TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 27, 2014

CHUO CHA DAR ES SALAAM CITY COLLEGE (DACICO) KINAWATANGAZIA NAFASI ZA MASOMO KWA KOZI ZA UTANGAZAJI KATIKA NGAZI ZA CHETI NA DIPLOMA. CHUO KIPO KIBAMBA CHAMA MITA 100 KUTOKA BARABARANI, CHUO KINA MAENEO MAZURI YA MADARASA YA KUSOMEA PAMOJA NA HOSTEL ZA KISASA KWA WALE WANAOPENDA KWA GHARAMA NAFUU, KWA MAWASILINO ZAIDI PIGA SIMU NAMBA 0767-869133

Miongobi mwa  Wanafunzi wa  Masomo ya Uandishi wa Habari Wakiwa kwenye Studio za Mazoezi za Radio hiyo inayotumiwa na Wanafunzi kupata  Elimu iliyo bora kwa ajili ya kukidhi Mahitaji ya Sanyansi na Tekinolojia kwa wanafunzi wa Chuo hicho.
Miongobi mwa  Wanafunzi wa  Masomo ya Uandishi wa Habari Wakiwa kwenye Studio za Mazoezi za Radio hiyo inayotumiwa na Wanafunzi kupata  Elimu iliyo bora kwa ajili ya kukidhi Mahitaji ya Sanyansi na Tekinolojia kwa wanafunzi wa Chuo hicho.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewatimua wanachama wake 42

index
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewatimua wanachama wake 42 wakiwemo wagombea walioshindwa kupita kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wa hivi karibuni.
Kwa mujibu wa taarifa ya chama hicho, kutimuliwa kwa wanachama wake hao ni hatua ya chama hicho kujisafisha kutokana na kile kinachodaiwa kwamba baadhi ya wagombea hao wanatuhumiwa kufanya hujuma wakati wa mchakato wa uchaguzi serikali za mitaa, vitongoji na vijiji uliofanyika Desemba 14, mwaka huu.
Akitangaza uamuzi huo mjini humo, Katibu wa Chadema Jimbo la Korogwe Mjini, Ezekiel Mbwilo alisema wahusika waliotimuliwa uanachama wanatuhumiwa kwa kukubali vitisho na wengine kurubuniwa kwa fedha za wapinzani wao, hatua iliyowalazimu kwenda kuondoa majina yao katika hatua za mwisho kuelekea kwenye kinyang’anyiro hicho.
“Tuligundua kuwa baadhi ya wahusiska walijihusisha na hujuma mbalimbali dhidi ya chama chetu, ikiwamo kukubali kupewa fedha na wapinzani wao ili wajiondoe. Tangu awali, tulishakubalina kwamba ikibainika watu waliofanya hujuma tutawatimua kundini na hapa ndipo tunahitimisha lile tulilokubaliana,” alisema.
Mbwilo alitaja maeneo wanayotoka wanachama hao waliotimuliwa na idadi yao kwenye mabano ni Kwamsisiwatu (6), Mahenge (10), Kitifu (25) pamoja na mmoja kutoka Manundukati ambaye alidai kwamba mhusika huyo aliamua kujitoa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi ukiwa katika hatua za mwisho baada ya kurubuniwa na wapinzani wa chama hicho.
Akizungumzia vitisho alivyodai vilitolewa baadhi ya wanachama wa vyama vingine dhidi ya wagombea wa Chadema, Mbwilo alisema tayari amewasilisha taarifa hizo kwenye vyombo vya usalama na katika jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi.

