TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 6, 2014

Kinana ahutubia mkutano Mkuu wa 6 wa ZANU PF Harare -Zimbabwe

unnamed
unnamed3
Baadhi ya viongozi mashuhuri na wajumbe walihudhuria mkutano huo
pppppppppp3 Ndg. Kinana akihutubia mkutano Mkuu wa ZANU PF
ppppppppppppp4 Ndg. Kinana akisalimiana na Rais Robert Mugabe mara baada ya kuhutubia mkutano huo
……………………………………………………………………………………………………………………………….. KATIBU Mkuu wa CCm Ndg. Abdulrahaman Kinana , amekipongeza Chama Cha ZANU PF Cha Zimbabwe kwa kusimama imara licha ya Changamoto mbalimbali zimazoikabili Zimbambwe ikiwemo vikwazo vya kiuchumi ambavyo vimewekwa dhidi ya nchi hiyo.
Amewataka wana ZANU PF kuendelea kuunga mkono chama chao na kuongeza mapambano dhidi ya maadui wote wanaotaka kurudisha nyuma jitihada za kupigania maslahi ya nchi yao.
Akisoma salamu za mshikamano za Chama Cha Mapinduzi kwenye mkutano Mkuu wa ZANU PF unaofanyika mjini Harare Ndg. Kinana aliwakikishia wana ZANU PF na wana Zimbabwe wote kuwa katika mapambano hayo CCM iko nyuma yao na kwamba haitaacha kupaza sauti dhidi ya vikwazo vya uchumi ilivyowekewa Zimbabwe.
Alisema vikwazo hivyo having uhalali na kwa ujumla wake vinatoa adhabu isiyo ya haki kwa Wananchi wa Zimbabwe wasio na hatia.
Ndugu Kinana alimpongeza Rais Mugabe ujasiri na kwa msimamo wake usioyumba wa kupigania maslahi ya wana Zimbabwe licha ya vitimbi vya wapiga maendeleo.
Alisema ujasiri na msimamo wa Mugabe pamoja na Chama anachokiongoza Cha ZANU PF ndiyo uliowezesha Zimbabwe kusimama ilivyo hivi sasa kama Taifa huru na lisilikubali kuyumbishwa.
Alisema Mugabe na Chama chake wameonyesha kwa mfano kwamba kume watu wakisimama imara chini ya uongozi wa chama imara hakuna anayeweza kukwamisha nyendo zao za kimapinduzi zinazoendana na matakwa ya umma.
Akizungumzia ushindi wa kishindo wa ZANU PF kwenye uchaguzi Mkuu June mwaka jana Kinana alisema hicho ndicho kiashiria cha kukubalika kwa Chama na sera zake.
Alisema CCM inaipongeza ZANU PF kwa ushindi huo na kwamba wana CCM wanajisikia fahari sana wanapoona ZANU PF ikiendelea kukua na kuimarika.
Aisha Ndg. Kinana alimpongeza Rais Mugabe na kueleza kuwa CCM na Watanzania kwa ujumla wanafurahishwa na msimamo wa dhati alionyesha Rais Mugabe katika majukwaa mbalimbali ikiwemo mkutano wa wakuu wa nchi za SADC uliofanyika Victoria Falls wa kueleza umuhimu wa kutambua na kuheshimu mchango wa Mwalimu Nyerere katika ukombozi wa Afrika na hasa kusini mwa Afrika.
Hotuba ya Ndg. Kinana ilipokelewa kwa shangwe na furaha kubwa sana na wajumbe wa mkutano huo ambao mara kwa mara walishangalia kuashiria kuridhika na kauli za kimapinduzi na kidugu kutoka kwa wana CCM.
Ndugu Kinana na ujumbe wake wataondoka kesho kurejea nyumbani. Ujumbe wa Katibu Mkuu kwenye mkutano ulimhusisha pia Mjumbe wa halmashauri Kuu ya Taifa CCM Ndg. Phares Magesa na afisa wa makao makuu ya CCM Ndg. Thobias Mwilapwa

