TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, October 23, 2014

KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) YAJADILI HESABU ZA MWAKA WA FEDHA WA 31 DESEMBA, 2012 BAADA YA RIPOTI YA CAG, KWA SHIRIKA LA BIMA LA TAIFA (NIC)

PIX 1Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Zitto Kabwe akiongoza kamati hiyo siku ya tarehe 23 Oktoba, 2014 katika Ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili hesabu za mwaka wa fedha wa 31 Desemba, 2013 kwa Shirika la Bima la Taifa (NIC) baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
PIX 5Mjumbe wa  Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Ismail Rage ambaye ni Mbunge wa Tabora mjini  akichangia mada wakati wa kamati hiyo siku ya tarehe 23 Oktoba, 2014 katika Ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam, kujadili hesabu za mwaka wa fedha wa 31 Desemba, 2013 kwa Shirika la Bima la Taifa (NIC) baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
PIX 6Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dkt. Edmund Mndolwa (kushoto) akijibu maswali toka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali kwa lengo la kujadili hesabu za mwaka wa fedha wa 31 Desemba, 2013 kwa Shirika la Bima la Taifa (NIC) baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
PIX 8Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Bw. Justine Mwandu akichangia mada kuhusu kujadili hesabu za mwaka wa fedha wa 31 Desemba, 2013 kwa Shirika la Bima la Taifa (NIC) baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
PIX 9Baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) wakichangia mada wakati wa Kamati ya kujadili hesabu za mwaka wa fedha wa 31 Desemba, 2013 kwa Shirika la Bima la Taifa (NIC) baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). kamati iliyofanyika siku ya tarehe 23 Oktoba, 2014 katika ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam,
PIX 11Wabunge na wadau wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali wakati wa kujadili hesabu za mwaka wa fedha wa 31 Desemba, 2013 kwa Shirika la Bima la Taifa (NIC) baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). Kamati hiyo ilifanyika siku ya tarehe 23 Oktoba, 2014 katika ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam,
PIX 12Wabunge na wadau wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali wakati wa kujadili hesabu za mwaka wa fedha wa 31 Desemba, 2013 kwa Shirika la Bima la Taifa (NIC) baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). Kamati hiyo ilifanyika siku ya tarehe 23 Oktoba, 2014 katika ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam,

2014 CNN – MULTICHOICE JOURNALIST AWARDS SHOWCASES TANZANIA DESPITE FAILURE TO WIN A SINGLE AWARD

image008Bento Venâncio, from Jornal Domingo and Brito Simango, from Televisão de Moçambique, posing with Victor Mlunde while holding their Portuguese Language General News Awards.
By Victor Mlunde
Last Saturday, the world witnessed a historic annual CNN-Multichoice Journalist Award ceremony on the continent, hosted for the first time in our commercial capital, Dar Es Salaam.
The choice of Tanzania is not only an unprecedented honor to the great peaceful nation on the continent, but a rare opportunity to showcase Tanzania and open its market to the world.
I congratulate the event organizers and His Excellency the President, Dr Jakaya Mrisho Kikwete, for being the Guest of Honour, for his outstanding economic diplomacy skills and unending efforts in showcasing Tanzania to the world.
As usual, the president’s speech looked at quantity rather than quality, boasting to have more media outlets in the country than neighbors – even with mounting insecurity of media practitioners and existence of Draconian Newspapers Act, 1976 and National Security Act, 1970 which limit press freedom as we approach 2015 general elections, the standard rhetoric maintained that the government will soon table the Freedom of Information and Media Services Bills in parliament, a promise left unattended by the Ministry of Information since begin of his second term in office back in 2006.
Despite government’s slow pace in implementing commitments on free press, we should acknowledge the fact that the head of state is at least committed to transparency and open government more than his predecessors, at least by signing international commitments and protocols on transparency such as the Open Government Partnership, though more work needs to be done in getting Media Freedom Bill and Services Act in place before busy and tense election period comes in.
image009Categories and winners
The award categories covered economics and business, press freedom, culture, sports, photo journalism, sports reporting and the environment. Others included Portuguese and French stories awards. Winners wrote moving and interesting stories. To mention a few; Bento Venâncio, Jornal Domingo, Mozambique investigated how lack of transparency in procurement of automobiles in Mozambique leads to fraud, Evelyn Watta, a sports reporter from Kenya revealed the value of Senegal’s mythical Wrestling heritage to the West African nation. The most touching of all was Press Freedom Award handed to the wife of jailed Swazi journalist, Bheki Makhubu who is facing sedition for penning columns supporting a state clerk who was charged for trying to put right the system that allowed judicial officers to misuse public cars.
My sincere congratulations should go to the only brave Tanzanian nominee, one Dickson Ng’hily whose Dar traffic jam story was a concern of all Dar commuters; too bad the judges underestimated the significance of his story in pushing authorities in fast growing African cities to expand the road network.
However, a question remains; where were the rest of Tanzanian journalists? it is believed the majority did not submit their work for some reason – probably due to the fact that everyone was very busy reporting on “katiba” stunning headlines “serikali mbili au tatu” instead of simple local stories that could create positive impact in the community! If the awards had a politics category, I am sure we would have beaten the Kenyans and West Africans for our genius in making stunning political headlines.
Yes! We would have defeated our neighbours in Kenya who have outperformed the whole of East Africa in this year’s awards, yet again. In fact it is not the first time; even in the prestigious annual Kili Marathon held in Tanzania’s Kilimanjaro region, Kenyans end up winning more trophies while we the hosts are reduced to mere spectators each year.
415President Jakaya Kikwete presents the overall ‘CNN MultiChoice African Journalist of the Year’ Award to Joseph Mathenge. Looking on is Mathenge’s son, Geoff Kihato.
Overall winner
I was personally moved by the story of the overall winner, Joseph Mathenge and his son who convinced father to abandon his private photography tender aimed at raising funds for son’s cancer treatment and instead rushed to the Westgate Mall to capture the very first photos that revealed the images of terror to the whole world.
Way forward
It is high time Tanzanian journalists be proud of their work and confident to present it in future awards, even when unsure of winning. More quantity will help identify quality stories that will make all of us proud.
Organizers should also add a social media category to honour and recognize excellent work by social media which uses the internet and citizen journalism to report sensational stories as they happen swifter than the traditional media itself.
On the other hand, award organizers should add a Swahili story category alongside Portuguese and French story awards for it is an African Union (AU) language widely spoken across East and Central Africa. Moreover, I would like to advise CNN to introduce a CNN Swahili language service in East and Central Africa, emulating BBC, Deutsche Welle, Radio France International and VOA in giving local journalists in the broader Swahili speaking East and Central African region to cover and explain local stories to the world.
Victor Mlunde is a Dar es Salaam-based Political and Development Consultant with expertise in media, good governance, elections and conflicts resolution in the Great Lakes region. He can be easily reached through +255 714 289428 and vicmlunde@yahoo.com

