MKE wa mlalamikaji katika kesi ya
 kughushi dhidi ya Mfanyabiashara Hans Macha (pichani), amedai 
mahakamani kwamba mumewe anadaiwa fedha nyingi na mshtakiwa, alishindwa 
kulipa akaamua kumuuzia nyumba.
Mke huyo Nurya Ahmad (34),ambaye 
ni shahidi wa upande wa utetezi, amedai hayo leo Desemba Mosi, katika 
Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu,Dar es Salaam, mbele ya Hakimu Mkazi 
Devotha Kisoka, kwa kuongozwa na wakili wa utetezi, Deo Ringia.
Nurya amedai mahakamani hapo 
kwamba nyumba iliyokuwa ya Balenga iliyopo eneo la Kigogo, Dar es 
Salaam, iliuzwa kihalali kwa Macha baada ya mumewe (Balenga), kushindwa 
kulipa deni.
“Nafahamu kwamba mume wangu 
(Balenga), alikuwa andaiwa na Macha, aliniambia mwenyewe kwamba ni fedha
 nyingi sana, deni halikuwahi kulipwa hatimaye akaniambia kuwa ameeamua 
kumuuizia nyumba.
“Alikuwa akikopa kwa kuweka rehani
 hati za nyumba, madeni mengine yalikuwa yakilipwa, tulikuwa katika ndoa
 kuanzia mwaka 2001 hadi 2012, sijawahi kuona mume wangu akiwa kichaa,” 
alidai Nurya baada ya kuulizwa kama aliwahi kuona mumewe akiwa kichaa.
Shahidi huyo alihoji mahakamani 
kwamba hati za nyumba halisi zilifikaje kwa Hans Macha, kama Balenga 
hakuzipeleka mwenyewe kwake, aliongeza kwamba hajawahi kumsikia mumewe 
akilalamika  kudhulumiwa nyumba na Macha.
Mfanyabiashara Hans Macha 
akijitetea alidai  kwamba Ramadhani Balenga alishindwa kumlipa deni la 
Sh. milioni 879 akamuuzia nyumba iyo ya Kigogo.
Alidai Balengo alikuwa akimtegemea
 kwa kukopa fedha mara kwa mara kwa ajili ya kuingiza makontena ya vifaa
 vya umeme au elektroniki.
“Aliletwa na wafanyabiashara 
wenzangu kwa ajili ya kukopa, nilimpa masharti ya kukopa, aliweka 
dhamana hati ya nyumba yake ya Mabibo, Manzese, Kigogo, Mbezi Beach, 
mara ya mwisho Balenga nilikuwa namdai jumla ya Sh. milioni 879, wakati 
huo nilikuwa na hati zake za nyumba nne.
“Balenga alishindwa kulipa akidai 
kwamba kontena zake zilikamatwa na kufilisiwa na TRA, aliamua kuniuzia 
nyumba ya Kigogo, Manzese na nimuongezee Sh. milioni 20 ili tumalizane 
deni lote.
“Nilipofanya hivyo mbele ya wakili
 nilikuwa nimempa jumla ya Sh. ilioni 899, nilipomkabidhi fedha ya 
nyongeza Sh. milioni 20 alinikabidhi hati, siku nyingine tulisaini hati 
ya kuhamisha umiliki, Balenga alinikabidhi nyaraka 
zingine ikiwemo michoro, mikataba ya ujenzi, kibali cha ujenzi, 
miakataba halisi waliyoingia na kampuni ya ujenzi pamoja na risiti 
mbalimbali,” Macha alidai.
“Si kweli kwamba nilighushi, 
Balengo aliniuzia nyumba baada ya kushindwa kulipa deni, naiomba 
mahakama iyatupe mashtaka yaliyofunguliwa dhidi yangu,”alidai Macha.
Shahidi wa tatu, Mohammed Waziri 
Mohammed ambaye ni mfanyakazi wa Balenga pia alidai mahakamani kwamba 
mlalamikaji katika kesi hiyo alikuwa akidaiwa na Macha.
