TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, February 20, 2015

SERIKALI KUAJIRI WALIMU 35,000 – WAZIRI MKUU

  NG7 WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali imepanga kuajiri walimu

zaidi ya 35,000 kwa ajili ya shule za sekondari ili kukabiliana na
tatizo la uhaba wa walimu nchini.
Ametoa kauli hiyo jana jioni (Alhamisi, Februari 19, 2015) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa kata ya Kiwere, mara baada ya kukagua ujenzi wa maabara na kuzindua nyumba nne za walimu kwenye shule ya sekondari ya Kiwere, tarafa ya Kalenga, wilayani Iringa.
Waziri Mkuu alisema walimu hao watagawanywa kwenye shule kulingana na mahitaji yaliyokwishawasilishwa na kwamba watakapopata mgao wao hawana budi kuziangalia kwanza shule zenye miundombinu iliyokamilika kama ilivyo kwa shule hiyo.

WAZIRI MKUU ATAKA WATANZANIA WAWE NA HOFU YA MUNGU

images 
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka Watanzania wasikilize na kufuata mafundisho yanayotolewa na viongozi wa dini ili Tanzania iwe nchi yenye watu waadilifu na wenye hofu ya Mungu.
Ametoa wito huo leo mchana (Ijumaa, Februari 20, 2015) wakati akizungumza na maelfu ya waumini na wananchi waliohudhuria ibada ya mazishi ya Askofu Mstaafu Magnus Mwalunyungu kwenye kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu la Tosamaganga, Jimbo Katoliki la Iringa.
“Leo ni siku ya pekee ya kuwasikiliza viongozi wa dini wakituasa tujiandae kwa maisha baada ya kifo. Tukio hili la leo litupe nguvu ya kukubali kwamba kifo kipo licha ya kuwa hakizoeleki na kinapotokea kinaleta simanzi kubwa,” alisema.

VIONGOZI WAUWAGA MWILI WA MAREHEMU SALMIN AWADH SALMIN BARAZA LA WAWAKILISHI.

TWIGA STARS KUINGIA KAMBINI JUMAPILI.

index 
Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake Tanzania (Twiga Stars), Rogasian Kaijage ametangaza kikosi cha wachezaji thelathini (30) kitakachoingia kambini siku ya jumapili kujiandaa na mchezo wa kufuzu Mataifa Afrika dhidi ya Zambia mwezi Machi mwaka huu.
Kaijage ametangaza program yake ya  mazoezi itakayochukua takribani wiki nne (4) ili kuhakikisha wachezaji wanakua tayari kwa ajili ya mchezo huo utakaochezwa kati ya Machi 21, 22 mwaka huu, huku akipanga kucheza mchezo mmoja wa kirafiki kabla ya kuelekea Lusaka Zambia kwenye mchezo wa awali.

SOKA LA UFUKWENI TANZANIA KUIVAA KENYA JUMAMOSI.

150217084600_soka_ufukweni_640x360_bbc_nocredit
Timu ya Taifa ya Tanzania ya Soka la Ufukweni (Beach Soccer) kesho jumamosi itacheza mchezo wa marudiano dhidi ya timu ya Taifa ya Kenya, mchezo utakaoanza majira ya saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Escape One Club Msasani jijini Dar es salaam.

ASASI YA “AIDS – free” KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI NDANI YA JESHI LA MAGEREZA

Wasanii wa nje na miaka 15 ya Tamasha la Pasaka

images 
Na Mwandishi Wetu
 
MSAMA Promotion kwa mara nyingine tena imeandaa Tamasha kubwa la nyimbo za kumsifu Mungu litakalofanyika wakati wa sikukuu ya Pasaka katika mikoa tofauti hapa nchini.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama anasema kwamba tamasha hilo mwaka huu litakuwa na utofauti mkubwa ukilinganisha na matamasha mengine yaliyopita, kwani limeboreshwa zaidi na watakuwa wanafurahia miaka 15 tangu lianzishwe.
 
“Kwanza kabisa tofauti na matamasha yaliyopita, mwaka huu tutakuwa na waimbaji wengi zaidi wa muziki wa Injili kutoka nchi za nje.
 
“Kutakuwa na waimbiaji kutoka Kenya, Zambia, Afrika Kusini, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na nje ya Afrika, ambapo lengo kubwa ni kulifanya tamasha hili kuwa na utofauti,” anasema.

Safari ya Mwisho ya DCP Mstaafu wa jeshi la Polisi Tanzania , Mzee Andrew Michael Kumalilwa huko Tabata Segerea.