DR. SHEIN AFUNGA MASHINDANO YA RIADHA UWANJA WA AMAAN ZANZIBAR

unnamedRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikabidhi Kombe la Ushindi wa Jumla kwa Kassim Hussein Saleh na fedha tasilimu Shilingi Millioni  Moja akiwakilisha wilaya ya Mjini  iliyopata medali 17 za zahabu,13 fedha na 5 za Shaba katika ufungaji wa Mashindano ya Riadha katika Wilaya kumi za Unguja na Pemba aliyoyafunga leo katika uwanja wa Amaani Studium (kushoto) Kaimu Waziri wa Habari,Utalii,Utamadunu na Michezo pia Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdilahi Jihadi Hassan [Picha na Ikulu.] unnamed1Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi zawadi Mtoto  Sofia Kombo Makame aliyekimbia umbali wa kilomita nyingi kutokana na umri wake katika mashindano ya Riadha zawadi hiyo alipewa wakati wa ufungaji wa Mashindano ya Riadha katika Wilaya kumi za Unguja na Pemba   katika uwanja wa Amaani Studium leo Mjini Unguja,[Picha na Ikulu,] unnamed2Mwenyekiti wa  Chama cha Riadha Zanzibar Abdulhakim Cosmas Chasama alipokuwa akitoa salamu za Chama Riadha mbele ya Rais wa Zanzibar na   Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein wakati wa ufungaji wa mashindano ya Riadha kwa Wilaya ya Kumi za Unguja na Pemba katika Uwanja wa Amanaan Studium Mjini Unguja leo.
[Picha na Ikulu.]
unnamed3Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoa hutuba yake ya ufungaji  wa Mashindano ya Riadha katika Wilaya kumi za Unguja na Pemba aliyoyafunga leo katika uwanja wa Amaani Studium [Picha na Ikulu.] unnamed4Wanamichezo kutoka wilaya ya Kaskazini A Unguja na Kusini Unguja wakiwa katika uwanja wa Amaan Studium wakati wa ufungaji  wa Mashindano ya Riadha katika Wilaya kumi za Unguja na Pemba aliyoyafunga leo katika uwanja wa Amaani Studium yaliyofungwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein [Picha na Ikulu.] unnamed5Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Baraza  la Michezo Bi Sharifa Khamis (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Zanzibar Abdulhakim Cosmas Chasama (kushoto)  baada ya kutoa nishani kwa wakimbiaji wa mashindano ya Riadha wakati wa ufungaji katika uwanja wa Amaan Studiam leo,[Picha na Ikulu.]

Jokate Mwegello atoa msaada kituo cha yatima cha Extrem cha Tandale

2
 Miss Tanzania namba mbili 2006, mwanamitindo na mcheza filamu, Jokate Mwegello, akicheza na mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Yatima cha Extrem cha Tandale kwa Bi Mwamvua Jumanne, alipotembelea kuwapa zawadi ya Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Zawadi alizotoa ni mchele, unga wa sembe, sabuni na ndala zenye nembo za Kidoti.  Picha na Jumanne Juma
7
Miss Tanzania namba mbili 2006, mwanamitindo na mcheza filamu, Jokate Mwegello, akimpa zawadi ya ndala mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Yatima cha Extrem cha Tandale kwa Bi Mwamvua Jumanne, alipotembelea kuwapa zawadi ya Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Zawadi alizotoa ni mchele, unga wa sembe, sabuni na ndala zenye nembo za Kidoti.  Picha na Jumanne Juma
IMG_2647
Miss Tanzania namba mbili 2006, mwanamitindo na mcheza filamu, Jokate Mwegello, akiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaolelewa katika Kituo cha Yatima cha Extrem cha Tandale kwa Bi Mwamvua Jumanne, alipotembelea kuwapa zawadi ya Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. Zawadi alizotoa ni mchele, unga wa sembe, sabuni na ndala zenye nembo za Kidoti.  Picha na Jumanne Juma
………………………………………………………………………….
MISS Tanzania namba mbili 2006, mbunifu mavazi na muigizaji wa filamu za kibongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’,  jana ilitoa msaada wa vitu mbalimbali katika Kituo cha Kulea Yatima cha Extrem kilichopo  Tandare kwa Bi Mtumwa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
 
Mrembo huyo ambaye pia ni mkurugenzi  wa kampuni ya  Kidoti inayojihusisha na masuala ya urembo, alitoa msaada huo kama zawadi yake ya Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya kwa watoto hao kama sehemu ya kuwafariji ili nao kujiona wako sawa na wengineo wanaioshi nawazazi wao.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Jokate alisema kuwa ameguswa na kituo hicho ambacho huwa hakikumbukwi na wahisani kutokana na mazingira ya eneo hilo.
 
