TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, March 13, 2012

Lipumba arejea kuinusuru CUF



*Apata mapokezi ya kihistoria akitokea Marekani
*Adai Tanzania hakuna utawala wa kidemokrasia
*Wanafunzi 808 Dodoma wakihama chama hicho


Na Peter Mwenda
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amewasili jana akitokea nchini Marekani na kupata mapokezi ya kihistoria.

Wachambuzi wa mambo ya siasa wanasema kuwa, kurejea kwa kiongozi huyo kutasaidia kukinusuru chama hicho ambacho hivi sasa kimekubwa na jinamizi la kuondokewa na wanachama wake.

Profesa Lipumba aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere saa 9:20 alasiri ambapo viongozi mbalimbali wa chama hicho walijitokeza kumpokea wakiwemo wabunge na wanachama wakiongozwa na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad.

Baada ya kushuka kwenye ndege, Prof. Lipumba alifanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wa CUF katika chumba maalumu cha mapumziko.

Baada ya kumaliza mazungumzo, Prof. Lipumba alitoka nje na kuvalishwa shada la maua huku vigelegele na nderemo zikitawala katika maeneo mbalimbali ya uwanja huo.

Eneo la uwaja lilijaa wafuasi wa CUF waliokuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za kumpongeza Prof. Lipumba kwa kuwa mwafrika pekee kuchaguliwa kwenye kamati ya kuchunguza chanzo cha mdororo wa uchumi duniani.

Kutokana na wingi wa watu walijitokeza kumpokea, Maofisa Usalama walimzuia Prof. Lipumba na Maalim Seif, kuhutubia wananchi katika uwanja huo.

Maofisa hao walishauri viongozi hao waondoke ndipo Prof. Lipumba aliamua kuzungumza na waadishi wa habari na kusema kuwa, kazi anyoifanya nchini Marekani angeweza kuifanya Tanzania kama mchumi aliyebobea lakini hapati ushirikiano.

“Nipo tayari kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania kuhusu masuala ya uchumi, hii itatokana na utawala na demokrasia ambao kwa sasa haupo nchini Tanzania,” alisema.

Aliwashukuru Watanzania na wafuasi wa CUF kwa kujitokeza kumpokea na kudhihilisha kuwa, wananchi wana imani na chama hicho.

Kwa upande wake, Shekhe Issa Ponda, akiongoza mashekhe wenzake 20 kutoka misikiti mbalimbali jijini Dar es Salaam, alisema mchango wa Prof. Lipumba ni heshima kubwa kwa Tanzania.

Ofisa Mawasiliano wa CUF, Bw. Salium Biman, alisema chama hicho kitachukua dola mwaka 2015 kutokana na umati mkubwa wa watu waliojitokeza uwanjani wenye imani na Prof. Lipumba.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu CUF Zanzibar, Bw. Ismail Jussa Ladhu, alisema umati uliojitokeza kumlaki Mwenyekiti huyo ni salamu tosha kwa mbunge wa Wawi, Bw. Hamad Rashid Mohammed kuwa chama hicho bado kina nguvu.

“CUF imeanza kazi rasmi ya kuimarisha chama ili 2015 tuchukue dola kwa kishindo,” alisema, Bw. Jussa.

Baada ya kuzungumza na waandishi wa habari, Prof. Lipumba aliondoka na msafari wa watu walifika kumpokea ukiongozwa na pikipiki, magari na watembea kwa miguu hadi Uwanja wa Karume.

Awali mapokezi hayo yaliingia dosari baada ya gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T 854 AMN, lililokuwa limejaza wafuasi wa chama hicho, kupinduka na kusababisha watu 10 kuumia.

Taarifa nyingine zinasema kuwa, gari lingine ambalo lilikuwa likitokea Rufiji mkoani Pwani kupeleka wafuasi wa chama hicho uwanjani hapo, lilimgonga mtembea kwa miguu na kufa papo hapo.

Wakati huo huo, Mwandishi wetu kutoka Dodoma anaripoti kuwa, zaidi ya wanafunzi 808 wa Vyuo Vikuu mkoani hapa ambao ni wananchama wa CUF, wametoa tamko la kujitoa na kurudisha kadi kwa uongozi wa chama hicho kwenye matawi ya vyuo vyao.

Wanafunzi hao walidai kuwa, wamelazimika kujiondoa katika chama hicho kutokana na kitendo cha viongozi wa ngazi ya juu kujali zaidi maslahi binafsi na kukidumaza chama.

Tamko la kujitoa katika chama limetolewa na Mwenyekiti wa Tawi la St. John  Bw. Muhamed Abdullha kwa niaba ya wanafunzi wezake katika kikao kifupi kilichofanyika kwenye Ukumbi wa mikutano chuoni hapo.

Bw. Abdullah alisema wanachama waliojitoa ni wasomi wa elimu ya juu katika vyuo vyote mkoani haapa ambao wamerudisha kadi za chama hicho na kila mmoja atachagua chama cha kwenda ambacho kina mtazamo wa kuleta maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

“Uongozi wa CUF kimsingi umetuchosha, hatujui unajali maslahi ya nani, inaonesha wazi kuwa viongozi wachache wa juu wanalinda maslahi binafsi na ndiyo maana chama hakikui.

“Kutokana na hali hiyo, wanafunzi ambao ni wanachana wa CUF tumelazimika kurudisha kadi, kila mmoja atachagua cham cha kwenda chenye mwelekeo wa kusaidia wananchi,” alisema.

Walisema Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Bw. Ismail Jussa Ladhu, amekuwa akitumia madaraka yake vibaya na kukiuka katiba ya chama hicho jambo ambalo limekuwa kilichangia kuwepo matakaba kati ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Katika tamko lao, wanafunzi hao walidai kuchoshwa na tabia za viongozi wa chama kuingiza udini kwa kuwabagua Wakristo na Waislamu na kujenga ukuta kati ya Wazanzibari na wenzao wa bara jambo ambalo ni kinyume na katiba yao.
Posted: 11 Mar 2012 11:49 PM PDT
Maelfu ya wanachama na wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF) wakiwa wamejaa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) kumpokea Mwenyekiti wao Profesa Ibrahim Lipumba aliyewasili jana alasiri akitokea Marekani, picha ndogo ni Profesa Lipumba na Katibu Mkuu  wake, Maalim Seif Sharif Hamad wakisalimia wananchi. (Picha na Peter Mwenda)
Posted: 11 Mar 2012 11:30 PM PDT
*Ataka mafisadi watoswe katika chaguzi za chama hicho
Na Mwandishi Wetu, Mwanza

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Samuel Sitta, amewapa mtihani mzito wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Mwanza na mikoa mingine nchini kuweka historia katika chaguzi mbalimbali ndani ya chama hicho kwa kukisaficha chama na kuwatosa wagombea wanaotaka uongozi kwa maslahi binafsi kwani wanachangia kukishushia hadhi chama hicho.

