TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 27, 2014

ESCROW: Ikulu yazidi kumweka kiporo Muhongo

Na:  Goodluck Eliona na Mwinyi Sadallah, Mwananchi

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
  • Profesa Muhongo akataa kuzungumzia hatima yake
Vyama vya upinzani Zanzibar vimeshangaa kitendo cha Rais Kikwete cha kutomwajibisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati huko nyuma kuna mawaziri akiwamo Waziri Mkuu waliwajibika kwa makosa yaliyofanywa na watendaji wao.
Katibu Mkuu wa Chama cha Tadea, Juma Ali Khatibu alisema kwamba kuna viongozi wengi ambao walilazimika kujiuzulu kwa makosa ambayo hawakuhusika lili kulinda misingi ya uwajibikaji wa pamoja na kushangaa serikali kuendelea kumlinda Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati kashfa hiyo imetia hasara taifa baada ya wahisani kusitisha misaada yao.
Alisema kwamba kama Rais Kikwete ameamua kumuachia Waziri Mkuu kuendelea na wadhifa wake wakati umefika kwa Serikali kuwaomba radhi viongozi wote ambao walijiuzulu nyadhifa zao kwa makosa ya wengine.
Upande wake Makamu Mwenyekiti wa Chadema Zanzibar, Said Issa Mohamed alisema kwamba licha ya kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, hakuhusika kuchota fedha hizo. lakini alitakiwa kujiuzulu ili kulinda heshima yake na kupunguza hasira za wananchi.
“Kwa heshima ya misingi ya Utawala bora Kiongozi hata kama hukuhusika moja kwa moja, unalazimika kuwajibika kulinda dhana ya uwajibikaji wa pamoja.” alisema Mohamed.
Balozi Sefue asema Rais Kikwete ataamua hatima yake wakati wowote, 

Upande wake Mkurugenzi wa Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salim Bimani Abdalla alihoji ni kigezo gani kilichomfanya Mzee Ali Hassan Mwinyi akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Abdallah Said Natepe (marehemu), Shamsi Vuai Nahodha, Dk  Emanuel Nchimbi na Balozi Khamis Kagasheki wajiuzulu lakini  Pinda abaki katika  Ofisi za umma.
Mwinyi hakuwapo  wakati mauaji yaliotokea mkoani Shinyanga, Natepe hakujua kama kina Pius Lugangira, Hatibu Gandhi na Christopher Kadego  waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya uhaini kama wangetoroka katika Gereza la Ukonga.
Nahodha, Dk Nchimbi na Balozi Kagasheki pia hawakuhusika wala kufika katika eneo la utesaji wa watu wakati utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili.
Bimani alisema kwamba viongozi wote walioguswa na kashfa ya escrow wanatakiwa kufukuzwa, kushtakiwa na mali zao kutaifishwa na Serikali na kusisitiza kama serikali itashindwa kazi hiyo itafanywa na Ukawa mara baada ya kuingia madarakani mwakani.
Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Ambar Khamis Haji alisema kwamba maamuzi ya Rais Kikwete yameshindwa kumaliza kiu ya Watanzania  wengi waliokuwa wakisubiri kuona viongozi waliohusika na kashfa ya escrow wanafukuzwa na kufikishwa mahakamani na mali zao kutaifishwa.
Alisema kinachoonekana sasa Serikali imeamua kuwalinda wahalifu, kitendo ambacho hakitasadia kujenga misingi ya utawala bora pamoja na kufanikisha vita dhidi ya rushwa na ufisadi.
Haji alisema kwamba ni jambo la kushangaza Rais Kikwete amekuwa mzito kutekeleza uamuzi ya Bunge, wakati Serikali ni sehemu ya bunge na ilishiriki katika kupitisha maazimio hayo baada ya kamati za uchunguzi kuwasilishwa ripoti za uchunguzi.

No comments:

Post a Comment