Mke
 wa aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini Bi. Gracia Machel akiwa na Waziri
 wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Sophia M. Simba (Mb) 
alipofika kutambulisha progamu ya ulinzi wa watoto kwa Mhe. Simba jijini
 Dar es salaam, tarehe 21/1/2015.
Mke
 wa aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini Bi. Gracia Machel akiwa na 
mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Sophia
 M. Simba (Mb), na Katibu Mkuu Bibi Nuru M. Millao (wa pili kulia) na 
baadhi ya wakurugenzi wa Wizara. 
………………………………………………………………………………
By: Erasto T. Ching’oro- Msemaji wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia an Watoto
 
Mke wa aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini (Bi Gracia Machel) 
yuko katika ziara fupi nchini Tanzania kusaidia kuhimiza Serikali na 
wadau kutokomeza tatizo la ndoa za utotoni hapa nchini kupitia programu 
na miradi mbalimbali atakayoifadhili ili kuwawezesha watoto wa kike 
kupata haki ya elimu ambayo ni nyenzo muhimu katika kujikomboa dhidi ya 
umaskini.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Wizara ya Maendeleo ya 
Jmaii, Jinsia Na Watoto, jana tarehe 21 Machi, 2015; Mama Machel 
aliipongeza Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya jamii, 
Jinsia na watoto kwa jitihada zake kubwa inazozifanya kupambana na 
tatizo la mimba na ndoa za utotoni. Aidha, ameshauri Wizara, asasi za 
kiraia na wadau mbalimbali hususan viongozi wa mila/jadi na dini 
kushirikiana naye na kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko 
chanya kupitia programu hizo anazotarajia kuzianzisha. Alifafanua kuwa 
mkoa wa Mara ndio utakaokuwa wa kwanza kunufaika na uanzishwaji wa 
programu hiyo kwani mkoa huo ni miongoni mwa mikoa iliyo na mila 
gandamizi dhidi ya wasichana na wanawake; na ukiwepo mfumo dume.
Akitoa akimshukuru Bi. Machel kwa jitihada zake za dhati 
anazozifanya, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mheshimiwa
 Sophia Simba (Mb) amesema ni kweli tatizo hilo lipo nchini lakini 
Serikali kwa kushirikiana na wadau wa haki za watoto yakiwapo mashirika 
yasiyo ya Kiserikali, asasi za kiraia na vyombo vya habari kwa pamoja 
wanashirikiana kupambana kikamilifu na tatizo hili kupitia mipango 
shirikishi jamii ili kufikia ufumbuzi endelevu. 
No comments:
Post a Comment