TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 23, 2015

SKYLIGHT BAND YAIBUA KIFAA KIPYA MITHILI YA KASUKU SI MWINGINE NI ASHURA KITENGE, NJOO LEO UMSHUHUDIE LIVE THAI VILLAGE

DSC_0014
Mratibu wa Skylight Band, Lubea akimkaribisha mdau wa bendi hiyo Miryam Kamaliza shot ya Tequila wakati wa show iliyobamba wakazi wa Dar Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki.
DSC_0018
Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 akipiga kilaji cha Tequila kupasha mwili joto kabla ya kupanda jukwaani, kinywaji hicho ni maalum kwa mashabiki wa bendi hiyo pindi wanapoingia kwenye kizingiti cha ukumbi huo wa Thai Village, Masaki jijini Dar.
DSC_0019
Msanii wa Skylight Band Joniko Music (katikati), akifungua dimba la burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo huku akipewa sapoti na Aneth Kushaba AK 47 pamoja na Sam Mapenzi (kulia) wakati show zao za kila Ijumaa ndani ukumbi wa Thai Village Masaki, jijini Dar.
DSC_0115
Aaaah Komando Kipensi weeeeeee… si mwingine ni Le Manager her self Aneth Kushaba AK 47 mutoto ya Kisukuma akifanya yake jukwaani Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar……Tukutane baadae pale kati
DSC_0034
Murembo mupya binti mwenye sauti ya kumtoa Nyoka pangoni, Ashura Kitenge akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar es Salaam Ijumaa iliyopita huku akipewa sapoti na Rapa mkongwe Joniko Flower pamoja na Aneth Kushaba AK47.
DSC_0037
DSC_0126
Mashabiki wa Skylight Band wakijimwaga kwa raha zao.
DSC_0053
Meneja wa Skylight Band, Aneth Kushaba AK47 a.k.a #KomandoKipensi akiwa kwenye hisia kali wakati akitoa burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo (hawapo pichani) Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar.
DSC_0056
Sam Mapenzi akiwapa raha mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) huku akipewa sapoti ya back vocal na Rapa Joniko Flower pamoja na Sony Masamba.
DSC_0068
Daudi Tumba akifanya yake jukwaani kuhakikisha mashabiki wa Skylight Band wanapata ladha nzuri ya muziki wa Live ndani ya kiota cha Thai Village, Masaki jijini Dar Ijumaa iliyopita.

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AENDELEA NA ZIARA UNGUJA KASKAZINI

1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Kikobweni jimbo la Chaani mkoa wa Unguja Kaskazini  akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali ikiwa ni pamoja  kuhimiza uhai wa Chama Cha Mapinduzi mahali ambapo kimelegalega na kuongeza nguvu mahali ambapo kinatekeleza vizuri ilani ya uchaguzi, Katika ziara hiyo Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi. 2 Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akielekea kwenye ukubi wa Mkorea mahali ambapo mkutano wa Halmashauri kuu ya Wilaya ya Unguja Kaskazini umefanyika. 3Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki shughuli za kupanda migomba wakati alipokitembelea kikundi cha akina mama cha  Tuko Imara kinachojishughulisha na shughuli za kilimo cha Migomba, Mbogambona na Mananasi katika kijiji cha  Banda Maji. 4 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai naye akishiriki kupanda migomba wakati  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokitembelea kikundi hicho na kujionea shughuli zao za uzalishaji wa mazao ya kilimo. 5Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya kilimo cha mananasi kutoka kwa Bi Mayasa Abdallah Juma Mwenyekiti wa kikundi cha Tuko Imara wakati alipokitembelea kikundi hicho. 6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika shughuli za kusafisha visiki katika mradi uliobuniwa na wananchi wakisaidiwa na TASAF kwa ajili ya utengenezaji wa barabara inayounganisha kijiji cha Kijini kwa Shauri Pili kwenda katika kijiji cha Kirwa. 7 8Baadhi ya wananchi wakiondoka mara baada ya kufanya kazi ya kusafisha barabara hiyo kwa pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. 9Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akishiriki ujenzi wa nyumba ya madaktari katika kijiji cha Kijini Hospitali jimbo la Matemwe. 10Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifurahia mchezo wa sarakasi uliochezwa na vijana  wa Kijini Hospitali wakati alipotembelea ujenzi wa nyumba wa madaktari katika kijiji hicho 11Baadhi ya viongozi wa timu mbalimbali za jimbo la Nungwi wakiwa na jezi na mipira yao mara baada ya kukabidhiwa kwenye uwanja wa Tazari ambapo pia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alishiriki katika ujenzi wa ukuta wa uwanja huo. 12Mwandishi wa habari kutoka kituo cha televisheni cha Star TV ambaye yuko katika ziara hiyo akishiriki kupiga Dufu katika kijiji cha Banda Maji.  13Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akiwahutubia wananchi wa jimbo la Nungwi katika uwanja wa Skuli mjini Nungwi. 14Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo. 15 16Baadhi ya wanahabari ambao wako katika ziara ya  Katibu Mkuu huyo wakiwa kazini. 17Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Vuai Ali Vuai akitema cheche zake mjini Nungwi. 18 19Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi kwenye uwanja wa Skuli mjini Nungwi. 20Baadhi ya wanachama wapya wa CCM wakila kiapo mara baada ya kukabidhiwa kadi zao za uanachama wa chama hicho. 21Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akiwaaapisha wanachama wapya wa CCM kwenye uwanja wa Skuli mjini Nungwi.