“Nimefika hapa kutoa msaada kama sehemu ya kuonyesha ninavyoguswa na jamii ya watoto kama hawa, lakini pia nikiwa na lengo la kuwafariji ili nao kujiona ni sehemu ya jamii ya Watanzania,” alisema.
Kidoti alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa watu wenye uwezo, kampuni na taasisi mbalimbali kuona umuhimu wa kusaidia makundi hayo maalumu katika jamii kwani nao wana haki ya kuishi na kufurahia maisha kama wengine.
 
Msaada aliokabidhi kwa ushirikiano na kampuni ya Raibow Shell, ni mchele, unga wa sembe, sabuni, jozi za viatu vyenye nembo za Kidoti.
Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, mlezi wa watoto hao, Mwamvua Jumanne, alitoa pongezi kwa Kidoti na kuwasihi wengine kuiga mfano wa mrembo huyo kusaidia makundi maalum.
 
Akielezea changamoto zilizopo katika kituo hicho, Mwamvua alisema ni kukosa uwezo wa kifedha kuwalipia ada watoto wanaosoma elimu ya msingi na sekondari, gharama za matibabu pamoja na kukosa watu wa kuwatembelea ili kuwafariji.

NYALANDU KUFANYA TAMASHA KUBWA ILONGELO JUMAPILI

WAZIRI*Zaidi ya watu 20,000 kuhudhuri
Na Mwandishi Wetu 

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu, Desemba 28, 2014 (kesho J’pili) atafanya mkutano mkubwa kwa ajili ya kumshukuru Mwenyezi Mungu na wananchi wa Singida Vijijini na Watanzania wote kwa kutimiza miaka 15 ya ubunge.
Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Mbunge huyo, Elia Diga, imesema kuwa mkutano huo ambao utaambatana na burudani mbalimbali, utafanyika katika Kata ya Ilongero na utahudhuriwa na viongozi wa Chama na serikali, viongozi wa dini zote na wananchi zaidi ya 20,000 kutoka kata zote zinazounda jimbo hilo na zile za jirani.
Katika mkutano huo, Nyalandu atahutubia wananchi pamoja na kueleza mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kipindi chote cha miaka 15.
Pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana mpaka sasa, Nyalandu pia ataeleza wananchi mwelekeo mpya wa jimbo hilo na mahali anapopenda lifike.
Viongozi wote wa CCM Wilaya ya Singida wakiongozwa na mwenyekiti wake, watahudhuria mkutano huo na kutoa hotuba fupi kwa wananchi.
Wasanii nyota wanaotamba nchini wakiongozwa na kundi la Makomandoo, Rose Muhando, Christina Shusho, H-Baba, Mchekeshaji Steve Nyerere na Bendi ya New Life Bandi watakuwepo kukonga nyoyo.
Pia kutakuwepo na vikundi  mbalimbali vya ngoma za asili vikiwemo Njagmba, Ilongero Group na vingine vingi vitakuwepo kutoa burudani.

