Mkuuu
 wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Profesa, Shadrack Mwakalila 
(kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam
 leo, kuhusu mipango na masuala mbalimbali ya chuo hicho. Kushoto ni 
Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Thomas Ndaluka. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)
 Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
………………………………………………………………………………………
Dotto Mwaibale
CHUO cha 
Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kimeiomba Serikali kurudisha utaratibu wa 
viongozi mbalimbali wa Serikali kwenye kupata mafunzo ya maadili na 
uongozi katika chuo hicho.
Hayo 
yalibainishwa na Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Shadrack Mwakalila wakati 
akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi.
“Tulikaa 
na kushauriana na wenzangu ambapo tulionelea ni muhimu kuiomba serikali 
kurudisha utaratibu huo ili kuwanoa viongozi wetu hasa katika eneo la 
maadili” alisema Mwakalila.
Alisema 
wana walimu waliobobea kitaaluma na wenye uwezo wa kutoa mafunzo hayo 
kwa viongozi hao na wangependa mafunzo hayo yaanze haraka iwezekanavyo.
Profesa 
Mwakalila akiongelea kuhusu mipango ya chuo hicho alisema wamejipanga 
kuhakikisha mipango yote iliyopangwa inakwenda vizuri hususani suala la 
kuongeza hosteli.
Alisema 
chuo hicho kinauhaba mkubwa wa hosteli kwa ajili ya wanafunzi ambapo 
baadhi yao wamepanga uraiani jambo ambalo si zuri hivyo shauku yao ni 
kuona wanazingongoza ili kukabiliana na changamoto hiyo.
Akiongelea
 kuhusu udahili wa wanafunzi alisema ni mzuri na kuwa unategemea na 
nafasi ya mwanafunzi muombaji kulingana na somo analotaka kusomea.
“Tunachangamoto
 za hapa na pale lakini kubwa ni ruzuku ndogo tunayopata toka serikalini
 ambayo haikidhi mahitaji ukilinganisha na mahitaji kwa mfano ikitolewa 
ruzuku ya sh.milioni 100 tunapata milioni 50 jambo ambalo linasabisha 
kukwama kiuendeshaji” alisema Mwakalila.
Alisema 
chuo hicho kilianzishwa kwa Sheria ya Bunge namba 6 ya mwaka 2005 ambapo
 ilianza kutumika rasmi Oktoba 1 mwaka 2005 kwa mujibu wa Tangazo la 
Serikali namba 433 la Desemba 23, 2005.
Alisema 
chuo hicho kinamilikiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kuwa majukumu yake makuu
 ni pamoja na kutoa mafunzo katika fani za Sayansi Jamii kwa kiwango cha
 cheti, Stashahada na shahada, mafunzo ya uongozi, mafunzo ya elimu ya 
kujiendeleza kielimu, kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaaluma kwa 
sekta ya umma na sekta binafsi.
No comments:
Post a Comment