Alisema kama mafisadi na makundi yao yatapewa nafasi za uongozi ndani ya chama, watajuta kupoteza nafasi muhimu ambazo zinapaswa kufanyiwa mabadiliko ya kihistoria na watakuwa wameshiriki kuisaliti CCM na kuiweka pabaya chaguzi zijazo.

Bw. Sitta aliyasema hayo juzi katika mkutano wa hadhara ambao ulihudhuriwa na maelfu ya wana CCM pamoja na waananchi katika Uwanja wa Magomeni, uliopo Kata ya Kilumba, jijini Mwanza.

Alisema njia pekee ya kuinusuru CCM ni wanachama kuhakikisha wanachagua viongozi waadilifu kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa.

Aliongeza kuwa, wananchi wengi bado wana imani na chama hicho lakini wanalalamikia mwenendo wa baadhi ya viongozi hivyo uchaguzi wa mwaka huu lazima uwe wa kihistoria.

“Hii ndio fursa ya kukinga’risha chama chaetu, wana CCM tumieni uchaguzi huu kuchagua viongozi wanaopinga aina zote za ubaguzi ukiwemo wa kipato, tuchague viongzoi wenye huruma na wanaotetea wanyonge ambao ndio wengi.

“Tusipofanya hivyo na kuwaachia wenye uchu na matajiri, tutakuwa hatujaitendea haki imani yetu, itikadi yetu na misingi yetu, tuweke historia katika uchaguzi huu kwa kuwaenzi waasisi wetu wa Taifa.

“Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, alituachia msingi wa CCM kutetea wanyonge na huu umedhihirika, tumekuwa wakombozi hadi nje ya nchi, ukombozi huo ndio aliomnfanya Mzee wetu Karume kuwajengea maghorofa wanyonge hivyo lazima turudi katika misingi hiyo,” alisema Bw. Sitta.

Bw. Sitta ambaye alialikwa na Kamati ya Siasa Wilaya ya Ilemela na Kata ya Kirumba kuzindua kampeni za kumnadi mgombea udiwani wa kata hiyo, alisema CCM imekuwa ikilaumiwa na Watanzania kwa kupoteza uelekeo, kushindwa kuendeleza sera na itikadi iliyomo ndani ya katiba yake.

“Imani yetu rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa, huu ndio wakati wa kurudisha chama chetu katika njia yake na kusafisha vumbi la kila aina ili CCM ing'ae mbele ya jamii, tusipofanya hivyo, tutakua hatukitakii mema,” alisema.

Akimnadi mgombea udiwani wa kata hiyo, Bw. Jackson Robert, maarufu kama 'Masamaki', Bw. Sitta alisema mgombea huyo anastahili kuchaguliwa kutokana na uadilifu na msimamo wake thabiti katika kusimamia sera za CCM.

Alisema ushindi alioupata wa asilimia 70 ndani ya chama hicho ni dalili ya ushindi wake katika uchaguzi huo.

Bw. Robert atachuana wagombea wengine wa vyama mbalimbali huku mpinzani wake mkuu akitarajiwa kutoka chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Posted: 11 Mar 2012 11:28 PM PDT
Pamela Mollel na Queen Lema, Arusha

RAIS mstaafu wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa, leo anatarajia kuzindua kampeni za mgombea ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki, mkoani Arusha, kwa tiketi Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Sioi Sumari.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa CCM mkoani hapa, Bi. Mary Chatanda, alisema kampeni hizo zitahudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho.

Alisema uzinduzi huo utakuwa tofauti na vyama vingine vya siasa ambavyo vinakodisha watu kutoka nje ya jimbo hilo.

“Tutazindua kampeni kwa kishindo ili kuwapa wananchi fursa ya kuona jinsi tulivyojipanga kushinda, kampeni zetu zitafunguliwa na Rais mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa na viongozi wengine wa kitaifa watakuwepo ila tumeojipanga kupambana,” alisema Bi. Chatanda.

Katika hatua nyingine, Bi. Chatanda alisema wananchi wanapaswa kutokubali kudanganywa na aina yoyote ya propaganda kuhusu madai ya mgawanyiko wa wanachama ndani ya CCM.

Alisema wanachama wote wapo katika kundi moja jambo ambalo linawapa matumaini ya ushindi. Akizungumzia pingamizi lilowekwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), dhidi ya mgombea wao, Bi. Chatanda alisema pingamizi hilo limefutwa.

Bw. Sumari alikuwa amewekewa pingamizi na CHADEMA kwa madai kuwa hajawahi kukana uraia wa nje.
Posted: 11 Mar 2012 11:24 PM PDT
FEBRUARI 2009, Rais Jakaya Kikwete alimvua madaraka na kumfukuza kazi aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, mkoani Kagera, Bw. Albert Mnali, kutokana na kitendo cha kuwacharaza bakora walimu wa shule za msingi wilayani humo.

Hatua hiyo ilitokana na Bw. Mnali kufanya kitendo cha udhalilishaji kisichokubalika katika jamii na kuwavunja moyo walimu.

Bw. Mnali aliamrisha polisi kuwacharaza viboko walimu ambao aliamini wao ndio wamechangia wanafunzi wa shule za msingi wilayani humo kufeli mitihani.

Tukiachana na hilo, wachambuzi wa mambo ya uchumi wanasema ufadhili unaotolewa na wahisani kutoka mataifa mbalimbali duniani una faida na madhara yake.

Mwishoni mwa wiki, gazeti moja linalotoka kila siku liliandika habari inayosema “Mholanzi amchapa vibao Mwalimu Mkuu”. Tukio hili lilitokea katika Shule ya Msingi Marera, iliyopo Kata ya Rhotia, Wilaya ya Karatu, mkoani Arusha.

Mashuhuda wa tukio hilo wanadai kuwa, raia wa Uholanzi, Bi. Marise Koch, ambaye ndiye mfadhili wa shule hiyo kwa kukarabati majengo ya shule, ofisi, nyumba ya walimu na kutoa kompyuta ndogo 'Laptop', alimdhalilisha Mwalimu Mkuu Bw. Emmanuel Ginwe kwa kumpiga vibao mbele ya wanafunzi, walimu wenzake.

Tukio hilo limeripotiwa katika Kituo cha Polisi Karatu na kufunguliwa jalada namba KRT/RB/835/2012. Bi. Koch aliwakuta walimu wa shule hiyo wakipanga ratiba ya shule na kuhoji kwanini hawajaingia darasani.

Walimu hao walijibu tayari wanafunzi wamepewa kazi za kufanya lakini majibu hayo hayakumridhisha. Aliamua kwenda ofisini kwa Bw. Ginwe na kudai yeye anafadhili vitu vingi lakini walimu hawafundishi, kuanza kukusanya kopyuta alizotoa kama msaada shuleni hapo lakini Mwalimu Mkuu alimsihi asifanye hivyo.

