TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, November 27, 2014

TUME YA MIPANGO YATEMBELEA BANDARI YA MBABA BAY

 Baadhi ya wajumbe wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiingia kwenye gati la Bandari ya Mbaba Bay iliyopo wilayani Nyasa mkoani Ruvuma.
 Mratibu wa shughuli za ukaguzi wa miradi ya maendeleo, Bw. Senya Tuni (Wapili kulia) akieleza jambo mara walipoingia kwenye eneo la gati la Bandari ya Mbaba Bay. Wanaomsikiliza ni Mkuu wa msafara huo, Bibi Florence Mwanri (Kulia), Afisa mazingira wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bw. Julius Edward (Watatu kulia). Na kushoto ni Bw. Jordan Matonya ambae ni Mchumi kutoka Tume ya Mipango.
 Afisa bandari ya Mbaba Bay, Bw. Jarome Urio (Wapili kushoto) akitoa maelezo kwa wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipofanya ziara kwenye bandari hiyo. Timu hiyo iliongozwa na Bibi Florence Mwanri (Kushoto).
 Kiongozi wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence kushoto akionesha kitu kwenye sehemu ya gati la Bandari ya Mbaba Bay (halionekani).
 Baadhi ya vijana wa Mbaba Bay wakijivinjari kwenye fukwe za Ziwa Nyasa.
 Afisa bandari ya Mbaba Bay, Bw. Jarome Urio (Watatu kushoto) akionesha sehemu ya gati iliyoofanyiwa matengenezo.
Baadhi ya utajiri unaopatikana kwenye Ziwa Nyasa. Dagaa wa Ziwa hili ni maarufu kwa utajiri wake wa lishe. Kwa mujibu wa wakazi wa Mbaba Bay, dagaa hao uuzwa hadi nje ya nchi.
=============================================

Na:Saidi Mkabakuli, Mbaba Bay

Timu wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Tume ya Mipango imetembelea Bandari ya kimkakati ya Mbaba Bay iliyopo wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Bandari hiyo.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, kiongozi wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri alisema kwamba Bandari hiyo ni muhimu kwa uchumi wa nchi kwa kuzingatia eneo la kijiografia la bandari hiyo.
“Bandari hii ni muhimu kwani kijiografia inaweza kuzifikia nchini nyingi zilizo kusini mwa nchi yetu hivyo inaweza kutumika kama lango la kibiashara miongoni mwa jirani zetu licha ya uhaba wa miundombinu yake,” alisema.
Aliwasihi wafanyakazi wanaoihudumia Bandari hiyo kufanya kazi kwa bidii bila ya kuchoka ili kuweza kuvutia wafanyabiashara na watumiaji wengine kuendelea kuitumia bandari hiyo.
Kwa upande wake, afisa bandari ya Mbaba Bay, Bw. Jarome Urio aliutaarifu ugeni huo kuwa Mamlaka ya Bandari ipo katika mkakati wa kuindeleza bandari hiyo ili kuweza kuihudumia wateja wengi zaidi.
Pia, Bw. Urio aliwashukuru wajumbe wa timu hiyo ya ukaguzi kwa kwenda kuitembelea na kujionea maendeleo ya bandari hiyo.
“Tunafarijika sana kuona viongozi wa serikali wanapokuja kututembelea kwani hali hii uongeza hamasa ya utendaji kazi wetu,” alisema.
Kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/2012 – 2015/2016) bandari ni mojawapo ya vipaumbele vitano vya kimkakati vyenye lengo la kufungulia fursa za ukuaji uchumi wa nchi ili kuweka misingi wa uchumi kwa watu walio wengi. 
Vipaumbele vingine ni Kilimo ambapo lengo kuu likiwa ni kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya kilimo ili kujitosheleza kwa chakula na kuwa na ziada ya kuuza nje ya nchi; Maendeleo ya viwanda: Msisitizo umewekwa katika kuvutia, kuanzishwa na kuendeleza viwanda vinavyotumia malighafi zinazopatikana nchini (kama vile viwanda vya nguo, mbolea, saruji, makaa ya mawe, chuma na bidhaa za chuma) na pia sekta ya madini kwa lengo la kuongeza mapato ya Serikali.
Pamoja na kipaumbele cha Maendeleo ya rasilimali watu na ujuzi: Mpango unahimiza kuwekeza katika elimu (hasa katika elimu ya juu na vyuo vya ufundi) na huduma za afya (kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma) katika kujenga nguvu kazi itakayotuletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii; na Utalii, Biashara, na huduma za Fedha ambapo jitihada zimewekwa kwenye uendelezaji uwezo wa kuuza katika masoko ya ndani na nje, kuongeza   idadi ya watalii na matumizi yao wawapo nchini, na kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha.

NACTE INTER COLLEGE TANZANIA- DAR ES SALAAM BONANZA

index
Kampuni ya Miss Demokrasia Tanzania & Entertainment C.o Ltd kwa kushirikiana na kituo bora cha Matangazo TIMES FM 100.5 kwa pamoja wanakuletea bonanza la vyuo SEASON TWO itakayofantika katika viwanja vya ustawi wa jamii kijitonyama siku ya jumamosi wiki hii tarehe 29/11/2014. Vyuo mbalimbali vya NACTE mkoa wa dar es salaam, vinatarajia kuchuana katika bonanza la hilo litakalokuwa na michezo ya soka, Basketball, Voleyball na netball, ikiwa ni sehemu ya pili ya mchujo wa kutafuta timu zitakazoshiriki ligi ya NACTE Tanzania katika msimu wa 2014/2015,baada ya sehemu ya kwanza kumalizika kwenye chuo cha DIT Mwishoni mwa juma na kuhusisha vyuo mbali mbali vya Dar es salaam.
Sehemu ya pili ambayo imepangwa kufanyika katika uwanja wa ustawi wa jamii kijitonyama jumamosi ya tarehe 29 mwezi huu inatarajia kuwa ya kusisimua kutokana na Michuano hii ya Mtoano kuwa kivutio kwa Wachezaji na Mashabiki ambao wengi wao ni wanafunzi kutoka vyuo mbali mbali wanaofika kushuhudia michuano hiyo inayoendeshwa kwa ubunifu wa hali ya juu. Timu zinazochuana juma hili ni pamoja na Institute of Adult Education, Institute of Social Work (ISW) – DSM, Lugalo Military Medical School – Dsm, St. Joseph College (University), Dar es salaam City College (DACICO, Dar-es-Salaam School of Journalism (DSJ) – DSM, National Institute of Transport (NIT) – DSM, Bandari College – DSM,huku timu mwalikwa ikiwa ni Timu ya wafanyakazi wa PPF Dsm.
Timu zilizofanikiwa kuingia hatua ya pili wiki iliyopita kwa upande wa soka ni Chuo cha IFM waliofanikiwa kuwafunga DIT katika fainali kwa njia ya penalt baada ya timu hizo kumaliza dakika 90 bika kufungana, kabla ya kutinga hatua hiyo ya fainali kikosi cha IFM kilifanikiwa kuwafunga CBE katika mchezo wa kwanza kwa 2-1 wafungaji wa magoli wakiwa ni Godlisten Kessy aliyepachika mabao yote mawili dakika ya 15 kipindi cha kwanza na dakika 51 kipindi cha pili huku bao la CBE likiwekwa wavuni na Mwendo Sitena mchezo uliochezeshwa na mwamuzi Mussa Charles. Wakati DIT wakafanikwa kutinga fainali baada ya kuwafunga Muhimbili kwa bao 1-0, TRA ikaambulia kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Times, wakati Voleyball wanaume CBE waliibuka kidedea dhidi ya wenyeji DIT, huku David Davic akiibuka (Best Spiker), Dickison Benjamini wa DTI, aliibuka (Best Broker), Gideon Joseph wa IFM aliibuka (Best Recever), Joseph Mafuru wa CBE aliibuka (Best Seter), Daniel Msambusi wa DIT aliibuka (Best Rebelo), na MVP katika ufunguzi huo akiwa ni nyota wa CBE Samweli Kitime. Kwa upande wa mpira wa mikono netball pia IFM ilijidhiilisha kuwa kijoo cha mjini baada ya kufuata nyayo za kaka zao kwa kuwafunga chuo cha DIT kwa 19 dhidi ya 14 huku wafungaji katika mchezo huo wakiwa ni Sarah Shaaban aliyefunga magoli 12(GS) na Teckila teas akifunga 7 (GA) katika mchezo wa Fainali pia uliofanyika kwenye viwanja vya DIT. CBE pia ilimg’ara katika mchezo wa Kikapu (Basketball) kwa upande wa wanaume baada ya kuwafunga DIT katika mchezo wa Fainali kwa vikapu 51-37 ambapo wahezaji waliong’ara ni Sarehe Ramadhani, Evance David, Edger Mwakase huku kwa DIT waking’ara wachezaji Evance Kamola na Charles Poul. Michuano hiyo ya NACTE INTER COLLEGE TANZANIA imeanza siku ya jumamosi tarehe 22/11/2014 ikiwa ni ufunguzi ambapo vyuo vilivyohusika katika ufunguzi huo ni pamoja na IFM, DIT, TRA, MUHIMBILI, CBE, ROYAL, MLIMANI Profesianal na timu Mwalikwa Times Fm 100.5. Aidha vyuo vyote vinavyohusika na michezo ya wiki hii zimetakiwa kuwahi Viwanjani ili kukamilisha taratibu za ukaguzi kabla ya michuano hiyo ya mtoano kuanza na ikumbukwe kwamba michuano hiyo inaendeshwa kwa mfumo wa Bonanza na inafanyika kila siku za jumamosi kutokana na wanafunzi kuwa masomoni katika siku za kawaida. kila mwaka michuano hii itakuwa ikifanyika kwa kushirikisha vyuo mbali mbali vya elimu ya kati hapa nchini Tanzania na vilivyopata usajili wa kudumu wa NACTE ambapo Kanda mbali mbali za Tanzania kupitia vyuo vyao vitashindana katika michezo mbali mbali kwa wavulana na wasichana ni vyuo 32 tu vitakavyokuwa vikishiriki baada ya kufanya mchujo wa awali kwa njia ya Bonanza na Timu mbili za juu kila BONANZA ndizo zitakazokuwa zikiingia katika idadi ya vyuo 32 vya NACTE ITER COLLEGE DAR ES SALAAM. Ukiachilia mbali michezo hiyo, michezo mingine itakayokuwa ikifanyika kati ya wanafunzi na wanafunzi ni DEBATE, Marathon, Modoling, Mashindano ya Vipaji kwa viongozi wanaosimamia serikali za wanafunzi kwa nafasi za Rais na Makamu, Waziri Mkuu, Mawaziri wa Michezo,Fedha, na Spika , watakaokuwa wakichuana katika kujielezea, kujibu maswali, na kuelezea Mada katika nafasi zao na changamoto wanazokabiliana nazo na washindi watakuwa wakipata tuzo mbali mbali kulingana na ushindi wa kila mmoja.
Wadhamini aliojitokeza mpaka sasa na kuonyesha nia ya kusaidia mashindano hayo ni pamoja na Coca Cola, Vodacom, MLONGE BY MAKAI, CXC –Tours, na 100.5 Times Fm. lakini hata hivyo dirisha la wadhamini bado liko wazi kwa maana bado gharama ni kubwa za uendeshaji ambapo wajitokeze waweze kusaidia michezo hii iliyoanza kwa shamrashamra nyingi na kuwa na mvuto kwa watazamaji ususani wanafunzi wa vyuo mbalimbali waliojitokeza.