 Jeneza lenye Mwili wa marehemu Mzee Andrew Michael Kumalilwa ukiwa tayari kushushwa nyumbani kwake Tabata Segerea ambapo misa ya kumuombea na kutoa heshima za mwisho zilifanyika kabla ya Kwenda kuupumzisha Mwili wake katika Nyumba yake ya Milele.
Askari wa Jeshi la Polisi Tanzania wakiwa wamebeba jeneza lenye Mwili wa aliyekuwa DCP Mstaafu wa Jeshi la Polisi Tanzania Mzee Andrew Michael Kumalilwa  wakiingia katika nyumba yake iliyopo Tabata Segerea kwaajili ya Misa na ndugu, jamaa na marafiki kutoa heshima za mwisho kabla ya kwenda kuupumzisha katika Nyumba yake ya Milele ambapo Marehemu alizikwa katika nyumba kwake Tabata Segerea.

Push Observer yazindua teknolojia ya kisasa ya ukusanyaji wa Taarifa ijulikanayo kwa jina la NewsRadar

 Mshauri mkuu wa mradi wa NewsRadar, Romana Gersuni kutoka Ujerumani akielezea jinsi teknolojia hiyo mpya na ya kisasa ya ukusanyaji taarifa mbalimbali ya Push Observer inavyofanyakazi zake.
 mkuu wa mikakati wa kampuni ya Six Telecoms ambayo ni kampuni mama ya Push Observer, Rashid Shamte akielezea faida ambazo watazipata kampuni mbalimbali nchini, husasani za kibiashara kwa kujiunga na huduma ya NewsRadar waliyoianzisha nchii.

MAHAKAMA KUU YA TANZANIA YAPOKEA MSAADA WA MASHINE 38 ZA KUPIGA CHAPA KUTOKA ICTR

images
Mahmoud Ahmad -Arusha
Mahakama kuu ya Tanzania imepokea msaada wa mashine 38 za kupiga chapa Kutoka Mahakama ya mauaji ya Kimbari(ICTR) itakayorahisisha upatikanaji wa nakala za hukumu na mwenendo wa kesi mbalimbali hapa nchini.
Akipokea Msaada huo Jaji Mkuu wa Tanzania Mohammed Chande Othman alisema kuwa msaada huo utasaidia upatikanaji wa haki kuwa rahisi pia, kwani umekuja wakati muafaka wakati mahakama ikiwa katika mabadiliko ya kuzifanya kesi kwenda kwa wakati.

Kusaga: Habari za kuuzwa Clouds Media Group ni uzushi wa kupuuzwa

index
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM TAHARUKI iliyosambaa jana kwenye mitandao kijamii juu ya kuuzwa kwa Clouds Media Group, inayomiliki Clouds FM, Clouds Tv na Choice FM, zimepata majibu baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Joseph Kusaga, kuibuka na kukataa habari hizo na kuziita ni uzushi wa kupuuzwa.
Habari za kuuzwa kwa kampuni hiyo dhidi ya mfanyabiashara maarufu na kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rostam Aziz, zilishika nafasi katika mitandao ya kijamii na hatimae kuzua usumbufu mkubwa kwa wafanyakazi, viongozi wa Clouds na Watanzania kwa ujumla.

DR SHEIN AKUTANA NA WIZARA YA UWEZESHAJI USTAWI WA JAMII,VIJANA WANAWAKE NA WATOTO.

wa1 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kuulia) akizungumza na Uongozi wa  Wizara ya Uwezeshaji,Ustawi wa Jamii, Vijana ,Wanawake na Watoto   katika mkutano wa siku moja uliozungumzia utekelezaji mpango kazi wa Wizara ya hiyo kwa kipindi cha mwezi Julai-Disemba 2014 katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar jana,[Picha na Ikulu.] wa2Watendaji wa Wizara ya  Uwezeshaji,Ustawi wa Jamii, Vijana ,Wanawake na Watoto   wakimsikiliza Waziri  wa Wizara hiyo Bi Zainab Omar Mohamed (hayupo pichani)   alipokuwa akitoa Taarifa ya Utekelezaji wa mpango kazi wa Wizara kwa kipindi cha mwezi Julai-Disemba 2014 katika mkutano uliofanyika jana ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar mbele ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,[Picha na Ikulu.)