SWEDEN YATOA BIL. 42/- KUSAIDIA MIRADI UN

DSC_0216Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mh. Lennarth Hjelmaker akizungumza na waandishi wa habari kwenye hafla ya kutiliana saini makubaliano kati ya nchi ya yake na Umoja wa Mataifa ambapo wametoa fedha kusaidia miradi ya Umoja wa Mataifa kwenye ofisi za ubalozi wa Sweden jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.(Picha na Zainul Mzige MOblog).
Na Mwandishi wetu
SWEDEN imeyapatia mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo hapa nchini jumla ya shilingi bilioni 42/- ili kusaidia katika miradi yake ya maendeleo inayofanya nchiini Tanzania.
Makubaliano ya fedha hizo yametiwa saini jana kati ya Balozi wa Sweden Lennarth Hjelmaker na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Alvaro Rodriguez.
Fedha hizo ambazo ni sawa na dola milioni 24, zitaelekezwa kwenye miradi ya UNDAP inayoendana na sera za Sweden za kuwezesha masuala ya utawala bora, ustawi wa jamii, wanawake na watoto na usawa wa kijinsia.
Kwa mujibu wa Balozi wa Sweden, fedha hizo zitasaidia utekelezaji wa Mkukuta, Mkuza na Matokeo makubwa sasa (BRN) mipango inayofadhiliwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa .
Alisema ni matumaini yake kuwa fedha hizo zitaboresha hali ya kufanya biashara, kuwekeza kwa lengo la kutoa ajira zaidi,kuwezesha uchaguzi huru, kuimarisha huduma za jamii, kuimarisha mipango, uwajibikaji na kuimarisha mawasiliano ya radio kwa ajili ya upashanaji habari vijijini ili kusaidia maamuzi yenye mtazamo mpana zaidi miongoni mwa watu wa vijijini.
IMG_2231Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mh. Lennarth Hjelmaker (kulia) na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakitiliana saini makubaliano ya msaada wa fedha hizo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla hiyo iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam kwenye ofisi za ubalozi huo.
Katika hafla hiyo Balozi wa Sweden alisema pamoja na kutoa fedha hizo kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa, nchi yake itaendelea na makubaliano yaliyofikiwa na serikali ya Tanzania na kuendelea kutoa misaada yake ya kimaendeleo.
Akijibu swali la kwanini wanatoa fedha kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa pekee, na kama wameacha kutoa misaada ya moja kwa moja serikalini, Balozi huyo alisema misaada ya taifa hilo imelenga kupata matokeo yanayotakiwa na kwamba itaendelea kusaidia pia taasisi nyingine zisizo za kiserikali na serikali yenyewe.
Aidha Balozi Lennarth Hjelmåker alisema kwamba Tanzania imekuwa mfano bora kabisa wa mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa kuwezesha ufanisi mkubwa wa miradi ya maendeleo yaliyolenga kuwawezesha watanzania kupiga hatua mbele na kuhakikisha kuwapo kwa amani.
Alisema wanafurahia kusaidia masuala ya utawala bora, kazi kwa vijana, usawa wa kijinsia na kuwapo kwa uchaguzi huru na wenye amani.
DSC_0264Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mh. Lennarth Hjelmaker (kulia) na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakionyesha hati za makubaliano hayo mara baada ya kutiliana saini.
Sweden imesema itaendelea kusaidia Umoja wa Mataifa nchini hasa inapotekeleza mradi wake wa misaada kwa Tanzania (UNDAP) kama mashirika hayo yalivyokubaliana na serikali ya Tanzania.
Naye Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez, ameishukuru Sweden kwa kuendelea kuwa mdau wa maendeleo.
Tanzania na Umoja wa Mataifa wanatekeleza mradi wa miaka mitano wa UNDAP ambapo mashirika ya UN yaliyopo nchini yanatoa kwa umoja wake huduma stahiki ili kupata Matokeo Makubwa.
DSC_0267Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mh. Lennarth Hjelmaker (kulia) na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakibadilishana hati hizo za makubaliano hayo.
DSC_0238Baadhi ya waandishi wa habari na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na Ubalozi wa Sweden waliohudhuria hafla hiyo.
DSC_0242
DSC_0278Naibu Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo kwenye Ubalozi wa Sweden nchini, Maria Van Berlekom, akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za ubalozi huo jana jijini Dar es Salaam.
DSC_0280Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu (kushoto) akimtambulisha Mwandishi wa habari kutoka East Africa Radio Nassa Kingu kwa Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati) mara baada ya hafla fupi ya kutiliana saini makubaliano ya fedha hizo baina ya Umoja wa Mataifa na Ubalozi wa Sweden nchini.
DSC_0165Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akiteta jambo na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mh. Lennarth Hjelmaker mara baada ya Umoja wa Mataifa na Ubalozi wa Sweden kutiliana saini makubaliano ya msaada huo.

