TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 23, 2015

MAMA GRACIA MACHEL AKUTANA NA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO, MHE. SOPHIA M. SIMBA

unnamed (37)Mke wa aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini Bi. Gracia Machel akiwa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Sophia M. Simba (Mb) alipofika kutambulisha progamu ya ulinzi wa watoto kwa Mhe. Simba jijini Dar es salaam, tarehe 21/1/2015.
unnamed (38)Mke wa aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini Bi. Gracia Machel akiwa na mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Sophia M. Simba (Mb), na Katibu Mkuu Bibi Nuru M. Millao (wa pili kulia) na baadhi ya wakurugenzi wa Wizara.
………………………………………………………………………………
By: Erasto T. Ching’oro- Msemaji wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia an Watoto
  Mke wa aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini (Bi Gracia Machel) yuko katika ziara fupi nchini Tanzania kusaidia kuhimiza Serikali na wadau kutokomeza tatizo la ndoa za utotoni hapa nchini kupitia programu na miradi mbalimbali atakayoifadhili ili kuwawezesha watoto wa kike kupata haki ya elimu ambayo ni nyenzo muhimu katika kujikomboa dhidi ya umaskini. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Wizara ya Maendeleo ya Jmaii, Jinsia Na Watoto, jana tarehe 21 Machi, 2015; Mama Machel aliipongeza Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya jamii, Jinsia na watoto kwa jitihada zake kubwa inazozifanya kupambana na tatizo la mimba na ndoa za utotoni. Aidha, ameshauri Wizara, asasi za kiraia na wadau mbalimbali hususan viongozi wa mila/jadi na dini kushirikiana naye na kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya kupitia programu hizo anazotarajia kuzianzisha. Alifafanua kuwa mkoa wa Mara ndio utakaokuwa wa kwanza kunufaika na uanzishwaji wa programu hiyo kwani mkoa huo ni miongoni mwa mikoa iliyo na mila gandamizi dhidi ya wasichana na wanawake; na ukiwepo mfumo dume. Akitoa akimshukuru Bi. Machel kwa jitihada zake za dhati anazozifanya, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mheshimiwa Sophia Simba (Mb) amesema ni kweli tatizo hilo lipo nchini lakini Serikali kwa kushirikiana na wadau wa haki za watoto yakiwapo mashirika yasiyo ya Kiserikali, asasi za kiraia na vyombo vya habari kwa pamoja wanashirikiana kupambana kikamilifu na tatizo hili kupitia mipango shirikishi jamii ili kufikia ufumbuzi endelevu.

No comments:

Post a Comment