Baada ya Bi. Koch kuona anazuiwa, alimpiga Bw. Ginwe vibao na kuendelea kuzikusanya kitendo ambacho kiliwashtua walimu na wanafunzi walioshuhudia tukio hilo.

Sisi tunasema kuwa, tukio hili halikubaliki kwani dhana ya ufadhili si kunyanyasa watu wanaopewa misaada na kuingiza mambo yao katika mitaala ya elimu nchini.

Kimsingi, kilichofanywa na Bi. Koch ni kosa kisheria hivyo tunaliomba Jeshi la Polisi wilayani Karatu, lichukue hatua stahiki za kuhakikisha mfadhili huyo anafikishwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Matatizo yaliyopo katika sekta ya elimu na nyinginezo si kigezo cha kuwafanya Watanzania wanyanyasike na kudhalilishwa ndani ya nchi yao. Tumechoka na manyanyaso ya aina hii, tunataka sheria imuadhibu Bi. Koch kama ilivyofanya kwa Bw. Mnari ambaye alifukuzwa kazi kwa kosa la kudharirisha walimu.

Kama Serikali itashindwa kuchukua hatua stahiki dhidi ya mfadhili huyu, upo uwezekano wa kukwamisha maendeleo ya elimu shuleni hapo kutokana na ukweli kwamba, walimu katika shule husika hawatakuwa na imani na serikali yao kwa sababu haijawali.
Posted: 11 Mar 2012 11:22 PM PDT
Na Pendo Mtibuche, Dodoma
SERIKALI mkoani Dodoma imesema suala la upandaji holela huduma za matibabu ya afya chini ya mifuko ya  afya ya jamii NHIF na CHF limekuwa likiathiri utendaji wa mifuko hiyo.

Hali hiyo imedaiwa kutokana na wauzaji wa dawa na watoa huduma kubadilisha
bei ya dawa wanavyotaka na kwa wakati wowote.

Hayo yalielezwa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt.Rehema Nchimbi wakati akifungua kongamano la siku moja la wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Dodoma.

Alisema, sekta hiyo ya afya imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi ambazo ambazo zimekuwa kuongeza malalamiko mengi kuhusu ukosefu wa dawa katika vituo vingi vya Serikali na hasa vilivyopo ndani ya Manispaa ya Dodoma na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa.

Alisema, kutokana na suala hilo kuwa nyeti basi ipo haja ya Serikali
kulitazama kwa makini suala hilo na kulitafutia ufumbuzi.

Mbali na changamoto hiyo ya kupanda kwa bei ya matibabu, lakini pia Mkuu huyo wa mkoa alibainisha kuwa  pia kumekuwepo na vituo vya afya ambavyo  vina uhaba wa watoa huduma wenye sifa hasa vijijini, hivyo suala hilo linasababisha utoaji huduma hafifu zisizokidhi kiwango kinachotakiwa kwa wanachama.

Alisema, hali ya afya katika Mkoa wa Dodoma inahitaji kufanyiwa tathimini ya uhakika ili kuona ni njia zipi zitakazoinua mifuko hiyo miwili ya afya ya jamii yaani NHIF na CHF ili iweze kufanya vizuri.
Posted: 11 Mar 2012 10:59 PM PDT
Na Mkwasi Issa, Pemba
ZAIDI ya miche 15,000 ya mikarafuu inatarajiwa kutolewa kwa wakulima kisiwani Pemba katika kipindi cha mvua za msimu wa masika ambazo zinatarajiwa kuanza kunyesha visiwani humo mwaka huu.

Ofisa wa Mashamba ya Serikali kisiwani Pemba, Bi.Asha Saleh Mbarouk aliyaeleza hayo wakati akizungumza na mwandishi wa gazeti hili kuhusiana na mikakati ya Serikali ya kuimarisha zao la karafuu katika msimu huu.

Alisema kuwa, ni vema wakulima kuanza kuyatayarisha mashamba yao mapema kabla ya mvua za masika hazijaanza ili kujiweka tayari kwa ajili ya kupanda mikarafuu mipya.

Bi. Mbarouk alisema, kila mkulima anayehitaji kupatiwa miche ya mikarafuu anatakiwa kujaza fomu ambazo zinapatikana kwa maofisa wa kilimo kwa kila shehia, fomu amabazo zitamuwezesha kupatiwa miche hiyo.

Aidha, alisema miche hiyo inapatikana vitalu vilivyoko Weni katika Wilaya  ya Wete, Kicha kwa wilaya ya Micheweni, Kigope Wilaya ya Mkoani pamoja na Kitalu Wilaya ya Chake.

Hata hivyo Ofisa huyo aliwataka wakulima kuwa tayari kwenda kuchukuwa na kujaza fomu ambapo kwa sasa watendaji wa kilimo wameanza kukagua na kupima mashamba operesheni ambayo kwa sasa inaendelea katika shehia ya Mtambwe Kaskazini.
Posted: 11 Mar 2012 10:57 PM PDT
Na Theresia Victor, Dodoma
MHANDISI Deogratius Assey ambaye amejitokeza katika kinyang’anyiro cha kugombea nafasi ya ubunge, Bunge la Afrika Mashariki (EAC) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amesema tayari amerejesha fomu katika ofisi ya chama hicho mkoani Dodoma kwa ajili ya kugombea nafasi hiyo.

Akizumgumza na Majira baada ya kurudisha fomu hiyo jana, Bw. Assey alisema, alilazimika kuingia katika ushindani huo kwa ajili ya kutaka kutetea maslahi ya vijana kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Bw. Assey alisema, pamoja na kuwepo kwa sera za kuwepo kwa jumuiya hiyo lakini bado haijapata mtu madhubuti ambaye yupo tayari kwa ajili ya kuwatetea na kuwapiagania vijana kuingia katika ushindani wa ajira kupitia EAC.

Alisema, alilazimika kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo kwani alikuwa hajiamini kuwa kama angeweza kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wananchi kwa kumuunga mkono kama ambavyo kwa sasa mambo yamekuwa mazuri kwa kupata ushirikianao wa kutosha.

“Lakini cha kushangaza nimeungwa mkono na wanacha wote wa Chadema na hata wale wasiyo kuwa wanachama, hata hivyo wamenichangia hata gharama za kulipia fomu ambayo ilikuwa inagharimu shilingi laki moja...lakini wamenichangia,”alisema Bw.Assey.

Aliongeza kuwa, ikiwa atafanikiwa kuipata nafasi hiyo atahakikisha kuwa vijana wanatetewa zaidi katika masuala ya ajira tofauti na ilivyo sasa ambapo Watanzania bado hawajaweza kunufaika na suala zima la ajira kwa vijana katika jumuiya.