Rais azungumza na Balozi wa Marekani

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania  Mark Bradley baada ya mazungumzo yao alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na  Ramadhan Othman Ikulu.] IMG_9469Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiagana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania  Mark Bradley baada ya mazungumzo yao alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi,[Picha na  Ramadhan Othman Ikulu.]

WAZIRI CHIKAWE AMKABIDHI MKUU WA WILAYA NACHINGWEA MABATI 2000 KWA AJILI YA UJENZI WA MAABARA SHULE ZA SEKONDARI

PIX 1Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo mabati 2000 kwa ajili ya ujenzi wa Maabara za Shule 20 za Sekondari wilayani humo. Waziri Chikawe ametoa msaada huo baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa agizo kwa kila mwana jamii nchini kuchangia ujenzi wa maabara katika shule za Kata nchini. Picha na Felix Mwagara.
PIX 2-Horizontal PixWaziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (wapili kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Abdalla Chikawe (wapili kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Valery Kwembe wakiyaangalia msaada wa mabati yaliyotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo kwa ajili ya kuzisaidia Shule za Sekondari za Kata kwa ajili ya ujenzi wa maabara. Makabidhiano ya mabati hayo 2000 yalifanyika nyumbani kwa Waziri Chikawe mjini Nachingwea leo. Picha zote na Felix Mwagara.

RAIS WA TOC KUFUNGA KOZI YA MAKOCHA

 Bayi 1 
Ndugu Filbert Bayi (Katibu ) wa TOC
………………………………………………………………………………
Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Gulam Rashid kesho (Oktoba 24 mwaka huu) atafunga kozi ya makocha ya Leseni C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Hafla ya ufungaji kozi hiyo iliyoshirikisha makocha 32 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar na kuandaliwa na TOC kupitia Olympic Solidarity kwa ushirikiano na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itafanyika saa 5 asubuhi kwenye hosteli za TFF zilizopo Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Kozi hiyo ya wiki mbili iliyoanza Oktoba 12 mwaka huu iliendeshwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) Ulric Mathiot kutoka Shelisheli.
Makocha walioshiriki kozi hiyo ni Ahmed Suleiman Simba (Alliance), Akida Saidi (Lindi), Ally Bushir Mahmoud (Zanzibar), Aloyce Akwilin (Pwani), Amin Rashid Mdowe (Zanzibar), Augustino Dakto Damian (Katavi), Athuman Bilal (Shinyanga), Bakari Shime (Tanga), Charles Mayaya (Shinyanga) na Choki Abeid(Geita).
Wengine ni Edna Lema (Morogoro), George Melchior (Kagera), Godfrey Kapufi (Katavi), Hamis Mabo (Kigoma), Hawa Bajangero (TWFA), Ibrahim Mulumba (Geita), Jemedari Said (TAFCA), Kenny Mwaisabula (TAFCA), Madenge S. Omari (Mara), Milambo Camil (Tabora) na Mohamed D (Ruvuma).
Pia wapo Mohamed Ismail Laiser (Manyara), Mohamed Muya (Dodoma), Ngawina Ngawina (Mtwara), Nicholas Kiondo (Ilala), Osuri Charles Kosuri (Simiyu), Rachel Palangyo (TWFA), Salvatory Edward (Temeke), Seif Bausi Nassor (Zanzibar), Yusuf Macho (Kigoma), Wilfred Mollel (Iringa) na Zacharia Mgambwa (Rukwa).
Makocha watakaofaulu kozi hiyo watapewa Leseni C za CAF wakati watakaoshindwa watapewa vyeti vya ushiriki tu.

Pata hapa nakala ya muswada wa Baraza la Vijana la Taifa; boresha tupate baraza bora

