TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 6, 2014

Kinana ahutubia mkutano Mkuu wa 6 wa ZANU PF Harare -Zimbabwe

unnamed
unnamed3
Baadhi ya viongozi mashuhuri na wajumbe walihudhuria mkutano huo
pppppppppp3 Ndg. Kinana akihutubia mkutano Mkuu wa ZANU PF
ppppppppppppp4 Ndg. Kinana akisalimiana na Rais Robert Mugabe mara baada ya kuhutubia mkutano huo
……………………………………………………………………………………………………………………………….. KATIBU Mkuu wa CCm Ndg. Abdulrahaman Kinana , amekipongeza Chama Cha ZANU PF Cha Zimbabwe kwa kusimama imara licha ya Changamoto mbalimbali zimazoikabili Zimbambwe ikiwemo vikwazo vya kiuchumi ambavyo vimewekwa dhidi ya nchi hiyo.
Amewataka wana ZANU PF kuendelea kuunga mkono chama chao na kuongeza mapambano dhidi ya maadui wote wanaotaka kurudisha nyuma jitihada za kupigania maslahi ya nchi yao.
Akisoma salamu za mshikamano za Chama Cha Mapinduzi kwenye mkutano Mkuu wa ZANU PF unaofanyika mjini Harare Ndg. Kinana aliwakikishia wana ZANU PF na wana Zimbabwe wote kuwa katika mapambano hayo CCM iko nyuma yao na kwamba haitaacha kupaza sauti dhidi ya vikwazo vya uchumi ilivyowekewa Zimbabwe.
Alisema vikwazo hivyo having uhalali na kwa ujumla wake vinatoa adhabu isiyo ya haki kwa Wananchi wa Zimbabwe wasio na hatia.
Ndugu Kinana alimpongeza Rais Mugabe ujasiri na kwa msimamo wake usioyumba wa kupigania maslahi ya wana Zimbabwe licha ya vitimbi vya wapiga maendeleo.
Alisema ujasiri na msimamo wa Mugabe pamoja na Chama anachokiongoza Cha ZANU PF ndiyo uliowezesha Zimbabwe kusimama ilivyo hivi sasa kama Taifa huru na lisilikubali kuyumbishwa.
Alisema Mugabe na Chama chake wameonyesha kwa mfano kwamba kume watu wakisimama imara chini ya uongozi wa chama imara hakuna anayeweza kukwamisha nyendo zao za kimapinduzi zinazoendana na matakwa ya umma.
Akizungumzia ushindi wa kishindo wa ZANU PF kwenye uchaguzi Mkuu June mwaka jana Kinana alisema hicho ndicho kiashiria cha kukubalika kwa Chama na sera zake.
Alisema CCM inaipongeza ZANU PF kwa ushindi huo na kwamba wana CCM wanajisikia fahari sana wanapoona ZANU PF ikiendelea kukua na kuimarika.
Aisha Ndg. Kinana alimpongeza Rais Mugabe na kueleza kuwa CCM na Watanzania kwa ujumla wanafurahishwa na msimamo wa dhati alionyesha Rais Mugabe katika majukwaa mbalimbali ikiwemo mkutano wa wakuu wa nchi za SADC uliofanyika Victoria Falls wa kueleza umuhimu wa kutambua na kuheshimu mchango wa Mwalimu Nyerere katika ukombozi wa Afrika na hasa kusini mwa Afrika.
Hotuba ya Ndg. Kinana ilipokelewa kwa shangwe na furaha kubwa sana na wajumbe wa mkutano huo ambao mara kwa mara walishangalia kuashiria kuridhika na kauli za kimapinduzi na kidugu kutoka kwa wana CCM.
Ndugu Kinana na ujumbe wake wataondoka kesho kurejea nyumbani. Ujumbe wa Katibu Mkuu kwenye mkutano ulimhusisha pia Mjumbe wa halmashauri Kuu ya Taifa CCM Ndg. Phares Magesa na afisa wa makao makuu ya CCM Ndg. Thobias Mwilapwa

No comments:

Post a Comment