ESCROW: Ikulu yazidi kumweka kiporo Muhongo

Na:  Goodluck Eliona na Mwinyi Sadallah, Mwananchi

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
  • Profesa Muhongo akataa kuzungumzia hatima yake
Vyama vya upinzani Zanzibar vimeshangaa kitendo cha Rais Kikwete cha kutomwajibisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati huko nyuma kuna mawaziri akiwamo Waziri Mkuu waliwajibika kwa makosa yaliyofanywa na watendaji wao.
Katibu Mkuu wa Chama cha Tadea, Juma Ali Khatibu alisema kwamba kuna viongozi wengi ambao walilazimika kujiuzulu kwa makosa ambayo hawakuhusika lili kulinda misingi ya uwajibikaji wa pamoja na kushangaa serikali kuendelea kumlinda Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati kashfa hiyo imetia hasara taifa baada ya wahisani kusitisha misaada yao.
Alisema kwamba kama Rais Kikwete ameamua kumuachia Waziri Mkuu kuendelea na wadhifa wake wakati umefika kwa Serikali kuwaomba radhi viongozi wote ambao walijiuzulu nyadhifa zao kwa makosa ya wengine.
Upande wake Makamu Mwenyekiti wa Chadema Zanzibar, Said Issa Mohamed alisema kwamba licha ya kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, hakuhusika kuchota fedha hizo. lakini alitakiwa kujiuzulu ili kulinda heshima yake na kupunguza hasira za wananchi.
“Kwa heshima ya misingi ya Utawala bora Kiongozi hata kama hukuhusika moja kwa moja, unalazimika kuwajibika kulinda dhana ya uwajibikaji wa pamoja.” alisema Mohamed.
Balozi Sefue asema Rais Kikwete ataamua hatima yake wakati wowote, 

Upande wake Mkurugenzi wa Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salim Bimani Abdalla alihoji ni kigezo gani kilichomfanya Mzee Ali Hassan Mwinyi akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Abdallah Said Natepe (marehemu), Shamsi Vuai Nahodha, Dk  Emanuel Nchimbi na Balozi Khamis Kagasheki wajiuzulu lakini  Pinda abaki katika  Ofisi za umma.
Mwinyi hakuwapo  wakati mauaji yaliotokea mkoani Shinyanga, Natepe hakujua kama kina Pius Lugangira, Hatibu Gandhi na Christopher Kadego  waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya uhaini kama wangetoroka katika Gereza la Ukonga.
Nahodha, Dk Nchimbi na Balozi Kagasheki pia hawakuhusika wala kufika katika eneo la utesaji wa watu wakati utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili.
Bimani alisema kwamba viongozi wote walioguswa na kashfa ya escrow wanatakiwa kufukuzwa, kushtakiwa na mali zao kutaifishwa na Serikali na kusisitiza kama serikali itashindwa kazi hiyo itafanywa na Ukawa mara baada ya kuingia madarakani mwakani.
Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Ambar Khamis Haji alisema kwamba maamuzi ya Rais Kikwete yameshindwa kumaliza kiu ya Watanzania  wengi waliokuwa wakisubiri kuona viongozi waliohusika na kashfa ya escrow wanafukuzwa na kufikishwa mahakamani na mali zao kutaifishwa.
Alisema kinachoonekana sasa Serikali imeamua kuwalinda wahalifu, kitendo ambacho hakitasadia kujenga misingi ya utawala bora pamoja na kufanikisha vita dhidi ya rushwa na ufisadi.
Haji alisema kwamba ni jambo la kushangaza Rais Kikwete amekuwa mzito kutekeleza uamuzi ya Bunge, wakati Serikali ni sehemu ya bunge na ilishiriki katika kupitisha maazimio hayo baada ya kamati za uchunguzi kuwasilishwa ripoti za uchunguzi.

MSHINDI WA BBA, IDRIS SULTAN AMTAMBULISHA MPENZI WAKE!


Idris Sultan akimtambulisha kwa mashabiki wa Dar Live mshikaji wake aliyekuwa naye kwenye mjengo wa BBA, Samantha wa Afrika Kusini.
Nyomi ya kutisha ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live