Aidha, kwa upande wake Katibu wa Mkoa wa Dodoma CHADEMA, Bw. Stivine Masawe alisema, ameipokea fomu ya mgombea huyo na kusema kuwa haina makosa yoyote na hivyo iko sawa na ataiwasilisha Makao Makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo jijini Dar es Salaam.

Bw. Masawe alisema, kujitokeza kwa Mhandisi Assey ambaye ni kijana na mwanachama hai katika chama hicho ni fursa pekee kwa vijana kutatuliwa matatizo yao kama atapata nafasi ya kuchukua nafasi hiyo ya ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki.
Posted: 11 Mar 2012 10:50 PM PDT
Kiungo wa timu ya Simba, Patrick Mafisango (kulia) akijaribu kuwatoka mabeki wa Toto African ya Mwanza wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.(Picha na Michael Machellah)
Posted: 11 Mar 2012 10:49 PM PDT
*Wadaiwa kumpiga mtoto, mechi yao yaingiza mil. 73/-
Na Zahoro Mlanzi
WACHEZAJI wa Yanga Nurdin Bakari, Athuman Idd 'Chuji' na Jerryson Tegete, wanadaiwa kumpiga mtoto anayeishi Mtaa wa Faru na Swahili, Kariakoo, Dar es Salaam na kumsababishia maumivu.
Tukio hilo lilitokea juzi usiku baada ya mtoto huyo kuwazomea kutokana na kipigo cha bao 3-1 dhidi ya Azam FC ambapo gari la Yanga lililokuwa limebeba wachezaji,  lilisimama na wachezaji hao kwenda kumpiga mtoto huyo ngumi na mateka.

Kwa mujibu wa shuhuda aliyekuwepo eneo la tukio (jina tunalo),  alisema “ Baada ya mtoto huyu kuwazomea, Chuji, Nurdin na Tegete walishuka kwenye gari la kumuadhibu, walipomaliza kiu yao walirudi katika basi lao na kuondoka,” alidai mtoa habari huyo.
Alidai kuwa, walipokwenda kumuangalia mtoto huyo walimkuta katika hali mbaya huku mwili wake ukiwa na majeraha.

Vyanzo mbalimbali vya kuaminika vilidai kuwa, mtoto huyo alikimbizwa hospitali kutokana na hali yake kuwa mbaya.

Alipotafutwa kwa njia ya simu ili aweze kuzungumzia tukio hilo, Kaimu Kamanda Mkoa wa Kipolisi Ilala, Saada Juma, alisema hana  taarifa zozote kwani hadi anaondoka ofisini juzi saa 1:30 usiku, hakuna mtu aliyetoa taarifa ya tukio hilo.

“Leo (jana) Ma-OCD wangu walikuwa wakinipa taarifa za mara kwa mara kuhusiana na tukio la kuwasili kwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Bw. Ibrahim Lipumba lakini taarifa za kupigwa mtoto hadi akafariki dunia au kukamatwa kwa wachezaji wa Yanga hilo sijalipata,” alisema Kamanda Juma.

“Kama lipo nadhani nitapata taarifa ila kinachonishangaza, tutaanzaje kupaata taarifa za kifo kabla ya kuumizwa mtoto husika kwani hizo ndio zingesaidia kupata majibu ya uhakika kwa hicho unachonieleza lakini siwezi kusema uongo ila ukweli ni kwamba sina taarifa na hilo,” alisema.

Majira halikuishia hapo pia lilimtafuta Mwenyekiti wa klabu hiyo, Llody Nchunga ambaye alisema hana taarifa za wachezaji wake kufanya fujo, kukamatwa au kufa kwa mtoto huyo.

“Sijui kama hilo tukio lina ukweli, ninachokiamini mimi ni kwamba, wachezaji wote walirudi klabuni na leo (jana) asubuhi, nilikwenda kuzungumza nao tukaamua kuwapa siku moja ya mapumziko hivyo wamekwenda majumbani kwao,” alisema Nchunga.

Alisema kama tukio hilo lilifanyika, labda ni baada ya kurudi klabuni na baadhi yao kutoka tena kwenda mitaani kufanya fujo lakini walipotoka uwanjani, warurudi klabuni.

Katika hatua nyingine, Kocha Mkuu timu hiyo, Kostadin Papic atawachukulia hatua wachezaji wote waliomfanyia fujo mwamuzi  Israel Mujuni kutoka Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya mechi iliyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Papic alisema kitendo kilichofanywa na wachezaji wake hakikuwa kizuri na utovu wa nidhamu hivyo atahakikisha anawachukulia hatua.
Wakati huo huo, mchezo kati ya Yanga na Azam umeingiza sh. milioni 72,731,000.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari Dar es Salaam na Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema watazamaji 19,339 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 3,000 viti vya bluu na kijani, sh. 5,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C na B wakati kwa VIP A ilikuwa sh. 15,000.

Sunday, March 11, 2012

RC awashukia watendaji wenye majungu ofisini

Posted: 08 Mar 2012 10:51 PM PST
Na Charles Mwakipesile, Mbarali
MKUU wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro, amewataka watumishi wenye tabia ya kuwasema wenzao ofisini 'majungu', kuacha mara moja ambapo watakaobainika kuwa na tabia hiyo, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Bw. Kandoro aliyasema hayo juzi katika hafla ya kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri Wilaya ya Mbaarali, mkoani hapa Bw. George Kagomba.

Hafla hiyo ilifanuyika katika Makao Makuu ya halmashauri hiyo baada ya kustaafu utumishi wa umma na kuongeza kuwa, siri ya mafanikio kwa mtendaji yeyote wa Serikali ni kuchapa kazi kwa bidii, kuepuka majungu.

Alisema kitendo cha kuwagawa wafanyakazi kinakwamisha maendeleo ya wannchi na utekelezaji wa shughuli za Serikali.

“Kiongozi ambaye leo tunamuaga, amefanya kazi kwa bidii na kufanikiwa kuleta mabadiliko makubwa, kufyeka kichaka porini na kujenga Makao Makuu ya Halmashauri.

“Bw. Kagomba ni kielelezo cha watendaji bora wa serikali wasio na majungu  ambaye amewaunganisha wafanyakazi kuwa kitu kimoja na kuharakisha maendeleo,” alisema.


Alisema watendaji wa Serikali ambao wanaendeleza majungu badala ya kufanya kazi, huambulia kufukuzwa na kutokumbukwa kwa lolote walilofanya wakati wa utumishi wao serikalini.