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE TANDAHIMBA LEO

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitembelea maghala ya kuhifadhia korosho wilayani Tandahimba, Mtwara wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi na kupkea kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
 Kinana akisaidia kumtwisha gunia la korosho mmoja wa wapagazi wa maghala ya kuhifadhia korosho, wilayani Tandahimba leo.
 Kinana akikagua mradi wa maji wa Mkupete katika Kata ya Mahuta.
 Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la Ofisi ya CCM Kata ya Mdimba, wilayani Tandahimba
 WANANCHI wakisikiliza kwa makini wakati Kinana akihutubia katika Kata ya Mahuta, wilayani Tandahimba
 Kinana akitembelea baadhi ya nyumba 100 zilizoezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa katika Kijiji cha Nanyanda, wilayani Tandahimba
Kinana akiwafariji baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Nanyanda ambao wameathirika baada ya nyumba zao kuezuliwa na upepo wa mvua
 Kinana akiendelea kukagua nyumba hizo zilizoezuliwa
 Kinana akipandisha bendera katika Shina la CCM la wakereketwa mjini Tandahimba leo
 Kwaya ikitumbuiza wakati wa mkutano wa hadhara Mjini Tandahimba
Aliyekuwa Katibu wa Chadema Wilaya ya Tandahimba, Jaffari Hassan ambaye amehamia CCM,  akielezea sababu zilizosababisha ahamie chama hicho wakati wa mkutano wa hadhara, mjini Tandahimba.Hassan hivi sasa ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wa wilaya hiyo.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF wa Kata ya Kitama akipongezwa na Kinana baada ya kuhamia CCM katika mkutano huo wa hadhara. Hivi sasa ni Mkobo ni Green Guard wa CCM Wilaya ya Tandahimba
  Katibuwa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara mjini Tandahimba ambapo alimtaka Katibu Mkuu wa CUF, Seif Shariff Hamad aache kuwahadaa wananchi kwamba wasiipigie kura Katiba inayopendekezwa akidai ni ya CCM na kwamba akitaka kuwa mkweli aachie ngazi nafasi ya Umakamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ya CCM inayoongozwa na CCM
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia katika mkutano huo wa hadhara, ambapo ameahidi kukutana wadau na viongozi wa mikoa ya inayolima korosho nchini, ili wajadili kero mbalimbali za wakulima wa zao hilo na kuzipatia ufumbuzi wa kudumu
Mbunge wa Jimbo la Tandahimba, akielezea utekelezji wa miradi mbalimbali jimboni humo wakati wa mkutano huo wa hadhara.

Big Brother Hotshots – (Sunday, 23 November 2014)

unnamed 
 On Sunday, Biggie revealed to the Hotshots housemates that he was playing a prank on them when he brought in the 10 former housemates. This week all Housemates are up for eviction apart from the head of house.  Africa’s biggest reality show Big Brother Hotshots, produced for M-Net’s AfricaMagic, is being screened live 24/7 on DStv 197/198. For more information log on to www.bigbrotherafrica.com

SYDS KWA KUSHIRIKIANA NA MAREKANI KUWAKOMBOA WAKULIMA PAWAGA IRINGA

Mwakilishi wa ubalozi wa marekani David Feldmann akihutubia mamia ya wakazi wa vijiji vya tarafa ya Pawaga (hawapo pichani) wilayani Iringa mkoa wa Iringa wakati sherehe ya kufunga mafunzo ya mradi wa kuwawezesha  wanachama  wa  vikundi 43 vyenye wanachama 300 katika kilimo kupitia asasi ya mpango salama wa maendeleo ya vijana (SYDS) chini ya ufadhili wa watu  
wa marekani(picha  na MatukiodaimaBlog)
…………………………………………………………………………….
TAASISI isiyo ya kiserikali ya mpango wa maendeleo salama wa maendeleo ya vijana (SYDS) chini ya ufadhili wa ubalozi wa marekani nchini Tanzania ikmekusudia kuwainua kwa kilimo wanachama wa vikundi 43 katika tarafa ya Pawaga wilaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa Akizungumza na waandishi wa habari wakati sherehe ya kufunga mradi huo wa mrejesho kwa vikundi, meneja mahusiano wa SYDS, Arnold Pangani alisema SYDS imejitoa kuendeleza mapambano dhidi ya changamoto zinazowakabili wengi wa akina mama katika sekta kilimo nchini. Pia alisema hadi sasa tayari wamekwisha toa mafunzo ya kilimo bora kwa wanachama zaidi ya 300 katika tarafa hiyo. “SDYS kwa udhamini wa serikali ya Marekani kupitia ubalozi wake nchini Tanzania tunaungana kwa pamoja na wananchi wa Pawaga zaidi tukitambua ushiriki wa wanawake katika kilimo,” alisema Panagani. Aidhi, wanavikundi walitoa shukrani ya dhati kwa SDYS kwa kuwapatia mwongozo bora ambao umewawezesha kupata uelewa juu ya elimu ya mpango biashara na uendashaji vikundi. Walisema kuwa kuja kwa asasi ya SDYS kumeweza kuhamasika na kuunda vikundi ambavyo vitasaidia katika shughulu za kilimo. Walisema kwa mafunzo hayo kama vijana wametambua umuhimu wao kama vijana ni nguvu kazi na wanatakiwa kushiriki shughuli za maendeleo na kujifunza zaidi juu ya mpango salama kwa maendeleo ya vijana. Kwa upande wake mwakilishi wa ubalozi wa marekani nchini Tanzania, David S. Feldmann alisema Tanzania itajengwa na watazania wenyewe na marekani itajengwa na wamarekani. Alisema kuwa matatizo ya watanzania hayawezi kumalizwa na marekani isipokuwa katika uwezekaji ndiyo suluhisho matatizo yote. Alisema ni jukumu kwa kila mwananchi kuhakikisha anashiriki kikamilifu katika kuinua na kukuza uchumi. Alisema watanzania lazima walipe kodi kwa serikali iliwaweze kupatiwa huduma stahiki kutoa kwa serikali kama ilivyo marekani. Alisema kuwa asilimia 90 ya serikali ya marekani inaendeshwa kwa mapato ya ndani kwa vile wananchi wengi wanalipa kodi kwa serikali bila kutegemea misaada ya nje.

MAADIMISHO YA SIKU YA TAKWIMU AFRIKA YAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM, SERIKALI YASISITIZA UWAZI KATIKA TAKWIMU.

unnamed1
Waziri wa Fedha wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Omar Yussuf Mzee akifungua maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam” na kuwashirikisha wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi  chini ya kauli mbiu isemayo “ Takwimu Huria kwa uwajibikaji na ushirikishwaji wa wadau wote. unnamed2Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi. Aldegunda Kombo akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi hiyo kuhusu matumizi ya takwimu sahihi katika kupanga shughuli za maendeleo  nchini wakati wa maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam. unnamed3
 Baadhi ya wadau mbalimbali na wataalam wa takwimu waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika wakifuatilia masuala mbalimbali  leo jijini Dar es salaam. unnamed4Mwakilishi kutoka nchi washirika wa maendeleo Bw. Jacques Morisset (kushoto)  akizungumza na wadau mbalimbali kuhusu mchango wa matumizi ya takwimu sahihi katika maendeleo ya taifa lolote wakati wa maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika leo jijini Dar es salaam. unnamed5 
Msanii Stara Thomas (kulia) akiwa na waimbaji wenzake akiwasilisha ujumbe wa matumizi ya takwimu sahihi kupitia wimbo maalum wakati wa maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyowashirikisha wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi  chini.
unnamed6Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Mohammed Hafidh akisisitiza jambo kuhusu athari, madhara  na  ya  matumizi ya takwimu zisizo sahihi. unnamed8 
Waziri wa Ferdha wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Omar Yussuf Mzee (wa nne kutoka kulia mbele) akiwa katika picha ya pamoja na watendaji na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu mara baada ya kufungua maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika leo jijini Dar es salaam.
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.
…………………………………………………………………………….
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
 Dar es salaam.
SERIKALI kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu imesema kuwa itaendelea kuwapatia wananchi takwimu sahihi zinazohusu sekta mbalimbali ili kuwajengea uwezo wa kushiriki katika ngazi za maamuzi na masuala mbalimbali nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Fedha wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Omar Yussuf  Mzee wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yanaoongozwa na kauli mbiu isemayo Takwimu Huria kwa uwajibikaji na ushirikishwaji wa wadau wote.
Amesema upatikanaji wa taarifa na  takwimu sahihi kwa wananchi unaongeza ushiriki wao katika maamuzi na kuwajengea uwezo wa kutathmini utendaji wa Serikali katika masuala mbalimbali yakiwemo mapato na matumizi.
Amesema Ofisi ya Taifa ya Takwimu itaendelea kuhakikisha kuwa takwimu mbalimbali zinapatikana kwa urahisi kupitia mtandao, machapisho na mifumo rahisi ili kuwawezesha wananchi na wadau mbalimbali kuzipata pindi wanapozihitaji.
“ Maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika mwaka huu yanaongozwa na kauli Mbiu isemayo Takwimu Huria kwa uwajibikaji na ushirikishwaji wa wadau wote ambayo inalenga kurahisisha upatikanaji wa takwimu sahihi kwa urahisi na kumwezesha mtumiaji kuzipata bila kizuizi chochote” Amesema.
Amefafanua  kuwa upatikanaji wa takwimu huria unawawezesha wananchi kujua sababu zinazoifanya serikali kutekeleza maamuzi mbalimbali, kuongeza uwajibikaji na kuwawezesha kupima matokeo ya sera za Serikali, kutathimini matumizi ya Serikali na kushiriki katika midahalo mbalimbali ya kitaifa.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi. Aldegunda Kombo akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi hiyo amesema kuwa maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika mwaka huu yameweka msisitizo katika kuweka miundombinu ya kuwarahisishia wadau kupata takwimu sahihi kwa wakati.
Amesema maadhimisho hayo licha ya kujadili masuala mbalimbali yanajikita katika kuweka msukumo wa kuhakikisha kuwa takwimu sahihi zinawafikia wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo bila vikwazo vyovyote ili kuongeza uwazi wa utendaji wa shughuli za serikali serikali.
Naye mwakilishi kutoka nchi washirika wa maendeleo Bw.Jacques Morisset akizungumza wakati wa maadhimisho hayo ameeleza kuwa takwimu sahihi ni ufunguo wa maendeleo kwa nchi yoyote duniani.
Amesema kuwa upatikanaji wa taarifa mbalimbali unawawezesha wananchi kutambua na kupima kiwango cha maendeleo ya nchi yao katika masuala mbalimbali yanayogusa maisha yao ya kila siku yakiwemo ya matumizi ya rasilimali, Elimu, ukuaji wa uchumi, shughuli za kilimo na sekta ya viwanda na Biashara.

