Mahmoud Ahmad Arusha
Watu wenye ulemavu nchini wameiomba serikali na taasisi binafsi 
zinazotoa huduma za kijamii ikiwemo hospitali,benki na shule kuhakikisha
 kuwa wanaweka miundombinu rafiki itakayowawezesha kuzifikia huduma hizo
 kwa urahisi.
Katibu wa Shirikisho la Vyama vya 
watu wenye Ulemavu Arusha ,Yunusi Urasa amesema kuwa kumekua na tatizo 
la la kukosekana kwa miundombinu rafiki kwa walemavu hali 
inayowakwamisha kupata huduma hizo muhimu kutokana na ulemavu walionao.
Yunusi aliyasema hayo jana katika 
semina ya watu wenye ulemavu iliyofanyika jijini Arusha na kuandaliwa na
 Shirikisho la Vyama vya watu wenye ulemavu nchini ,ambapo amesema kuwa 
amehimiza serikali kuwakumbuka walemavu katika upangaji wa miji,ujenzi 
wa barabara na majengo ili waweze kupata haki zao za msingi za kunufaika
 na huduma za jamii.
Katibu huyo amependekeza kuwepo 
kwa dawati maalumu la kuwahudumia watu wenye mahitaji maalumu 
litakalowasaidia walemavu kupata huduma kwa urahisi.
“Mlemavu asiyeona akienda benki 
hawezi kutumia ATM card ni rahisi kuibiwa akikutana na mtu ambaye si 
mwaminifu,pegine zitengenezwe ambazo wataweza kuzisoma pia ATM ziko juu 
kwa walemavu wanaotambaa ni vigumu kuzifikia” Alisema Yunusi
Naye Katibu wa Chama cha Watu 
wenye ulemavu wa ngozi Arusha Happiness Raphael amesema kuwa 
wanashangazwa kuona mauaji ya albino yanaendelea huku mashirika ya haki 
za binadamu ya kimataifa yakikaa kimya hivyo ameiataka jamii ya 
kimataifa kuchukua hatua kukomesha vitendo hivyo.
Mratibu wa Shirikisho la Watu 
wenye Ulemavu nchini Francis Mhina amesema kuwa wanafanya juhudi za 
kutoa elimu kwa walemavu juu haki zao za msingi na namna ambayo wanaweza
 kujikwamua kimaisha ,ameeleza kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni 
uhaba wa fedha hivyo kushindwa kuwafikia walemavu wengi ambao wako 
vijijini na kuishia mijini.
No comments:
Post a Comment