katika kufikia muafaka wa rufani zilizowasilishwa na Klabu ya Yanga.
Kikao hicho kilianza juzi jioni na kuendelea tena jana chini ya Mwenyekiti wake Kamanda Mstaafu wa Polisi, Alfred Tibaigana akiwa na baadhi ya wajumbe wake pamoja na viongozi wa Yanga, wajumbe wa Kamati ya Ligi na wawakilishi wa TFF.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana baada ya kuulizwa kilichofikiwa katika kikao cha kamati hiyo iliyokutana juzi, Ofisa Habari wa shirikisho hilo, Boniface Wambura alisema kikao kilishindwa kumalizika na kwamba kilitarajiwa kumalizika jana usiku.

"Kwa kweli hatutaweza kutoa taarifa juu ya kilichoamuliwa katika kikao hicho kama nilivyoahidi kutokana na kuwa hakikumalizika, hivyo kinaendelea leo (jana) jioni na kwamba watakalofikia lolote kesho (leo) au keshokutwa tutatoa taarifa," alisema Wambura.

Kikubwa katika rufani hiyo, Yanga walipinga adhabu iliyotolewa na Kamati ya Ligi ya kuwafungia wachezaji wao watano, pamoja na kupinga maamuzi yaliyotolewa na mwamuzi Israel Nkongo, katika mechi yao hiyo dhidi ya Azam FC.

Wachezaji waliofungiwa ni Stephano Mwasika aliyefungiwa mwaka mmoja na faini ya sh. milioni moja, Jerry Tegete kifungo cha miezi sita na faini ya sh. 500,000, Nadir Haroub 'Cannavaro' alifungiwa mechi sita na faini ya sh. 500,000, Omega Seme na Nurdin Bakari wao walifungiwa mechi tatu kila mmoja.

Kutokana na adhabu hiyo, Yanga ilikata rufani kwa Kamati ya Tibaigana ambapo baada ya kamati hiyo kuomba vielelezo kwa kamati husika na kukosekana iliamua kuzisimamisha kwa siku 14 kutoa nafasi ili kupata ushahidi wa kutosha isipokuwa kwa zile zilizotolewa ndani ya dakika 90 ya mchezo.

Wakati hilo, likiwa bado halijapatiwa ufumbuzi kamati ya ligi ikaipoka Yanga pointi tatu na kuipa Coastal Union ya Tanga, pamoja na mabao mawili kutokana na kumchezesha Canavaro ikidaiwa hajamaliza adhabu aliyotakiwa kuitumikia ya kukosa mechi tatu kitu ambacho kimeibua mjadala mwingine upya.

Katika hatua nyingine, alipotafutwa Ofisa habari wa Yanga, Louis Sendeu kuthibitisha kwamba wamekata rufani juu ya kupokwa pointi, alisema wanasubiri kwanza maamuzi ya Kamati ya Nidhani, ndipo watajua la kufanya.

Hata hivyo wakati gazeti hili linakwenda mitamboni, zilipatikana taarifa kwamba katika hicho cha Kamati ya Nidhamu kulikuwa na mvutano mkubwa huku Kamati ya Ligi ikionekana kuzidiwa hoja na wajumbe wengine juu ya adhabu walizotoa kwa wachezaji wa Yanga.

Maskini Lulu, ombi lake latupwa

                                  
Na: Elizabeth Michael
 Suleiman Mbuguni

MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael 'Lulu' jjuzi ameshindwa kutoa salamu za mwisho kwa msanii mwenzake katika tasnia hiyo, Steven Kanumba ambaye anadaiwa kabla ya kifo chake walikuwa pamoja nyumbani kwa marehemu Sinza Vatcan jijini Dar es Salaam.
Lulu ambaye anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Osterbay, Kinondoni jijini Dar es Salaam inadaiwa kwamba aliomba kwenda kutoa salamu za mwisho kwa msanii huyo nguli wa filamu ambaye alifariki Aprili 7, mwaka huu nyumbani kwake Sinza, Dar es Salaam.

Hata hivyo msanii huyo alishindwa kutokea katika shughuli za kumuaga Kanumba, kutokana na habari zilizodai kwamba ni za kiusalama.

Juzi Kamanda wa Mkoa wa Polisi Kinondoni, Charles Kenyela alinukuliwa katika vituo vya televisheni nchini akisema kwamba Lulu anashikiliwa katika cha Oysterbay, lakini kwa kuwa suala hilo lipo kisheria alikuwa anasubiri matokeo ya daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Kanumba.

"Ni kweli tunamshikilia Lulu, lakini hata hivyo hatuwezi kulizungumzia lolote kwa kuwa suala hili lipo kisheria na bado mwili wa marehemu unafanyiwa uchunguzi hospitalini," alisema Kenyela.

Hata hivyo katika shughuli za kuuga mwili wa Kanumba yaliyofanyika katika viwanja Leaders Klabu, Dar es Salaam maelfu waliojitokeza kutoa salamu za mwisho kwa nyota huyo wa filamu nchini walishindwa kufanya hivyo kutokana na wingi wa watu waliojitokeza.

Ilikuwa ni simanzi, majonzi na vilio katika viwanja hivyo baada ya mwili wa Kanumba kuwasili sehemu iliyotayarishwa, huku baadhi ya wanawake wakidondoka na kupoteza fahamu.

Hatua hiyo iliwafanya watoa huduma ya kwanza kutoka Msalaba Mwekundu kuwa na shughuli pevu ya kuwapeleka katika magari yao kwa ajili ya kuwahudumia.

Kutokana na tafrani hiyo MC alilazimika kutangaza kusitisha shughuli ya kumuaga Kanumba, kitu ambacho watu waliofika katika viwanja hivyo kuanza kupiga kelele za kutoridhishwa.

Hata hivyo kabla ya kutangaza kusitisha viongozi wa serikali walioongozwa na Makamu wa Rais, Mohamed Ghalib Bilal kupewa nafasi ya kuuga mwili huo pamoja na baadhi ya ndugu wa karibu.

Viongozi wengine waliopata nafasi ya kutoa salamu za mwisho kwa marehemu Kanumba, alikuwa mke wa Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete, Mke wa Makamu wa Rais Mama Bilal, Waziri Ardhi Anna Tibaiujka, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe.

Viongozi wengine ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Mecky Sadiq, Mbunge wa Kinondoni Idd Azzan, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana na Meya wa Manispaa hiyo, Yusuf Mwenda.