Miss Tanzania at miss world in London 2014

kkkkkk kkkkkk2 kkkkkk5 kkkkkkkk3 kkkkkkkkk1Miss happiness is in town in time for the festive season, the she will experience the famous Christmas spirit that can be found in England’s capital city. For a little over 3 weeks, the contestants will experience the wonder of England’s vibrant multicultural metropolis whilst she takes part in the Miss World Challenge Events and prepare herself for the Big Final!
Events start from 20th November, culminating in the Grand Final on 14th December. She is in high spirit and for the first time , Tanzania has a big chance of becoming one of the big three.
Tanzanians and friends of Tanzania, there is so much you can do to help her out:
 So how does it work?
 Simply download the Miss World App, and you will find you have three slots available for your vote. Once you have decided who your top three are, you can lock in your vote and voila!, you have helped your favourite contestants on their way to being the People’s Choice Award Winner! The winner of the People’s Choice Award is announced during the latter stages of the Miss World Final, and the winner, if she is not already selected, will join the final few contestants on stage. These contestants will then face the judges questions before the winner of Miss World 2014 is announced!
                                                            How many votes do I get?
 This year, you will be allowed one set of three votes, with a bonus set of three votes if you choose to subscribe to the app, which also includes the full Miss World TV coverage of the competition. The most votes any one contestant can receive from an individual is 2 votes. Each set of votes must be for 3 different contestants.
 I can’t find the voting page on the App, am I doing something wrong?
 Voting begins on the 20th of November. Until then you will not be able to vote for your favourite contestant. This is to ensure no votes are lost if a contestant has to pull out at the last minute!
 I haven’t decided yet who my 3rd favourite is, when do I have to submit my vote?
Don’t worry! You have plenty of time to decide. The app will hold onto your choices until you make your final submission. Voting closes one hour after the start of the Miss World Final Show. Once you have submitted your votes, there is no going back, so make sure you vote right!
The time is now to support Tanzania beauty at the world stage

Friday, December 5, 2014

60 wanusurika kufa mtoni

Mkuu wa wilaya ya Busega, Paul Mzindakaya

Zaidi ya abiria 60 waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya Mwanza Coach, kwenda Musoma mjini wamenusurika kufa baada ya tairi la mbele kupasuka na kutumbukia mtoni.

Tukio hilo limetokea juzi na kulihusisha basi lenye namba za usajili T714 BJB ambalo baada ya tairi kupasula liliacha kuacha njia.

Mkuu wa wilaya ya Busega, Paul Mzindakaya, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba watu tisa walipata michubuko kidogo baada ya basi hilo kutumbukia katika daraja la Mto Masanza kata ya Kiloleli wilayani hapa.

Alisema baada ya tairi kupasuka basi hilo lilipoteza mwelekeo hatimaye kutumbukia katika mto huo uliokuwa umejaa maji kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha wilayani hapa. Kwa upande wake dereva wa basi hilo, Edward Juma, alisema baada ya tairi kupasuka alijitahidi kulizuia gari hilo lisitumbukie mtoni lakini ilishindikana.

Naye mmoja wa abiria wa basi hilo, Mary Mwita, aliyekuwa akitoka Musoma kwenda Mwanza, alisema kazi kubwa iliyofanywa na dereva wa basi hilo ilisaidia kuokoa maisha yao.

Abiria mwingine Francis Mongela, alisema iwapo dereva wao asingekuwa makini basi hilo lingesababisha vifo vya abiria wengi.

Askari wa jeshi la polisi, Joseph Christopher wa kituo cha Busega aliyekuwa akipeleka mahabusu wilayani Magu, alisema basi hilo lilikuwa katika mwendo wa kawaida na iwapo mwendo ungekuwa wa kasi ingesababisha maafa makubwa.

Kampuni ya Mwanza Coach na ile ya J4, yalifungiwa na serikali kuendesha huduma za usafishaji abiria kati ya Mwanza na Musoma baada ya kugongana na kusababisha vifo vya abiria zaidi ya 30 eneo la sabasaba wilayani Serengeti Agosti mwaka huu.