Waziri alidai mara kadhaa alikuwa 
akienda na mlalamikaji kwa Macha kwa ajili ya kukopa fedha. Kesi hiyo 
inatarajiwa kuendelea kesho Jumanne, Desemba 2, 2014
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI, KITAIFA MKOANI NJOMBE
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 Mkuu wa mkoa wa Njombe, Dkt. Rehema Nchimbi, kwa pamoja wakisimama 
kupokea maandamano wakati wa sherehe za Maadhimisho ya siku ya Ukimwi 
Duniani iliyofanyika leo Desemba 1, 2014 Kitaifa kwenye Uwanja wa 
Sabasaba Mkoani Njombe. Picha na OMR 
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akihutubia katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani 
zilizofanyika Kitaifa katika Uwanja wa Sabasaba Mkoani Njombe leo, 
Desemba 2014. Picha na OMR 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
 Bilal, akiagana na baadhi ya viongozi wakati akiondoka katika uwanja wa
 Sabasaba baada ya kuhutubia katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya 
Ukimwi Duniani zilizofanyika Kitaifa kwenye Uwanja wa huo Mkoani Njombe.
 Picha na OMR 
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akipunga mkono kuwaaga wananchi wakati akiondoka uwanjani hapo baada ya
 kuhutubia katika Sherehe za maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, 
zilizofanyika Kitaifa Mkoani Njombe. Picha na OMR 
Mkuu
 wa Mkoa wa Njombe, Dkt. Rehema Nchimbi, akijumuika na wasanii wa 
Kikundi cha Sanaa cha Kanisa la KKKT, wakati wakitoa burudani yenye 
ujumbe kuhusu maadhimisho hayo ya siku ya Ukimwi Duniani. Picha na OMR 
 Baadhi ya wanadamanaji wakipita mbele ya jukwaa kuu na mabango yenye 
ujumbe mbalimbali kuhusu siku ya Ukimwi Duniani wakati wa sherehe hizo 
zilizofanyika Kitaifa katika Uwanja wa Sabasaba Mkoani Njombe leo 
Desemba 1, 2014. Picha na OMR 
 
==============================================
TMF YAFADHILI WANAHABARI TISA KWENDA ACCRA NCHINI GHANA KUPATA MAFUNZO
 
        on December 1, 2014 
 Wanahabari hao wanaosafiri wakimsikiliza Mkufunzi wa Masuala ya Biashara za Habari kutoka Ghana,  Nuamah Eshun.
Dotto Mwaibale
MFUKO wa 
Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), umewafadhili wanahabari kutoka vyombo 
mbalimbali nchini kwenda Accra nchini Ghana kupata mafunzo. Mafunzo haya
 yanalenga kuwajengea uwezo katika maeneo ya utawala na uongozi, 
biashara, masoko na kuboresha maudhui katika vipindi vyao kama namna ya 
kuchochea mabadiliko ya kimfumo katika vyombo vyao.
Akizungumza
 katika hafla ya kuwaaga wanahabari hao wapatao 9 iliyofanyika Makao 
Makuu ya TMF Upanga Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa TMF, 
Ernest Sungura alisema TMF imekuwa ikiwawezesha wanahabari kupata 
mafunzo ya aina mbalimbali ndani nan je ya nchi.
Alisema wanahabari hao wanakwenda nchini humo ambapo watapata mafunzo kwa siku 10 kuanzia Disemba 2 hadi 13 mwaka huu.
“Waliochaguliwa
 kwenda kupata mafunzo hayo ni baadhi ya wakuu wa vitengo kutoka vyombo 
vya habari, mameneja, wamiliki wa vyombo vya habari na maofisa masoko na
 mauzo na waandaaji wa vipindi mbalimbali vya redio” alisema Sungura.