Mpango wa BRN Sekta ya Elimu Unamapungufu – HakiElimu

Kaimu Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia mkutano huo uliofanyika katika ofisi za HakiElimu leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia mkutano huo uliofanyika katika ofisi za HakiElimu leo jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………………………………………..
Na Joachim Mushi
TAASISI ya HakiElimu imeukosoa mpango wa Matokeo Makubwa Sasa ‘Big Results Now’ (BRN) unaotekelezwa na Serikali katika sekta nyeti ikiwemo elimu kwa madai kuwa matokeo yake kwenye sekta ya elimu sio ya kuridhisha.
Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya tathmini ya kitaalamu iliofanywa katika utekelezaji wa BRN kweye sekta ya elimu.
Boniventura alisema Serikali isitumie kigezo cha kuongezeka ufaulu kama ishara tosha ya kuimarika kwa elimu, kwani licha ya ufaulu huu kuonekana kupanda ghafla kuna changamoto nyingi katika sekta ya elimu ambazo bado hazijatatuliwa na juhudi kubwa zinahitajika.
“…Mfano migogoro ya mara kwa mara kati ya walimu na mwajiri, utoro wa walimu, ukosefu wa maabara, vifaa vya kufundishia na tofauti kubwa iliyopo katika gharama za utoaji elimu nchini kati ya shule za serikali na shule za binafsi. Mpango wa BRN ni mzuri lakini muda uliowekwa kutekeleza malengo yake ni mfupi kwa kuzingatia mazingira ya utoaji elimu na changamoto zake,” alisema Boniventura.
Kaimu huyo Mkurugenzi alibainisha kuwa kumekuwepo na mabadiliko ya mara kwa mara katika sekta ya elimu likiwemo la hivi karibuni la alama za ufaulu na mabadiliko ya viwango vya upimaji wa matokeo ya wanafunzi ambayo yameleta mabadiliko katika takwimu za ufaulu lakini yasitumike kama ishara ya kuimarika kwa ubora wa elimu itolewayo.
Aidha aliongeza kuwa matokeo mazuri yoyote ya mipango ya maendeleo ikiwemo elimu yanahitaji uwekezaji wa kutosha, ilhali shule za msingi na sekondari zina changamoto nyingi za upungufu wa miundombinu jambo ambalo linahitaji kufanyiwa kazi kiufasaha zaidi tofauti na inavyofanyika sasa.
“…Serikali haina budi kutafakari na kuona kama uwekezaji uliofanyika mpaka sasa umefanyika kiasi cha kutosha kuleta matokeo kusudiwa. Hali ya uwekezaji kwenye sekta ya elimu si nzuri ambapo asilimia 24 tu ya fedha ya bajeti inapangwa kwenye miradi ya maendeleo inayohusu miundominu ilihali matumizi ya kawaida yakiwa asilimia 74 ya bajeti ya elimu,” alisema.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia mkutano huo uliofanyika katika ofisi za HakiElimu leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia mkutano huo uliofanyika katika ofisi za HakiElimu leo jijini Dar es Salaam.
Akifafanua zaidi alisema sekta ya elimu malengo yaliyopangwa kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja 2013/2014, ni pamoja na;- Kuongeza ufaulu kufikia asilimia 70 mwaka 2014; kutoa ruzuku iliyopangwa kwa kila mwanafunzi, kutoa mafunzo ya uongozi kwa walimu 19,035 kufikia Septemba 2013, lakini kwenye uhalisia hali hairidhishi.
Alisema BRN ilipanga pia kutoa mafunzo kwa waalimu 12,300 juu ya ufundishaji wa KKK, kujenga nyumba za walimu 500 kwa shule za sekondari, kukarabati miundombinu kwa shule 1,200 za sekondari na kuhakikisha kuwa uwino wa mwanafunzi kwa kitabu unashuka kutoka kitabu kimoja kwa wanafunzi watano hadi vitabu sita kwa mwanafunzi mmoja lakini hakuna mafanikio ya kuridhisha.
“…HakiElimu imefanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa BRN katika sekta ya elimu kwa karibu sana na kubaini kuwa hali ya utekelezaji wake bado si ya kuridhisha. Mathalani, BRN ilipanga kuongeza kiwango cha ufaulu kwa shule za sekondari na msingi hadi kufikia asilimia 60 mwaka 2013, na asilimia 70 mwaka 2014.”
“Pamoja na matokeo kuonesha ongezeko la ufaulu, kutoka asilimia 50.6 Mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 58 mwaka 2013 kwa sekondari na kutoka 30.7 mwaka 2012 hadi 50.6 Mwaka 2013 kwa shule za msingi, bado lengo la asilimia 60 halikufikiwa.”
“…Hii inamaanisha lengo la ufaulu kwa sekondari kufikia asilimia 60 kwa mwaka 2013 limefanikiwa kwa asilimia karibu 79 na kwa asilimia 42 tu kwa shule za msingi. Hatahivyo ufaulu wa sekondari si wa kujivunia kwa sababu matokeo ya mtihani wa mwaka 2013 yametumia viwango vipya vya madaraja, na hivyo hatuwezi kusema yametokana moja kwa moja na utekelezaji wa BRN,” alieleza Boniventura kwa wanahabari.
Hata hivyo alishauri ili kutekeleza Matokeo Makubwa Sasa hatuna budi kujifunza toka kwa nchi zilizofanikiwa kutekeleza mipango kama Malaysia kwamba; Matokeo Makubwa Sasa maana yake ni viongozi kufanya tofauti na wafanyavyo sasa, kuwajibika kwa hali ya juu, viongozi kuwa wabunifu, viongozi kupanga mipango na kuitafutia fedha za utekelezaji, viongozi kufanya kazi na kutenda ili kutekeleza ahadi zao ili kupata matokeo ya haraka.
Mwaka 2013 serikali ya Tanzania ilizindua mpango maalumu wa ufuatiliaji utekelezaji wa mipango na utoaji huduma kwa umma unaojulikana kama BRN huku lengo la mpango likiwa kusukuma maendeleo na kuharakisha utekelezaji mipango na kuleta matokeo yaliyokusuduwa upesi.. *Imeandaliwa na www.thehabari.com

Halmashauri ya Wilaya ya Momba yahaidi kuunda Saccoss ya Vijana kwa maendeleo ya Vijana.