indexKatika Mkutano wa 14 wa Bunge tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 niliouwasilisha tarehe 31 Oktoba 2013.
Narudia tena kuwashukuru vijana na wadau tulioshirikiana kuandaa muswada huo na naomba kuendelea kupata ushirikiano wenu wa karibu katika hatua zinazoendelea.
Kuanzia tarehe 21 Oktoba 2014 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii imeanza vikao vya kupokea maoni ya wadau kuhusu muswada huo. Nakala tete ya muswada huo inapatikana hapa, tafadhali pakua pitia na wasilisha maoni yako sasa.
Unaweza kuandika maoni yako kwenye mtandao wa http://mnyika.blogspot.com au kutuma kwa barua pepe kwenda mbungeubungo@gmail.com na nakala kwa Kamati husika ya Bunge kupitia tanzparl@parliament.go.tz.
Ikiwa unataka kutumia njia nyingine kuwasilisha maoni yako tafadhali wasiliana na Gaston Garubimbi 0715/0767-825025 kwa maelezo zaidi. Mdau wa masuala ya vijana zingatia kwamba zaidi ya miaka 18 ahadi za kukamilisha mchakato wa kuanzishwa kwa baraza la Vijana la Taifa zimekuwa zikitolewa bila utekelezaji kamili na wa haraka.
Baraza la Vijana la Taifa pamoja na malengo mengine litawezesha vijana kuanzia kwenye vijiji/mitaa mpaka taifa kuweza kuwa na vyombo vya kuwaunganisha vijana kwa kike na wa kiume kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa.
Aidha, Baraza hilo litafuatilia pia kwa karibu utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya vijana kwenye Halmashauri, Serikali kuu, katika vyombo mbalimbali vya maendeleo na wadau wa maendeleo.
Pia, Baraza la Vijana litafuatilia kwa karibu utendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kuhakikisha kwamba fedha zinatengwa za kutosha na kufika kwa walengwa kuwawezesha vijana kujiajiri, kukuza vipaji vyao na kushughulikia maendeleo yao kwa ujumla.
Kwa upande wangu nitashukuru ikiwa nitapokea maoni hayo kabla ya tarehe 28 Oktoba 2014, niweze kuyachambua na kutoa mrejesho mapema kuwezesha muswada kusomwa kwa mara ya pili Bungeni katika Mkutano wa 16 uliopangwa kuanza tarehe 3 Novemba 2014.
Kwa mujibu wa Hansard tarehe 21 Disemba 2013 baada ya Muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, Spika wa Bunge Anna Makinda alisema yafuatayo Bungeni “…muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye kamati zitakazohusika wakati muafaka”.
Majibu yanapaswa kutolewa na mamlaka husika ni kwanini toka wakati huo haukuwahi kuwekwa kwenye Tovuti ya Bunge pamoja na kukumbushwa. Hata hivyo nashukuru kuwa hatimaye sasa muswada huo umepelekwa kwenye Kamati, hivyo ni wakati muafaka kwa vijana na wadau wote kupata nakala ya muswada huo hapa na kutoa maoni ya kuboresha ili Baraza la Vijana la Taifa liweze kuundwa.
Kujadiliwa kwa muswada huo ni hatua ya pekee katika historia ya harakati za vijana nchini kwa kuzingatia kuwa Sera ya zamani ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 ilitamka kwamba kutaanzishwa Baraza la Vijana na suala hilo kurudiwa katika Sera mpya ya mwaka 2007.
Hata hivyo Serikali imekuwa ikikwepa kuhakikisha kwamba matakwa hayo ya sera tajwa yanatekelezwa kwa wakati pamoja na kuwa suala hilo linahusu mustakabali wa maendeleo ya vijana nchini. Hivyo pakua nakala pekua toa maoni; boresha muswada tupate baraza bora.
Wenu katika uwakilishi wa wananchi,
John Mnyika (Mb)
23 Oktoba 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA BALOZI WA BOTSWANA NCHINI TANZANIA IKULU DAR

unnamedMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na  Balozi wa Botswana nchini Tanzania, anayemaliza muda wake, Oliphant Tuelonyana, aliyefika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam jana kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini. Picha na OMR

Airtel yatatua changamoto za uhaba wa vitabu vya sayansi Katika shule ya Sekondari Mukulati Mkoani Arusha

unnamedMakamu mkuu wa shule ya sekondari Mukulati ya mkoani arusha mwalimu Vitalisi Martine akiwakabidhi baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo vitabu vya sayansi vilivyo tolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel wakati wa mahafali ya 17 ya kidato cha nne katika shule hiyo. unnamed1Meneja Mauzo wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel mkoa wa kilimanjaro Paschal Bikomagu kushoto akimkabidhi baadhi ya vitabu vya sayansi kwa Diwani wa  kata ya Olkokola Joseph laizer  kwa niaba ya shule ya sekondari Mukulati  mkoani arusha  wakati wa mahafali ya 17 ya kidato cha nne ya shule hiyo.
……………………………………………………………….
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel  imeedelea kuungana na serikali katika kusaidia kuboresha maendeleo ya sekta ya elimu  nchini ambapo imetoa vitabu vya ziada na kiada  katika masomo ya sayansi kwa shule ya sekondari mukulati wilayani Arumeru mkoani Arusha
Licha ya Kada ya sayansi kuwa ndio chimbuko kubwa  la wataalamu wengi katika fani mbalimbali bado  inatajwa kutofanya vizuri kutokana na uhaba wa miundombinu na vifaa stahiki ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya kada hiyo. 
Meneja wa Airtel mkoa wa Kilimanjaro  Paschal Mikomagu  akizungumzia mchango wa kampuni hiyo wakati wa mahafali ya 17 ya shule ya sekondari mukulati amesema Airtel kwa kutambua changamoto mbalimbali ndani ya kada ya sayansi nchini ikiwemo uhaba wa vitabu vya kujifunzia  imeamua kuwa na utaratibu wa kugawa vitabu hivyo.  Leo tumehudhuria mahafali  na kuchangia kutatua moja ya kero zinazokumba sekta ya elimu na tuaamini kwa msaada huu wa vitabu vitaongeza ufaulu wa wanafunzi na kusaidia shule kufanya vizuri kitaaluma
Tutaendelea kutimiza dhamira yetu kwa vitengo ya kusaidia kutatua changamoto mbalimbali mashuleni na kuhakikisha tunaboresha uwiano wa vitabu kwa wanafunzi hadi kitabu kimoja kwa mtoto moja au wawili.
Kwa upande wake Diwani wa  kata ya Olkokola Joseph laizer  leo ni sisi Airtel imetoa msaada huu wa vitabu ambavyo vitasaidia shule hapa , lakini zaidi tunawaomba Airtel waendelee kujitolea kushirikiana nasi  na kutufadhili katika ujenzi wa maabara katika shule hii ili kuweza kufikia malengo tuliyowekewa ya kuhakikisha kila shule ya sekondari inajenga maabara kwa ajili ya mafunzo ya ziada
Akiongea mara baada ya kupokea vitabu hivyo MkeeVitalisi Martine mkuu wa shule  kwa msaada huu umeongeza uwiano wa vitabu shule hapa ambapo kwa sasa kitabu kimoja kitatatumika na wanafunzi wawili,  napenda kuwhakikishia vitabu hivi havitakaa kwenye kabati bali vitatumika kwa manufaa yaliyokusudiwa ili atimaye watoto waweze kupata ujuzi kupitia vitabu hivi
Nao baadhi ya wanafunzi walito maoni yao kuhusu mchango huu shule ni hapo ambapo Happy Lyimo alisema natoa shukurani za dhati kwa niaba ya wanafunzi wenzangu kwa Airtel kwa kutupatia mchango wa vitabu vingi vya sayansi. Nimatumaini yangu kuwa vitabu hivi vitasaidia kuinua taaluma kwa wanafunzi na  shule kwa ujumla.