Aliongeza
 kuwa tangu mwaka 2008 TMF imeweza kufadhili vyombo zaidi ya 120 na 
wanahabari zaidi ya 500 kupitia aina ya ruzuku mbalimbali. Kati ya 
vyombo 120 vilivyofadhiliwa na TMF, 31 vimepewa ruzuku inayolenga 
kuimarisha utendaji wao katika masuala ya utawala na uongozi, biashara, 
masoko na kuboresha maudhui katika vipindi mbalimbali.
Alisema 
katika safari hiyo vituo vya redio vitano vimebahatika kuchaguliwa 
ambavyo ni CG Fm (Tabora), Standard FM (Singida), Kahama FM (Kahama), 
Triple A FM (Arusha) na Jogoo FM (Songea)-(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com)
================================================ 
Dk.BILAL KUWEKA JIWE LA MSINGI CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO
MAKAMU wa Rais, Dk.Mohammed Gharib Bilal (pichani) Desemba 2 anatarajiwa Kuwa mgeni
rasmi katika sherehe za uwekwaji wa jiwe la Msingi la Chuo Kikuu Cha
Bagamoyo(UB), zitakazofanyika Kijijini Kiromo,Bagamoyo Mkoani Pwani.
rasmi katika sherehe za uwekwaji wa jiwe la Msingi la Chuo Kikuu Cha
Bagamoyo(UB), zitakazofanyika Kijijini Kiromo,Bagamoyo Mkoani Pwani.
Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Mikocheni Dar es
Salaam Ofisa Habari wa (UB), Happiness Katabazi alisema sherehe hizo
zitafanyika Kijijini Kilomo Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani na kwamba
uwekwaji wa jiwe hilo ni ufunguzi rasmi wa ujenzi wa Chuo Kikuu Cha
Bagamoyo Katika Kijiji hicho ambao utaanza mapema Januari Mwaka 2015.
Katabazi alisema Dk. Bilal ndiye atakuwa mgeni rasmi katika sherehe
hiyo ya kihistoria katika Wilaya ya Bagamoyo kwasababu Somo la Historia
linatufundisha kuwa mji wa Bagamoyo ilikuwa ukikaliwa na watumwa.
” Sasa sisi UB tunaitambua hiyo historia na ndiyo maana tukaamua
kuanzisha Chuo Kikuu ambacho tumekipa jina la Bagamoyo.Na kwakuwa
kupitia Mji wa Bagamoyo tulikuwa watumwa, basi sasa kupitia UB ambayo
inajenga makazi yake ya kudumu katika mji huo, binadamu wote watakuwa
huru kwasababu tutapata elimu” alisema Katabazi.
Alisema UB
ambayo ilianzishwa rasmi mwaka 2011 ambayo ina makazi yake yake ya muda
,Mikocheni ,Dar es Salaam na kwamba ujenzi wa Makazi ya kudumu ya UB
kijijini Kilomo , utasaidia kukuza shughuli za uchumi, wananchi wa eneo
hilo kupata huduma ya elimu ya ngazi ya Chuo Kikuu kwa ukaribu.
Aidha aliwaomba wananchi Wilaya Bagamoyo na Mkoa wa Pwani kwa ujumla
kujitokeza kwa Wingi Katika sherehe hiyo. UB ilianzishwa rasmi Mwaka
2011.
========================================================
MKUTANO KATI YA DR. SHEIN NA MABALOZI WETE KISIWANI PEMBA
 BAADHI ya WanaCCM  wa Wilaya ya Wete Pemba wakimkaribisha   Rais wa 
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa 
CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein  alipofika kuzungumza na Mabalozi na 
Wenyeviti wa  Maskani  wa  Mkoa wa Kaskazini Pemba katka ukumbi wa 
Jamhuri akiwa katika ziara za kuimarisha Chama .[Picha na Ikulu.] 