unnamed (57)Afisa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga akitoa mada wakati wa semina ya Vijana kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, Ujasiriamali, Stadi za Maisha na Ujuzi jana katika Wilaya ya Momba Mkoa wa Mbeya.
unnamed (58)Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele akitoa mada wakati wa semina ya Vijana kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, Ujasiriamali, Stadi za Maisha na Ujuzi jana katika Wilaya ya Momba Mkoa wa Mbeya.
unnamed (59)Kijana Adam Zacharia Kinyakile wa pili kulia anayeinua vipaji vya vijana na kutengeneza ajira kwa vijana katika fani ya ufundi gereji Mji wa Tunduma Wilaya ya Momba akiwaonyesha maafisa waliomtembelea katika shughuli zake “Mobile Garage” aliyoitengeneza mwenyewe kwa kutumia vyuma chakavu inayoitumia kufanyia kazi za gereji mahali popote anapohitajika. Kushoto ni Mwenzeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamduni na Michezo Bibi Ester Riwa pamoja na timu kutoka Wizara hiyo.
unnamed (60)Afisa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga wa pili kushoto (waliokaa) akizungumza na Vijana wa kikundi cha Matunda Wilaya ya Momba walipowatembelea wakati wa ziara ya kukagua miradi ya Vijana Wilaya ya Momba Mkoa wa Mbeya. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele na wa pili kushoto ni Mwenzeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Ester Riwa.
(Picha zote na Genofeva Matemu – Maelezo. Momba, Mbeya)

INDABA 2015, a platform to optimise African tourism business growth

index
South African Tourism CEO, Mr Thulani Nzima: “Every single INDABA element must give exhibitors an unrivalled and effective platform to showcase their products and services, and to do business. INDABA belongs to them” South African Tourism is working to make sure that INDABA 2015 exceeds the business expectations of both exhibitors and buyers.
South African Tourism Chief Executive Officer, Mr Thulani Nzima says: “INDABA is the single biggest platform for African tourism businesses to come and meet global buyer delegates. This tradeshow attracts the cream and the best cross section of the African tourism and travel trade which in turn, attracts the best buyers in the world to INDABA.”
INDABA 2015 takes place at the Inkosi Albert Luthuli International Convention Centre from 09 to 11 May, 2015.
INDABA Early Bird registrations for exhibitors closed on 30 November 2014. Over 400 exhibitors have confirmed their places on the tradeshow floor. Applications for the INDABA buyer lounge have opened, and registrations are now open for both hosted- and non-hosted buyer applicants. For more information, visit: www.indaba-southafrica.co.za/.
The already very useful online diary system will be refreshed to ensure INDABA 2015 delivers an optimal number of exhibitor and buyer connections. INDABA 2014 saw increased use of the matchmaking system, with 4.4 meetings per participant scheduled as opposed to 3.3 meetings per participant in 2013. In 2015, there will be better matching of exhibitor offerings to the individual business interests of buyers. The system will also incorporate search filters to help exhibitors easily and quickly identify buyers of most relevance to them.
Nzima also says: “Every single element of INDABA will give exhibitors an unrivalled and effective platform to showcase their products and services, and to do business. There would be no INDABA if it were not for the exhibitors, and the larger African and South African travel and tourism trade. INDABA belongs to them. This is the biggest team of African trade exhibitors in the world who come to Durban each year to do business.”
For more information: www.indaba-southafrica.co.za/

BALOZI SEIF ASHIRIKI HARAMBEE CHUO CHA CBE, AKUSANYA MILIONI 540.8.