“Sipendi kusikia Mkoa wetu unakosa maendeleo kwa sababu watumishi hutumia muda mwingi kuzungumza habari za majungu badala ya kufanya kazi kwa bidii,” alisema.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Bw. Keneth Ndingo, alisema Bw. Kagomba atakumbukwa kwa mambo mengi pamoja na kujenga Makuu Makuu ya halmashauri hiyo ambayo ina majengo ya kisasa yaliyozinduliwa na Rais Jakaya Kikwete.

Mbali ya kufanikisha ujenzi wa majengo hayo pia ameweza kukuza pato la halmashauri na ujenzi wa majengo ya sekondari za kata hivyo aliiomba Serikali iangalie uwezekano wa kumuongezea muda wa utumishi kwa mkataba maalumu.

Kwa upande wake, Bw. Kagomba alisema bila kupata ushirikiano kutoka kwa watumishi wengine, asingeweza kufanikisha majukumu aliyopewa ambayo yamezaa matunda.
Posted: 08 Mar 2012 10:45 PM PST
Na Zahoro Mlanzi
SERIKALI imesema mpaka kufikia mwishoni mwa Aprili mwaka huu Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam utakuwa tayari umekamilika kwa asilimia 75 na utaanza kutumika kwa shughuli mbalimbali rasmi Juni, mwaka huu.

Uwanja huo awali ulitakiwa kukamilika kabla ya sherehe za miaka 50 ya Uhuru lakini mpaka kufikia Desemba 9, mwaka jana ulikuwa haujakamilika, hivyo sherehe hizo kulazimika kufanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Serikali ulisimamisha shughuli za uwanja huo, tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2010/2011.

Akijibu swali kuhusu uwanja huo utakamilika lini, baada ya kushindwa kukamilika kabla ya kuanza kwa sherehe za Uhuru wa miaka 50 Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini, Leonard Thadeo alisema ni kweli ulitakiwa kukamilika kabla ya sherehe za Uhuru, lakini kikubwa kilichokwamisha ni mkandarasi alichelewesha baadhi ya mambo muhimu.

“Hivi sasa ujenzi unaendelea kama kawaida na ninakuhakikishia mpaka kufikia mwishoni mwa Aprili, mwaka huu utakuwa umekamilika kwa asilimia 75, kwani kazi kubwa iliyobaki ni kuweka viti katika jukwaa mbalimbali zilizojengwa,” alisema Thadeo.

Alisema wakati maboresho hayo yakiendelea kwa kuhakikisha viti vinawekwa na mambo mengine, mpaka kufikia Juni mwaka huu ana imani kila kitu kitakuwa kimekamilika na shughuli mbalimbali zilizokuwa zikifanyika katika uwanja zitaendelea kama kawaida.

Thadeo alisema kukamilika kwa uwanja huo kutapunguza matumizi ya Uwanja wa Taifa, kwani mechi zitakazokuwa si za lazima kuchezewa kwenye uwanja huo, zitafanyika Uwanja wa Uhuru kama ilivyokuwa hapo awali.

Pia alitoa wito kwa mashabiki na wanamichezo kwa ujumla kuhakikisha kuutumia vizuri uwanja huo, pindi utakapokamilika ili kuepusha madhara yatakayoweza kujitokeza kama ilivyokuwa katika mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba na Kiyovu ya Rwanda.

Katika mechi hiyo ya Simba, viti 152 viliharibiwa na 11 vilivunjwa kutokana na mashabiki hao kuvunja na kurushiana wakati mechi hiyo ikiwa mapumziko.

MNYAMA SIMBA ASHINDWA KUUNGURUMA MWANZA,

Mchezaji wa timu ya Simba Felix Sunzu akimtoka beki wa timu ya Toto Africa ya Mwanza katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jioni hii, Mpira umekwisha na hakuna timu iliyofanikiwa kupata goli katika dakika tisini matokeo yamekuwa 1-1. Kocha Milovan ameipongeza timu ya Toto Africa kwa kucheza vizuri, wao walitaka kushinda lakini hawakuweza kufanya vizuri.
Wachezaji wa Simba ta Toto Africa ya Mwanza wakisalimiana kabla ya kuanza kwa mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa.
Kikosi cha timu ya Toto Africa ya Mwanza kikiwa katika picha ya pamoja.
Timu zikiingia uwanjani tayari kwa kukipiga katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom.

Na Mwandishi Wetu MALKIA wa muziki wa Injili nchini, Rose Muhando, naye atakuwa miongoni mwa waimbaji watakaopamba tamasha la nyimbo za Injili litakalofanyika Aprili 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Alex Msama, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati inayoratibu tamasha hilo chini ya Kampuni ya Msama Promotions ya Dar es Salaam, Muhando amethibitisha kushiriki tamasha hilo. "Katika tamasha la Pasaka mwaka huu ndipo Rose Muhando atapata fursa ya kutambulisha albamu yake ya nne ya Utamu wa Yesu ambayo haijawahi kuzinduliwa tangu aikamilishe," alisema Msama. Albamu ya Utamu wa Yesu inabeba nyimbo saba ambazo ni Utamu wa Yesu uliobeba jina la albamu hiyo, Raha Tupu, Tamalaki, Ndivyo Ulivyo, Woga Wako, Imbeni na Kusifu na Achia. Mbali na Utamu wa Yesu, Rose Muhando pia amewahi kutamba na albamu za Uwe Macho, Nyota ya Ajabu (Zawadi ya Krismasi) na Jipange Sawa Sawa. Msama alisema pia Muhando ataimba pamoja na Anastazia Mukabwa wa Kenya aliyeshirikiana naye katika albamu ya Vua Kiatu, na baada ya kutikisa Uwanja wa Taifa, mashambulizi mengine yatahamia kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma Aprili 9 mwaka huu. "Mpaka sasa tunaendelea na mazungumzo na waimbaji wengine mahiri wa muziki wa Injili, lakini Muhando atakuwepo na Mukabwa atakuja na kundi la waimbaji wake," alisema Msama. Albamu ya Vua Kiatu inabeba nyimbo nane ambazo ni Vua Kiatu uliobeba jina la albamu hiyo, Ee Mungu, Usiwe Manamba, Nzizilela, Nishike Mkono Bwana, Wanaokudharau na Mfalme. Mbali na Mukabwa, wengine waliothibitisha kushiriki tamasha hilo litakalofanyika Sikukuu ya Pasaka ni Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Christina Shusho wa Dar es Salaam, kundi la Glorious Celebration na Atosha Kissava kutoka Iringa. Kwa mujibu wa Msama, tamasha hilo baada ya kufanyika Dar es Salaam, pia litarindima kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 9 mwaka huu. Tamasha la mwaka huu malengo yake makubwa ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji wanawake wajane. Kiingilio katika tamasha hilo kimetengwa katika kategoria tatu na kitakuwa sh. 2,000 kwa watoto, sh. 5,000 kwa viti vya kawaida na viti maalumu sh. 10,000. Tamasha la Pasaka la mwaka huu pia litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi sita za Afrika ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Afrika Kusini na Zambia. Pia kutakuwa na kwaya.