RUSHWA YATAWALA CCM- LOWASA AMWAGA MAMILIONI ZANZIBAR NA TANZANIA BARA KUSAKA URAIS

Naomba kuwauliza CCM kuipitia kamati ya maadili inayoongozwa na mzee wangu Philip Mangula, haya yanayofanywa na Edward Lowassa na Genge lake ya kumwaga mamilioni huko Unguja, Pemba na Tanzania bara kwa
wajumbe wa NEC na mkutano mkuu hamyajui au mmeyabariki?
Naomba kuiuliza EL ni nani mpaka akidharau chama namna hii? mamilioni haya yanayogaiwa hadharani kuanzia huko Unguja na Pemba kuelekea nchi nzima hamyaoni? Tena yakiwahusisha baadhi ya mawaziri wa SMZ na Jamuhuri ya Muungano?
Tangu juzi, kundi la wapambe wa Edward Lowassa na yeye mwenyewe wakiwa Zanzibar, wamekuwa wakigawa shilingi 1,000,000/= kwa kila mjumbe wa NEC CCM, na shilingi 500,000/= kwa kila mjumbe wa mkutano mkuu.
UNGUJA
Rushwa ya huku ilikuwa ikiratibiwa na kusambazwa na wana CCM wafuatao:-

-Jamali Juma (naibu katibu mkuu wa UVCCM Zanzibar zamani)
-Omar Yusuf Mzee (waziri wa serikali ya SMZ)
-Masauni Masauni (mbunge JMT)
-Machano Othman Machano (naibu waziri SMZ)
-Haji Omar Kheri

PEMBA:
Fuko la rushwa la Pemba lililoanza kugawiwa jana linaratibiwa na wafuatao:-

-Makongoro Mahanga (naibu waziri wa kazi JMT)
-Mwenyekiti wa CCM (w) Ilala
-Muhammed Abdulaziz (mkuu wa mkoa mstaafu)

Hivi sasa wagawaji wa rushwa wako wilaya ya MKOANI huko Pemba.
Tunakwenda wapi?
Kamati ya maadili CCM iko wapi?
Lowassa wajumbe wa NEC wako zaidi ya 200, wajumbe wa mkutano mkuu wako zaidi ya 3000, pesa hizi wewe na genge lako mtazirudishaje mkiingia Ikulu?
Watumishi wa Mungu mko wapi? Genge hili linatuvurugia nchi?
Philip Mangula uko wapi?
Tanzania nakupenda.

Korea Kazkazini yamtusi Obama

Rais Barrack Obama wa marekani amefananishwa na tumbili wa msitu wa Tropiki
Korea kaskazini imeilaumu Marekani kutokana na mataizo ya mtandao ambayo yameikumba siku chache zilizopita.
Tume ya taifa ya ulinzi nchini Korea Kaskazini inasema kuwa Marekani inavuruga mifumo ya mitandao ya nchi hiyo huku ikimfananishi rais wa marekani Barack obama na tumbili wa misitu ya tropiki mbali na kumshutumu kwa kuhusika katika kuonyeshwa ka filamu yenye utata inayojulikana kama The Interview.
Filamu ya the interview ambayo rasi Obama alishinikizwa ionyeshwe
Filamu hiyo iliyotengenezwa na kampuni ya Sony ambayo ni ya ucheshi inayoonyesha kuuawa kwa kiongozi wa korea kaskazini Kim Jong Un.
Korea kaskazini imekana kuhusika kwenye uhalifu wa mtandao dhidi ya kampuni ya Sony uliosababisha kampuni hiyo kusitisha maonyesho ya filamu hiyo.

Mwigulu Nchemba mgeni rasmi Tamasha la Upendo wa Mama Dar

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akizungumza.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akizungumza.