 unnamed (50) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akikabidhi mchango wake wa shilingi milioni 3 kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uongozi ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Prof. Mathew Luhanga (katikati) kusaidia uboreshaji wa miundombinu ya chuo hicho jana usiku wakati wa harambee  maalum ya ukusanyaji wa fedha iliyofanyika  Hotel ya Serena jijini Dar es salamm.Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho Prof. Emanuel Mjema.Picha na Aron Msigwa – MAELEZO. unnamed (51)Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd na viongozi wa Chuo cha CBE wakitoa mkono wa shukrani kwa wadau mbalimbali waliotoa michango yao wakati wa harambee ya kuchangia maendeleo ya chuo cha CBE jana usiku jijini Dar es salaam wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya chuo hicho .
unnamed (52)Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akisoma majumuisho ya michango na ahadi zilizotolewa na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee ya kuchangia maendeleo ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) jana usiku jijini Dar es salaam. Kiasi cha shilingi milioni mia tano arobaini, laki nane na elfu ishrini na tisa (540,829,000/=) zikiwa ni ahadi na fedha taslimu zilikusanywa.
unnamed (53)Baadhi ya wadau wa maendeleo wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) wakitoa ahadi na michango mbalimbali kusaidia maendeleo ya chuo hicho jana usiku wakati wa chakula cha hisani cha miaka 50 ya CBE kilichoandaliwa na uongozi wa chuo hicho kusaidia ukusanyaji wa fedha za ujenzi wa miundombinu,vyumba vya mihadhara na madarasa vya chuo hicho.
unnamed (54)Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd na viongozi wa Chuo cha CBE wakitoa mkono wa shukrani kwa wadau mbalimbali waliotoa michango yao wakati wa harambee ya kuchangia maendeleo ya chuo cha CBE jana usiku jijini Dar es salaam wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya chuo hicho .

FURAHA YA UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA KUNGANISHA CHAMA CHA SPLM CHA SUDANI KUSINI JIJINI ARUSHA

unnamed (49)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Naibu Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa (kulia) na Bw. Bw. Deng Alor Kuol wakifurahia wakati Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (wa pili kushoto) na Makamu waRais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeanamikono na kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wamakubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusinikatika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015usiku.PICHA NA IKULU
………………………………………………………………………………
MKATABA wa kujenga tena umoja na kukiunganisha upya Chama Tawala cha Sudan Kusini cha Sudan People’s Liberation Movement (SPLM) ulitiwa saini usiku wa jana, Jumatano, Januari 22, 2015, katika sherehe ya kufana iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Ngurdoto, Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha. Mkataba huo unaojulikana kama Agreement on the Re-unification of Sudan People’s Liberation Movement umepongezwa kuwa ni hatua muhimu katika kulitoa taifa changa la Sudan Kusini katika hali ya machafuko, vita vya wenyewe kwa wenyewe, kutoelewana na kutoaminiana, mambo ambayo yameligubika taifa hilo tokea mwishoni mwa 2013 wakati kutokuelewana kulipozuka ndani ya SPLM na hatimaye katika Serikali ya nchi hiyo. Baada ya siku nzima ya