Mkuu wa mkoa wa Arusha Daud Ntibenda
 ameamua kutoa kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu huria cha 
Arusha baada ya kutoridhishwa na majngo ya chuo hicho na kudai kuwa 
hayana hadhi ya chuo hicho na kuwa yanaonekana kama nyumba ya mtumishi 
wa serikali kuishi.
Pia mkuu huyo ametoa siku 30 kwa 
Afisa Ardhi wa mkoa huo kutafuata kiwanja kwa ajili ya kuanza ujenzi 
rasmi wa chuo ambacho kitakuwa na hadhi ya kuitwa chuo Kikuu.
Aliyasema hayo wakati alipofanya 
ziara ya kukitembelea na kuonana na wafanyakazi na kufanya nao maongezi 
pamoja na wahitimu wa chuo hicho kwenye mahafali ya 26 chuo hapa jijini 
hapa.
Ntibenda alisema kuwa majengo hayo ya chuo yamemsikitisha kiasi 
cha kutoa machozi hali ambayo inatakiwa kupatiwa ufumbuzi ndani ya mwezi
 mmoja ilikuongeza umaridadi wa elimu inayotolewa chuoni hapo.
“Kweli kabisa mimi kama mkuu wa 
mkoa ambaye raisi ameniona nafaa kuongoza mkoa huu sintakubali kuona eti
 wanafunzi hata kama ni wa vyuo huria wanasoma katika majengo kama haya 
badala yake nitahakikisha kuwa wanahama hapa na mnapata majengo mazuri 
na ni haki yenu ninyi wanafunzi”aliongeza Ntibenda
Alifafanua kuwa chuo hicho hasa 
masomo huria kinapokuwa na majengo mazuri kinasaidia wanafunzi kuweza 
kupata hamasa kubwa katika masomo lakini kinapokuwa na majengo ambayo 
hayana hadhi ya chuo basi hayapendezi wala kuvutia katika mazingira ya 
masomo.
“Pamoja na kuwa mmesoma na matokeo
 yenu ni mazuri sana tena ya kupigiwa mfano mimi nasema bado 
kunauwezekano wa kufanya chuo hichi kikawa bora ni kwamba sote sisi 
tukiungana na tuwe kimoja”aliongeza Ntibenda
Katika hatua Nyingine katibu wa 
chama cha wanafunzi wa chuo kikuu huria Kasimu Mfinanga alisema kuwa 
mapendekezo ya chuo hicho ni pamoja na kusogeza huduma ya elimu karibu 
zaidi na wananchi hasa wale wa vijini lakini hata kwenye Wilaya Zote.
Mfinanga alimaliza kwa kusema kuwa mapendekezo mengine ni pamoja
 na kuendelea kuelimisha jamii umuhimu wa kujiunga nacho kwani amendeleo
 thabiti hayapatikani bila ya kuwa na elimu.
No comments:
Post a Comment