SKYLIGHT BAND ILIVYOWABAMBA MASHABIKI WAKE ‘VALENTINES’S DAY’ NDANI YA THAI VILLAGE

DSC_0334Mkali wa R & B Skylight Band, John Music akitoa burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo kwenye usiku maalum wa wapendanao (Valentine’s Night Party) iliyofanyika siku ya Jumamosi ikiwa lengo la kusambaza upendo kwa mashabiki wao Valentine’s day. Kulia ni Ashura Kitenge na kushoto ni Baby wakipiga back vocal kumsapoti John Music.
DSC_0343Ashura Kitenge akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band sambamba na kusindikizwa na Baby.

ZIARA YA PINDA KATIKA JIMBO LA ISIMANI NA KALENGA MKOANI IRINGA

Tigo kuwekeza dola za Kimarekani 120 kutanua mtandao wake 2015

tigo1
Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania Cecile Tiano akiongea na waandishi wa habari kuhusu kampuni yake itakavyowekeza mwaka huu, pembeni yake Meneja Mawasiliano wa Tigo John Wanyancha. Sent from Huawei Mobile

Tigo Tanzania imepanga kutumia kiasi cha dola milioni 120 (Shilingi bilioni 221) mwaka huu kwa ajili ya upanuzi wa mtandao wake utakao ongeza ufanisi wa huduma zake nchini. Akizungumza mipango hiyo ya kampuni kwa mwaka 2015, Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo Bi.Cecile Tiano alisema kwamba uwekezaji wa mwaka huu ni ishara ya nyongeza ya asilimia 20 kutoka dola milioni 100 za kimarekani (shilingi bilioni 184) ambazo kampuni ilitumia katika kuboresha ufanisi wake kwa mwaka 2014.

UNATAKA KUFANYA TRANSFER (KUBADILI JINA) LA KIWANJA/NYUMBA,UTARATIBU WA HARAKA NI HUU.

 images

Na Bashir Yakub.
0784482959, 0714047241 bashiryakub@ymail.com Watu wengi wamenunua viwanja/nyumba lakini mali hizo zimeendelea kubaki katika majina ya waliowauzia. Wapo ambao imepita hata miaka kumi tangu wanunue maeneo lakini bado hawajabadili jina kuingia jina lake. Zipo sababu nyingi zinazosababisha hali hiyo lakini moja ni watu kutokujua umuhimu wa kubadili jina kwa haraka. Hapa sizungumzii tu kubadili jina isipokuwa nazungumzia kubadili jina kwa haraka. Kupitia makala haya napenda kuwaamsha watu kuhusu umuhimu mkubwa wa kubadili jina kwa haraka iwapo umenunua nyumba/kiwanja kwa mtu. Ni muhimu sana kufanya hivyo na itakuepusha na mambo mengi. 1.KAMA HUJABADILI JINA ALIYEKUUZIA BADO NDIYE MMILIKI.

WAZIRI CHIKAWE AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA KUPAMBANA NA VURUGU NA UGAIDI, WASHINGTON MAREKANI

ob1Rais wa Marekani, Barack Obama akitoa hotuba yake katika Mkutano wa Kimataifa wa Kupambana na Vurugu na Ugaidi duniani uliofanyika katika Ukumbi wa Loy Henderson, Wizara ya Mambo ya Nje, jijini Washington DC nchini humo leo. Mkutano huo uliowashirikisha Mawaziri wanaoshughulika na masuala ya usalama kutoka mataifa mbalimbali duniani, Maafisa Waandamizi wa Umoja wa Mataifa (UN), Vyama vya Kiraia na Sekta Binafsi ulijadili masuala mbalimbali ya jinsi ya kupambana na ugaidi pamoja na vurugu mbalimbali dunaini. Katika hotuba yake, Obama alisema mapambano dhidi ya watu wenye msimamo mkali hayawezi kulinganishwa na mapambano dhidi ya waislamu. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe aliiwakilisha Tanzania katika mkutano huo. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
ob2Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akimsikiliza kwa makini Rais Barack Obama (hayupo pichani) wakati alipokuwa anatoa hotuba yake katika Mkutano wa Kimataifa wa Kupambana na Vurugu na Ugaidi duniani uliofanyika katika Ukumbi wa Loy Henderson wa Wizara ya Mambo ya Nje, jijini Washington DC nchini humo leo. Mkutano huo uliowashirikisha Mawaziri wanaoshughulika na masuala ya usalama kutoka mataifa mbalimbali duniani, Maafisa Waandamizi wa Umoja wa Mataifa (UN), Vyama vya Kiraia na Sekta Binafsi ulijadili masuala mbalimbali ya jinsi ya kupambana na vurugu na ugaidi dunaini. Katika hotuba yake, Obama alisema mapambano dhidi ya watu wenye msimamo mkali hayawezi kulinganishwa na mapambano dhidi ya waislamu, hivyo hakuna dini yoyote inayowajibika kwa ugaidi, isipokuwa watu ndio wanaowajibika kwa vurugu na ugaidi. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

