TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 4, 2014

Mapambano ya Ukatili Yanaitaji Nguvu za Pamoja – Tume ya Haki za Binadamu

Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi.  Mary Massay akizungumza.
Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi. Mary Massay akizungumza.
Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi.  Mary Massay akizindua eneo la kula kiapo kwa washiriki kupinga ukatili.
Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi. Mary Massay akizindua eneo la kula kiapo kwa washiriki kupinga ukatili.
Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi.  Mary Massay akizungumza.
Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi. Mary Massay akizungumza.
Kaimu Mkurugenzi wa TGNP Mtandao, Bi. Lilian Liundi akizungumza katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP.
Kaimu Mkurugenzi wa TGNP Mtandao, Bi. Lilian Liundi akizungumza katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP.
Maandamano ya washiriki wa mjadala wa kupinga ukatili, katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyoandaliwa na TGNP Mtandao jijini Dar es Salaam.
Maandamano ya washiriki wa mjadala wa kupinga ukatili, katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyoandaliwa na TGNP Mtandao jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi.  Mary Massay pamoja na meza kuu wakipokea maandamano ya washiriki mjadala wa kupinga ukatili.
Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP, Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi. Mary Massay pamoja na meza kuu wakipokea maandamano ya washiriki mjadala wa kupinga ukatili.
Msanii Christian Bella (kushoto) akicheza na MC Scholar kutoka TGNP katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP jijini Dar es Salaam. Maadhimisho hayo yameandaliwa na TGNP Mtandao.
Msanii Christian Bella (kushoto) akicheza na MC Scholar kutoka TGNP katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP jijini Dar es Salaam. Maadhimisho hayo yameandaliwa na TGNP Mtandao.
Msanii Christian Bella akiwatumbuiza washiriki katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP jijini Dar es Salaam. Maadhimisho hayo yameandaliwa na TGNP Mtandao.
Msanii Christian Bella akiwatumbuiza washiriki katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia TGNP jijini Dar es Salaam. Maadhimisho hayo yameandaliwa na TGNP Mtandao.
VITA dhidi ya mapambano ya vitendo vya ukatili wa kijinsia nchini Tanzania havina budi kuungwa mkono na makundi yote kutokana na umuhimu wake. Hali hii ni kutokana na kwamba madhara ya ukatili katika jamii yanaathiri jamii nzima bila kujali jinsia.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania, Bi. Mary Massay katika Maadhimisho ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyoandaliwa na TGNP na kufanyika katika viwanja vya ofisi yao, Mabibo jijini Dar es Salaam.
Bi. Mary Massay aliyekuwa pia mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo ya Siku 16 Kupinga Ukatili wa Kijinsia alisema kila jamii hainabudi kuanza kwa kuangalia mazingira inayoishi na kuona namna gani ya kupambana na vita ya nukatili wa kijinsia.
“…Kila mmoja analojukumu kubwa, vyombo vya umma/dola, taasisi za umma, watu binafsi, mitandao na wanaharkati wanajukumu kubwa katika kupambana na ukatili wa kijinsia, huwezi kuleta maendeleo kama watu wanteseka, kwa hiyo kila kundi lina jukumu la kupambana na ukatili wa kijinsia,” alisema Bi. Massay.
“Vita dhidi ya Ukatili wa Kijinsia inahitaji nguvu ya pamoja kutoka kwa wanaanchi na viongozi ngazi zote ili ikomeshwe. Vita dhidi ya ukatili wa kijinsia haina mwanamke wala mwanamume, ni lazima tupate watu wa kutosha kutoka jinsi zote watakaouangana kudai mabadiliko. Wanaume mlioko hapa ninyi ni wadau muhimu sana katika kuleta mabadiliko chanya ya kukomesha kabisa ukatili wa kijinsia,” alisisitiza Katibu Mtendaji huyo wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora –Tanzania.
Aliwataka wazazi wasikubali kugeuka mawakala wa ndoa za utotoni, ambazo zimesababisha idadi kubwa ya wanafunzi hasa wa kike kukatishwa masomo na badala yake kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa vyombo vya sheria kuwawajibisha wakosaji.
“…Msikubali kuzungumza na wabakaji au wanaowatia watoto mimba nje ya mahakama, mtu akishafanya kosa akafikishwa mbele ya sheria viachinei vyombo hivyo vifanye kazi yake, sheria zipo na zitatumika,” alisema.
Hata hivyo alisema zipo hatua zilizochukuliwa na Serikali kukabiliana na vitendo vya ukatili ikiwa ni pamoja na kurekebisha baadhi nya sheria kandamizi na kutunga sheria mpya zinazozingatiwa usawa wa kijinsia na haki za binadamu.
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa TGNP Mtandao, Bi. Lilian Liundi alizitaka mamlaka husika kuangalia namna ya kukabiliana na tatizo la ajira nchini kwani limechania kuongezeka kwa vitendo vya ukatili kwa wasichana hususan ule wa ajira zisizo na utu, usafirishaji haramu wa wasichana, biashara ya ngono, rushwa ya ngono, ndoa za utotoni na ukatili mwingine.
“…Tunasisitiza uwepo wa mabweni ya kutosha katika shule zote za sekondari za kata na nyigine hususan ya wasichana ili kupunguza umbali na mazingira hatarishi kwenda shuleni. TGNP Mtandao na GTI tumejitahidi kupambana na ukatili wa Kijinsia kwa kutoa elimu kwa Jamii katika ngazi zote, kufanya mafunzo mbali mbali kwa wadau mbalimbali mfano; Jeshi la polisi yakiwemo madawati ya jinsia, viongozi wa Dini, Viongozi wa Mila, Mahakama, viongozi mbalimbali wa serikali za mitaa, watendaji wa halmashauri, wahudumu wa afya, na wanaharakati wa ngazi ya Jamii kupitia vituo vya taarifa na maarifa mikoa ya Mara, Shinyanga, Morogoro, Mbeya, Dar e salaam na Pwani,” alisema Bi. Liundi katika hotuba yake.
Maadhimisho hayo yalioambatana na mijadala ya wazi kwa washiriki yalishirikisha makundi ya wanaharakati mbalimbali ngazi ya jamii kutoka mikoa anuai nchini pamoja na makundi ya wanafunzi wa kutoka jijini Dar es Salaam. Kauli mbiu ya mjadala huo ilikuwa “Siyumbishi, Najilinda Mnilinde” ambayo inalenga vijana kuamini tunaamini kuwa mapambano yanahitaji nguvu kubwa na ya pamoja.

No comments:

Post a Comment