TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 4, 2014

Mwenyekiti wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi ashauri wajumbe kufanya kazi kwa ushirikiano

unnamedMwenyekiti wa Bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Dkt Ibrahim Msengi akifungua kikao cha tano cha bodi ya barabara Mkoa kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Rajabu Rutengwe  ambaye awali alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi  sasa amehamishiwa mkoa wa Tanga na Nafasi yake kuchukuliwa na Dkt Msengi aliyemkabidhi uwenyekiti wa bodi ya Barabara.(Picha zote na Kibada Kibada -Katavi) unnamed2Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Ibrahimu Msengi Mwenye suti ya Bluu na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Rajabu Rutengwe wakibadilishana mawazo nje ya ukumbi wa mikutano mjini Mpanda muda mfupi baada ya kutoka kwenye Kikao  cha Tano cha Bodi ya  Barabara kilichofanyika leo mjini Mpanda. unnamed4Wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi wakifuatilia mjadala wa kikao hicho mbele ni Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Mpanda Estomhn Chang’ah mwenye suti ya kahawia na Selemani Lukanga Mkurugenzi wa Mji Mpanda. unnamed5Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpanda Estomihn Chang’ah akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya barabara kwenye kikao cha bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi.
………………………………………………………………………………..
Na Kibada Kibada –Katavi
Mwenyekiti wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Dkt Ibrahim Msengi ameshauri wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara kufanya kazi kwa ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha barabara za Mkoa huo zinajengwa kwa kiwangokinachokubaliki kuliko kukaa kinywa kusubiria hadi kikao kiitishwe ndiyo waseme mapungufu yaliyojitokeza.
Dkt Msengi alitoa kauli hiyo wakati akifungua Kikao cha tano cha Bodi ya Barabarakilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Mji Mpanda Mkoani Katavi na kuzungumzia changamoto mablimbali zinazoikabili sekta ya miundo mbinu Mkoani humo hasa sekta ya Barabara.
Alisema kikao cha Bodi ni cha kisheria hivyo Wajumbe wake wanawajibu na jukumu la kusimamia na kufuatilia kazi zote zinazofanyika katika Mkoa kwa kufuata taratibu zinazotakiwa bila kuingilia mchakato mingine ya kisheria kama mambo ya zabuni na masuala ya Kifedha lakini kubwa zaidi ni ushirikiano wa karibu miongoni mwao taasisi nyingine kwa kuwa kila kitu kinahitaji ushirikiano na mawasiliano ya karibu.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema haitakuwa busara barabara zinajengwa chini ya kiwango na wajumbe wa bodi wapo waaona na kuacha kushauri hadi  kazi inakamilika ndipo wanaanza kuhojii wakati ungeweza kusimamia mapema na kusaidia kuondoa kasoro hizo kwa kutoa ushauri mapema.
Akashauri kuwa ni vyema ufuatiliaji uwepo tangu mwanzo ili kuhakikisha taratibu zote zinafuatiliwa kwa kufuata utaratibu na sheria na kuona  barabara kama zinajengwa kwa wakati,akaeleza kuwa hiyo ni moja ya kazi ya bodi ya barabara.
Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Mhandisi Emmanuel Kalobelo alieleza  Bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi ilizinduliwa mwaka 2012 wakati linazinduliwa Mkoa ulikwa na mtandoa wa barabara  zinazohudumiwa  zikiwa katika hali mbaya lakini bodi imefanya jitihada mbalimbali na   kazi mbalimbali  zimeendelea kufanyika chini ya uongozi wa Bodi hii.
AIisema kazi mbalimbali zimefanyika na zinaendelea kufanyika akataja  barabara ya Mpanda – Uvinza,iko katika hali ya usanifu pia barabara ya Mpanda – Ugalla hadi Kaliua undyankulu Kahama, Mpanda –Inyonga, shughuli zinaendelea katika kuhakikisha Mkoa unafunguka.
Kwa upande wake aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara na Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambaye amehamia Mkoa wa Tanga Dkt Rajabu Rutengwe akimkaribisha Mwenyeiti Mpaya wa Bodi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa mpya wa Katavi Dkt Ibrahim Msengi ameeleza kuwa Mkoa wa Katavi ni moja ya Mkoa ambao uko nyuma kwa maendeleo ya Barabara za lami nchini hadi wakati unaanzishwa mwaka 2012 ulikuwa na kilometa (2)mbili za lami tofauti na maeneo mengine nchini lakini sasa unamtandao wa barabara za lami kilometa 34 hayo ni maendeleo kwa kipindi cha miaka miwili tu juhudi zimefanyika.
Amesema Mkoa una sura ya Samaki ya Pweza ili uende sehemu nyingine kutoka makao makuu ya mkoa lazima uende moja kwa moja halafu lazima urudi ulikoanzia safari  hivyo ameshauri wajumbe wa bodi ya Barabara na wananchi kwa ujumla kutoaushirikiano wa karibu kwa Mkuu wa Mkoa Mpya kama waliompatia wakati yeye alipokuwa mkuu wa mkoa na mwenyekiti wa Bodi ya Barabara hivyo na mwenzake apewe ushirikianokam aliokuwa akipewa ilikuleta maendeleo katika Mkoa huo.

No comments:

Post a Comment