WATU WATATU WAFARIKI DUNIA NA KUMI NA NNE KUKIMBIZWA HOSPITAL YA IGOGWE BAADA YA AJALI YA GALI KUBWA LA MAFUTA YA PETROL T821ARF KUANGUKA KIJIJI CHA ISONGOLE (NO ONE) WILAYANI RUNGWE MKOA WA MBEYA IKIWA NI ENEO HILOHILO MITA CHACHE ILIPOTOKEA AJALI ILIYOUA WATU WENGI KWA TUKIO KAMA HILI NA KUZIKWA KATIKA KABURI MOJA

SEHEMU ILIPOTOKEA AJALI YA GALI T821ARF KATIKA KIJIJI CHA ISONGOLE (NO ONE) NA KUSABABISHA WATU WATATU KUFA NA KUMI NA NNE WAKIWA WAJERUHI NA KUKIMBIZWA KATIKA HOSPITAL YA IGOGWE WILAYANI RUNGWE HUKU WATU WATATU WAKIWA KATIKA HALI SIO NZURI
CHANZO CHA MOTO KIKIWA NI MAFUTA YALIYOKUWA KATIKA MTALO HUU AMBAPO MAMA MMOJA AKAENDA NA KIBATALI KUANGALIA YANAYOPITA MTALONI NI MAFUTA AU MAJI NDIPO MAFUTA YAKASHIKA MOTO WA KIBATALI  NA KUSABABISHA MOTO MKUBWA KWENYE TUKIO

Thursday, February 19, 2015

mkutano wa nne wa wanachama na wadau wa PSPF, wamazika mjini Dodoma

 3
Kaimu mkurugenzi wa fedha na utawala wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Yahaya Ally, akitoa taarifa ya fedha ya Mfuko huo wakati wa mkutano wa nne wa wanachama na wadau wa PSPF, mjini Dodoma. Mkutano huo ulioanza Februari 18, umefungwa leo Alhamisi Februari 19, 2015
4
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akisikiliza kwa makini majadiliano ya wanachama na wadau wa Mfuko huo wakati wa mkutano mkuu wa nne wa wanachama na wadau wa PSPF mjini Dodoma ,

TACCEO KUTUMA WAANGALIZI 160 NCHI NZIMA KUANGALIA UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA

Ofisa Mratibu wa Shughuli za Uchaguzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Hamis Mkinde (kushoto), akisisitiza jambo wakati akizyungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, leo, kuhusu Mtandao wa Asasi za Kiraia wa kuangalia Chaguzi Tanzania (Tacceo) kutuma waangalizi 160  nchi nzima kwa ajili ya kuangalia uandikishaji wapiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa BVR katika wilaya zote za Tanzania Bara. Kulia ni Mwenyekiti wa mtandao huo, Martina Kabisama.
……………………………………………….
 
Na Dotto Mwaibale
 
MTANDAO wa Asasi za Kiraia wa kuangalia Chaguzi Tanzania (Tacceo) unategemea kutuma waangalizi 160  nchi nzima kwa ajili ya kuangalia uandikishaji wapiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa BVR katika wilaya zote za Tanzania Bara.

WAZIRI MKUU: WASAIDIENI WAKULIMA WA MPUNGA KUNUFAIKA NA ZANA ZA KISASA

index 
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameutaka uongozi wa mkoa wa Iringa utafute njia bora ya kuwasaidia wakulima wanaotumia na skimu ya umwagiliaji ya Magozi katika tarafa ya Pawaga, wilayani Iringa ili waweze kunufaika na matumizi ya zana za kisasa kwenye kilimo cha mpunga.
Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Afisa Kilimo wa Wilaya hiyo na uongozi wa vijiji hivyo, mara baada ya kukagua eneo zima la mradi huo pamoja na zana za kilimo walizonazo leo mchana (Alhamisi, Februari 19, 2015), Waziri Mkuu alisema kwa zana walizonazo hawawezi kufikia lengo lao la uzalishaji wa tani nane kwa ekari moja kama wataendelea na kilimo cha majaruba.
“Hii combine harvester umesema inavuna ekari 12 kwa siku moja, sasa hapa kuna mtu ana robo eka, jirani yake ana nusu eka, pale kuna mwingine ana ekari mbili utawezaje kutumia mashine hii? Kimsingi haiwezekani,” alihoji Waziri Mkuu.