MAKAMU WA RAIS DKT. BIALA AKUTANA NA MKURUGENZI MKUU MSTAAFU WA UBA TANZANIA GENERAL ROBERT MBOMA NA UJUMBE WAKE, IKULU DAR.

1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Ujumbe wa UBA Tanzania ulioongozwa na aliyekuwa Mkurugenzi wake Mkuu mstaafu, General Robert Mbomba, wakati walipofika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, jana Oktoba 22, 2014. Picha na OMR 2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Ujumbe wa UBA Tanzania ulioongozwa na aliyekuwa Mkurugenzi wake Mkuu mstaafu, General Robert Mbomba (kulia) wakati walipofika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, jana Oktoba 22, 2014. Picha na OMR 3Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Ujumbe wa UBA Tanzania ulioongozwa na aliyekuwa Mkurugenzi wake Mkuu mstaafu, General Robert Mbomba (kulia) wakati walipofika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, jana Oktoba 22, 2014. Picha na OMR 4 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa UBA Tanzania, baada ya mazunguzmo yao yaliyofanyika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, jana Oktoba 22, 2014. Picha na OMR 5 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa UBA Tanzania, General Robert Mboma, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI

indexDEREVA MMOJA KATI YA WAWILI AMBAYE HAKUWEZA KUFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE, JINSI YA KIUME, UMRI KATI YA MIAKA 25 – 30 AMEFARIKI DUNIA BAADA YA MAGARI YA ABIRIA WALIYOKUWA WAKIENDESHA YENYE NAMBA ZA USAJILI T.473 CNT AINA YA TOYOTA HIACE NA GARI T.135 AJF AINA YA TOYOTA HIACE KUGONGANA USO KWA USO ENEO LA MWISHO WA WAYA.
AJALI HIYO IMETOKEA MNAMO TAREHE 22.10.2014 MAJIRA YA SAA 22:20 USIKU HUKO MAENEO YA MWISHO WA WAYA, KATA YA IYUNGA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA KATIKA BARABARA YA MBEYA/TUNDUMA.
AIDHA, WATU WATATU WALIJERUHIWA KATIKA AJALI HIYO AMBAO NI 1. LAMECK LIMO 2. ANGOLISYE MWAKALOBO NA 3. JOYCE ASAJILE AMBAO WAMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA MATIBABU.
CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO IKIWA NI PAMOJA NA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
TAARIFA ZA MISAKO:
KATIKA MSAKO WA KWANZA, MTU MMOJA MKAZI WA MKWAJUNI WILAYA YA CHUNYA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA PRISCA SINKALA (31) ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA NA POMBE YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 05.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 22.10.2014 MAJIRA YA SAA 18:00 JIONI HUKO KATIKA KITONGOJI CHA MAJENGO, KIJIJI NA KATA YA MKWAJUNI, TARAFA YA KWIMBA, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA MBEYA. MTUHUMIWA NI MUUZAJI WA POMBE HIYO, TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.
KATIKA MSAKO WA PILI, JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAMSHIKILIA MTU MMOJA AITWAYE ISAYA DARON (27) MKAZI WA SOWETO AKIWA NA POMBE KALI [VIROBA] ZILIZOPIGWA MARUFUKU AINA YA BOSS PAKETI 30.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 22.10.2014 MAJIRA YA SAA 14:00 MCHANA HUKO SOWETO, KATA YA RUANDA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. MTUHUMIWA NI MUUZAJI WA POMBE HIZO.
KATIKA MSAKO WA TATU, MTU MMOJA MKAZI WA AIRPORT JIJINI MBEYA AITWAYE SALEHE SEKILE (32) ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA NA KETE 12 ZA BHANGI SAWA NA UZITO WA GRAMU 60.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA KATIKA MSAKO ULIOFANYIKA MNAMO TAREHE 22.10.2014 MAJIRA YA SAA 17:30 JIONI HUKO MAENEO YA FOREST MPYA, KATA YA FOREST, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. MTUHUMIWA ALIKUTWA NA KETE HIZO BAADA YA KUPEKULIWA KWENYE MIFUKO YAKE YA SURUALI. AIDHA, MTUHUMIWA NI MTUMIAJI NA MUUZAJI WA BHANGI HIYO.