The Girl Empowerment Program” under the theme ” Build Your Future”, aimed at empowering Secondary school girls Saturday 10th March 2012, As part of our Corporate Social Responsibility initiative, Airtel Tanzania has today launch ”The Girl Empowerment Program” under the theme ” Build Your Future”, aimed at empowering Secondary school girls aged 14 to 18 years, in achieving their future career goals and build self confidence amongst young women. The Girl Empowerment Program is key to Airtel as it goes hand in hand with Airtel’s mission of educating the girl child and creating brand loyalty. Apart from the fact that they need clear rules, consistent consequences for breaking rules and encouragement to do their best, young girls need opportunities outside of school curriculum to learn and develop new skills and interests with other youth and adults. Speaking during the launch held at Canossa Girls Secondary School in Tegeta, Dar es Salam Airtel customer Care Director Adrianna Lyamba said ”Today we kick start the program this quarter with “Canossa Girls Secondary School in Tegeta, The Girl Empowerment Program will be an ongoing program which will be done quarterly to Girls Secondary Schools around Tanzania and in this program we will be covering different topics relating to career management, building self confidence and making the right decisions in life. We will be requesting our own employees to volunteer to speak in schools and share their career experiences and skills with the students. This will enable the students understand what it takes to build a career and select the right career path in life”. “There is the say that saying, when you educate a women you have educated the whole community, we therefore believe the knowledge acquired will be a great significance to girl’s destiny and for the upcoming generation. She added We are highly committed towards supporting Tanzanian community, apart from Girl empowerment program we have been supporting education sector through Shule yetu program were we provide books to Secondary schools in the country, our aim is to improve education level through availability books to secondary schools students. Since we started our books support programme, approximately seven years ago, we have reached more than 800 secondary schools that are spread across the country”

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Azam lililochezwa Machi 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 72,731,000.
Jumla ya watazamaji 19,339 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 3,000 viti vya bluu na kijani, sh. 5,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C na B wakati kwa VIP A ilikuwa sh. 15,000.
Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 11,303,932.20 kila timu ilipata sh. 14,726,592.20, uwanja sh. 4,908,864.07.
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,963,545.63, TFF sh. 4,908,864.07, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,454,432.03, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 490,886.41 na asilimia 10 ya gharama za mechi ni sh. 4,908,864.07.
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000. waamuzi wa akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa kamishna sh. 40,000, tiketi sh. 3,540,000, maandalizi ya uwanja (pitch) sh. 400,000, umeme sh. 300,000, usafi na ulinzi kwa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000.
Gharama nyingine ni Jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila tiketi; kila klabu ilipata tena sh. 1,353,730 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kilipata tena sh. 1,160,340.

Saturday, March 10, 2012

Mwamuzi Israel Mujuni pamoja na wasaidizi wake akitoka nje kwa kusindikizwa na askali wa kikosi cha kutuliza Ghasia FFU mara baada ya kupuliza kipenga cha mwisho kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom uliokutanisha timu ya Yanga ya Jangwani na timu ya Azam FC kutoka Chamazi ambapo Yanga imekandamizwa magoli 3-1 na wauza Sembe hao wa Chamazi kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mwanzo ulikuwa ni mchezo mzuri uliokuwa wa vuta nikuvute kwa kila upande lakini mambo yalibadilika mara baada ya Azam kuandika goli la kwanza, mchezaji Haruna Niyonzima wa Yanga alionekana kumlalamikia refa mara kwa mara jambo ambalo refa alimuonya mara kadhaa lakini, hata hivyo Niyonzima aliendelea baada ya muda, alitolewa nje kwa kadi nyekundu, jambo ambalo lilizua tafrani uwanjani huku makonde yakirushwa hovyo, baadae naye mchezaji Nadir Haroub Canavaro alipewa kadi nyekundu kutokana na vurugu hizo na kuzua tifu lingine uwanjani. Hali ilikuwa kama hivi angalia matukioo ya picha hizi.
Canavaro akitolewa nje huku huku akilia na kocha wake Papic akimtuliza.
Papic akiwatuliza wachezaji na baadhi ya maafisa wa benchi la ufundi
Canavaro akizuiwa na wenzake asimshushie kipondo refa huyo.
Polisi akiwa ameingia uwanjani ili kutuliza fujo hizo na kutoa ulinzi kwa refa huyo.
Mchezaji John Boko wa Azam FC akimtoka beki wa Yanga Haroub Nadir Canavaro.
Mashabiki wa Azam FC wakishangilia kwa furaha.
John Boko akishangilia mara baada ya kuipatia timu yake goli la kwanza.
Timu zikiingia uwanjani tayari kwa kuanza mchezo huo 

Mratibu wa Kitaifa Mradi wa athari za Mabadiliko ya tabia Nchi Bw Faraja Ngeregeza akitoa Mada kwa Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais juu ya athari za mabadiliko ya tabianchi leo Ukumbi katika wa Karimjee jijini Dar es Salaam[Picha na Ali meja]
Baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rasi wakimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Bw Richard Muyungi[Pichani hayupo]akitoa Mafunzo ya Utaratibu wa Utekelezaji wa Miradi ya Kupunguza Gesi joto huko kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.[Picha na Ali Meja]
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Sazi Salula akizungumza na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sera na Mipango Tathimini na Ufuatiliaji Bi Grace Ngallu wakati wa Mafunzo ya Utaratibu wa Utekelezaji wa Mradi wa Kupunguza Gesi Joto Mafunzo hayo yalioandaliwa Kwenye Ukumbi wa Karimjee Mjini Dar es Salaam Katikati Naibu Katibu Mkuu Ofisiya Makamu wa Rais Eng Ngosi Mwihava[Picha na Ali meja]
Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais Idara ya Mazingira Bw Richard Muyungi akitowa Mafunzo ya Utaratibu wa Utekelezaji wa Miradi ya Kupunguza Gesi ya Joto kwa Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais yaliofanyika Leo Kwenye Ukumbi wa Karimjee Mjini Dar es Salaam.[picha na Ali Meja]

