TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 5, 2014

Tamasha la Krismasi Msama Video Productions yajipanga

index
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Msama Video Productions imetoa tamko kwamba mwaka huu wamejipanga vizuri kufikisha ujumbe wa neon la Mungu katika Tamasha la Krismas kwani wanavifaa vipya na vya kisasa vyenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi katika mazingira yoyote yale na wafanyakazi wakutosha wenye weledi katika fani hiyo. Akizungumza na Dira ya Mtanzania, Meneja wa kitengo hicho, Alpha Kigalla alieleza sababu za kufanikisha vilivyo katika tamasha hilo ni kwa sababu ya umahiri wa  watendaji wa kirengo hicho ndio chachu itakayofanikisha kutekeleza ibada hiyo kwa waumini na mashabiki watakaojitokeza katika Tamasha hilo. Kigalla alitoa wito kwa wakazi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kujitokeza kwa wingi kushuhudia kazi za kitengo hicho kilicho katika kampuni ya Msama kwani wana vifaa vya kisasa zaidi. “Msama Video Productions ina vifaa vipya na vya kisasa zaidi  na hata watendaji wake wako makini zaidi na utekelezaji wa kazi zao, hivyo wadau wa muziki nchini kujitokeza kufanikisha kazi zao,” alisema Kigalla. Meneja huyo alisema wakazi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kujiandaa na kazi bora za Msama Video Productions ambazo zitafanikishwa kupitia waimbaji mbalimbali wa muziki huo.

No comments:

Post a Comment