
 Kaimu
 Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na 
waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia 
ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.

 Kaimu
 Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na 
waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia 
ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.

 Kaimu
 Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura (katikati) akizungumza na 
waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wengine kushoto na kulia 
ni maofisa wa taasisi ya HakiElimu wakiwa katika mkutano huo.

 Baadhi
 ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia
 mkutano huo uliofanyika katika ofisi za HakiElimu leo jijini Dar es 
Salaam.
………………………………………………………………………………………..
Na Joachim Mushi
TAASISI ya HakiElimu imeukosoa 
mpango wa Matokeo Makubwa Sasa ‘Big Results Now’ (BRN) unaotekelezwa na 
Serikali katika sekta nyeti ikiwemo elimu kwa madai kuwa matokeo yake 
kwenye sekta ya elimu sio ya kuridhisha.
Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu 
Mkurugenzi wa HakiElimu, Godfrey Boniventura alipokuwa akizungumza na 
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya tathmini ya kitaalamu 
iliofanywa katika utekelezaji wa BRN kweye sekta ya elimu.
Boniventura alisema Serikali 
isitumie kigezo cha kuongezeka ufaulu kama ishara tosha ya kuimarika kwa
 elimu, kwani licha ya ufaulu huu kuonekana kupanda ghafla kuna 
changamoto nyingi katika sekta ya elimu ambazo bado hazijatatuliwa na 
juhudi kubwa zinahitajika.
“…Mfano migogoro ya mara kwa mara 
kati ya walimu na mwajiri, utoro wa walimu, ukosefu wa maabara, vifaa 
vya kufundishia na tofauti kubwa iliyopo katika gharama za utoaji elimu 
nchini kati ya shule za serikali na shule za binafsi. Mpango wa BRN ni 
mzuri lakini muda uliowekwa kutekeleza malengo yake ni mfupi kwa 
kuzingatia mazingira ya utoaji elimu na changamoto zake,” alisema 
Boniventura.
Kaimu huyo Mkurugenzi alibainisha 
kuwa kumekuwepo na mabadiliko ya mara kwa mara katika sekta ya elimu 
likiwemo la hivi karibuni la alama za ufaulu na mabadiliko ya viwango 
vya upimaji wa matokeo ya wanafunzi ambayo yameleta mabadiliko katika 
takwimu za ufaulu lakini yasitumike kama ishara ya kuimarika kwa ubora 
wa elimu itolewayo.
Aidha aliongeza kuwa matokeo 
mazuri yoyote ya mipango ya maendeleo ikiwemo elimu yanahitaji uwekezaji
 wa kutosha, ilhali shule za msingi na sekondari zina changamoto nyingi 
za upungufu wa miundombinu jambo ambalo linahitaji kufanyiwa kazi 
kiufasaha zaidi tofauti na inavyofanyika sasa.
“…Serikali haina budi kutafakari 
na kuona kama uwekezaji uliofanyika mpaka sasa umefanyika kiasi cha 
kutosha kuleta matokeo kusudiwa. Hali ya uwekezaji kwenye sekta ya elimu
 si nzuri ambapo asilimia 24 tu ya fedha ya bajeti inapangwa kwenye 
miradi ya maendeleo inayohusu miundominu ilihali matumizi ya kawaida 
yakiwa asilimia 74 ya bajeti ya elimu,” alisema.

 Baadhi
 ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia
 mkutano huo uliofanyika katika ofisi za HakiElimu leo jijini Dar es 
Salaam.
Akifafanua zaidi alisema sekta ya 
elimu malengo yaliyopangwa kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja 
2013/2014, ni pamoja na;- Kuongeza ufaulu kufikia asilimia 70 mwaka 
2014; kutoa ruzuku iliyopangwa kwa kila mwanafunzi, kutoa mafunzo ya 
uongozi kwa walimu 19,035 kufikia Septemba 2013, lakini kwenye uhalisia 
hali hairidhishi.
Alisema BRN ilipanga pia kutoa 
mafunzo kwa waalimu 12,300 juu ya ufundishaji wa KKK, kujenga nyumba za 
walimu 500 kwa shule za sekondari, kukarabati miundombinu kwa shule 
1,200 za sekondari na kuhakikisha kuwa uwino wa mwanafunzi kwa kitabu 
unashuka kutoka kitabu kimoja kwa wanafunzi watano hadi vitabu sita kwa 
mwanafunzi mmoja lakini hakuna mafanikio ya kuridhisha.
“…HakiElimu imefanya ufuatiliaji 
wa utekelezaji wa BRN katika sekta ya elimu kwa karibu sana na kubaini 
kuwa hali ya utekelezaji wake bado si ya kuridhisha.
 Mathalani, BRN ilipanga kuongeza kiwango cha ufaulu kwa shule 
za sekondari na msingi hadi kufikia asilimia 60 mwaka 2013, na asilimia 
70 mwaka 2014.”
“Pamoja na matokeo kuonesha 
ongezeko la ufaulu, kutoka asilimia 50.6 Mwaka 2012 hadi kufikia 
asilimia 58 mwaka 2013 kwa sekondari na kutoka 30.7 mwaka 2012 hadi 50.6
 Mwaka 2013 kwa shule za msingi, bado lengo la asilimia 60 
halikufikiwa.”
“…Hii inamaanisha lengo la ufaulu 
kwa sekondari kufikia asilimia 60 kwa mwaka 2013 limefanikiwa kwa 
asilimia karibu 79 na kwa asilimia 42 tu kwa shule za msingi. Hatahivyo 
ufaulu wa sekondari si wa kujivunia kwa sababu matokeo ya mtihani wa 
mwaka 2013 yametumia viwango vipya vya madaraja, na hivyo hatuwezi 
kusema yametokana moja kwa moja na utekelezaji wa BRN,” alieleza 
Boniventura kwa wanahabari.
Hata hivyo alishauri ili 
kutekeleza Matokeo Makubwa Sasa hatuna budi kujifunza toka kwa nchi 
zilizofanikiwa kutekeleza mipango kama Malaysia kwamba; Matokeo Makubwa 
Sasa maana yake ni viongozi kufanya tofauti na wafanyavyo sasa, 
kuwajibika kwa hali ya juu, viongozi kuwa wabunifu, viongozi kupanga 
mipango na kuitafutia fedha za utekelezaji, viongozi kufanya kazi na 
kutenda ili kutekeleza ahadi zao ili kupata matokeo ya haraka.
Mwaka 2013 serikali ya Tanzania 
ilizindua mpango maalumu wa ufuatiliaji utekelezaji wa mipango na utoaji
 huduma kwa umma unaojulikana kama BRN huku lengo la mpango likiwa 
kusukuma maendeleo na kuharakisha utekelezaji mipango na kuleta matokeo 
yaliyokusuduwa upesi..
 *Imeandaliwa na www.thehabari.com
No comments:
Post a Comment