Mwenyeliti
 wa Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa) Juma Pinto 
(Wa kwanza kulia) akitoa neno la shukrani kwa kampuni ya Selom Wireless,
 baada ya kutangaza udhamini wa Sh Milioni 30 kwa ajili ya udhamini wa 
Tuzo za wanamichezo bora wa 2013/14. Wengine katika picha ni Meneja  
Biashara, ukuzaji na Masoko wa Selcom Wireless, Juma Mgori na Gallus 
Runyeta ambaye ni Meneja Miradi.
…………………………………………………………….
Kampuni ya malipo ya Kielektroniki
 ya, Selcom Wireless imetoa Sh Milion 30 kwa Chama cha waandishi wa 
habari za michezo nchini (Taswa) kwa ajili ya kudhamini tuzo za 
wanamichezo bora wa msimu wa 2013/14 zitakazofanyika ijumaa ijayo kwenye
 ukumbi wa Diamond Jubilee VIP.
Udhamini huo umetangazwa na Meneja
 wa Ukuzaji Biashara wa kampuni ya Selcom Woreless, Juma Mgodi katika 
mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa City Sports 
Lounge wa jijini.
Mgori alisema kuwa wanajivunia 
sana kuwa miongoni mwa wadhamini katika tuzo ambazo zitamtoa rasmi 
mwanamichezo bora wa msimu wa 2013/14. Wadhamini wengine ni Said Salim 
Bakhresa & Co Ltd , IPTL, mifuko ya hifadhi ya jamii, PSPF na NSSF.
 Alisema kuwa  huo ni mwanzo tu wa kushirikiana na Taswa kwani 
wameingia katika dakika za mwisho kutokana na kujali umuhimu wa michezo 
nchini na kuona bora kutoa mchango wao.
 “Kama unavyojua, kampuni yetu inashughulikia malipo ya 
kielektoniki kwa taasisi za fedha 30 na tuna vituo vya malipo (Point of 
Services) zaidi ya 8,000, sisi ndiyo tunayoiwezesha jamii katika kila 
kona ya nchi yetu, hivyo mwakani tutaingia kwa nguvu zaidi,” alisema 
Mgori.
 Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taswa, Juma Pinto aliipongeza 
kampuni hiyo kwa kuwasaidia na pia kuendelea kuziomba kampuni nyingine 
na wadau wa michezo nchini kuwasaidia pamoja na muda kukaribia mwishoni.
 “Naishukuru Selcom Wireless na wadhamini wengine kwa kutoa 
‘ubani’ wao katika shughuli hii muhimu, bado ni tunahitaji msaada na 
tunaamini kuwa wadau wengine watajitokeza kutusaidia,” alisema Pinto.
 Katika Tuzo hizo, Taswa itatoa jumla ya tuzo 47 kwa wanamichezo
 mbali mbali ikiwa pamoja na mwanamichezo bora wa jumla na aliyetukuka.
No comments:
Post a Comment