Wakati huo huo, Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imesema kuwa mvua za vuli zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya mikoa mbalimbali nchini zinatarajia kufikia ukingoni katika maeneo ambayo kwa mwaka hupata misimu miwili ya mvua.

Mkurugenzi wa Utabiri wa mamlaka hiyo,Dk. Hamza Kabelwa, alisema mvua za vuli na msimu zinakaribia kufikia ukingoni ili msimu wa mvua za masika kwa baadhi ya maeneo ambayo hupata mvua kwa misimu miwili kuanza kunyesha.

“Hizi ni mvua za vuli na msimu wala siyo mvua za masika kama ambavyo wananchi wanafikiria, wakati ukifika tutatoa taarifa kuwajuulisha Watanzania,”alisema.

Mtandao wa Kuchepuka wa Zari the Lady Boss ni Kiboko Diamond ni wa 13


diamond na zari the boss

 Ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha kila kukicha, mrembo tajiri mwenye maskani yake nchi jirani ya Uganda na Afrika Kusini, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady, anadaiwa kuwa na mtungo mrefu wa wanaume ambapo kama ni kweli anatoka na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ basi jamaa huyo atakuwa anashika nambari 13.
Kwa mujibu wa jarida la linalodili na habari za showbiz (biashara ya shoo) la E-Vibe la nchini Uganda la hivi karibuni, Zari ambaye wikiendi iliyopita alimng’arisha Diamond katika zulia jekundu kwenye Tuzo za Channel O (Choamva) zilizofanyika Johannesburg nchini Afrika Kusini ‘Sauz’, anadaiwa kuwa ‘klozi’ na idadi hiyo ndefu ya wanaume.
Jarida hilo lilieleza kwamba ndani ya kipindi cha miaka 14 baada ya kutimiza umri wa mtu mzima wa miaka 18, Zari mwenye umri wa miaka 32 sasa, ameshajiachia na wanaume wa kada mbalimbali wakiwemo vigogo serikalini, wafanyabiashara, mastaa wa tasnia mbalimbali na hata vijana wadogo.

MABUSU

Kabla ya Diamond, picha za Zari zilivuja akiwa anabusiana kwa hisia na mwanaume, Farouk Sempala anayesifika kwa dili za mjini. Mara nyingi, Zari amekuwa akishangaza watu na kuacha maswali kuwa nini huwa kinamsukuma kumzoea mwanaume haraka na kuingia naye kwenye urafiki?
Kwa mujibu wa jarida hilo, kuna mtandao maalum wa kundi la watu uliundwa kwa ajili ya kufuatilia nyenendo za Zari katika sekta ya mapenzi ndipo data zikamwagwa.

MUMEWE

Jarida hilo liliweka wazi baadhi ya wanaume walioko kwenye listi hiyo kuwa ni pamoja na mumewe, Ivan Semwanga ambaye alizaa naye watoto watatu kabla ya kumwagana mwaka jana bila talaka.

STAA WA KIKAPU

Mwingine anayetajwa kwenye listi hiyo ni Isaac Lugudde ambaye ni staa wa mpira wa kikapu nchini Uganda. Hata hivyo naye hakudumu naye.

MIKONONI MWA MTOTO WA MJINI

Lilidai kwamba baada ya Zari kuondoka kwa mumewe Semwanga na  kumwacha na watoto nchini Afrika Kusini, mwanadada huyo aliangukia kwenye penzi la mtoto wa mjini nchini Uganda, Farouk Sempala ambaye aliposikia tetesi kuwa anatoka na Diamond ndipo akatangaza kuachana naye.

WENGINE

Wengine waliotajwa katika jarida hilo ni pamoja na Jenerali Jeje Odong, wasanii wa muziki, Mozed Radio na  Weasel. Katika listi hiyo ndefu pia wamo Aziz Azion, Isaiah, Robert Ogwal a.k.a Rasta Rob, Exodus, Dj Shiru, mfanyabiashara wa Nigeria na sasa ni zamu ya Diamond.

