Baadhi ya viongozi mashuhuri na wajumbe walihudhuria mkutano huo
………………………………………………………………………………………………………………………………..
 KATIBU Mkuu wa CCm Ndg. Abdulrahaman Kinana , amekipongeza 
Chama Cha ZANU PF Cha Zimbabwe kwa kusimama imara licha ya Changamoto 
mbalimbali zimazoikabili Zimbambwe ikiwemo vikwazo vya kiuchumi ambavyo 
vimewekwa dhidi ya nchi hiyo.
 Amewataka wana ZANU PF kuendelea 
kuunga mkono chama chao na kuongeza mapambano dhidi ya maadui wote 
wanaotaka kurudisha nyuma jitihada za kupigania maslahi ya nchi yao.
 Akisoma salamu za mshikamano za 
Chama Cha Mapinduzi kwenye mkutano Mkuu wa ZANU PF unaofanyika mjini 
Harare Ndg. Kinana aliwakikishia wana ZANU PF na wana Zimbabwe wote kuwa
 katika mapambano hayo CCM iko nyuma yao na kwamba haitaacha kupaza 
sauti dhidi ya vikwazo vya uchumi ilivyowekewa Zimbabwe.
 Alisema vikwazo hivyo having uhalali na kwa ujumla wake vinatoa adhabu isiyo ya haki kwa Wananchi wa Zimbabwe wasio na hatia.
 Ndugu Kinana alimpongeza Rais 
Mugabe ujasiri na kwa msimamo wake usioyumba wa kupigania maslahi ya 
wana Zimbabwe licha ya vitimbi vya wapiga maendeleo.
 Alisema ujasiri na msimamo wa 
Mugabe pamoja na Chama anachokiongoza Cha ZANU PF ndiyo uliowezesha 
Zimbabwe kusimama ilivyo hivi sasa kama Taifa huru na lisilikubali 
kuyumbishwa.
 Alisema Mugabe na Chama chake 
wameonyesha kwa mfano kwamba kume watu wakisimama imara chini ya uongozi
 wa chama imara hakuna anayeweza kukwamisha nyendo zao za kimapinduzi 
zinazoendana na matakwa ya umma.
 Akizungumzia ushindi wa kishindo 
wa ZANU PF kwenye uchaguzi Mkuu June mwaka jana Kinana alisema hicho 
ndicho kiashiria cha kukubalika kwa Chama na sera zake.
 Alisema CCM inaipongeza ZANU PF 
kwa ushindi huo na kwamba wana CCM wanajisikia fahari sana wanapoona 
ZANU PF ikiendelea kukua na kuimarika.
 Aisha Ndg. Kinana alimpongeza 
Rais Mugabe na kueleza kuwa CCM na Watanzania kwa ujumla wanafurahishwa 
na msimamo wa dhati alionyesha Rais Mugabe katika majukwaa mbalimbali 
ikiwemo mkutano wa wakuu wa nchi za SADC uliofanyika Victoria Falls wa 
kueleza umuhimu wa kutambua na kuheshimu mchango wa Mwalimu Nyerere 
katika ukombozi wa Afrika na hasa kusini mwa Afrika.
 Hotuba ya Ndg. Kinana ilipokelewa
 kwa shangwe na furaha kubwa sana na wajumbe wa mkutano huo ambao mara 
kwa mara walishangalia kuashiria kuridhika na kauli za kimapinduzi na 
kidugu kutoka kwa wana CCM.
 Ndugu Kinana na ujumbe wake 
wataondoka kesho kurejea nyumbani. Ujumbe wa Katibu Mkuu kwenye mkutano 
ulimhusisha pia Mjumbe wa halmashauri Kuu ya Taifa CCM Ndg. Phares 
Magesa na afisa wa makao makuu ya CCM Ndg. Thobias Mwilapwa




No comments:
Post a Comment