TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 5, 2014

CELCOM YADHAMINI TUZO ZA TASWA KWA MILIONI 30

TASWA 1 Mwenyeliti wa Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa) Juma Pinto (Wa kwanza kulia) akitoa neno la shukrani kwa kampuni ya Selom Wireless, baada ya kutangaza udhamini wa Sh Milioni 30 kwa ajili ya udhamini wa Tuzo za wanamichezo bora wa 2013/14. Wengine katika picha ni Meneja  Biashara, ukuzaji na Masoko wa Selcom Wireless, Juma Mgori na Gallus Runyeta ambaye ni Meneja Miradi.
…………………………………………………………….
Kampuni ya malipo ya Kielektroniki ya, Selcom Wireless imetoa Sh Milion 30 kwa Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa) kwa ajili ya kudhamini tuzo za wanamichezo bora wa msimu wa 2013/14 zitakazofanyika ijumaa ijayo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee VIP.
Udhamini huo umetangazwa na Meneja wa Ukuzaji Biashara wa kampuni ya Selcom Woreless, Juma Mgodi katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa City Sports Lounge wa jijini.
Mgori alisema kuwa wanajivunia sana kuwa miongoni mwa wadhamini katika tuzo ambazo zitamtoa rasmi mwanamichezo bora wa msimu wa 2013/14. Wadhamini wengine ni Said Salim Bakhresa & Co Ltd , IPTL, mifuko ya hifadhi ya jamii, PSPF na NSSF. Alisema kuwa  huo ni mwanzo tu wa kushirikiana na Taswa kwani wameingia katika dakika za mwisho kutokana na kujali umuhimu wa michezo nchini na kuona bora kutoa mchango wao. “Kama unavyojua, kampuni yetu inashughulikia malipo ya kielektoniki kwa taasisi za fedha 30 na tuna vituo vya malipo (Point of Services) zaidi ya 8,000, sisi ndiyo tunayoiwezesha jamii katika kila kona ya nchi yetu, hivyo mwakani tutaingia kwa nguvu zaidi,” alisema Mgori. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taswa, Juma Pinto aliipongeza kampuni hiyo kwa kuwasaidia na pia kuendelea kuziomba kampuni nyingine na wadau wa michezo nchini kuwasaidia pamoja na muda kukaribia mwishoni. “Naishukuru Selcom Wireless na wadhamini wengine kwa kutoa ‘ubani’ wao katika shughuli hii muhimu, bado ni tunahitaji msaada na tunaamini kuwa wadau wengine watajitokeza kutusaidia,” alisema Pinto. Katika Tuzo hizo, Taswa itatoa jumla ya tuzo 47 kwa wanamichezo mbali mbali ikiwa pamoja na mwanamichezo bora wa jumla na aliyetukuka.

No comments:

Post a Comment