KATIKA MSAKO WA NNE, JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI WAKAZI WA MANGA JIJINI MBEYA AMBAO NI 1. TERESIA MWAISAKILE (31) NA 2. ELIZABETH LONDELE (29) WAKIWA NA POMBE YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 01.
WATUHUMIWA KWA PAMOJA WALIKAMATWA KATIKA MSAKO ULIENDESHWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA MNAMO TAREHE 22.10.2014 MAJIRA YA SAA 13:30 MCHANA HUKO MAENEO YA MANGA, KATA YA MANGA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. WATUHUMIWA NI WAUZAJI WA POMBE HIYO, TARATIBU ZA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA/POMBE YA MOSHI PAMOJA NA POMBE KALI ZILIZOPIGWA MARUFUKU NCHINI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI. AIDHA, ANATOA WITO KWA WANANCHI KUTOA TAARIFA ZA MTU/WATU WANAOJIHUSISHA NA UINGIZAJI/USAMBAZAJI NA UUZAJI WA POMBE KALI NA POMBE YA MOSHI ILI WAKAMATWE NA HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAO.
Imesainiwa na:
[BARAKAEL N. MASAKI – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Adha ya maji yaendelea kuwatesa wakazi wa Kijiji cha Songambele Halmashauri ya Nsimbo Wilayani Mlele.

Madiwani na watalaam wa Halmashauri ya Nsimbo wakijadili mstakabali wa maendeleo ya Halmashauri yao Nsimbo,pamoja na kujadili masuala ya elimu, Afya, Miundo mbinu ya barabara,utawala,na maengineyo lakini suala la maji lilichukua nafasi ya kipekee katika kikao hicho cha baraza la madiwani kilichomalizika mwishoni mwa wiki iiliyo
(Picha zote Kibada Kibada -Nsimbo Mlele Katavi).
???????????????????????????????
Mama akisukuma maji kwenye kisima kifupi kilichopo hapo huku akina mama wengine na watoto wakisubiri zamu yao ifike ili waweze kuchota maji  ambayo yanatoka kidogokidogo kwenye kisima hicho hapo madumu yanaonekana hayana maji,  dumu  moja kujaa inawachukua zaidi ya saa, hivyo kuwafanya watumie muda mwingi kutafuta   maji badala ya kufanya shughuli nyingine za maendeleo.
……………………………………………….
Na Kibada Kibada –Nsimbo Mlele
Wakazi wa Songambele Halmashauri ya Nsimbo Wilayani Mlele wanakabiliwa na Changamoto ya uhaba wa maji kufuatia visima vifupi vilivyopo kutokuwa maji ya kutosha.
Hali  hiyo ya uhaba wa maji kwa baadhi ya Vijiji vya Kata ya Nsimbo na maeneo mengine ya Halmashauri hiyo  inayowafanya akina mama na watoto kuamka  kila siku alfajiri  majira saa kumi usiku kwenda kutafuta maji kwa au  kusubiria  maji  kwenye visim vifupi vilivyopo ambavyo navyo havitoi maji ya kutosha hivyo kutumia muda mrefu kutafuta na kukosa muda wa kufanya shughuli nyingine za maendeleo.
Akizungumzia  hali ilivyotete  kuhusu upatikanaji wa maji katika Kijiji  cha Songambele  na Kata ya Nsimbo kwa ujumla Afisa Mtendaji wa Kata ya Nsimbo Wilbroad Milala anasema kwa kweli hapo maji ni shida kubwa kwa wakazi wa hapo.
Milala anasema hata visima vilivyopo havitoi maji ya kutosha wakati mwingine kama msimu huu wa kiangazi maji hukata hata miezi miwili bila kutoa maji hali inayofanya wakazi hao hasa akina mama na watoto kufuata maji kwenye mbuga umbali wa takribani kilometa tatu hadi nne maji amabyo siyo safi wala salama.
Kufuatia kuwepo kwa changamoto hiyo ya Maji wawakilishi wa wananchi ambao ni madiwani kupitia kwenye vikao vya baraza la madiwani suala la maji lilionekana kuchukua nafasi ya kipekee kuzungumzia ikiwa ni pamoja na kutafuta mbinu za kulipatia ufumbuzi.
Akiongea katika kikao cha Baraza la madiwani kwa nyakati tofauti Mjini Nsimbo Diwani wa Kata ya NsimboMichael Kasanga, Diwani wa Kata ya Mtapenda Eliezer Fyula,walieleza kuwa lazima hatua zichukuliwe kwa haraka ili kulipatia ufumbuzi suala la upatikanaji wa maji kwa wakazi wa Halamshauri hiyo hasa maeneo yale yenye visima vifupi vichimbwe visima virefu.
Wakaeleza kuwa pia visima vinapoharibika taarifa iwe inatolewa mapema kwenye Idara ya Maji ili kuona namna ya kuweza kulipatia ufumbuzi pale panapo wezeakana kama kununua vifaa vya ukarabati wa pump.
Awali Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu na Maji  Raphael Kalinga akiwasilisha taarifa ya Kamati yake alieleza mikakati inayochukuliwa na halmashauri ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maji ikiwa ni pamoja na kutenga fedha kupitia bajeti zake na fedha kutoka kwenye mifuko ya maji ili kusaidia upatikanaji wa maji ikiwa pia na kuomba ufadhili kutoka kwa wahisani mbalimbali kusaidia suala la maji.
Aidha aliwashauri madiwani kuwahamasisha wananchi kuanzisha kamati za mifuko ya maji ili fedha inayopatikana iwe inasaidia katika matengenezo madogo madogo pindi pump za visima vya maji vinapo haribika fedha hizo zitasaidia ukarabati mdogo mdogo.
Katika hatua nyingine Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Nsimbo limemwagiza Kaimu Mhandisi wa Mji katika Halmashauri  Enock Msengi kuhakikisha anapoondoka awe anakaimisha ofisi kwa mwenzake anayekuwa ofisini kuliko kuacha amefunga ofisi na pia mali za ofisi inatakiwa awe anacha ofisi ikiwa wazi na awe anaandika barua ya kukabidhi ofisi kuliko kijiondokea kama anavyofanya kwa kuwa ofisi siyo mali yake bali ni mali ya Serikalai.