mawasiliano na majadiliano baina ya pande zinazovutana ndani ya chama hicho pamoja na viongozi wa nchi jirani na rafiki na Sudan Kusini, viongozi watatu wa vikundi vinavyopingana ndani ya SPLM walitia saini Mkataba huo muhimu sana. Viongozi waliotia saini ni Mheshimiwa Salva Kiir Mayardit, Rais wa Sudan Kusini ambaye pia ni Mwenyekiti wa SPLM na anayeongoza kundi linalojulikana kama SPLM in Government (SPLM-IG), Mheshimiwa Dkt. Riek Machar ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa SPLM na pia aliyekuwa Makamu wa Rais wa Sudan Kusini anayeongoza kundi la SPLM in Opposition (SPLM-IO) na Dkt. Deng Alor Kuol ambaye anaongoza kundi la SPLM Leaders- Former Detainees (SPLM Leaders – FD). Sherehe hiyo ilishuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndicho kimesimamia mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo. Rais Kikwete pia ndiye mdhamini mkuu wa Mkataba huo. Wengine walioshuhudia tukio hilo muhimu ni Rais wa Uganda, Mheshimiwa Jenerali Yoweri Kaguta Museveni; Rais Uhuru Muigai Kenyatta wa Kenya; Naibu wa Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa, Makamu Mwenyekiti wa zamani wa CCM Mheshimiwa John Samwel Malecela ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo na Katibu Mkuu wa CCM Mheshimiwa Abdulrahman Kinana ambaye alikuwa mwezeshaji wa mazungumzo. Mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo yalianza mwishoni mwa mwaka jana baada ya Rais Kikwete na Chama cha CCM kuombwa na Rais Kiir Mayardit kukubali chama hicho tawala cha Tanzania kutumia uzoefu na ujuzi wake wa miaka mingi wa uongozi na siasa kujaribu kuleta suluhu ndani ya SPLM. Mazungumzo hayo ya kutafuta suluhu ambayo yamefanyika kwa awamu mbili, ya kwanza yakiwa yamefanyika Oktoba mwaka jana na pili yakiwa yameanza mwanzoni mwa mwezi huu, Januari 2015, yameongeza thamani kwenye mazungumzo mengine yanayofanyika Addis Ababa, Ethiopia chini ya usimamizi wa taasisi ya IGAD na yanayojadili jinsi ya kurejesha amani nchini humo. Viongozi wa SPLM wanaamini kuwa kwa sababu mgogoro wa kisiasa nchini mwao ulianzia ndani ya chama hicho na kwa sababu SPLM ndicho chombo pekee ambacho kinawaunganisha wananchi wote wa Sudan Kusini, basi busara inaelekeza kuwa suluhu ianze kutafutwa ndani ya chama hicho. Mkataba wa jana, kimsingi, unalenga kuweka mazingira ya kujenga utulivu, maelewano, amani na umoja wa kudumu ndani ya chama hicho na nchini humo kwa kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mambo ya msingi yaliyokubaliwa kuhusu shughuli za siasa, uongozi na oganisheni ya chama hicho yanafanyika bila kukawia. Mkataba huo pia unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinabuni na kutekeleza sera za kuondokana na ukabila, makundi yenye mitazamo finyu na mwenendo wa kijeshi katika siasa za Sudan Kusini. Aidha, Mkataba huo unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinafanya mageuzi ya kuanza kujenga utamaduni wa kuvumiliana na ujenzi wa misingi ya demokrasia. Mkataba huo pia unataka watu wote ambao walishiriki katika mauaji na umwagaji damu katika vita vya wenyewe kwa wenyewe wasiruhusiwe kugombea wala kushika nafasi ya uongozi wa umma ndani ya chama hicho. Pia viongozi wote wa Sudan Kusini wanatakiwa, chini ya Mkataba huo, kuwaomba radhi wananchi wa nchi hiyo ya Sudan Kusini kwa kuruhusu nchi hiyo kuingia katika machafuko ya umwagaji damu mkubwa. Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu – Dar es Salaam. 22 Januari,2015