Baadhi ya washiriki wa semina maalum ya mafunzo kwa waandishi wa habari kutoka nchi 20 duniani iliyofanyika hivi karibuni nchini Misri wakiwa katika picha ya pamoja nje ya ofisi za gazeti la Serikali la Al Haram Jijini Cairo. Wa pili kushoto ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (Maelezo) Ismail Ngayonga na anayemfutia ni Afisa Habari wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Concilia Niyibitanga.
Afisa Habari wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Concilia Niyibitanga akiwa katika picha ya pamoja na watoto katika eneo la Tahrir Square Jijini Cairo nchini Misri hivi karibuni wakati wa kumbukumbu ya maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kutokea kwa vurugu katika sehemu hiyo ambazo zilimwondoa madarakani Rais wa zamani wa nchi hiyo, Hosni Mubarak.
Afisa Habari wa Idara ya Habari (Maelezo) Ismail Ngayonga akitazama sehemu ya mitambo inayochapisha gazeti la Al Haram linalomilikiwa na Serikali ya Misri wakati wa ziara ya mafunzo kwa waandishi kutoka nchi 20 duniani iliyofanyika hivi karibuni nchini humo.
Afisa Habari wa Idara ya Habari (Maelezo) Ismail Ngayonga akiwa katika eneo la Tahrir Square Jijini Cairo nchini Misri hivi karibuni. Sehemu hiyo ni chimbuko la vuguvugu la wananchi katika kupinga na hatimaye kuung’oa madarakani utawala wa Rais wa zamani wa nchi hiyo, Hosni Mubarak.
Matumizi ya wanyama kazi kama farasi na punda Farasi na Punda ni makubwa sana katika nchi ya Misri. Pichani ni Farasi wakiwa wamebeba miti na kuwekwa pembeni mwa barabara katika mtaa wa Zamalek Jijini Cairo kama walivyokutwa na kamera yetu hivi karibuni nchini humo.
Waandishi wa habari na wapigapicha kutoka nchi 20 duniani wakiwa katika picha ya pamoja hivi karibuni mara baada ya kuwasili katika piramidi za Misri zilizopo katika mji wa Giza nje kidogo ya Jiji la Cairo nchini Misri, aliyechumaa mstari wa mbele wa pili kushoto ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (Maelezo) Ismail Ngayonga. Piramidi za Misri ni miongoni mwa vivutio vya utalii ambavyo vipo katika orodha ya maajabu saba ya dunia.
(PICHA KWA HISANI YA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO)

Operations Manager, MultiChoice Tanzania, Ronald Shelukindo awards Jane Mhina of Hotspot Media an HD PVR which she won in a lucky draw during DStv Customer Day.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua ujenzi wa Kituo cha kimataifa cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Kambarage Nyerere kwenye Mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es salaam March 10,2012. Kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Kulia kwake ni Balozi wa China nchini, LV Youqing. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mzengo Pinda akijadili jambo na Waziri wa mamboya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (kulia) , Balozi wa China Nchini, LV Youqing baada ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere , Mtaa wa Shaban Robert jijini Dar es salaam March 10,2012. Wengine pichani na wahadisi kutoka China wanaosimmia ujezi huo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amezitaka kampuni na taasisi zinazohusika na kutoa huduma muhimu katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ziharakishe kufanya hivyo ili ujenzi wake ukamilike mapema.
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumamosi, Machi 10, 2012) mara bada ya kupokea taarifa ya ujenzi wa kituo hicho na kukagua ujenzi wake katika mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam.
Kampuni zinazotakiwa kufanya hivyo ni TANESCO kwa ajili ya umeme wa jengo hilo, Kampuni ya Simu (TTCL) kwa ajili ya mkonga wa mawasiliano na Idara ya Kodi ya Mapato (TRA).
Waziri Mkuu amesema ujenzi wa kituo hicho cha mikutano ni ishara ya urafiki wa muda mrefu ulikuwepo baina ya Tanzania na China na kwamba kukamilika kwake kutaboresha mandhari ya Jiji la Dar es Salaam.
Mapema, akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa jengo ambalo litagharimu yen milioni 183.5 sawa na dola za Marekani milioni 30, Balozi wa China nchini Tanzania, Bw. Lv Youqing alisema ujenzi wa jengo hilo ulianza mara baada ya sherehe za uzinduzi Januari 15, 2010.
Awali, ujenzi wa jengo hilo ulitarajiwa kukamilika Aprili, 2012 lakini kutokana na uchelewashaji wa miundombinu hiyo muhimu hivi sasa linatarajiwa kukamilika Agosti, mwaka huu.
Litakapokamilika jengo hilo litakuwa na uwezo wa kuchukua watu zaidi ya 1,000; litakuwa na kumbi ndogo ndogo nne zenye uwezo wa watu zaidi ya 20, ukumbi wa chakula wa watu zaidi ya 700 na ofisi za watumishi wa ukumbi huo. Vilevile, kutakuwa na ukumbi mmoja ambao unaweza kugawanywa (partitioned) na kutengeneza ofisi za muda kwa watu wanaoendesha mkutano mkubwa katika ukumbi huo.
Naye Mkurugenzi wa mradi wa ujenzi wa kituo hicho, Bw. Huang Meiluan alisema ujenzi wa ghorofa ya chini umekamilika kwa asilimia 40 kwa sababu bado wanasubiri huduma muhimu zikamilike ili waanze kuweka sakafu. “Tunasubiri kuunganishwa na mkonga wa mawasiliano wa Taifa, bado hatujaweka njia kuu za umeme za kuingia katika jengo... kasi ya ujenzi imeathirika kutokana na kutokamilika kwa huduma hizi muhimu,” alisema.
Alisema ujenzi wa ghorofa ya kwanza na ya pili umekamilika kwa asilimia 90 na imebakia kazi ya kumalizia kuweka nakshi za ndani tu (interior decoration). “Kwa nje, kazi ya ujenzi imekamilika na tumeanza kuweka nakshi, kazi hii imekamilika kwa asilimia 75,” alisema.
Alisema wanakabiliwa na changamoto ya wizi wa vifaa vya ujenzi unaofanywa na vibaka kila mara na kwamba inawapa mtihani kwani itawalazimu kuagiza upya vifaa hivyo kutoka China. Aliomba polisi wawasaidie kuimarisha ulinzi katika eneo la ujenzi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe alimweleza Waziri Mkuu kwamba wizara yake imeanza kushughulikia upatikanaji wa kifaa muhimu cha umeme ambacho kilishindwa kupatikana hapa nchini.
Alisema vyuma vilivyotumika katika hatua za awali za ujenzi wa kituo hicho ni tani nyingi, na kwamba yanahitajika malori ya kuvisomba na kibali kutoka TRA ili yaweze kupelekwa katika eneo jingine kwa kuhifadhiwa. Alimhakikishia Waziri Mkuu kwamba wizara yake inafuatilia suala hilo pia.
Kuhusu uwekwaji wa nyaya za mkonga wa mawasiliano ambao unapaswa kufanya na TTCL, waziri Membe aliomba apewe wiki moja zaidi kwani amekuwa akisumbuana nao kwa zaidi ya mwezi mmoja bila mafanikio yoyote. Suala la ulinzi pia alisema ameshaanza kulishughulikia.