HYUNDAI presents Heavy Construction Equipment at Oil & Gas Conference.

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA AKABIDHI ZAWADI YA BASI DOGO BWAWANI SEKONDARI KATIKA MAHAFALI YA KUMI NA MOJA YA KIDATO CHA NNE YALIYOFANYIKA MKOANI PWANI

imageKamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kulia) akikabidhi funguo za Basi dogo kwa Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bwawani, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga(kushoto). Basi hilo litatumiwa na Wanafunzi katika ziara mbambali za Mafunzo hivyo kuondoa kero kubwa ya Usafiri shuleni hapo. image_1Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bwawani Sekondari, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga akijaribisha kuwasha gari jipya lililokabidhiwa na Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) katika Mahafali ya Kumi na moja ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari yaliyofanyika leo Oktoba 22, 2014.
image_2Muonekano wa Basi dogo lenye Na. MT. 0341 lililokabidhiwa leo Oktoba 22, 2014 na Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) katika Mahafali ya Kidato cha Nne ya Shule ya Sekondari Bwawani, Mkoani Pwani. Basi hilo litatumiwa na Wanafunzi wa Bwawani Sekondari katika ziara mbalimbali za Mafunzo. image_3Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(aliyevaa skafu) akiwa meza Kuu amesimama na Viongozi mbalimbali Waalikwa wakati Wahitimu Wakiimba Wimbo Maalum wa Shule katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari leo Oktoba 22, 2014(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga(wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro,  Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kato Rugainunula (wa kwanza kulia) ni Kaimu Mkuu wa Shule ya Bwawani Sekondari, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga. image_4Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akikabidhi cheti kwa Mhitimu wa Kidato cha Nne katika Mahafali ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari leo Oktoba 22, 2014. Jumla ya Wahitimu 95 wametunukiwa cheti cha kuhitimu Elimu ya Kidato cha Nne katika Shule hiyo inayomilikiwa na Jeshi Magereza, Mkoani Pwani.
image_5Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza John Casmir Minja akitoa hotuba yake fupi katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari yaliyofanyika leo Oktoba 22, 2014 Mkoani Pwani.
image_6Sehemu ya Wahitimu katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne, Bwawani Sekondari wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi, Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani).
image_7Kikundi cha Wasanii kinachoundwa na Wanafunzi wa Bwawani Sekondari kikijiandaa kutumbuiza mbele ya Mgeni rasmi katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne Shule ya Bwawani Sekondari, Mahafali hayo yamefanyika leo Oktoba 22, 2014, Mkoani Pwani.
image_8Mama mzazi wa Mhitimu wa Kidato cha Nne kutoka familia ya Kifugaji ya Kimasai akimbusu mkono Mtoto wake ambaye amehitimu Elimu ya Kidato cha Nne katika Shule inayomilikiwa na Jeshi la Magereza, Bwawani Sekondari iliyopo Mkoani Pwani. Mahafali hayo yamefanyika leo Oktoba 22, 2014.

WAZIRI MKUU AZINDUA JARIDA LA FIRST JIJINI LONDON

7a
*Ni Toleo Maalum la Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania
*Linatumika kuitangaza Tanzania kwa watu mashuhuri
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amezindua jarida la kimataifa la FIRST ambalo limesheheni taarifa za kuitangaza Tanzania kwa wadau wa nchi mbalimbali duniani huku likielezea hatua mbalimbali za ustawi kwa miaka 50 tangu nchi ipate uhuru.
Uzindusi huo ulifanyika kwenye ofisi za ubalozi wa Tanzania jijini London, Uingereza ambako pia Waziri Mkuu alikabidhiwa nakala ya kwanza ya toleo la sasa ambayo iliwekwa kwenye jalada jekundu la ngozi (leather bound red cover).
Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Mkuu alisema Serikali ya Tanzania imepata fursa nzuri ya kujinadi kwa watu maarufu na wafanyabiashara wa kimataifa duniani kupitia jarida hilo na akataka uwekwe utaratibu wa kujinadi kisekta.
Alimtaka Balozi wa Uingereza, Bw. Peter Kallaghe aweke mkazo na kusimamia suala hilo ili kuhakikisha matoleo yanayofuata yanakuwa ya kisekta zaidi. “Balozi hapa umefanya kazi nzuri sana ya kuinadi nchi yetu, wala usichoke. Tujitahidi sasa kila mwaka waandike kuhusu fursa za uwekezaji kwa miradi ya kisekta kama utalii, nishati, madini na kadhalika,” alisema.
Waziri Mkuu alimshukuru Mwenyekiti wa taasisi ya First, Bw. Rupert Goodman kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa ajili ya Taifa la Tanzania. “Kazi uliyoifanya ni nzuri lakini katika tolea lijalo tuangalie jinsi ya kuitangaza miradi ya uwekezaji ambayo inauzika na iende sekta kwa sekta. Ukisirikiana na Balozo wetu hapa, lazima utapata kitu kizuri,” alisema.
Mapema, akielezea kuhusu jarida hilo la FIRST, Balozi Kallaghe alisema jarida hilo linasambazwa kwenye mashirika mbalimbali ya ndege kama vile British Airways, Air Astana, Lufthansa, United Airlines, Gulf Air, American Airlines, South African Airways, Korean Airways, Etihad Airways, Qatar Airways na Continental Airlines.
“Siyo tu kwamba linasambazwa katika mashirika haya ya ndege, bali pia linawekwa kwenye vyumba vya kupumzikia (First Class and Business Class Lounges) abiria wa daraja la kwanza na la pili wa mashirika haya kwenye viwanja vingi vya ndege,” alisema.
Alisema hili ni toleo la sita ambalo limeandaliwa kwa ushirikiano na ofisi yake (Ubalozi wa Uingereza) ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania lakini pia ikilenga kutangaza fursa za uwekezaji lakini pia ikitangaza hatua mbalimbali za maendeleo ambazo nchi hii imepitia.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Fedha, Bw. Mwigulu Nchemba; Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Mahadhi Maalim na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Charles Kitwanga. Wengine ni Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Said Mwambungu ambao pia wamefuatana na Waziri Mkuu.

