TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 25, 2015

Amazing Talent ! Haya sasa wanao muweza He Kills The Dance !




TUKIO LA KUSIKITISHA LILILOWAHI KUTOKEA




MAREKANI YAZIDI KUWA GUMZO



MICHEZO YA HATARI DUNIANI WATANZANIA WATAKA KUINGIA KWENYE MAPAMBANO WWE



angalia maajabu ya huyu kijana Msanii wa wasanii duniani




BULEMBO AGEUKWA NA WAJUMBE WAKE SAKATA LA KWENDA KWA LOWASSA
















Life of Pageant Planet Episode 10



Mbunge wa Monduli Edward Lowassa ameibuka na kupinga tuhuma zilizotolewa na baadhi ya watu kwamba amekusanya makundi ya kumuuga mkono huku akidai hana sababu ya kufanya hivyo na hana uwezo wa kuwagharamia watu hao wanao muunga mkono.




Monday, March 23, 2015

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA WAWEKEZAJI WA NCHI 5 ZA AFRIKA MASHARIKI.

Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
23/3/2015. Dar es salaam.

Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa wawekezaji (Round Table Investment Forum) na Marais wa nchi 5 za ukanda wa Afrika Mashariki utakaofanyika jijini Dar es salaam kuanzia  Machi 25 hadi 26 mwaka huu. 

Akitoa taarifa ya mkutano huo Mkuu wa wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki  amesema kuwa Marais hao Paul Kagame wa Rwanda, Pierre Nkurunzinza wa Burundi, Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyatta wa Kenya na Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo watahudhuria mkutano huo wakiwa wameambatana na  jumla ya wawekezaji 350.

Amesema Tanzania kwa mara nyingine imepata heshima ya kuandaa mkutano huo na kufafanua  kuwa wawekezaji hao wamekwisha anza  kuwasili jijini Dar es salaam kuanzia  Machi 22 , Machi huku marais nchi hizo wakitarajiwa kuwasili jijini humo kuanzia Machi 24,2015.

Amesema wakiwa nchini Tanzania Marais hao watashiriki kwenye mkutano wa wawekezaji utakaofanyika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Mwalimu J.K.Nyerere kuanzia Machi 23 hadi 26, watatembelea bandari ya Dar es salaam ili kuona namna nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki zinavyoshirikiana katika masuala ya ushuru wa forodha na usafirishaji wa bidhaa mbalimbali.

Amebainisha kuwa kabla ya kuaondoka nchini  Tanzania Machi 26, 2015 Marais hao pia watatembelea miundombinu ya reli inayotumika kusafirisha mizigo nchi za maziwa makuu kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika usafirishaji wa bidhaa mbalimbali baina ya nchi zao.

KUHUSU  MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA JIJINI DAR ES SALAAM.

Aidha, kuhusu mvua zinzoendelea kunyesha katika jiji la Dar es salaam  na kusababisha madhara, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki amewataka wananchi kuzingatia agizo la kuhama mabondeni na maeneo mengine hatarishi ili waepuka maafa kufuatia watu 7 kupoteza maisha kutokana na kutokana na athari za mvua zinazoendelea kunyesha.

Akifafanua kuhusu matukio hayo Mhe. Sadiki amesema maeneo yaliyokumbwa na mafuriko hayo  na kupata maafa hayo ni bonde la Mto Msimbazi na eneo la Buguruni kwa Myamani.

Amesema kuwa maeneo yaliyokumbwa na mafuriko hayo yameonekana kuwa  na wingi wa takataka ngumu na wingi wa mifuko ya plastiki  iliyotupwa na wakazi hao hali iliyochangia kuziba mifereji inayopeleka maji katika bonde la mto Msimbazi na maji hayo kuhamia kwenye makazi ya watu.

Ameeleza kuwa kazi ya uokoaji , kumwaga dawa kwenye maji yaliyotuama ili kuzuia athari ya magonjwa ya milipuko, kuzibua mifereji na kukusanya taka katika maeneo hayo inaendelea ili kuruhusu maji kupita kwa urahisi  na kuwataka wakazi hao kuepuka kutupa taka ngumu zinazoziba mifereji ya maji.

Amesema Serikali inasubiri taarifa kutoka kwa viongozi wa Serikali za Mitaa kwa maeneo ambayo wakazi wake wanaishi kihalali ili waweze kupatiwa misaada ya kibinadamu.

Kwa upande wake Kamishina wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova amethibitisha vifo vya watu hao 7 waliopoteza maisha kutokana na maeneo yao kukumbwa na mafuriko pamoja na athari ya Umeme.

Akitoa ufafanuzi wa vifo hivyo amesema kuwa watu 5 wamepoteza maisha kwa kusombwa na maji na wengine 2 wamepoteza maisha kutokana na ajali iliyosababishwa na Lori moja kugonga Transfoma ya umeme eneo la Buguruni Mnyamani.

Kamishna Kova amesema tayari Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji na Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) wameunda kikosi kazi cha uokoaji.

Ametoa wito kwa madereva wa magari ya mizigo, mgari binafsi na yale ya abiria kuepuka kupita katika maeneo yaliyojaa maji ili kuepuka ajali na vifo vinavyoweza kuzuilika.
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akitoa taarifa ya mkutano wa wawekezaji (Round Table Investment Forum) na wakuu wa nchi 5 za ukanda wa Afrika Mashariki utakaofanyika jijini Dar es salaam kuanzia  Machi 25 hadi 26 mwaka huu.
Kamishina wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova akitoa taarifa ya hali ya ulinzi na usalama katika jiji la Dar es salaam na vifo vya watu  7 waliopoteza maisha  kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa  zinazoendelea kunyesha katika jiji la Dar es salaam.

The fallout reached a fever pitch at at New Galilean Baptist Church this Sunday.


NINI MTAZAMO WAKO KUHUSU BUNGE LETU NA SERA ZA VIONGOZI WETU?


ANGALIA TECKNOLOJIA ILIPOFIKIA KATIKA UPIKAJI WA MANDAZI