UTIAJI SAINI MKATABA WA MAKUBALIANO YA KUKIUNGANISHA CHAMA CHA SPLM CHA SUDAN KUSINI JIJINI ARUSHA

unnamed (42) Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Salva Kiir Mayardiy wa
Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek
Machar Teny (wa pili kulia) na Bw. Deng Alor Kuol wakitia saini
mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha
Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari
21, 2015 usiku. Nyuma yao ni mjane wa marehemu John Garang aliyekuwa
Mwenyekiti wa SPLM Mama Rebecca Nyandeng de Mabior na Afisa wa Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. Thobias Makoba. Nyuma
yao wakishuhudia utiaji saini huo ni Makamu wwa Rais Dkt Mohamed
Ghalib Bilali, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Rais Yoweri Museveni wa
Uganda
unnamed (43) Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Salva Kiir Mayardiy wa
Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek
Machar Teny (wa pili kulia) na Bw. Deng Alor Kuol wakionesha hati
baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha upya
chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini
Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
unnamed (44) Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa pongezi kwa Rais Salva Kiir
Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa
Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) na Bw. Deng Alor Kuol
baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha upya
chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini
Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
unnamed (45) Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wakati  Rais Salva
Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani
wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na
kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya
kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya
Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
unnamed (46) Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wakati  Rais Salva
Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani
wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na
kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya
kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya
Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
unnamed (47) Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu
wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny wakipeana mikono kwa
furaha baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha
upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini
Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
unnamed (48)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Bw Deng Alor Kuol wakifurahia wakati Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
PICHA NA IKULU