BONDIA THOMAS MASHALI AJIFUA KUMKABILI MKENYA HENRY WANDERA NOVEMBA MOSI FRENDS CORNE

Bondia Tomas Mashali kushoto akijifua wakati wa mazoezi ya kujiandaa kupambana na Bondia Henry Wandera kutoka kenya novemba 1 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese, akisimamiwa na Kocha wa Mchezo wa Masumbwi kutoka Sweeden, Juma Ntuve (Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu BON DIA Thomasi Mashali yupo katika maandalizi mazito ya kumkabili bondia kutoka kenya Henry Wandera Novemba mosi katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam Akizungumza wakati wa mazoezi yake juzi Mashali amesema kuwa yupo fiti wakati wowote yeye kufanya kazi hivyo aofii ata kiogo mpambano huo na kuwataka mashabiki wake waje waone anavyo mgalagaza vibaya sana siku hiyo mkenya Wandera
Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na ulinzi wa kutosha kabisa kutokana na kujipanga vizuri katika swala hilo kingilio ni shilingi, 7000; kwa kila mtu mchezo huu utapambwa na burudani mbalimbali

MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE NA MATUKIO YA PICHA KATIKA ZIARA YA RAIS DR. JAKAYA KIKWETE NCHINI CHINA

1Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea ua kutoka kwa mfanyakazi wa Hoteli ya Diaoyutai iliyoko Beijing mara baada ya kuwasili hotelini hapo. Mama Salma ameambatana na mumewe Rais Dkt. Jakaya Kikwete ambaye amewasili nchini China tarehe 21.10.2014 kwa ziara ya kiserikali. 2Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwapungia wafanyakazi wa Hoteli ya Diaoyutai ya mjini Beijing mara baada ya kuwasili nchini China kwa ziara ya kikazi tarehe 21.10.2014. 3Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa pamoja na Bwana Yang Hua, Mmoja wa viongozi wakuu wa China National Offshore Oil Corporation (CNOOC), wakisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwenyekiti wa Shirika hilo Bwana Wang Yilin kwa Rais Dkt. Jakaya Kikwete alipotembelea makao makuu ya Shirika hilo yaliyoko Beijing nchini China tarehe 22.10.2014. Shirika hilo hujishughulisha na utafiti wa mafuta na gesi baharini, uchimbaji na uuzaji wa maliasili hizo. 4Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mwenyekiti wa China National Offshore Oil Corporation Bwana Wang Yilin wakizindua rasmi mtambo mpya wa utafutaji wa mafuta na gesi baharini, Uzinduzi huo ulifanyika kwenye Makao Makuu ya Shirika hilo huko Beijing tarehe 22.10.2014. 5Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiongoza ujumbe wa Tanzania unaozuru nchini China wakiangalia vifaa mbalimbali vinavyotumiwa na Shirika la  CNOOC la China katika kazi ya utafutaji wa mafuta na gesi baharini wakati walipotembelea Makao Makuu ya Shirika hilo huko Beijing tarehe 22.10.2014. 6Rais Dkt. Jakaya Kikwete akishirikiana na Mkewe Mama Salma Kikwete na Professa Li Songshan (kushoto kwa Rais Kikwete), Mwanzilishi wa Kijiji cha Sanaa cha Afrika kuondoa kitambaa ikiwa ni ishara ya kufungua rasmi kijiji hicho kilichopo katika wilaya ya Songzhuang nchini China tarehe 22.10.2014. 7 8 Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiangalia baadhi ya ngoma za asili ya Afrika zilizokuwa zikipingwa na vijana wa kichina mara baada ya ufunguzi rasmi wa kituo cha sanaa za Afrika huko Songzhuang tarehe 22.10.2014. 9Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiandika kumbukumbu yake katika kitambaa maalum mara baada ya kuzindua rasmi Kijiji cha sanaa za Afrika. Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anaonekana wa kwanza kushoto akifuatiwa na Professa Li Singshan. Kulia kwa Rais Kikwete ni Dkt. Han Rong, Mke wa Professa Li na Mwanzilishi mwenza wa Kijiji hicho na wa kwanza kushoto ni Bwana Joseph Kahama. 10Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiandika kumbukumbu yake katika kitambaa maalum mara baada ya kuzindua rasmi Kijiji cha sanaa za Afrika. Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anaonekana wa kwanza kushoto akifuatiwa na Professa Li Singshan. Kulia kwa Rais Kikwete ni Dkt. Han Rong, Mke wa Professa Li na Mwanzilishi mwenza wa Kijiji hicho na wa kwanza kushoto ni Bwana Joseph Kahama. 11Waanzilishi wa Kijiji cha Sanaa za Afrika Professa Li Songshan na Mke wake Dkt. Han Rong wakimkabidhi zawadi ya picha Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mke wake mara baada ya ufunguzi rasmi wa kijiji hicho tarehe 22.10.2014.
unnamedMke wa Rais Mama Salma Kikwete akiandika kumbukumbu yake kwenye kijiji cha sanaa za Afrika mara baada ya Rais Dkt. Kikwete kuandika kumbukumbu yake.
PICHA NA JOHN  LUKUWI.