Na Mwandishi Wetu
 
MWIMBAJI wa nyimbo za injili nchini Edson Mwasabwite anayetamba 
kwa sasa na kibao chake kijulikanacho kwa jina la ‘Ni kwa Neema na 
Rehema’ amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika Tamasha la 
Krismasi litakalofanyika katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Songea Desemba
 mwaka huu.
Mwasabwite alisema amejipanga kikamilifu kukonga nyoyo za 
mashabiki wake katika tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Desemba 25, 
26 na 28 hivyo mashabiki zake wajitokeze kwa wingi kupata burudani ya 
nguvu kutoka kwake.
Mwasabwite alisema mwaka huu watanzania wakae mkao wa kula kwa 
kusifu na kuabudu katika Tamasha la Krismasi kwani tayari amezindua 
albamu yake ya pili ijulikanayo kwa jina la ‘Asilimia mia Mungu 
amenihurumia’ yenye nyimbo tisa.
“Nimejipanga vizuri kutoa burudani kwa mashabiki wangu katika 
tamasha la mwaka huu la Krismasi kwani maandalizi ni mazuri, safari hii 
itakuwa zaidi ya mwaka jana kwa sasa nina nyimbo nyingi zitakazowabariki
 mashabiki zangu na tayari nimeshazindua albamu mpya,” alisema 
Mwasabwite. 
Aidha amempongeza Mkurugenzi wa Msama Promotions kwa kuweza 
kuandaa Tamasha kubwa la Kikristo lenye mafanikio makubwa kwa kuweza 
kuwakutanisha waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania kwa 
lengo la kutangaza injili Tanzania.
“Makampuni ya Msama yanaaminika na kukubalika kwa watanzania na 
nchi nyingine za jirani ndio maana hata tamasha linafanikiwa, tunaomba 
wananchi waendelee kununua kazi zetu, tunaomba sapoti kutoka kwa waumini
 na mashabiki wa muziki wa Injili,” alisema Mwasabwite.

No comments:
Post a Comment