DIAMOND NA ZARI

Awali walianza kama utani ikisemekana kwamba kuna ‘projekti’ wanaifanya kwa kuwa wote ni mastaa wa Afrika Mashariki.
Hata hivyo, kwa kadiri siku zilivyosonga mambo yakazidi kuwa hadharani na sasa kila kitu kipo wazi na kwamba kama hujui kusoma, angalia picha wanavyojiachia kama baba na mama.
Wakiwa nchini Afrika Kusini wikiendi iliyopita, Zari anadaiwa kujitambulisha rasmi kwa mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ ambapo walikuwa beneti hadi watu wakawa wanamsifia Zari kwa kujua umuhimu wa mama mkwe na kumhudumia vizuri.

ZARI ANASEMAJE?

Kwa kuwa kila tukimuuliza Diamond ana uhusiano gani na Zari amekuwa akichenga, kwa upande wa mwanadada huyo amekuwa akichekacheka na kudai wapo kikazi zaidi huku akimsifia jamaa huyo kwenye mitandao ya kijamii.

TATIZO UMRI

Kwa mujibu wa makabrasha ya gazeti hili, Diamond ana umri wa miaka 25 wakati Zari ana miaka 32 hivyo amemzidi kwa miaka 7 hivyo kuonekana ‘anambemenda’ Mbongo Fleva huyo.

WATOTO

Mwanadada Zari ana watoto watatu aliozaa na mumewe, Semwanga huku Diamond akiwa hana hata wa kusingiziwa (kama yupo mwenye mtoto wa Diamond ajitokeze).

WEMA AMWITA DIAMOND KAKA

Tofauti na walivyozoea kuitana ‘Baby’, siku hizi upepo umebadilika kwani aliyekuwa mwandani wa Diamond, Wema Isaa Sepetu amekuwa akimwita jamaa huyo kaka, siku alipompongeza kwa ushindi huo na hivyo kuibua maswali ya kufa mtu.

WABONGO WATAKUNYIMA MSOSI SI MANENO

Wakizungumzia uhusiano wa Diamond na Zari, Wabongo waliozungumza na gazeti hili walionekana kugawanyika.
Wapo waliodai kuwa mwanamama huyo haendani na Diamond kwa kuwa umri umeenda lakini wapo wanamsifia jamaa huyo kwa kufanikiwa kumnasa Zari mwenye umbo bomba, mrembo ambaye fedha zimemtembelea.

CHADEMA HAKINA MFUMO THABITI WA KIUONGOZI WA KUUNDA SERIKALI YA TANZANIA MWAKA 2015.


 
NAIBU Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema anatamani kuona Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikiingia Ikulu, ikibidi katika Uchaguzi Mkuu wa 2015. 
Ndugai, amesema hatua hiyo inatokana na jinsi umma na taasisi zake vikiwamo vyombo vya habari, ‘vinavyokibeba’ chama pasipo hicho kutafakari kuhusu udhaifu wa Chadema.


Naibu Spika alisema, Chadema ni chama kinachoungwa mkono, lakini hakina mfumo thabiti wa kiuongozi unaoshawishi ama kukipa hadhi ya kuunda serikali.

“Lakini sasa watu wanakiona kama ndio mbadala kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kitu amba

cho si kweli…ninatamani sana kuiona Chadema inaingia Ikulu ili watu wauone udhaifu huo na waandishi wataiandika vipi itakapokuwa madarakani,” alisema.

Ndugai alisema pamoja na azma hiyo inayolenga kuiaminisha jamii kwamba Chadema haina mfumo bora wa uongozi, CCM inabaki kuwa chama imara, lakini kikikabiliwa na changamoto mbalimbali.
 
Alisema, miongoni mwa changamoto hizo ni dalili za kuporomoka kwa umoja miongoni mwao, huku miongoni mwao wakielekea katika kuzitukuza pande za Muungano wanazotoka.


“Hata ndani ya Bunge wakati mwingine unaweza kuona mgawanyiko kwa wabunge wa CCM, lakini sasa bado kinaendelea kubaki kuwa chama tawala,” alisema.
 