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba anatarajiwa kuongoza Tamasha Maalumu la ‘Upendo wa Mama’ linalotarajiwa kufanyika katika Kanisa la Rutheran Mabibo Extenal jijini Dar es Salaam na kushirikisha waimbaji wengi kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Akizungumzia tamasha hilo leo jijini Dar es Salaam, Rais wa taasisi ya Upendo kwa Mama Foundation yenye makao makuu yake mkoani Arusha, Injinia Carlos Mkundi alisema Naibu Waziri Nchemba ndiye mgeni rasmi wa Tamasha hilo maalumu ambalo pamoja na mambo mengine linafanyika kutambua mchango mkubwa wa mama kuanzia katika ngazi ya familia na jamii nzima.
Injinia Mkundi alisema tamasha hilo litakalofanyika Januari Mosi, 2015 chini ya uratibu wa Taasisi ya Upendo kwa Mama Faundation, litashirikisha waimbaji wa injili akiwemo Faraja Ntaboba kutoka Congo, Stella Joel, Ado Novemba, Jane Misso, Edson Mwasabwite wote kutoka jijini Dar es Salaam. Na Rose Molel, Helen Kigazi wote kutoka mkoani Arusha.
Injinia Carlos Mkundi na mwimbaji wa muziki wa injili ambaye naye atatumbuiza katika tamasha hilo, aliwataja waimbaji wengine ambao watashiriki katika tamasha ni pamoja na Mbunge, Matha Mlatta, Kwaya ya Mamajusi kutoka Moshi, mwimbaji Tumaini Njole, Messi Chengula na waimbaji wengine wengi.
“…Washiriki kila mmoja anaweza kuja na mamayake anayempenda pamoja na zawadi yake maalum, ambayo atamkabidhi wakati itakapotangazwa…kutakuwa na waimbaji wa muziki wa injili kutoka nje na ndani ya nchi ili kuleta mvuto zaidi tunawaomba wananchi wajitokeze zaidi kuja kutambua mchango wa mama na kuonesha upendo kwa mama zao,” alisema Injinia Mkundi.
Akifafanua zaidi alisema Tamasha la Upendo kwa Mama litakuwa la bure na litaanza majira ya saa saba mchana siku hiyo na kuendelea hadi jioni litakapofungwa. Alisema siku hiyo washiriki wanaombwa kuja na zawadi maalumu ambayo kila mmoja atamkabidhi mamayake anayempenda katika familia zao.
Rais wa Taasisi ya Upendo kwa Mama Faundation, Injinia Caros aliongeza kuwa lengo lingine ni pamoja na kuwatia moyo akinamama na kuwaonesha upendo juu ya kazi kubwa wanayoifanya katika familia zao na jamii kwa ujumla.
Alisema baada ya uzinduzi wa tamasha hilo kanisani hapo yataandaliwa matamasha mengine makubwa na kufanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaa pamoja na mengine katika mikoa mbalimbali. Aidha aliongeza tamasha kama hilo pia lilifanyika mkoani Arusha Novemba 16, 2014 katika uwanja wa Sheikh Amri Abeib na kuwashirikisha akinamama zaidi ya 40,000.

Ushindani wazidi katika ligi ya EPL

Olivier Giroud alipewa kadi nyekundi katika ushindi wa arsenal dhidi ya QPR
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amekiri kuwa Olivier Giroud alihitaji kupewa kadi nyekundu katika mechi dhidi ya QPR,lakini akathibitisha kuwa mshambuliaji huyo ameomba msamaha baada ya kisa hicho.
Giroud mwenye miaka 28 alionekana akimpiga kichwa Nedum Onuoha katika kipindi cha pili cha ushindi wa 2-1.
Wakati huohuo mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho anasema kuwa beki John Terry anacheza kama wakati alivyoiongoza the blues kushinda ligi ya Uingereza miaka kumi iliopita.
Ana motisha chungu nzima.
John Terry alifunga bao la kwanza la Chelsea
''Sioni tofauti ya John wa miaka ya 2004,05,06 sioni tofauti yoyote'',alisema Mourinho.
Terry alifunga katika ushindi wa 2-0 dhidi ya West Ham na kuifanya timu hiyo kusalia kileleni mwa ligi hiyo.
Kwengineko mkufunzi wa Manchester United Louis Van Gaal amesema kuwa ametosheka na uongozi unaotolewa na nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney ambaye alicheza katika safu ya kati na kuisadia timu hiyo kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Newcastle katika uwanja wa Old Trafford.
Rooney aliifungia Manchester United mabao mawili katika ushindi wa mabo 3-1 dhidi
ya Newcastle
Rooney alifunga mabao mawili na kutoa usaidia wa bao la tatu kwa Robin Van Persie.
Nayo Manchester City ilifunga mabao matatu katika kipindi cha kwanza dhidi ya West Bromwich licha ya barafu iliokuwa ikianguka katika uwanja huo na kusalia nyuma ya Chelsea kwa alama tatu.
Fernando aliifungia City bao la kwanza,baada ya Ben Foster kutoa kross nzuri kutoka kwa Jesus Navas.
Yaya Toure alicheka na wavu wa Westbromwich alipopiga mkwaju wa Penalti
Yaya Toure alifunga bao la pili kupitia mkwaju wa Penalty kabla ya David Silva kufunga bao la tatu.
West Bromwich walifunga bao la kufutia machozi wakati wa kipindi cha pili.
Hivi ndivyo ilivyokuwa:
Chelsea 2 - 0 West Ham
Burnley 0 - 1 Liverpool
Crystal Palace 1 - 3 Southampton
Everton 0 - 1 Stoke
Leicester 1 - 2 Tottenham
Man Utd 3 - 1 Newcastle
Sunderland 1 - 3 Hull
Swansea 1 - 0 Aston Villa
West Brom 1 - 3 Man City
Arsenal 2-1 QPR