MAELEZO YA SERIKALI KUHUSU TAARIFA YA UKAGUZI MAALUM KUHUSIANA NA MIAMALA ILIYOFANYIKA KATIKA AKAUNTI YA “ESCROW” YA TEGETA PAMOJA NA UMILIKI WA KAMPUNI YA IPTL

unnamed1
1.  Historia ya Mradi
 
Mheshimiwa Spika, Katika miaka ya tisini (1990s), Tanzania ilikuwa ikikabiliwa na tatizo la uhaba wa maji katika mabwawa ya kuzalisha umeme, hali iliyopelekea kuwepo kwa upungufu wa umeme na kuathiri shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini. Ili kukabiliana na tatizo hilo, Serikali ilichukua hatua za dharura za kuanzisha mradi wa kufua umeme wenye uwezo wa kuzalisha Megawati (MW) 100.
 
2.  Upatikanaji wa IPTL
 
Mheshimiwa Spika, Mwaka 1994 Serikali ilitoa kazi ya uwekezaji kwa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) iliyokuwa inamilikiwa na Kampuni za VIP Engineering and Marketing Ltd ya Tanzania iliyokuwa na Asilimia 30 na MECHMAR Corporation ya Malaysia (MECHMAR) iliyokuwa na Asilimia 70. Kampuni ya IPTL ilipewa leseni ya kujenga, kumiliki na kuendesha (Build-Own-Operate) Mtambo wenye uwezo wa kuzalisha umeme wa MW 100 kwa kutumia mafuta mazito eneo la Tegeta-Salasala, Dar es Salaam.
 
Katika Ukurasa wa 52 Aya ya 2 ya Taarifa ya PAC, Kamati imependekeza Mtambo huo utaifishwe.
 
Ufafanuzi:
 
Mheshimiwa Spika, Kulingana na Mkataba wa PPA kati ya TANESCO na IPTL, majukumu ya IPTL yalikuwa ni kujenga, kumiliki na kuendesha (Build, Own and Operate – BOO). Hivyo, kutaifisha Mtambo huo ni kukiuka makubaliano katika Mkataba wa PPA wa tarehe 26 Mei 1995, ukiukwaji wa aina hii ukitokea unaweza kuingiza Serikali katika mgogoro mkubwa ikiwa ni pamoja na kushtakiwa kwenye Mahakama za kibiashara za kimataifa. Aidha utaifishaji wa miradi ya uwekezaji binafsi itakuwa ni njia ya kufukuza wawekezaji binafsi.
 
Mheshimiwa Spika, Tarehe 26 Mei, 1995, TANESCO na IPTL walisaini Mkataba wa PPA kwa muda wa miaka ishirini (20), kwa ajili ya kununua umeme utakaozalishwa na IPTL. Kwa mujibu wa Mkataba huo, IPTL ilitakiwa kuiuzia TANESCO umeme usiopungua Asilimia 85 ya uwezo wa Mtambo (minimum off take). Hata hivyo, uzalishaji wa umeme haukuanza mara moja kutokana na mgogoro uliotokea kati ya TANESCO na IPTL kuhusu gharama halisi za uwekezaji na namna ya kukokotoa Capacity Charges. Hivyo, IPTL ilianza kuzalisha umeme tarehe 15 Januari, 2002. Kutokana na hali hiyo muda wa miaka 20 ya Mkataba ulianza kuhesabiwa tarehe 15 Januari, 2002 baada ya kuanza uzalishaji (Commercial Operation Date).
 
Mheshimiwa Spika, Pamoja na mambo mengine muhimu yaliyokuwemo katika PPA, Kifungu Na. 6 cha Mkataba huo kinaipa TANESCO wajibu wa kulipa malipo yaliyotajwa hapo juu na kwamba endapo kutakuwa na mgogoro wowote kuhusiana na malipo hayo (Disputed Amount), itafunguliwa Akaunti maalum (Escrow Account) ya kuhifadhi fedha hizo hadi pale pande mbili zitakapokubaliana juu ya uhalali wa malipo yanayobishaniwa. Aidha chini ya PPA, migogoro yote kuhusiana na masuala ya utekelezaji wa Mkataba huo ilitakiwa kuwasilishwa na kuamuliwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) ya London. Hivyo, ilikuwa ni jukumu la kila mhusika katika Mkataba huu kuwasilisha malalamiko yake ICSID yanapotokea. 
 
Katika Ukurasa wa 8 Aya ya 2 ya Taarifa ya PAC imeelezwa kuwa mwaka 2004 TANESCO ilifungua shauri la ICSID 2 kupinga kiasi kikubwa cha tozo ya Capacity Charge.
 
Ufafanuzi
 
Mheshimiwa Spika, Taarifa hiyo siyo kweli kwani TANESCO haijawahi kufungua shauri lolote ICSID ya London au Mahakama yo yote dhidi ya Standard Charterd Bank kupinga kiasi kikubwa cha Capacity Charge kama inavyoelezwa katika Taarifa ya PAC. Shauri la ICSID 2 lilifunguliwa tarehe 31 Oktoba 2010 na Standard Chatered Bank Hong Kong (SCBHK) kwa ajili ya kudai malipo ya deni ililonunua kutokana na mkopo uliotolewa na mabenki ya ushirika ya Malaysia kwa IPTL.  Wahusika katika Shauri hilo la ICSID 2 ni SCBHK na TANESCO na wala siyo TANESCO na IPTL.
 
Mheshimiwa Spika, Tarehe 12 Februari, 2014 ICSID ilitoa uamuzi kuhusiana na Shauri la SCBHK na TANESCO na kuwashauri wakae kukokotoa upya malipo ya Capacity Charge. Hata hivyo, ilikuwa vigumu kwa pande hizo kutekeleza uamuzi huo kutokana na pande hizo kutokuwa na Mkataba wa kibiashara baina yao. Vile vile, kupitia Shauri la Madai Na. 60/2014, lililofunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania na IPTL tarehe 4 Aprili, 2014 ilizuia utekelezaji wa maelekezo hayo.
 
3.  Mgogoro kati ya IPTL na TANESCO
 
Mheshimiwa Spika, Migogoro kati ya TANESCO na IPTL ilianza muda mfupi baada ya PPA kusainiwa tarehe 26 Mei 1995. IPTL waliitaka TANESCO wakubaliane bei za kununua umeme kwa kuzingatia gharama za uwekezaji. Pande hizo mbili zilishindwa kukubaliana gharama za Capacity Charge kwa vile TANESCO walidai kuwa gharama zilizoainishwa na IPTL ni kubwa kuliko gharama halisi za uwekezaji. Mwaka 1998, TANESCO iliajiri Kampuni ya Mawakili ya Mkono & Co Advocates kutoa huduma za kisheria kwa kushirikiana na Huntons & Williams ya Marekani. Kutokana na tofauti za gharama za Uwekezaji, Mawakili hawa waliishauri TANESCO ifungue Kesi ICSID nchini Uingereza dhidi ya IPTL ili kupinga gharama hizo.
 
Mheshimiwa Spika, Kwa kuzingatia ushauri huo wa Mawakili, TANESCO ilifungua Kesi Na.ARB/98/8 ya mwezi Agosti, 1998 ikidai kuwa gharama halisi za uwekezaji ni Dola za Marekani milioni 90 na siyo milioni 163.53 kama ilivyodaiwa na IPTL. Aidha, IPTL ilidai kuwa kiwango cha marejesho ya uwekezaji (Internal Rate of Return-IRR) ni Asilimia 23.10 ambacho pia kilipingwa na TANESCO.
 
Mheshimiwa Spika, Tarehe 12 Julai, 2001, ICSID ilitoa uamuzi wa Kesi hiyo pamoja na mambo mengine kwamba:-
 
i.     Gharama halisi za uwekezaji zikiwemo Mtambo na nyumba za wafanyakazi wa IPTL zilizoainishwa katika hesabu ya IPTL zilikuwa ni Dola za Marekani milioni 163.53 lakini ICSID iliona kuwa gharama halisi ni Dola za Marekani milioni 127.20;
 
ii.     Kiwango cha marejesho ya uwekezaji (Internal Rate of Return-IRR) ilikuwa Asilimia 22.31 badala ya Asilimia 23.10 iliyodaiwa na IPTL; na
iii.  TANESCO na IPTL wakubaliane mfumo wa malipo ya kununua umeme ukizingatia gharama halisi za uwekezaji na kiwango cha marejesho ya uwekezaji (IRR) cha Asilimia 22.31 kwa kutumia financial model iliyokubalika na ICSID.
 
Katika Ukurasa wa 11 Aya ya 2 ya Taarifa ya PAC, imeelezwa kuwa mtaji wa uwekezaji katika Mtambo wa IPTL ni Shilingi 50,000/= na kwamba huo ndio ungetumika kukokotoa Capacity Charges ili kulipa tozo ndogo kuliko ilivyo sasa.
 
Ufafanuzi
 
Mheshimiwa Spika, Maelezo hayo siyo sahihi. Ukweli ni kwamba kutokana na maamuzi ya ICSID 1 ya tarehe 12 Julai, 2001, gharama za ujenzi wa Mtambo wa Tegeta ni Dola za Marekani 127.20 kama ilivyoelezwa katika Ukurasa wa 47 Aya ya 4 ya Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Katika Taarifa hiyo, pia imeelezwa kuwa ilikubalika kuwa uwiano wa deni na mtaji utakuwa 70:30. Hii ikiwa na maana kwamba, deni ni Dola za Marekani milioni 89.04 na mtaji ni Dola za Marekani milioni 38.16. Uamuzi huo haujabadilishwa na Mahakama yo yote au mtu ye yote.
 
Mheshimiwa Spika, Tunakubaliana kwamba fedha iliyopokelewa kutoka Mabenki ya Ushirika ya Malaysia kama mkopo ni Dola za Marekani milioni 85.86 ambazo kati ya Dola za Marekani milioni 105 zilizokuwa zimeidhinishwa. Swali la kujiuliza, je Mtambo huo ulikamilikaje kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 85.86, huku gharama halisi ya ujenzi wa Mtambo wa Tegeta ikawa Dola za Marekani milioni 127.20?
 
Mheshimiwa Spika, Ni dhahiri kwamba kuna matumizi ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 38.16 ambazo pia zimetumika kwenye uwekezaji. Taarifa ya Kamati ya PAC haikuonesha fedha hiyo kuwa sehemu ya uwekezaji.
                                        
Mheshimiwa Spika, Tarehe 30 Juni, 2004, Kampuni ya Mawakili iliyokuwa ikiiwakilisha TANESCO katika kesi ya kwanza ya usuluhishi, Kampuni ya Mkono & Co Advocates, iliishauri TANESCO iendelee kupinga kiwango cha malipo ya Capacity Charge kilichokuwa kimeafikiwa tarehe 12 Julai, 2001 na pande hizi mbili katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICSID) ya London. Hii ilikuwa ni miaka miwili tu baada ya usuluhishi uliochukua miaka minne kukamilika na Mtambo kuanza kuzalisha umeme tarehe 15 Januari, 2002.
 