Mbunge mmoja wa Chadema ambaye hata hivyo hakutaka jina lake kutajwa gazetini, aliungana na Ndugai, kwa nyakati tofauti, akisema chama hicho bado kina upungufu katika safu yake ya uongozi.
 
Kwa mujibu wa Mbunge huyo, uongozi wa Chadema bado unakabiliwa na changamoto nyingi kuanzia maadili binafsi, stadi na uwezo wa ki-uongozi katika kuchukua madaraka ya nchi.


“Tunakabiliwa na changamoto nyingi ambazo kwa Bahati mbaya, viongozi wetu hawapo tayari kutusikiliza sisi tulio ndani, matokeo yake ni kupunguza kasi ya ukuaji wake,” alisema.
 
Hata hivyo, Mbunge huyo alisema Chadema inahitaji kupata wabunge wengi katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 na viongozi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji mwakani, ili kukifanya kitime wajibu wa kujiimarisha katika ngazi za msingi.


Alisema uwepo wa wabunge wengi wa Chadema, kutasaidia kuchagiza kasi ya mabadiliko hasa ya kimfumo ikiwa ni njia ya kukifanya chama hicho kikidhi hitaji la kuunda serikali kwa miaka ijayo.
 
 

VITA DHIDI YA UFISADI.
 

Mbunge huyo aliikosoa Chadema kwa namna inavyoshiriki vita dhidi ya ufisadi, na kusema inawakwaza baadhi ya watu wenye uwezo mkubwa kujiunga. 
Alisema ni kweli kwamba ufisadi hautakiwi kwa vile unakwamisha azma ya kufikia maendeleo endelevu na ustawi wa jamii, lakini nadharia inayoelekezwa kwa baadhi ya viongozi, pasipo kujali uadilifu wao na uwezo wa kiuongozi, unakifanya chama hicho kuwakosa ‘watu makini’ zaidi.
 
“Kuna watu wengi ambao wakijiunga Chadema, CCM itapasuka na kuwa mwanzo wa kuondoka madarakani, lakini wanashindwa kuja kwa sababu wameshatajwa na wengine wanaogopa kuhusishwa na ufisadi,” alisema.
 
 

CHADEMA YAMJIBU.
 

Hata hivyo, Chadema imemkosoa Ndugai na kusema kiongozi huyo ameonyesha udhaifu katika kuliongoza Bunge. 
“Ndugai ameonesha udhaifu kuliongoza Bunge na mara zote, udhaifu huo uliibuliwa na kuwekwa wazi na wabunge wa CHADEMA, hawezi kusema chama kina uwezo duni wa kiuongozi,” alisema Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene.
 
Makene, alisema kwa takribani miaka 10 sasa, Chadema kupitia viongozi na wabunge wake, imekuwa ikiilekeza serikali ya CCM (kwa niaba ya Umma), namna bora ya kuutumikia umma, ingawa (serikali hiyo) sio sikivu.
 
Alisema umma unakiunga mkono chama hicho kutokana na wanaona ubunifu, matumaini, haki, uwezo, ufahamu, umakini, uwajibikaji, utayari, maadili, misimamo na mawazo mbadala kwa ajili ya maslahi ya watanzania.
 
“Watanzania si wajinga kuamua kuchagua kwenda na Chadema, wameuona uongozi bora, sera endelevu, mikakati thabiti na oganaizesheni imara,” alisema.
 
Kuhusu ‘kubebwa’ na vyombo vya habari, Makene alisema hiyo ni hoja iliyokufa na kwamba ni dharau kwa wanahabari.

VISA VILIVYOTOKEA BAADA YA KUMKEJELI MWENYEZI MUNGU NA HIKI NDICHO KILICHOWATOKEA HAWA

MARILYN MONROE  

1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)
WAKATI alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. 


Mafundisho ya Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle). Ilikuwa mwaka 1966.

Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.

2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)
Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata MUNGU asingeweza kumtoa katika urais huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.

3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)
Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la Rio De Janeiro, alichukua sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na kusema "Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute"

Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule.