KAMPUNI YA SIMU YA TIGO KUWEKEZA SH.BILIONI 221 KATIKA MTANDAO WAKE 2015


 Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Cecile Tiano akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu  mipango ya kampuni hiyo kwa mwaka 2015 ambapo imepanga kuwekeza sh. bilioni 221 katika mtandao wake kwa mwaka 2015. Kulia ni Meneja  Mawasiliano wa Tigo, John Wanyancha.

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AFUNGUA RASMI MKUTANO WA KIKANDA JUU YA UKUAJI NA MAISHA YA BAADAE YA MIJI YA AFRIKA MASHARIKI

1
Afisa mtendaji mkuu waTaasisi ya Uongozi wa Afrika kwa Maendeleo Endelevu (UONGOZI Institute) Prof.Joseph Semboja, (Kulia) akimkaribisha Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar , Mh. Balozi Seif Ali Iddi, (kushoto) kufungua rasmi Mkutano wa kikanda uliokutanisha viongozi na watunga sera kutoka nchi za Afrika mashariki , kuzungumzia changamoto za ukuaji wa miji na kushughulikia hali ya baadae ya miji ya Afrika mpaka ifikapo 2050, katikati ni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick. Mkutano huo wa siku mbili umefanyika katika hotel ya Hyatt Regency Kilimanjaro Hotel ya jijini Dar es Salaam.
2
Afisa mtendaji mkuu wa Taasisi ya Uongozi wa Afrika kwa Maendeleo Endelevu (UONGOZI Institute) Prof. Joseph Semboja, (Kulia) akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar , Mh, Balozi Seif Ali Iddi, wa tatu toka kulia, kufungua rasmi mkutano wa kikanda uliokutanisha Viongozi na watunga Sera kutoka Nchi za Afrika mashariki , uliozungumzia changamoto za ukuaji wa miji na kushughulikia hali ya baadae ya miji ya Afrika mpaka ifikapo 2050, Kushoto ni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick, na wa Pili kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu , tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia , mkutano huo wa siku mbili umefanyika leo katika hotel ya Hyatt Regency Kilimanjaro ya jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Saudi Arabia Nchini Tanzania akutana na Dr. Shein

AMB1Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi wa Saudi Arabia Nchini  Tanzania Hani Bin Abdulla Mominah leo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya kumuaga Rais baada ya kumaliza muda wake wa kazi Nchini.[Picha na Ikulu.]
AMB2Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi wa Saudi Arabia Nchini  Tanzania Hani Bin Abdulla Mominah leo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya kumuaga Rais baada ya kumaliza muda wake wa kazi Nchini.[Picha na Ikulu.]

DR. SHEIN AKUTANA NA UONGOZI WIZARA YA FEDHA

NINI WANAFUNZI WAFANYE BAADA YA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

images 
Huzuni ikipitiliza humpelekea mtu kukata tamaa na kutoona thamani ya maisha na hata kufikia hatua ya kunywa sumu au kujiua wakati furaha ikizidi humfanya mtu akasahau majukumu mengine mazito yaliyo mbele yake. Matokeo ya kidato cha nne yaliyotoka hivi karibuni yamewaacha wanafunzi na wazazi wengi kwenye majonzi huku wengine wakiwa na furaha. Hii ni kutokana na idadi ya wanafunzi waliomaliza kuwa na matokeo ya wastani katika mitihani yao.

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI TAREHE 8 MACHI, 2015

imagesd1 

Tarehe 8 Machi, 2015 Tanzania itaungana na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani. Kwa mwaka huu, tunaadhimisha siku hii adhimu katika ngazi ya kitaifa ambapo mkoa wa Morogoro utakuwa mwenyeji wa Maadhimisho haya. Mikoa mingine itakuwa na fursa ya kuandaa maadhimisho haya katika maeneo yao kwa kuzingatia mazingira yao.
Maadhimisho haya hutoa fursa kwa Taifa, mikoa, wilaya na wadau wengine kupima mafanikio yaliyopatikana katika kuwendeleza wanawake na kubainisha changamoto zilizojitokea katika kuwawezesha wanawake na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo.
Maadhimisho ya mwaka 2015 ni ya kipekee kutokana na kuwepo kwa matukio muhimu ambayo yote yatagusa masuala ya haki za wanawake na usawa wa jinsia. Matukio hayo ni: Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge, na madiwani; tathmini ya mafanikio ya utekelezaji wa Azimio la Ulingo wa Beijing baada ya miaka 20 (1995 – 2015); tathmini ya Malengo ya Millenia (2005-2015) na mwelekeo wa Agenda 2063; kuhusu kuwa na ‘Afrika Tunayohitaji’ ifikapo mwaka 2063.