Mheshimiwa Spika, Hata hivyo, baada ya ushauri huu, Mawakili hawa (Mkono & Co. Advocates) hawakuishauri TANESCO ifungue kesi katika Mahakama za Tanzania wala katika Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kimataifa (ICSID) ya London.
 
Mheshimiwa Spika, Hadi kufikia tarehe 5 Septemba, 2013 wakati Mheshimiwa Jaji Utamwa anatoa hukumu yake juu ya mgogoro wa Wanahisa wa IPTL hapakuwepo na kesi yo yote kwenye Mahakama yo yote ya kupinga gharama za Capacity Charge kati ya TANESCO na IPTL, iwe katika Mahakama za ndani au za nje. Kwa kutokuwepo Msuluhishi (Broker) katika suala hili, madai yo yote ya TANESCO yanakuwa ni madai ya upande mmoja ambayo kisheria hayawezi kuchukuliwa kuwa ndiyo madai halisi.  Kwa sababu hiyo haikuwepo formula rasmi ya kuutatua mgogoro huo zaidi ya majadiliano na maafikiano kati ya pande mbili (TANESCO na IPTL).
 
4.  Uuzaji wa Hisa za VIP
 
Continue reading →

MATUKIO YA PICHA KUTOKA BUNGENI DODOMA LEO

unnamed 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Novemba 27, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
unnamed3 
Spika wa Bunge Anne Makinda akizungumza, Bungeni Mjini Dodoma Novemba 27, 2014. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
unnamed5 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Novemba 27, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
unnamed8
unnamed9
Waziri  Mizengo Pinda  akizungumza na Mbunge wa Maswa Magaribi, John Cheyo, kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Novemba 27, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
 unnamed10
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole- Sendeka kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Novemba 27, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) unnamed11 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (katikati) na Mbunge wa Lshoto, Henry Shekifu kwenye jengo la Utawala la  Bunge mjini Dodoma Novemba 27, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MWANAMUZIKI BILEKU MPASI KUTOKA CONGO (DRC) NA MASHUJAA BAND KUFANYA ONESHO LA PAMOJA DISEMBA 12-2014

 Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz  Baba (kushoto), akitoa burudani mbele ya wanahabari Dar es Salaam leo, kuhusu onesho hilo litakalofanyika katika ukumbi huo.. Kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel na Ofisa Uhusiano wa Band ya Mashujaa, King Dodo la Buche. 
 Ofisa Uhusiano wa Band ya Mashujaa, King Dodo la Buche (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu onesho hilo. Kulia ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel na Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz Baba
 Meneja Matangazo wa Band ya Mashujaa, Maxmilian Luhanga (katikati), akizungumza katika mkutano huo.
 Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel (katikati), akizungumza katika mkutano huo. Kampuni ya Bia ya Mabibo imedhamini onesho hilo. Kulia ni Ofisa Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Salumu Kabanda.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo. ………………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu MWANAMUZIKI mkongwe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Bileku Mpasi, atafanya onesho maalum katika utambulisho wa nyimbo mbili mpya za bendi ya Mashujaa utakaofanyika Desemba 12 mwaka huu kwenye ukumbi wa Ten Lounge zamani Business Park. Akizungumza Dar es Salaam leo mratibu wa onesho hilo, King Dodoo la Buche, alisema kuwa Mpasi ambaye alitamba katika tasnia ya muziki wa dansi alipokuwa na gwiji, marehemu, Pepe Kale, atakuja na wasanii wengine ili kutoa burudani ya kiwango cha juu. Dodoo alitaja nyimbo hizo mbili ambazo zitatambulishwa ni pamoja na Rafiki Sokoni na My Queen. Aliwataka mashabiki wa muziki wa dansi nchini kujiandaa kushuhudia onyesho hilo linalotarajiwa kuwa la kihistoria hapa nchini.
Rais wa Mashujaa Musica, Chalz Baba, alisema kuwa wamejiandaa kutoa burudani nzuri na kuendeleza heshima yao ya bendi bora kwa mwaka wa pili mfululizo
” Napenda kuwahakikishia wapenzi wa bendi yetu tutafanya kazi ya ubora wa juu, ni kawaida yetu kufanya kazi nzuri, tuna usongo,” alisema Chalz. Katika onesho hilo lililodhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Mabibo kupitikia kinywaji chake cha Windhoek.
Akizungumza kwa niaba ya kampuni hiyo meneja biashara wa kampuni hiyo Joseph Emmanuel, alisema wameamua kudhamini utambulisho huo ili kuendeleza muziki wa dansi nchini kufikia hadhi ya kimataiif Alisema kuwa wapenzi 100 wa kwanza watakaoingia kwenye onesho hilo watapewa bia moja ya Windhoek Draught bure. Mashujaa pia itatumbuiza nyimbo zake zilizotamba katika albamu zake za Risasi Kidole na Ushamba Mzigo.
Naye Rais wa Mashujaa Chalz Baba amewataka wapenzi wajiandae kupata burudani ya aina yake katika uzinduzi. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)

TPDC YAOMBA TOZO EWURA KUSAFIRISHA GESI ASILIA

index 
Na Beatrice Lyimo- Maelezo.
GESI asilia ni bidhaa muhimu kwa maendeleo ya wananchi na uchumi wa nchi yeyote ikiwemo Tanzania.
Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Said Meck Sadick wakati wa ufunguzi wa taftishi juu ya maombi la Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuhusu mapendekezo ya tozo ya uchakataji na usafirishaji wa Gesi asilia uliofanyika.
Mhe. Sadick amesema  kuwa, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ilipokea maombi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuhusu mapendekezo ya tozo ya uchakataji na usafirishaji wa Gesi asilia, hivyo EWURA inatarajia kuandaa mkutano wa wadau wa gesi asilia ili kupata maoni juu ya maombi hayo.
Alibainisha kuwa, kutokana na upungufu wa maji ya kuendeshea mitambo ya umeme uliosababishwa na ukame nchini Tanzania, zaidi ya asilimia 40 ya uzalishaji wa umeme kwa sasa unategemea hiyo. “Gesi asilia inayozalishwa kwa sasa inategemewa katika uzalishaji wa umeme nchini ambapo asilimia 88 ya gesi hii inatumika katika kuzalisha nishati ya umeme”, alisema Mhe Sadick.
Aliongeza kuwa, mitambo iliyopo inayotumia gesi asilia ina uwezo wa kuzalisha Megawati 441, lakini huzalisha Megawati 300 kutokana na uhaba wa miundombinu ya kuchakata na kusafirisha hiyo.
Aidha, Serikali inatarajia utendaji mahiri wa EWURA kuwa chachu ya kuboresha utoaji wa huduma za uchakataji na usafirishaji wa gesi asilia hapa nchini, kwani kwa kufanya hivyo itaongeza upatikanaji na ubora wa huduma na kuleta ufanisi endelevu wenye kuzingatia uboreshaji wa mazingira nchini.
“Hii ni miongoni mwa juhudi za EWURA katika kushirikiana na wadau na kupata maoni kuhusu huduma zitolewazo na TPDC pamoja na mipango itakayowasilishwa katika sekta hii muhimu ya Gesi asilia”, aliongeza Mhe. Sadick.
Wito ulitolewa kwa wadau hao kuwa makini, kujenga hoja kushiriki kwa nia njema, pamoja na kutoa maoni yakiwa na lengo la kuhakikisha kuwa mizania kati ya watumiaji huduma za uchakataji na usafirishaji wa gesi asilia inawepo, kwani TPDC na Taifa linafikia malengo ya matumizi ya gesi hiyo katika kukuza uchumi wa nchi.

MKUTANO WA CCM WA MABALOZI KASKAZINI A UNGUJA.

unnamed1
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali alipofika katika Hoteli ya Bravo Club Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini A kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani akiwa katika ziara  zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi katika Mkoa wa Kaskazini Unguja,{Picha na Ikulu.] unnamed2 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Meja Mstaafu Juma Kassin Tindwa (kulia) na Mwenyekiti wa CCM Kaskazini Unguja Juma Haji Juma mara  alipowasili katika Hoteli ya Bravo Club Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika kuimarisha Chama,{Picha na Ikulu.]
unnamed4 unnamed5
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai (kulia) Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kaskazini A Ali Makame Khamis  wakiwa katika ukumbi wa  Hoteli ya Bravo Club Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika kuimarisha Chama,{Picha na Ikulu.] unnamed6
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai (kulia) wakati wa mkutano wa maalum wa kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM kwa  Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani Wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa Kaskazini Unguja leo,{Picha na Ikulu.] unnamed7 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika ukumbi wa Hotel ya Bravo Club Kiwengwa wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa kaskazini Unguja katika  ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM, {Picha na Ikulu.]
unnamed8 
Baadhi ya Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika Wilaya ya Mfenesini Kichama wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Viongozi hao katika Ukumbi wa  Hotel ya Bravo Club Kiwengwa wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa kaskazini Unguja katika  ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM, {Picha na Ikulu.]

Nyalandu launched hot springs boardwalk way and hippo pool viewpoint in Lake Manyara

unnamedChairman of the Tanzania Association of Tour Operators Wilbard Chambulo was also there to emphasis the importance of National Parks.
unnamed3Chairman of the Tanzania Association of Tour Operators Wilbard Chambulo was also there to emphasis the importance of National Parks.
unnamed4 
Chief Park Warden for Lake Manyara National Park Domician Njau (right) explain a point to Hon. Lazaro Nyalandu, Minister for Natural Resources and Tourism as they walk through the Lake Manyara Hot springs boardwalk way yesterday.
unnamed5 
Chief Park Warden for Lake Manyara National Park Domician Njau explaining about the newly launched projects during the official launching of the hot springs boardwalk way and hippo view point at Lake Manyara National Park yesterday.
unnamed6Director General of TANAPA Allan Kijazi giving out welcoming remarks during the official launching of the hot springs boardwalk way and hippo view point at Lake Manyara National Park yesterday.
unnamed7 
2. Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu (2nd left) cut off ribbon to officially launch Lake Manyara hot springs boardwalk way and hippo pool view point in Lake Manyara. Others in the picture from left are Manyara Regional Commissioner Hon. Elaston Mbwilo; Director General of TANAPA Allan Kijazi and the Chairman of the Parliamentary Committee on Lands, Natural Resources and Environment Hon. James Lembeli.
………………………………………………………………..
Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu has commended a remarkable initiative by Tanzania National Parks in introducing new tourism products at Lake Manyara National Park. Nyalandu said this during the official launching of the hot springs boardwalk way and hippo pool viewpoint projects at the park yesterday. Nyalandu said that the two projects will add value to the tourism sector by increasing the number of tourist arrivals in the country and urged other stakeholders to be innovative in introducing products that will attract more tourists. The Manyara boardwalk way and hippo pool viewpoint projects worth about 200 millions were initiated to counter the decreased trend of tourist numbers in the park following the flashfloods hit the park in March 2013 which damaged most of tourist infrastructures. The first ever tourism product in the national parks, the boardwalk way is featured with 1.5 meters wide impressive wooden structure, creating a 300 meters long trail standing 1.5 meters above ground winding up in an observation platform that is 15 meters long and 2.5 meters wide. The trail meanders through the hot springs and lakeshore around a marsh and finally into the lake. The boardwalk will give visitors a unique view and wonderful photo opportunities at every turn of the boardwalk trail. Hot springs boardwalk way is designed to simply give people a nice place to walk along the numerous hot springs and be close to the attractions and enjoy the wide view of the lake. Visitors will use the facilities boardwalk way for free and have opportunity of walking around 600 meters on a return trip to the lakeshore and over the hot springs. Educational signage with entertaining themes will be erected in key locations to allow visitors’ easy reading and understanding of the nature and the resources found in the area. These signs will educate visitors about the ecology and adaptation of plants and animals to the area. Moreover, it will explain the fragility of the ecosystem and why it is so important to use the boardwalks to avoid, as much as possible, disturbing the environment. Moreover, the viewpoint is a freestanding wooden platform rising by 8 feet above the ground measuring 56 feet in length and 5 feet in width. It is about 8 km away from main gate. Standing at the top of the viewing platform enables the viewer a spectacular view of the marshland and its inhabitants – waterfowl, hippo, buffalo and wildebeest – from a point of vantage while affording the visitor a high sense of security.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI

