TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 5, 2014

Mwasabwite kukonga Tamasha la Krismasi

index
Na Mwandishi Wetu
  MWIMBAJI wa nyimbo za injili nchini Edson Mwasabwite anayetamba kwa sasa na kibao chake kijulikanacho kwa jina la ‘Ni kwa Neema na Rehema’ amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika Tamasha la Krismasi litakalofanyika katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Songea Desemba mwaka huu. Mwasabwite alisema amejipanga kikamilifu kukonga nyoyo za mashabiki wake katika tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Desemba 25, 26 na 28 hivyo mashabiki zake wajitokeze kwa wingi kupata burudani ya nguvu kutoka kwake. Mwasabwite alisema mwaka huu watanzania wakae mkao wa kula kwa kusifu na kuabudu katika Tamasha la Krismasi kwani tayari amezindua albamu yake ya pili ijulikanayo kwa jina la ‘Asilimia mia Mungu amenihurumia’ yenye nyimbo tisa. “Nimejipanga vizuri kutoa burudani kwa mashabiki wangu katika tamasha la mwaka huu la Krismasi kwani maandalizi ni mazuri, safari hii itakuwa zaidi ya mwaka jana kwa sasa nina nyimbo nyingi zitakazowabariki mashabiki zangu na tayari nimeshazindua albamu mpya,” alisema Mwasabwite. Aidha amempongeza Mkurugenzi wa Msama Promotions kwa kuweza kuandaa Tamasha kubwa la Kikristo lenye mafanikio makubwa kwa kuweza kuwakutanisha waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania kwa lengo la kutangaza injili Tanzania. “Makampuni ya Msama yanaaminika na kukubalika kwa watanzania na nchi nyingine za jirani ndio maana hata tamasha linafanikiwa, tunaomba wananchi waendelee kununua kazi zetu, tunaomba sapoti kutoka kwa waumini na mashabiki wa muziki wa Injili,” alisema Mwasabwite.

No comments:

Post a Comment