MWAKILISHI WA JIMBO LA MAGOMENI ZANZIBAR AFARIKI GHAFLA

Taasisi ya WAMA na Serikali ya Japani watiliana saini mkataba wa mradi wa upanuzi wa shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama iliyopo Rufiji mkoani Pwani utakaogharimu shilingi milioni mia tisa.

3
Na Anna Nkinda – Maelezo
 Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na Serikali ya Japani wametiliana saini mkataba wa mradi wa upanuzi wa shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama iliyopo Rufiji mkoani Pwani utakaogharimu shilingi milioni mia tisa.

Balozi wa Saudia Amuaga Rais Kikwete

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha ikulu na kufanya mazungumzo na Balozi wa Saudi Arabia anayemaliza muda wake Mhe.Hani Abdullah Mominah wakati baliozi huyo alipokwenda ikulu kuagana na Rais leo(picha na Freddy Maro) rai1Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazungumzo na Balozi wa Saudi Arabia anayemaliza muda wake Mhe.Hani Abdullah Mominah wakati baliozi huyo alipokwenda ikulu kuagana na Rais leo(picha na Freddy Maro)

Tamko la THBUB kulaani mauaji ya Mtoto Yohana Bahati

index 
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imesikitishwa na mauaji ya kikatili ya mtoto Yohana Bahati aliyetekwa nyara hivi karibuni katika kijiji cha Ilelema, Chato Mkoani Geita.
Pia Tume inalaani kuumizwa kwa mama yake, Ester Jonas wakati anatetea uhai wa mwanae wakati wa tukio lililotokea Februari 15, 2015.

MAMA SALMA KIKWETE ATILIANA SAINI MKATABA WA UPANUZI WA SHULE YA WAMA-NAKAYAMA NA BALOZI WA JAPAN HAPA NCHINI MHE. MASAKI OKADA.

1
Balozi wa Japan nchini Tanzania Mheshimiwa Masaki Okada akizumgumza na Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete pamoja na uongozi wa Taasisi hiyo muda mfupi kabla ya kutiliana saini mkataba wa mradi wa kupanua Shule ya Sekondari WAMA-Nakayama iliyoko Rufiji, Mkoani Pwani tarehe 19.2.2015.
2
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akitiliana saini na Balozi wa Japan hapa nchini Mheshimiwa Masaki Okada kwenye mradi wa upanuzi wa Shule ya Sekondari WAMA-Nakayama utakaogharimu dola za kimarekani 498,738. Sherehe ya utiaji saini ilifanyika kwenye ofisi za WAMA zilizopo karibu na Ikulu.

TIMU ya Coastal Union ya Tanga kucheza na Ndanda SC Jumamosi wiki hii

100_0628-610x400 
NA MWANDISHI WETU,TANGA.
TIMU ya Coastal Union ya Tanga imeondoka mkoani hapa leo asubuhi kuelekea mkoani Mtwara kwa ajili ya mechi yao ya Ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Ndanda SC itakayochezwa Jumamosi wiki hii.
     Coastal Union ambayo mechi yao iliyopita dhidi ya Mbeya City iliyochezwa kwenye uwanj wa
                CCM Mkwakwani haikupata matokeo mazuri sana baada ya kulazimishwa sare hivo itaingia kwenye mechi hiyo mithili ya mbogo aliyejeruhiwa msituni

JIPATIE NAKALA YAKO YA GAZETI LA UWAZI MIZENGWE YA UCHAGUZI KILA IJUMAA

mahafali ya tatu Chuo cha Travelport yafana

11
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zenith Tour Ndg Salim, akizungumza wakati wa mahafali hayo ya Vijana 18 waliohitimu mafunzo ya huduma ya kieletronic ya huduma ya ukataji wa tiketi za ndege yanayotolewa na Travelport kwa kushirikiana na kampuni ya Zenith Tour ya Zanzibar.
33
Wahitimu wakimsikiliza Mkurugenzi wa Zenith Tour akitowa nasaha zake kwa wahitimu hao.wakati wa hafla ya mahafali ya tatu ya chuo hicho.