index
MTOTO MDOGO MWENYE UMRI WA MWAKA MMOJA ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA ANGEL RAMADHANI ALIFARIKI DUNIA BAADA YA KUTUMBUKIA KWENYE KISIMA KILICHOPO JIRANI NA NYUMBA YAO.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 26.11.2014 MAJIRA YA SAA 15:30 JIONI HUKO IKUTI, KATA NA TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. INADAIWA KUWA, MTOTO HUYO ALITAMBAA KUELEKEA KWENYE KISIMA HICHO NA NDIPO ALIPOTUMBUKIA NA KUPELEKEA KIFO CHAKE.
AIDHA, WAKATI TUKIO HILO LINATOKEA MAMA MZAZI WA MTOTO HUYO ALIKUWA JIKONI ANAPIKA NA KUMUACHA MTOTO HUYO AKIWA ANACHEZA NA NDIPO ALITAMBAA NA KUTUMBUKIA KWENYE KISIMA KILIKUWA JIRANI NA NYUMBA YAO. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA WAZAZI/WALEZI KUWEKA UANGALIZI WA KUTOSHA KWA WATOTO WADOGO ILI KUEPUKA MADHARA YANAYOWEZA KUJITOKEZA. AIDHA, ANATOA WITO KWA JAMII KUFUNIKA VISIMA/VYOO NA KUFUKIA MASHIMO YENYE MAJI KWANI NI HATARI KWA WATOTO WADOGO HASA KATIKA KIPINDI HIKI CHA MVUA. TAARIFA ZA MISAKO:
MTU MMOJA MKAZI WA KATUMBA WILAYA YA RUNGWE ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA ALEX PHILIPO (25) ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA NA BHANGI KETE 22 SAWA NA UZITO WA GRAMU 110 KWENYE MFUKO WAKE WA SURUALI.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 26.11.2014 MAJIRA YA SAA 13:00 MCHANA HUKO KATIKA KATA YA IBIGI, TARAFA YA UKUKWE, WILAYA YA RUNGWE, MKOA WA MBEYA. MTUHUMIWA NI MUUZAJI NA MTUMIAJI WA BHANGI HIYO. TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI. Imesainiwa na; [BARAKAEL N. MASAKI – ACP] KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

UNCDF VACANY ANNOUNCEMENT

vacanciesBasically, professionals with this background:
Required Skills and Experience
Education:
At least a Master’s Degree in Business Administration, Finance, Banking or related areas, plus preferably a Bachelor Degree in engineering, finance or economics.
Experience:
Preferably a minimum of 5 years of relevant experience;
Ability to build partnerships and deliver results that meet the needs and long-term interest of clients within and outside the institution;
Demonstrated experience in preparation of project financial analysis and creation/evaluation of advanced and complex Ms Excel spread sheet financial models;
Demonstrated experience with private equity/venture investments, credit and risk assessment, with solid financial modelling and risk assessment skills. Project financing experience in the private sector is a plus;
Demonstrated experience in preliminary evaluation of project proposals for assessing their feasibility for private sector funding and/or technical support by LFI.
Here is the link with more information
https://jobs.undp.org/cj_view_job.cfm?cur_job_id=51739

BALOZI WA TANZANIA NCHINI CANADA AKUTANA NA DR. SHEIN


unnamed
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi Mpya wa Tanzania Nchini Canada Jack Mugendi Zoka alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha leo kwa Rais baada ya kuteuliwa rasmi.[Picha na Ikulu.]
unnamed1

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi Mpya wa Tanzania Nchini Canada Jack Mugendi Zoka aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar leo  kujitambulisha  kwa Rais baada ya kuteuliwa .[Picha na Ikulu.] unnamed2 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana  na Balozi Mpya wa Tanzania Nchini Canada Jack Mugendi Zoka baada ya mazungumzo  alipofika   kujitambulisha leo Ikulu Mjini Zanzibar baada ya kuteuliwa.[Picha na Ikulu.]

Matukio ya picha wakati wa uwasilishaji wa Ripoti ya GAG kuhusu akauti ya ESCROW Bungeni Dodoma

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe Zitto Kabwe akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini,Mhe. Ismail Aden Rage wakati akiwasili bungeni kuwasilisha Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (GAG) kuhusu akauti ya ESCROW.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Anne Makinda akifafanua jambo wakati akiendesha Bunge hilo leo mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe Zitto Kabwe akienda kusoma Ripoti ya GAG kuhusu akauti ya ESCROW.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mhe Zitto Kabwe akisoma Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (GAG) kuhusu akauti ya ESCROW Bungeni Mjini Dodoma leo.

Waheshimiwa Wabunge wakimsikiliza Mhe. Zitto Kabwe (hayupo pichani) wakati akisoma ripoti ya CAG.
Baadhi ya wahudumu wa Bunge wakigawa Ripoti ya GAG kuhusu akauti ya ESCROW kwa Wabunge
Waheshimiwa Wabunge wakipitia ripoti ya GAG kwa makini wakati ikisomwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, Mhe Zitto Kabwe.
Baadhi ya waandishi wanaoripoti habari za Bunge wakifuatilia mjadala kwa makini.
Naibu katibu wa Bunge, John Joel akijadiliana jambo na Mhe. Spika Anna Makinda.
Wabunge wakiwa wamesimama kuashiria kuunga mkono taarifa iliyosomwa Bungeni leo na Mhe. Zitto Kabwe.
Mhe Said Arfi akimpongeza Mhe.Zitto Kabwe ,mara Baada ya kumaliza kusoma ripoti ya GAG.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe DEO Filikunjombe akiwasilisha maazimio ya kamati yake.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Anne Makinda akitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirisha Bunge mpaka kesho ambapo Serikali inatarajiwa kutoa majibu.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Mhe. Stephen Masele akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya Bunge kuahirishwa. Picha zote na Deusdedit Moshi wa Globu ya Jamii kanda ya kati

MHE. DKT. TITUS MLENGEYA KAMANI (Mb) AZINDUA MRADI WA UFUGAJI WA SAMAKI NDANI YA ZIWA VICTORIA, KITEULE CHA BULAMBA WILAYA YA BUNDA


unnamed1
Mgeni Rasmi Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Kamani (wa tatu kushoto) pamoja na wageni wengine waliohudhuria Sherehe hizo. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uchumi, Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Felix Samilani, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Raphael M. Muhuga, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Mhe. John Henjewele, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mara, na Mkuu wa Kiteule cha Bulamba Meja David Msakulo. unnamed2
Mgeni Rasmi Waziri wa Maendeleao ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Kamani (MB) akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Mradi wa Ufugaji wa Samaki ndani ya Ziwa Viktoria Kiteule cha Bulamba kwa kutumia teknolojia mpya ya vizimba (Cages). Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime Mhe.John Henjewele, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mara. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Raphael M. Muhuga. unnamed3 
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Kamani akipandikiza vifaranga vya samaki ndani ya Ziwa Victoria, mradi unaotekelezwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Wilaya ya Bunda, Kiteule cha Bulamba kwa kutumia teknolojia mpya hapa nchini ya kuzalisha samaki kwenye vizimba.
unnamed4 
Picha ya vizimba ambavyo ufugaji wa samaki umeanza mara baada ya Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kuzindua mradi huo na kupandikiza vifaranga vya samaki. Mradi unatekeleza na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Wilaya ya Bunda, Kiteule cha Bulamba kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Economic Social Research Foundation (ESRF), Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango. Ufugaji wa samaki kwa kutumia teknolojia ya vizimba ndani ya Ziwa Victoria, umekuwa ukitekelezwa pia na wenzetu wa Kenya na Uganda ambao wamepiga hatua kubwa .
unnamed6Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP),  Mratibu Mwandamizi wa Mradi Bw. Nehemia Murusuri (wa kwanza kulia) pamoja na Mwakilishi wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Mratibu wa Mradi wa Kuondoa Umaskini, Kukuza Uchumi na Utunzaji Endelevu wa Mazingira, Bw. Telesphory Kamugisha (wa pili kulia). Wengine ni baadhi ya wageni waliohudhuria sherehe hizo. unnamed7
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Raphael M. Muhuga akiongea na wananchi wa Kijiji cha Bulamba wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa Ufugaji wa samaki katika Ziwa Victoria kwa kutumia teknolojia ya vizimba (Cages) ambayo ni teknolojia mpya ndani ya nchi yetu. unnamed8
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Kamani akitoa hotuba kwa wananchi wa kijiji cha Bulamba (hawapo pichani) mara baada ya kuzindua Mradi wa Ufugaji wa Samaki ndani ya Ziwa Viktoria. Aliwasisitiza wananchi kujiunga katika vikundi ili kujijengea uwezo wa kuanza kutumia teknolojia ya kisasa ya kuzalisha samaki kwa kutumia vizimba (Cages) katika ziwa Victoria. unnamed9 
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Kamani (mwenye Kaundasuti nyeusi) akionyesha umahiri wake wa kucheza ngoma ya asili mara baada ya uzinduzi wa mradi huo. 