4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC.
Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, mwanahabari akamuuliza ni kwa kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na hata Mungu hawezi kuizamisha"
Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.

5. BON SCOTT (MUIMBAJI)
Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya
"Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'.

Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.

6. Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa mtoto wake. Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu" Yule binti akajibu "Gari imejaa mama, huyo Mungu labda akae kwenye boneti la gari".

Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari lilikuwa.

Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa. Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka mpaka kutokutambulika.

7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)
Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya...kibaya na kibaya kama Biblia"
Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.

8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)
Huyu alifuatwa na Bill Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa makini, alipomaliza akasema "Simhitaji Yesu wako, unaweza kuondoka nae". Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi walijaribu kuchunguza kipi kilikua chanzo cha kifo chake.

TAZAMA PICHA 40 ZA YALIYOJIRI KWENYE MAZISHI YA BILIONEA ERASTO MSUYA HUKO KAIRO - MIRERANI.


 Mbunge wa Simanjiro Ole Sendeka alipowasili Msibani.
Mc wa Shughuli ya Mazishi alikua ni JB.
Maelfu ya Waombolezaji waliokaa kila kona ya Eneo la Msiba wakifuatilia taratibu ya Mazishi.
Waombolezaji wakifuatilia Taratibu za Mazishi kupitia Luninga zilizokua zimewekwa kila kona
Waombolezaji wakiwa katika kwenye foleni ndefu ya watu wakiwa wanaelekea kwenda kutoa heshima za Mwisho kwa Marehemu.
Hili ndilo Jeneza Lililokua limebeba mwili wa marehemu lililowashangaza wengi kwa vile lilivyokua likifunguliwa kwa rimoti "Remote control"
Mwili wa Bilionea Erasto Msuya ukiwa kwenye Jeneza.
Mke wa marehemu (Mrs. Erasto Msuya) akitoa heshima za mwisho.
 Askofu akiandika kitabu cha rambirambi.
Viongozi wa dini wakiandika daftari la rambirambi.
Mamia ya watu wakiwa katika foleni ya kuaga mwili wa Marehemu.
 Askofu akitoa heshima za mwisho.

Watoto wa Marehemu.
 Mtoto wa Marehemu akiaga mwili wa baba yake.
Mbunge wa Simanjiro Ole Sendeka akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakitoa pole kwa familia ya Marehemu.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Erasto Msuya likiwa tayari kupelekwa eneo maalum kwaajili ya kumpumzisha.
 Watoto wa Marehemu wakiwa wanaongoza safari ya kuelekea kaburini utakapohifadhiwa mwili wa baba yao.
 Hii ndio ilikua safari ya kuupeleka mwili wa Bilionea Erasto Msuya kaburini.
Wananchi wakiwa wamejipanga pembeni wakati mwili wa marehemu ukipitishwa.
Mwili wa Marehemu ukiwasili eneo maalum kwa ajili ya maziko.
Dada wa Marehemu akitoa neno la familia.
Mwili ukiwa eneo maalumu kwa ajili ya ibada ya mazishi na nazishi.
 
Askofu akiendesha ibada ya Mazishi.
 Wachimbaji wadogo wadogo wa madini maarufu kama wanaapolo wakiwa makini kufuatilia taratibu za mazishi.
Mkuu wa jimbo akibariki eneo la maziko.
Jeneza lenye mwili wa Marehemu likishushwa kaburini kwa mashine maalum.
 Jeneza lenye Mwili wa Erasto Msuya likiwa kaburini.
Familia ya marehemu ikiweka udongo kaburini.
Mafundi wakifanya kazi ya kufunika kaburi.
 
 
 
 
 
 
 
 Askofu akiweka taji la maua juu ya kaburi la marehemu Erasto Msuya.

 Nyumba ya Milele ya Bilionea Erasto ikiwa Tayari.
 
 Hawa ni baadhi ya waombolezaji waliokua wamezagaa kila mahali baada ya shuhuli nzima ya mazishi ya Erasto Msuya kukamilika.

Hii ndiyo gari aina ya vogue ya Marehemu Erasto Msuya aliyoendesha mara ya mwisho.