Bi Gbagbo ashtakiwa Ivory Coast

Mke wa aliyekuwa rais wa Ivory Coast laurent Gbagbo,bi Simone Gbagbo amefunguliwa mashtaka ya ghasia za baada ya uchaguzi nchini Ivory Coast
Mke wa rais wa zamani wa Ivory Coast Laurent Gbagbo, Simone Gbagbo amefikishwa mahakamani kutokana na mashtaka ya kuhusika kwenye ghasia za baada ya uchaguzi ambapo zaidi ya watu 300 waliuwa.
Bi Gbagbo na watu wengine 82 akiwemo waziri mkuu wa zamani wameshtakiwa kwa kuhujumu usalama wa nchi, ukabila na kwa kubuni makundi ya uhalifu.
Rais wa zamani Laurent Gbagbo ambaye alikataa kukubali kushindwa kwenye uchaguzi mkuu miaka minne iliyopita anasubiri kesi yake kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC kutokana na mashtaka ya uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Zaidi ya watu 3000 waliuawa katika ghasia hizo baada ya rais huyo wa zamani kukataa kushindwa katika kura ya awamu ya pili.
Bi Gbagbo ambaye alikuwa anazuiliwa katika kifungo cha nyumbani kwa miaka mitatu ameshtakiwa kwa jaribio la kuhujumu usalama wa taifa hilo.
Aliyekuwa waziri mkuu Gilbert Ake N'Gbo na kiongozi wa chama cha FPI Affi N'Guessan pia wamefunguliwa mashtaka na bi Gbagbo.

Friday, December 26, 2014

MKE WA TYSON ASHINDA MIRATHI

Mke wa muandaaji mahiri wa filamu George Tyson, Beatrice Shayo.
Stori: Mayasa Mariwata na Hamida Hassan
 
MKE wa muandaaji mahiri wa filamu George Tyson, Beatrice Shayo amefanikiwa kushinda kesi na kuwa msimamizi wa mirathi baada ya mtafaruku mkubwa uliotokea wa kugombea mali na mwanadada aliyekuwa akiishi na msanii huyo kipindi cha mwisho cha uhai wake, Lucy Sepetu.
Akizungumzia ishu hiyo Beatrice alisema anashukuru Mungu amempigania maana ndugu wengi wa mume hawakuwa upande wake, wengi wao walimuunga mkono Lucy lakini Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni imempitisha kuwa msimamizi wa mirathi.
“Nililia sana na kumuomba Mungu kila kukicha kutokana na hili, nashukuru nimeshinda kesi na kuwa msimamizi wa mirathi yakiwemo mashamba, kiwanja, magari mawili na akaunti benki na hivi vyote navisimamia kwa ajili ya watoto wake watatu, ambao ni mwanangu, wa Monalisa na mwingine ambaye aliibuka baada ya kifo cha mume wangu,” alisema Beatrice.