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AMALIZA ZIARA YAKE NEWALA, LEO YUKO TANDAHIMBA

1 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Neawala Mh George Mkuchika mara baada ya kuwasili mjini  Newala akiwa katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Mtwara ziara yenye lengo la kukagua na kuhimiza Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali kwa kushirikiana na wananchi, Katibu Mkuu Kinana emeembelea na kukagua miradi mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa miondombinu ya maji , Zahanati Ofisi za Chama cha Mapinduzi na kuzungumza na wananchi katika mikutano mbalimbali, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi. 2 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana viongozi wa kiwanda cha kubangua korosho mjini Newala kulia Niry Patel Mratibu wa Usafirishaji  na katikati ni Ednyadayu Meneja wa ufundi. 4 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kubangua korosho na wafanyakazi wa kiwanda hicho.
10
Wafanyakazi wa kiwanda hicho wakiendelea na kazi ya kubangua korosho
6
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mhandisi wa Maji Newala Bw. Nsajigwa Said wakati alipotembelea chanzo cha maji cha Malatu mjini Neawala.
7
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua mradi wa maji katika kata ya Malatu kushoto ni mkuu wa mkoa wa Mtwara B. Halima Dendegu.
8
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kusuka nondo katika ujenzi wa tanki la maji la kijiji cha Kilidu kwa pamoja na wafanyakazi wa katika mradi huo wa tatu kutoka kulia aliyesimama ni Mbunge wa jimbo la Neawala Mh. George Mkuchika.
9
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Dr Yudas Ndugile Mganga mkuu wa wilaya ya Newala wakati alipokagua jengo jipya la Kituo cha Afya Mkwedu kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa wilaya ya Newala BwMarx Simon Kamaoni na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Bi. Halima Dendegu.
11
Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishuhudia aliyekuwa  Kaimu Mwenyekiti  wa Wilaya ya Newala Chadema Bw. Adam Nangwanda Sijaona akivua shati la CHADEMA na kuvaa la CCM mara baada ya kuondoka katika chama hicho na kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Mahakama mjini Newala.
12
 Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitupa shati hilo
13
Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti  wa Wilaya ya Newala Chadema Bw. Adam Nangwanda akiwa amekabidhi kadi yake na ya mke wake kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kujiunga na CCM mjini Newala kulia ni Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
14
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Mahakama mjini Newala
15
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakisisitiza jambo katika mkutano huo.
16
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakikabidhi pikipiki kwa vijana ambazo zimekopeshwa kwao ili kujikomboa kiuchumi.
17
Umati wa watu wakisikiliza mkutano huo.

Wafanyakazi wa Airtel kuwaunganisha wadau katika kusaidia shule ya msingi Kumbukumbu-Dar

SONY DSC
    Wafanyakazi wa Airtel kutembea ili kukusanya jumla ya zaidi ya milioni 10
  • Wafanyakazi wa Airtel kukarabati darasa na kununa madawati shule ya kumbukumbu.
  • ………………………………………………………………..
Wafanyakazi wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mpango wake maalumu wa “Airtel tunakujali” imeandaa matembezi ya hisani huku ikialika wadau wote wenye wito wa kuchangia elimu kuungamkono jitiada hizo ili kukamilisha lengo la kuikarabati shule ya msingi kumbukumbu iliyopo kinondoni jijini Dar es Saalam.
Matembezi hayo yanayoandaliwa na wafanyakazi wa Airtel yatashirikisha wadau mbalimbali na yatafanyika siku ya Jumamosi tarahe 29/11/2014 kuanzia saa moja asubuhi katika viwanja vya ofisi ya Airtel Makao makuu Morocco.
Akiongea kuhusu Matembezi haya Meneja huduma kwa jamii Hawa Bayumi alisema “wafanyakazi wa Airtel nao wameona mapungufu yaliopo shuleni hapo na kuamua kujitosa kwa kutumia sehemu ya kipato chao kuihudumia jamii kwa njia hii, kila mfanyakazi wa airtel ambae amehamasika tayari ameshachangia.
Na sasa tumeona ni vyema kuishirikisha jamii pia wakiwemo wanafamilia, marafiki na wote wenye wito wa kuchangia elimu kuungana nasi kuhakikisha watoto wanaosoma shule ya kumbukumbu wanasoma katika mazingira mazuri
“Lengo ni kukusanya zaidi ya shilingi milioni 10 ili kukarabati darasa moja na kununua madawati kwa ajili ya darasa la wanafunzi wa darasa awali”
Tutafanya Matembezi ya Kilomita 5 ambapo ni ya wazi ili kila mtanzania aweze kushiriki na kuchangia, pia kutakuwa na Tshirt maalumu zinapatikana katika ofisi ya Airtel Makao Makuu kwa gharama ya shilingi 15,000. Kwa kununua lengo ni kumfanya kila mmoja aweze kuchangia.
Tunatoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza na kuungana nasi katika matembezi haya kwa kununua tshirt hizi maalumu na kwa kujitokeza kutembetea nasi ili kuwezesha vijana wetu ambao ni taifa la kesho kupata elimu bora ,katika mazingira mazuri  na yaliyoboresha zaidi. Aliongeza Hawa
Airtel chini ya mpango wa”Airtel Tunakujali” unaoendeshwa na wafanyakazi katika vitengo mbalimbali umeshika kasi ambapo kitengo cha huduma kwa wateja kilifanya burudani na kumshirikisha banana zoro na mzee king Kikii na sasa kitengo cha rasilimali watu na ofisi ya mkurugenzi imeandaa matembezi ya hisani lengo likiwa ni kukusanya fedha kwa ajili ya kusaidia maeneo mbalimbali yanayozunguka jamii hususani kwenye elimu ambapo utekelezaji wake unategemea kutafanyika mapema mwakani.

KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI ARUSHA LEO

unnamed
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil   wa pili kutoka kushoto akimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bw.Adoh Mapunda muda mfupi kabla ya Bw. Mapunda kufungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kilichoanza leo jijini Arusha katika hoteli ya Corridor Springs unnamed1 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil   wa tatu kutoka kulia akimkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bw. Adoh Mapunda kwenda kufungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kilichoanza leo jijini Arusha katika hoteli ya Corridor Springs, wa kwanza kutoka kulia ni Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Abdulrahman Kaniki anayefuatia ni Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Sylivester Ambokile .
unnamed3
Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bw. Adoh Mapunda wa kwanza kutoka kulia akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil   baada ya Bw. Mapunda kufungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kilichoanza leo jijini Arusha katika hoteli ya Corridor Springs. unnamed4 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil   wa pili kutoka kulia akiimba wimbo wa Solidarity Forever pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wa pili kutoka kulia ni Katibu wa Baraza hilo la Wafanyakazi la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Jenitha Ndone.Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi limeanza leo jijini Arusha katika hoteli ya Corridor Springs.
unnamed5 
Sehemu ya wajumbe wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakiimba wimbo wa Solidarity Forever wakati wa kikao hicho, kinnachoendelea jijini Arusha katika hoteli ya Corridor Springs, wa pili kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Jamii Fidelis Mboya.
unnamed6 
Sehemu ya wajumbe wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakishiriki kikao hicho kinachoendelea jijini Arusha katika hoteli ya Corridor Springs, wa kwanza kutoka kushoto ni Avelin Momburi ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Fedha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).
unnamed8

SAIDI ALI MBAROUK AKUTANA NA BALOZI WA UFARANSA OFISINI KWAKE KIKWAJUNI MJINI ZANZIBAR.

unnamed
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk akizungumza na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Bi. Malika Berak alipomtembelea Ofisini kwake Kikwajuni. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar. unnamed1
Ofisa  Ubalozi wa Ufaransa anaeshughulikia Ushirikiano na Utamaduni Philippe Boncour akisisitiza jambo katika mazungumzo na Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Said Ali Mbarouk (hayupo pichani) Ofisini kwake Kikwajuni.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar. unnamed3 
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk akimkabidhi zawadi ya kanga Balozi Malika baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Wizarani kwake Kikwajuni. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.

MKUTANO WA MABALOZI NA WENYEVITI MASKANI WILAYA KUSINI UNGUJA.

unnamed1
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali alipofika katika viwanja vya  Visitors Inn  Hotel Jambiani Wilaya ya Kusini Unguja alipofika leo kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  akiwa katika ziara zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Unguja,{Picha na Ikulu.] unnamed2 Wasoma  Utenzi Nezi Khamis na Amina Haji kutoka Jambiani wakihani utenzi wao wakati wa Mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika  ukumbi wa Visitors Inn Hotel Jambiani Wilaya ya Kusini akiwa katika ziara zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM katika Mkoa wa Kusini Unguja, {Picha na Ikulu.] unnamed4
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai (kulia) Mwenyekiti wa Wilaya ya Kusini Unguja Abdul-Aziz Hamad Vuai wakiwa katika ukumbi wa Visitors Inn Hotel Jambiani Wilaya ya Kusini Unguja katika mkutano maalum wa kuimarisha Chama kwa Mabalozi na Wenyeviti wa Wilaya hiyo,{Picha na Ikulu.] unnamed5Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani Wilaya ya Kusini Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipookuwa akizungumza na Viongozi hao wa Mashina wa Jimbo la Muyuni katika ukumbi  wa Visitors Inn Hotel Jambiani Wilaya Kusini akiwa katika ziara zake za kuimarisha Chama Mkoa wa Kusini Unguja leo, {Picha na Ikulu.] unnamed6 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akipokea Risala ya Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika  ukumbi wa Visitors Inn Hotel Jambiani Wilaya Kusini wakati wa Mkutano maalum wa kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM katika Mkoa wa Kusini Unguja, {Picha na Ikulu.] unnamed8 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali alipofika katika viwanja vya  Visitors Inn  Hotel Jambiani Wilaya ya Kusini Unguja alipofika leo kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  akiwa katika ziara zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Unguja,{Picha na Ikulu.]

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA KIMATAIFA DAR

unnamed1 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Kongamano la Kimataifa la kuchochea mwamko wa nafasi ya mabingwa wa uchunguzi tiba katika kuboresha huduma za tiba. Kongamano hilo linalofanyika katika Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam, limewakutanisha mabingwa wa tiba za afya kutoka nchi mbalimbali za Afrika na nje ya Afrika. Picha na OMR
unnamed2 
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akihutubia katika ufunguzi wa Kongamano hilo leo Novemba 26, 2014. Picha na OMR
unnamed3Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akihutubia katika ufunguzi wa Kongamano hilo leo Novemba 26, 2014. Picha na OMR  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tunnamed5 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano hilo mara baada ya ufunguzi. Picha na OMR unnamed6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano hilo mara baada ya ufunguzi. Picha na OMR unnamed7
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi waratibu wa Kongamano hilo wakati alipowasili kwenye Hoteli ya Kunduchi Beach leo Novemba 26, 2014 kwa ajili ya kufungua rasmi kongamano hilo. Picha na OMR unnamed4 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi waratibu wa Kongamano hilo wakati alipowasili kwenye Hoteli ya Kunduchi Beach leo Novemba 26, 2014 kwa ajili ya kufungua rasmi kongamano hilo. Picha na OMR

BILIONEA DANGOTE AKAGUA TENA UJENZI WA KIWANDA CHAKE CHA SARUJI MTWARA

 Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote (Dangote Industries Group), mfanyabiashara maarufu Afrika, Alhaji Aliko Dangote akitumia gari kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda chake kikubwa cha saruji katika Kijiji cha Msijute, mkoani Mtwara leo.
Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote
(Dangote Industries Group), mfanyabiashara maarufu Afrika, Alhaji Aliko Dangote (kushoto) akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Dangote nchini, Esther Baruti kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara leo.
 Ndege ya bilionea huyo wa Afrika, Alhaji Dangote ikitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara
 Alhaji Aliko Dangote kutoka Nigeria, akilakiwa na Mwakilishi Mkazi wa Dangote nchini, Esther Baruti alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara leo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Balozi wa Nigeria nchini, Dk. Ishaya Manjanbu akimlaki Alhaji
Dangote.
 Dangote akiwa na Mwakilishi Mkazi wa Kampuni yake hapa nchini, Esther Baruti
Dangote akikaribishwa na viongozi wa kampuni ya Dil & Sinoma
alipowasili eneo la Kiwanda cha simenti cha Dangote.
 Alhaji Dangote akiwa na maofisa wake  katika kikao na viongozi wa kampuni inayojenga kiwanda hicho ya Dil & Sinoma kwa ajili ya kupewa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho ambacho kitakuwa cha tatu kwa ukubwa Afrika.
 Waandishi wa habari wakimhoji Dangote kuhusu maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho
           Alhaji Aliko Dangote
Alhaji Dangote akiwa kwenye msafara wa magari akikagua maendeleo ya ujenzi ya kiwanda cha saruji Mtwara
Mwakilishi Mkazi wa Kampuni hiyo ya Dangote hapa nchini, Esther Baruti akiwa na mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni ya Dangote
Alhaji Dangote akisindikizwa kwenda kupanda ndege kwenda nchini Ethiopia kuendelea na ziara yake
Ofisa Mnadhimu wa Poilisi Mkoa wa Mtwara, George Salala akiagana na Alhaji Dangote
Alhaji Dangote akipanda ndege tayari kuondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Mtwara
Mwakilishi Mkazi wa Dangote hapa nchini, Esther Baruti akiondoka baada ya kuagana na Dangote
Ndege iliyombeba Alhaji Dangote ikipa

MWILI WA MPENDWA WETU SEBASTIAN MGIMBA WAPUMZISHWA KWA AMANI KATIKA MAKABURI YA KINONDONI

 Ndugu wa Marehemu Sebastian Mgimba Philipo Mgimba (katikati) akiwa amebeba msalaba huku pembeni ndugu mwingine akiwa pamoja na picha ya marehemu wakati wa misa fupi ya mazishi yaliyofanyika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar Es Salaam leo.
Dada wa Marehemu Sebastian Mgimba, Mariam akiwa na ndugu zake wakati wa sala ya mazishi iliyofanyika katika makaburi ya Kinondoni leo
 Rafiki wa Marehemu akiweka udongo kwenye kaburi la Marehemu Sebastian Mgimba mara baada ya sala fupi ya mazishi kufanyika
 Baba Mzazi wa Marehemu Sebastian Mgimba, Mzee Mgimba pamoja na Mama wakiwa na shada la maua tayari kwa kuweka juu ya kaburi la Mtoto wao Marehemu Sebastian Mgimba
 Ndugu wa Marehemu Sebastian Mgimba wakiweka shada la Maua juu ya kaburi la Marehemu Sebastian Mgimba
 Dada wa Marehemu Sebastian Mgimba, Bi Mariam Lukaza akiwa na mumewe Johnson Lukaza wakijiandaa kuweka shada la Maua juu ya Kaburi la Marehemu Sebastian Mgimba katika mazishi yaliyofanyika leo katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar Es Salaam.
Mama Leoncia Lukaza akijiandaa kuweka Shada la Maua kwa niaba ya familia ya Lukaza katika kaburi la Marehemu Sebastian Mgimba kwenye mazishi ya marehemu Sebastiani Mgimba yaliyofanyika leo katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar Es Salaam.
Umati wa Watu waliojitokeza kwaajili ya Kumpumzisha Ndugu yetu Sebastian Mgimba katika makaburi ya Kinondoni.Picha na Josephat Lukaza – http://www.josephatlukaza.com

Marehemu Sebastian Mgimba alifariki dunia tarehe 20 Nov 2014 nchini Malaysia, Marehemu ameacha Mke na mtoto mmoja. Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Peponi Amin

SIKU YA TAKWIMU AFRIKA KUADHIMISHWA KESHO NOVEMBA 27-2014 UKUMBI WA JUMBA LA MAKUMBUSHO MKABALA NA CHUO CHA USIMAMIZI WA FEDHA (IFM) JIJINI DAR ES SALAAM

 Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Iphrahim Kwesigabo, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu Siku ya Takwimu Afrika itakayo adhimishwa Dar es Salaam kesho. Kulia ni Mtakwimu Mkuu, Adella Ndesengia.
 ” Nilazima picha hii niipate hata iweje’ kama anaongea Ofisa Habari wa NBS, Veronika Kazimoto wakati akichukua taarifa hiyo kwa njia ya picha- kweli mama yupo kazini -chezea kazi wewe.
 wanahabari wakichukua tukio hilo.
 Mkrugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Iphrahim Kwesigabo (kushoto), akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
………………………………………………………………………..
Dotto Mwaibale
OFISI ya Taifa yaTakwimu imeitaka jamii  kutoa ushirikiano wakati wa ukusanyaji wa taarifa za matumizi,kwamba husaidia kuandaa sera na kupanga mipango ya maendeleo nchini.
 
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam  na Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ephraim Kwesigabo wakati akitoa taarifa ya maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yatakayofanyika kesho.
 
“Maadhimisho ya siku ya siku ya takwimu Afrika hufanyika kila ifikapo Novemba 18 kila mwaka, kwa Tanzania tumechelewa kwa sababu ya utekelezwaji wa majukumu mengine ya kiserikali, hivyo maadhimisho hayo yanafanyika leo,” alisema Kwesigabo.
 
Kwesigabo alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuongeza ufahamu kuhusu nafasi na mchango wa tasinia ya takwimu katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii barani Afrika.
 
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa  kuwa ni Waziri wa Fedha kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Yosuf Mzee na kwamba wadau wengine watakaoshiriki ni  wizara, Idara na Taasisi za Serikali, wadau wa maendeleo,vyuo vya elimu ya juu,wadau wengine wa takwimu nchini.OFISI ya Taifa yaTakwimu imeitaka jamii  kutoa ushirikiano wakati wa ukusanyaji wa taarifa za matumizi,kwamba husaidia kuandaa sera na kupanga mipango ya maendeleo nchini.
 
Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam  na Mkurugezi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii,Ephaim Kwesigabo wakati akitoa tarifa ya maathimisho ya siku ya takwimu Afrika.
 
“Maadhimisho ya siku ya siku ya takwimu Afrika hufanyika kila ifikapo novemba 18 kila mwaka,kwa Tanzania tumechelewa kwa sababu ya utekelezwaji wa majukumu mwengine ya kiserikali,hivyo maadhimisho hayo yanafanyika leo,”alisema.
 
Kwesigambo alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuongeza ufahamu kuhusu nafasi na mchango wa tasinia ya takwimu katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii barani Afrika.
 
Mgeni rasmi anaetarajiwa katika maadhimisho hayo ni waziri wa fedha kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Yosuf Mzee na kwamba wadau wengine watakaoshiriki ni  wizara,Idara na Taasisi za Serikali,wadau wa maendeleo,vyuo vya elimu ya juu,wadau wengine wa takwimu nchini. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)

MAANDALIZI YA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA YAKAMILIKA KUFANYIKA DISEMBA 14-2014

  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali ya Mtaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, kuhusu maandalizi ya uchaguzi huo. Kushoto ni  Mkurugenzi Msaidizi Idara za Serikali za Mitaa, ambaye pia ni Mratibu wa Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa, Denis Bandisa. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)
  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali ya Mtaa (Tamisemi), Jumanne Sagini (katikati), akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano huo. 
 Mkurugenzi Msaidizi Idara za Serikali za Mitaa, ambaye pia ni Mratibu wa Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa, Denis Bandisa, akiwaonesha wanahabari daftari la kura wakati akitoa ufafanuzi wa masuala kadhaa.
 Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo kuchukua taarifa hiyo.
 
Dotto Mwaibale
 
WAKATI wananchi wakijishauri kujiandikisha katika uchaguzi wa serikali za mitaa, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (Tamisemi ) imekiri kuzorota kwa zoezi hilo,na hivyo kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo.
 
Akizungumza na waandishi wahabari Dar es salaam leo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Jumanne Sagini alisema kuzorota huko kumetokana na serikali kuchelewa kutoa elimu kwa wananchi na hivyo kusababisha kukosa muelekeo.
 
Alifafanua kuwa kwa kawaida uchaguzi huo hufanyika mwezi oktoba na hivyo waziri mkuu anatakiwa kutoa taarifa hiyo siku 30 kabla lakini kutokana na kuwepo kwa bunge lakatiba hali hiyo ilibadilika na hivyo kuiilazimu serikali kusogeza mbele mchakato huo.
 
“Nikweli hali hiyo ipo kama mnavyosema wandishi,lakini nyie ndio mnatakiwa kutusaidia kuzidi kutoa elimu,tumekuwa tukifanya vipindi katika vyombo mbalimbali vya habari lakini bado elimu inahitajika zaidi”alisema.
 
“Na wiki ya kwanza jambo hili lilionekana kuzorota kwa sababu ilikuwa ni wiki ya wagombea kuchukua fomu,wananchi wakajua ni siku ya kujiandikisha,lakini mchakato unakwenda vizuri kwasiku hizi mbili”aliongeza.
 
Sagini alipoulizwa na wandishi kuhusu mkanganyiko wa vituo vya kupigia kura alisema vituo vyoye vilivyopo katika mazingira ya huduma za Afya zinatakiwa kuondolewa na kupelekwa kwenye shule za msingi ilikuepusha usumbufu kwa kwa wagonjwa.
 
kauli hiyo ilitokana na kuwepo kwa kituo cha Zahanati ya Tandale kugeuzwa kuwa kituo cha uandikishaji kwa wapiga kura hali inayopeleka wagonjwa kulalamika kuwa wanapata usumbufu,hivyo kuwataka wahusika kuhamisha kituo hicho.
 
Akizungumzia bajeti ya uchaguzi huo, Mratibu wa uchaguzi Taifa, Denis Bandisa alisema serikali imetenga bilioni 20 kwa ajili ya uchaguzi huo ambapo,kati ya hizo bilioni nane kwa ajili ya malipo ya makarani,bilioni sita vifaa vya kujiandikishia,na bilioni sita kwa ajili ya matumizi mengine.
 
Hata hivyo Denis hakutaka kubainisha kuwa matumizi mengine ni yapi katika fedha hizo,na kusema kila karani atakuwa atalipwa sh. 10,000 kwa siku kutokana bajeti ya serikali kuwa ndogo.
 
“Kipindi cha mwanzo tlikuwa hatulipi kabisa,kwasababu sio kazi ngumu,ila kwasasa tukaona sio vema kwa sababu wanatumia nauri zao,tukaamua kutenga kiasi hicho cha fedha ila badae tutaangalia utaratibu wa kuwaongezea katika uchaguzi mkuu”alisema Denis.
 
Hata hivyo alitaja idadi ya kata zinazo husika na uchaguzi kuwa ni 3,802,mitaa 3741,Vijiji 12,443 na vitongoji 64,616.
 
Hata hivyo gazeti hili lilipa baadhi ya vituo na kushuhudia makarani wakisema kuwa kwasiku huandikisha wananchi 30.