Mbunge wa Arusha Godbless Lema akiwa amebebwa juu juu mara baada ya kuwasili hapo Meru Wilayani Arumeru ambapo mkutano mkubwa wa uzinduzi wa kampeni wa chama cha Deomkrasia na maendeleo CHADEMA unafanyika kuanzia muda huu katika viwanja vya Shule ya Msingi Leganza, Mwandishi Wetu ambaye yuko katika eneo la tukio, anasema "Tayari helkopta zilizowachukua viongozi kadhaa wa chama hicho zimeanza kutua katika viwanja hivyo tayari kwa uzinduzi na mkutano huo utarushwa moja kwa moja na televisheni kadhaa za hapa nyumbani.
Umati wa watu ukiwa unaelekea eneo la mkutano katika viwanja vya shule ya Msingi Leganza.
Waendesha pikipiki hawako nyuma kama wanavyoonekana katika picha hii. (PICHA KWA HISANI YA MJENGWABLOG)

Meneja Mkuu wa Multchoice Tanzania Bw. Peter Fuel akifurahia jambo na Meneja wa Uendeshaji Ronald Shelukindo wakati wa hafla ya wateja iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya wateja wake, katika siku hii ya leo ving'amuzi vya DSTV vinauzwa kwa silingi 120.000 pamoja na kukuunganishia nyumbani kwako na ofaa hii ni ya leo tu.
Hafla hiyo inafanyika katika ofisi za Multichoice zilizopo Saint Peter Oysterbay jijini Dar es salaam. Mwanafunzi Diana Kimaro wa Chuo Kikuu cha Nilai Malasia akisomea masuala ya biashara ambaye yuko katika benki ya NMB kwa mazoezi akimpatia huduma mmoja wa wateja wa benki ya NMB aliyefika katika hafla hiyo, Benki ya NMB pia imeshiriki katika hafla hiyo kwa ajili ya kuwaelezea wateja wao huduma mbalimbali wanazozitoa.
Watoto wakicheza
Wanenguaji wa kiume wa bendi ya African Stars wakicheza katika hafla hiyo.
Mwimbaji wa bendi hiyo Lwiza Mbutu akiimba pamoja na wanamuziki wenzake katika hafla hiyo.
Meneja uendeshaji wa Multchoice Ronald Shelukindo akizungumza na wateja wa kampuni hiyo katika hafla hiyo.
Wateja mbalimbali waliohudhuria katika hafla hiyo wapata burudani mbalimbali.
Baadhi ya wateja pia wameongozana na watoto wao katika kuonyesha upendo.
Kulia ni Ronald Shelukindo Meneja Uendeshaji, Barbara Kambogi Meneja Uhusiano na katikati ni Orest Kawau kutoka African Media Group.
Mdau Julio Batalia akitangaza bidhaa yake ya PayPoint katika hafla hiyo.
Wadau kutoka benki ya NMB nao wakiwa katika hafla hiyo tayari kwa kuelimisha wateja juu ya huduma zao.

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara Jana (Machi 10 mwaka huu) amechangia sh. milioni moja kwenye uzinduzi wa akaunti ya Twiga Stars kupitia Tigo Pesa kuichangia timu hiyo ambayo inashiriki michuano ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC).
Akizungumza kwenye hafla hiyo iliyofanyika Dar es Salaam, Dk. Mukangara alisema ni jukumu la kila Mtanzania kuichangia Twiga badala ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuachiwa pekee mzigo huo wa kuendesha timu hiyo.
Wachangiaji wa Twiga Stars wanatakiwa kutuma mchango wao kwenda namba 13389 ambapo kiwango cha juu kinachoweza kutumwa kwa muhamala (transaction) mmoja ni sh. 500,000. Kwa Waziri Dk. Mukangara kuchangia sh. milioni moja alifanya mihamala miwili.
Naye Makamu wa Kwanza wa Rais wa TFF, Athuman Nyamlani alisema Twiga Stars kwa sasa haina mdhamini na Shirikisho limekuwa likibeba mzigo wa kuhakikisha inashiriki katika mechi za kirafiki na mashindano mbalimbali kwa vile imekuwa ikifanya vizuri.
Twiga Stars inayofundishwa na kocha Charles Boniface Mkwasa iko kwenye raundi ya pili ya mashindano ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) ambapo Mei 26 mwaka huu itacheza na Ethiopia jijini Addis Ababa.

Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa shirika la Millenium Challenge Account Tanzania Dar es Salaam(MCA-T Dsm) Bw. Bernard Mchomvu akimkabidhi zawadi ya Khanga yenye nembo ya shirika hilo kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya walipoonana ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu (kulia) jana kujadili miradi ya barabara inayodhaminiwa na shirika la Millenium Challenge Cooperation (MCC) kupitia Tanzania Millenium Challenge Account (MCA-T Dsm). (Pichana Hamza Temba-Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa) Shirika hilo linafadhili ujenzi wa barabara kuu za lami zinazojengwa Mkoani Rukwa zenye jumla ya Km. 224 kwa miradi ya Tunduma-Ikana, Ikana-Laela, na Laela-Sumbawanga. Kwa mujibu wa Bwana Mchomvu miradi hiyo yote pamoja na changamoto zote kuzingatiwa itakuwa imekamilika ifikapo mwezi June 2013 na barabara zote zitakuwa zimekabidhiwa kabla ya mwezi wa nane 2013. Kwa upande wa Ruvuma shirika hilo linafadhili ujenzi wa barabara itokayo mjini Songea kuelekea Wilaya ya Mbinga ambapo ujenzi huo unaendelea na unategemewa kukamilika mwakani. Hata hivo Mkurugenzi huyo aliushukuru uongozi wa Mkoa wa Rukwa kwa ushirikiano wanaoutoa kuwaeleimisha wananchi wao juu ya umuhimu wa miradi hiyo na ulinzi wa vifaa vya ujenzi kwani umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza wizi wa vifaa vya ujenzi vilivyokuwa vinafanywa na baadhi ya wananchi na wafanyakazi wasiokuwa waaminifu. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya allishukuru shirika hilo kwa jitihada zao za kuchangia maendeleo nchini. Aliwashukuru pia kwa hatua za hivi karibuni walizochukua kujenga daraja la Laela ambalo ni kiunganishi muhimu kwa wananchi wa eneo hilo katika shughuli zao za kila siku hususani kuwaunganisha na kituo cha afya cha Laela.
Picha ya pamoja kati Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu, Injinia Stella Manyanya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Tarimo na wawakilishi wa Jumuiya ya Millenium Challenge Cooperation (MCC) Bw. Carl Fickenscher Mkurugenzi Mkazi nchini (kushoto) na Bw. Bernard Mchomvu Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa shirika la Millenium Challenge Account Tanzania Dar es Salaam(MCA-T Dsm).
Kushoto Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa shirika la Millenium Challenge Account Tanzania Dar es Salaam(MCA-T Dsm) Bw. Bernard Mchomvu akijadiliana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya.