TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, April 25, 2015

MWALIMU NYERERE, BANDARI WATOSHANA NGUVU -NACTE INTER COLLEGE CHAMPIONSHIPS-KIGAMBONI.


-DACICO MWENDO MDUDO
-USTAWI WA JAMII YATUMIA VYEMA UWANJA WA NYUMBANI.

 Na: Mwandishi Wetu,

Michuano ya NACTE INTER COLLEGE CHAMPIONSHIPS TANZANIA-DAR ES SALAAM 2015, Leo imeendelea tena kwenye Viwanja vya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, ambako Timu za kundi A zimecheza na mchezo uliokuwa gumzo ni baina ya Chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere dhidi ya Chuo cha Bandari, ambapo hadi Mwisho wa Mchezo Timu hizo zimeweza kufungana 3-3.
Timu ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ndiyo waliokuwa wa kwanza kupachika mabao 2 kipindi cha kwanza, ambapo hadi timu hizo zinakwenda Mapumziko Mwalimu Nyerere ilikuwa mbele kwa 2-0.
Msaidizi wa Katibu Mkuu wa NACTE, Mheshimiwa Alex Nkondola wa kwanza kushoto, akipokea Kombe la Michuano ya NACTE INTER COLLEGE CHAPIONSHIPS TANZANIA 2015. wengine ni Mwanasheria Mkuu wa NACTE Exemarry Mize wa pili kushoto na wawakilishi wa Mawaziri wa Michezo wa Serikali za Vyuo Tanzana, Ladislaus Thumbu wa kwanza kulia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na Samweli Gukwi kutoka chuo cha Taasisi ya Elimu ya Watu wazima. Michuano hiyoinatazamiwa kufikia kilele May 30.
kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote zilifanya mabadiliko ya hapa na pale lakini ni ya Mwalimu nyerere tena iliyoweza kupata bao la tatu kabla ya Timu ya Bandari Kusawazisha mbao yote kwenye dakika za Mwisho za mchezo huo  ambao hakika ndiyo uliokuwa gumzo katika siku ya leo.
Mchezo mwingine ilikuwa ni kati ya IFM dhidi ya chuo cha Taasisi ya  Elimu ya Watu wazima, ambapo mchezo huo timu hizo zimekubali kugawana pointi moja moja sambamba na wenzao wa chuo cha Kilimanjaro kwa mama ngoma waliogawana pointi na chuo cha Taifa cha Usafirishaji(NIT).
Matokeo ya kundi la Uwanja wa Ustawi wa Jamii timu ya Chuo cha Biashara CBE, wamefanikiwa kujipatia Pointi zao 3 na magoli mawili baada ya timu ya chuo cha Uhasibu kushindwa kutokea Uwanjani katika kipindi kilichopangwa.
mchezo mwingine ilikuwa ni baina ya timu ya Chuo cha kodi ambao wamecheza na timu ya kitivo cha engeneering ya chuo Kikuu cha Dar es Salaam zimeweza kugawana Pointi baada ya timu zote kushindwa kufika Uwanjani.

wakati mchezo wa Mwisho wenyeji timu ya chuo cha ustawi wa jamii imeweza kujipatia Ushindi mnono wa Mabao mawili na hivyo kujizolea pointi zote tatu dhidi ya timu ya chuo cha Wauguzi wa Muhimbili, ambapo michezo hiyo awali ilipangwa kufanyika kwenye Viwanja vya chuo Kikuu cha Dar es Salaam lakini imelazimu kubadili Uwanja kutokana na Viwanja vya Chuo Kikuu kuwa na ratiba katika kipindi hiki hivyo michezo yote sasa itafanyika kwenye viwanja vya Ustawi wa jamii katika hatua hii ya makundi.
Kundi B ambao michezo yake inafanyika kwenye Viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha, mchezo wa kwanza ulizikutanisha timu za chuo cha St.Joseph, ambapo katika mchezo timu ya St. JOSEPH ilifanikiwa kuibua na ushindi wa mabao mawili kwa bila (2-0) dhidi ya timu ya chuo cha Njuweni Insititute.
mchezo mwingine Timu ya chuo cha Wauguzi Tumbi ikafanikiwa kupata Point 3 baada ya kujipatia mabao mawili dhidi ya kitivo cha UDBS ambao walishindwa kutokea uwanjani kabla ya DACICO kidedea dhidi ya timu ya chuo cha taifa cha Teckinolojia (D.I.T) .
Washindi wawili katika kila kundi ndiyo watakaoingia hatua ya Robo fainali itakayoshirikisha jumla ya timu nane huku timu mbili zikipewa nafasi ya kuingia kwa njia ya upendeleo(Best Looser).
Michezo hii inaratibiwa na Kampuni ya Miss Demokrasia Tanzania & Enter tainment C.o Ltd, ya jijini Dar es Salaam kwa Udhamini wa NACTE, SBC TANZANIA, Vodacom, CXC Tours, Zinduka, Mlimani Radio & Mlimani Tv, Clouds Media, Michuzi Media, Tanzania Daima, Free Media, Global Publishers, Gazeti la Champion, Njuweni Institute Kibaha na Mpaluleblog:

Mawasiliano Tupigie: +255-713-86-91-33 au +255-767-8691-33

Friday, April 24, 2015

PEPSI YANG'ARISHA MAONYESHO YA SYRIAN YAFUNGULIWA LEO DIANOND JUBILEE HALL- JIJINI DAR ES SALAAM.

 Baadhi ya wanafunzi jijini Dar es Salaam, ndani ya maonyesho ya hayo
 Baadhi ya wanafunzi jijini Dar es Salaam, ndani ya maonyesho.
 Baadhi ya wanafunzi jijini Dar es Salaam, ndani ya maonyesho.
 Baadhi ya wakazi wa jiji wakiwa kwenye Mapumziko kwenye mabanda ya Pepsi
 wakazi wa jiji wakipumzika kwenye mabanda ya Pepsi
 wakazi wa jiji baada ya kufurahia maonyesho hayo
 Baadhi ya wafanyabiashara jijini wakiwa kwenye maonyesho ndani ya Viwanja vya Diamond jubilee
 Baadhi ya wafanyabiashara jijini wakiwa kwenye maonyesho ndani ya Viwanja vya Diamond jubilee
Fuatilia Maonyesho hayo kupitia hapa hapa kila siku, au piga simu +255-713-869133