STARTIMES YASHUSHA BEI YA VING’AMUZI VYAKE MSIMU HUU WA KUELEKEA SIKUKUU ZA KRISMASI NA MWAKA MPYA

  Meneja Mauzo, wa StarTimes, David Kisaka (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu StarMedia kushusha bei ya ving’amuzi vyake msimu huu wa Sikukuu. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Kampuni ya .Startimes, Jack Yu(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com)
 Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Kampuni ya 
Startimes, Jack Yu (kulia), akionesha moja ya siku za kisasa wanazoziuza msimu huu wa sikukuu.
 Ofisa wa Kampuni ya StarTimes, Lan Chen. akiwa mbele ya simu za kisasa zinazouzwa wakati wa kipindi hiki cha kuelekea kwenye sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 ……………………………………………………………………………………
Taarifa kwa vyombo vya habari
 
StarMedia yashusha bei ya ving’amuzi vyake msimu huu wa sikukuu.
·        Ni kutoka sh. 79,000/- mpaka 59,000/- ambapo endapo mteja akilipia kifurushi chochote na kufikia kiwango cha sh. 120,000/- atapatiwa simu ya bure aina ya S100 hii ni katika sharamshamra za msimu wa sikukuu za Krisimasi na Mwaka Mpya.
 
Dar es Salaam, Novemba 26, 2014 … Katika kuhakikisha kila mtanzania anapata fursa ya kufurahia huduma ya matangazo ya  digitali nchini kampuni ya StarMedia Tanzania wameamua kushusha bei ya ving’amuzi vyao vya StarTimes kutoka shilingi 79,000/- mpaka 59,000/- katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu za Krisimasi na Mwaka Mpya.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Mauzo wa kampuni hiyo, David Kisaka alibainisha kuwa bei hiyo iliyoshushwa ni kwa ving’amuzi vinavyotumia antena za nje na ndani au DTT na hii ni katika jitihada zetu kuhakikisha kila mtanzania anafikiwa na huduma zetu kwa gharama nafuu.
 
Kisaka amesema, “StarTimes tumedhamiria kuwahakikishia watanzania kuwa huduma zetu zitaendelea kuwa nafuu kulingana na hali halisi ya maisha tuliyonayo. Kulithibitisha hilo, ninayofuraha kubwa leo kuwatangazia bei mpya ya ving’amuzi vya antena za nje na ndani itakuwa ni shiling 59,000/- na sio shilingi 79,000/- kama ilivyokuwa awali. Bei hii mpya ni dhamira yetu ya dhati kabisa ya kuwapatia wateja matangazo ya digitali ya uhakika na kwa bei nafuu ambayo kila mtu ataimudu hata yule mwenye kipato cha chini kabisa.”
 
“Punguzo hili la bei linakwenda sambamba na ofa kabambe ambapo endapo mteja wa StarTimes atalipia kifurushi chochote kile na kunafikia kiwango cha shilingi 120, 000/- basi atapatiwa simu ya bure na ya kisasa kabisa aina ya S100 na hapa ninamaanisha kwa watumiaji wa ving’amuzi vya kawaida na madishi. 
 
Kwa ving’amuzi vya kawaida inamaana akilipia kwa kiwango hicho ni sawa na kulipia kifurushi cha Mambo kwa mwaka mzima (10,000/-), Uhuru kwa miezi sita (20,000/-) na Kili kwa miezi minne (30,000/-). Na kwa upande wa madishi pia ni hivyo hivyo endapo akilipia vifurushi vya smart ambacho ni shilingi 32,000/- na special kwa shilingi 16,000/-,” aliendelea Bw. Kisaka.
“Mbali na ofa ya punguzo la bei na zawadi za simu pia mteja wa StarTimes akilipia kifurushi chochote kwa miezi mitatu atapatiwa ofa ya mwezi mmoja wa bure na atakayelipia mwezi mmoja na nusu au siku 45 atapatiwa nusu mwezi au siku 15 bure,” alisema na kuongezea Bw. Kisaka, “Lengo la kufanya hivi ni kuwafanya wateja wetu waendelee kufurahia zaidi chaneli na vipindi vyetu na pia kuwashawishi waendelee kulipia zaidi na chaneli zingine ili kupata uhondo zaidi kwani haitoshi tu kutazama chaneli na vipindi vya nyumbani.”
 
“Hivyo basi ningependa kuwasihi wateja wetu na watanzania kwa ujumla ambao mpaka sasa bado hawajaunganishwa na huduma za StarTimes basi wakati ndio huu kwani tumewashushia gharama za chini kabisa kwa lengo la kumfikia kila mtu. Ili kuweza kupatiwa huduma zetu basi ningewaomba mtembelee ofisi na maduka yetu, kwa sasa tunayo maduka sita jijini Dar es Salaam likiwemo hili la hapa mtaa wa Samora, Tegeta, Buguruni, Bamaga, Msimbazi-Kariakoo na Ukonga huku mengine kumi yakiwa mikoani zilizo huduma zetu.” Alimalizia Bw. Kisaka
Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa StarTimes Tanzania, Jack Yu alitumia fursa hiyo pia kuwapatia watanzania habari njema kuhusu simu mpya na za kisasa zitakazopatikana katika msimu huu. 
“Kwa mara nyingine tena StarTimes tunawaletea simu za kisasa ambazo zitapatikana kwa bei nafuu kabisa katika maduka yetu ya Bamaga, Msimbazi na hili la Samora. Mbali na maduka hayo pia simu hizi zitapatikana kwenye maduka ya mawakala na washirika wetu kama vile Vodacom na Airtel.” Alisema Bw. Yu
“Simu hizi ambazo zitapatikana kwa bei nafuu ni zawadi yetu kwa wateja wetu na watanzania kwa ujumla watakaotembelea ofisi na maduka yetu. Aina ya simu ambazo zitakazopatikana ni P40 yenye garantii ya miezi 13, Planet 5 na Solar 5 ambayo mteja atapatiwa na power bank ya bure, zote hizi zitapatikana kwa bei ya shilingi 129,000/-, 225,000/- na 270,000/-”
“Simu hizi zina uwezo mkubwa wa kupata huduma zote ikiwemo kutumia laini mbili za simu, uwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu (memory card ya GB 8 ya bure) kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya matukio mbalimbali, kamera ya mebele na nyuma kwa kupiga picha nzuri na za kuvutia, uwezo wa kupata intaneti yenye kasi (3G) itakayokuwezesha kuperuzi mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter, Whatsap, Viber, Wechat na kadhalika. Ningependa kuchukua fursa hii kuwataka watu wajitokeze na kujinunulia simu hizi kwani ni chache.” Alihitimisha bosi huyo wa StarTimes. 

SEND OFF PARTY YA NOREEN MHINA YAFANA KATIKA UKUMBI WA DELUXE SINZA.

 
 Bibi Harusi Mtarajiwa Noreen Mhina  akiwa katika nyuso ya Furaha, jana tarehe 25.11.2014
  
 Bibi Harusi Mtarajiwa Noreen akiwa amempata Mume wake mtarajiwa Leonard  Baada ya kumsaka ukumbi Mzima kwa ajili ya kumtambulisha kwa wageni waalikwa .
 Bibi harusi Mtarajiwa Noreen akimvisha Mume wake mtarajiwa Leonard  zawadi ya Saa Mara baada ya kutambulishwa Rasmi wa wageni waliofika katika Sherehe ya kumuaga
Mc wa Sherehe hiyo ya Kumuaga Noreen Akiendelea na yake
 
 Bwana Harusi Mtarajiwa Leonard  akionesha zawadi yake ya saa aliyonunuliwa na Mke wake mtarajiwa Noreen ikiwa ni moja ya zawadi ya kufika kwake katika sherehe hiyo
 
 Mume Mtarajiwa Leonard  wa Noreen akiwa anamlisha  Chakula Mkewe Mtarajiwa ishara ya Upendo
Msemaji wa upande wa Bwana harusi mtarajiwa akiwakaribisha Rasmi katika harusi upande wa wazazi wa Noreen, Ndugu jamaa na marafiki na kutoa nasaha chache. Jana Tarehe 25.11.2014
Meza ya wazazi wa upande wa Bibi harusi mtarajiwa wakiwa wanasikiliza Nasaha kutoka kwa msemaji wa upande wa Bwana Harusi mtarajiwa.
Wadada wa Mujini nao walimwagia pesa za kutosha Noreen..
Baadhi ya Marafiki wakubwa wa Noreen aliosoma nao katika chuo cha CBE Dodoma
Palikuwa hapatoshi hapa ambapo Noreen na Bwana Harusi Mtarajiwa Leonard  pamoja na wageni wengine waalikwa walicheza kwaito ya nguvu..
Burudani ya Nguvu inaendelea hapa..
Kama kawaida wale mapaparazi wa kujitegemea hawakosi kupata ukodaki wa nguvu kwa ajili ya Facebook, Twitter, Instagram, Whatsapp na kwengine kwingi kuifanya sherehe kuwa inanoga zaidi
Baadhi ya Wageni waalikwa wakifuatilia Sherehe na kufurahi.
Bibi Harusi Mtarajiwa akiwa anapunga mikono kuaga wageni waalikwa ishara ya kuondoka ukumbini kwenda kupumzika na kujiandaa na harusi huku akisindikizwa na wapambe wa kutosha.
 
 

MATUKIO YA PICHA ZA KUJIANDIKISHA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

unnamed
Mkazi wa Mtaa wa Mivinjeni ,Evod Millinga(kushoto) akijiandikisha akionesha kitambulisho chake leo kwa mwandikishaji wa kituo cha cha kujiandikisha  cha kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Beatrice Likundo(kulia)  kilichopo kwenye Shule ya Msingi Mivinjeni jijini Dares Salaam. unnamed2
Mkazi wa Mtaa wa Mivinjeni , Asha Bakari (kushoto) akijiandikisha  leo kwa mwandikishaji wa kituo cha cha kujiandikisha  cha kura  kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Beatrice Likundo  kilichopo kwenye Shule ya Msingi Mivinjeni jijini Dares Salaam. unnamed3Mwandikishaji wa kituo cha cha kujiandikisha  cha kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Beatrice Likundo (kulia) kilichopo kwenye Shule ya Msingi Mivinjeni jijini Dares Salaam akimwandikisha jina leo  Mkazi wa Mtaa wa Mivinjeni ,Evod Millinga kwa ajili ya uchaguzi huo. unnamed4
Mkazi wa Mtaa wa Shimo la Udongo, Abdallah  Rashid Abdallah (kushoto) akitia saini leo   mara baada ya kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa leo jijini Dares Salaam katika kituo cha polisi cha Shimo la Udongo.Kulia ni mwandikishaji wa kituo hicho, Nongaki Hassan. unnamed5 
Mkazi wa Mtaa wa Mivinjeni ,Gilbert Katoto (kulia) akitia saini leo mara baada ya kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali Mitaa  katika kituo cha kujiandisha k cha Katakiu  kwa Bea  kilichopo kwenye  Mtaa wa  Mivinjeni  jijini Dares Salaam.Kushoto ni Mwandikishaji wa kituo hicho, Isabela  Mwera.
PICHA NA MAGRETH KINABO – MAELEZO

MATUKIO BUNGENI DODOMA


Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki na Mbunge wa Urambo, Samuel Sitta  (katikati) akizungumza na baadhi ya wabunge wa Upinzani, Bungeni mjini Dodoma Novemba 26, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
unnamed2 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizugumza na Mbunge wa Viti Maalum Rachel Mashishanga kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Novemba 26, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)