MANCHESTER YAIUA NEWCASTLE

Rooney

Manchester United 3-1 Newcastle United and Burnley 0-1 Liverpool LIVE: Plus the rest of the Premier League Boxing Day action

  • Manchester United 3-1 Newcastle: Wayne Rooney scores twice and Robin van Persie adds a third at Old Trafford as Papiss Cisse responds with penalty
  • Burnley 0-1 Liverpool: Raheem Sterling gives Reds second half lead
  • West Brom 1-3 Manchester City: Visitors lead through Fernando, a Yaya Toure penalty and David Silva strikes
  • Leicester 1-2 Tottenham: Christian Eriksen free-kick retakes lead for Spurs after Leonardo Ulloa equalised Harry Kane opener
  • Everton 0-1 Stoke: Bojan nets first half penalty at Goodison Park
  • Crystal Palace 1-3 Southampton: Sadio Mane, Ryan Bertrand and Toby Alderweireld strike with Scott Dann heading reply
  • Sunderland 1-2 Hull: James Chester gives Tigers lead after Gaston Ramirez levelled Adam Johnson opener
  • Swansea 1-0 Aston Villa: Gylfi Sigurdsson scores free-kick

CHELSEA YAUA LIGI KUU UINGEREZA

Costa scored on the hour as he fired into the far corner beyond West Ham goalkeeper Adrian to double Chelsea's lead at Stamford Bridge

Costa akiifungia bao la pili Chelsea Uwanja wa Stamford Bridge

TIMU ya Chelsea leo imeshinda mechi ya tatu mfululizo ya Ligi Kuu ya England baada ya kuichapa West Ham United mabao 2-0 Uwanja wa Stamford Bridge, London.

Beki na Nahodha, John Terry aliifungia Chelsea bao la kwanza dakika ya 31 akimalizia kazi nzuri ya mshambuliaji Diego Costa.
Diego Costa mwenyewe akafunga bao la pili dakika ya 62 akimalizia pasi ya Eden Hazard, kabla ya kumpisha mkongwe Didier Drogba dakika ya 83.

PAMOJA NA MVUA KUBWA, TAMASHA LA KRISMAS LAACHA HISTORIA MJINI IRINGA

1Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akimtunza Mwimbaji wa muziki wa Injili kutoka nchini DRC Congo wakati akiima kwenye tamasha la Krismasi lililofamyika kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa na kushirikisha waimbaji mbalimbali wa muziki wa injili wakiwemo Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Bony Mwaiteje, Faraja Ntaboba kutoka DRC Congo, Solomon Mukubwa, Edson Mwasabwite Joshua Mlelwa, Ambwene Mwasongwe, Tumaini Njole, Emmanuel Mgogo na wengine wengi, hata hivyo mvua kubwa iliyonyesha mkoani Iringa imewafanya mashabiki wengi kutojitokeza katika tamasha hilo, Kundi zima la wanamuziki hao limekonga nyoyo za mashabiki mjini Iringa na linatarajiwa kuondoka kesho kuelekea Songea mkoani Ruvuma ambapo tamasha kama hilo litafanyika Desemba 29 kwenye uwanja wa majimaji. 2Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akicheza wakati mwimbaji Faraja Ntaboba akiimba kushoto ni mwimbaji Upendo Kilahiro akishiriki kucheza. 4Mwimbaji Edson Mwasabwite akiimba mbele ya mashabiki wake katika tamasha la Krismas kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa. 5Mwimbaji Edson Mwasabwite akiimba mbele ya mashabiki wake katika tamasha la Krismas kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa. 6Tumaini Njole na kundi lake wakitumbuiza kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa. 7Tumaini Njole akitumbuiza kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa.
.17
Upendo Nkone kulia na Tumaini Njole wakicheza jukwaani.
19Mwimbaji Bony Mwaiteje akifanya vitu vyake jukwaani.