TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 21, 2015

Muziki wa Bongo Dansi wageuka mzimu na kuwapeleka puta washabiki barani Ulaya

ngoma
Imebainika kuwa bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band aka FFU-ughaibuni almaarufu viumbe wa ajabu Anunnaki Alien,inayoongoza na mwanamuziki Ebrahim Makunja aka kamanda Ras Makunja,bendi hiyo imejikuta ipo katika hali ya kukosa usingizi tena baada ya kutakiwa kutumbuiza maomyesho zaidi katika msimu ujao wa joto.
Watayarishaji wa maonyesho makub
wa ya nje barani Ulaya wanashinikizwa na washabiki wao lazima waipandishe jukwaani Ngoma Africa Band kutokana na mdundo wao Bongo dansi,maporota hao baada kuwekwa roho juu na washabiki wao nao wamedhamiria kuwapambanisha washabiki hao na bendi hiyo yenye makao yake nchini Ujerumani,habari za uhakika zimetonya kuwa bendi hiyo imekubali kuenda kutumbuiza katika nchi za Latvia na Austria na maonyesho mengine katika msimu wa joto.
Habari zimetonya kuwa hali hiyo inatokana na tabia za washabiki kushinikiza bendi ya Ngoma Africa  kuwepo katika ratiba ya  mzunguko wa maonyesho makubwa pamoja na  wanamuziki hao kukosa muda wa kupumzika.
Hata hivyo  inasemekana kamanda Ras Makunja na kikosi chake wanauwezo wa aina yake wa kuwamudu ratiba hiyo ngumu na kuwaburudisha washabiki wao waliodata akili na jinamizi la muziki wa dansi wa bongo kule barani ulaya.Ffu-Ughaibuni pia wanasikika online at www.ngoma-africa.com

No comments:

Post a Comment