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  
pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akitia saini kitabu cha wageni 
alipofika katika ukumbi wa Jamhuri Wete  kuzungumza na Mabalozi na 
Wenyeviti wa Maskani Wilaya ya Wete Pemba akiwa katika ziara za 
Kuimarisha Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Pemba leo .[Picha na 
Ikulu.] 
Viongozi
 wa Chama cha Mapinduzi waliofuatana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti 
wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM
 Zanzibar katika mkutano wa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika 
Wilaya ya Wete wakifuatilia kwa makini taraatibu za Mkutano huo 
uliofanyika leo katik na a Ukumbi wa Jamhuri  ikiwa ni katika kuimarisha
 Chama ,[Picha na Ikulu.]  
BAADHI
 ya WanaCCM  wa Wilaya ya Wete Pemba wakimsikiliza  Rais wa Zanzibar na 
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar 
Dk.Ali Mohamed Shein  alipokuwa akizungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa 
 Maskani  wa  Mkoa wa Kaskazini Pemba katka ukumbi wa Jamhuri akiwa 
katika ziara za kuimarisha Chama .[Picha na Ikulu.]
 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Wete akizungumza na katika Mkutano wa 
Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani wa Wilaya hiyo uliofanyika leo katika 
ukumbi wa Jamhuri Wete Pemba na kuhutubiwa na Makamo Mwenyekiti wa CCM 
Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Map[induzi 
Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika ziara zake za kuimarisha Chama Mkoa wa
 Kaskazini Pemba.[Picha na Ikulu.] 
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  
pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akipokea Utenzi  baada ya kusomwa 
 na Asha Msanif wakati wa  Mkutano wa kuimarisha Chama alioufanya leo 
kwa Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani za CCM akiwa katika ziara zake za 
kuimarisha Chama cha Mapinduzi Wilaya ya  Wete Mkoa wa Kaskazini 
Pemba.[Picha na Ikulu.] Kaskazini Pemba.[Picha na Ikulu.] 
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein 
 pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akipokea risala ya Mabalozi 
 kutoka kwa Bina Khamis  wakati Mkutano wa kuimarisha Chama akiwa katika
 ziara zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi (CCM)Mkoa wa 
 on December 1, 2014  
       
       
       
         
       
       
        
Kikosi cha Taifa Stars Maboresho 
kimeingia kambini leo (Desemba 1 mwaka huu) Bulyanhulu mkoani Shinyanga 
kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi itakayochezwa Desemba 9
 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Ikiwa chini ya Kocha Mart Nooij, 
Stars Maboresho itapiga kambi mkoani humo hadi Desemba 6 mwaka huu 
ambapo itarejea jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya mechi hiyo 
itakayochezwa Uwanja wa Taifa.
Wachezaji walioingia kambini ni 
Abubakar Ally (Coastal Union), Abubakar Ally Mohamed (White Bird), Aishi
 Manula (Azam), Andrew Vicent (Mtibwa Sugar), Atupele Green (Kagera 
Sugar), Edward Charles (Yanga) na Emmanuel Semwanda (African Lyon).
Gadiel Michael (Azam), Hashim 
Magoma (Stand United), Hassan Banda (Simba), Hassan Mwasapili (Mbeya 
City), Joram Mgeveke (Simba), Kassim Mohamed Simbaulanga (African Lyon),
 Kelvin Friday (Azam) na Makarani Ally (Mtibwa Sugar).
Miraji Adam (Simba), Mohamed 
Hussein (Simba), Muzamir Ally (Mtibwa Sugar), Omari Nyenje (Ndanda), 
Pato Ngonyani (Yanga), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Said Hamisi 
(Simba), Salim Hassan Mbonde (Mtibwa Sugar) na Shiza Ramadhan (Mtibwa 
Sugar).
Shirikisho la Mpira wa Miguu 
Tanzania (TFF) linaishukuru kampuni ya kuchimba madini ya Acacia Mining 
PLC (zamani African Barrick Gold PLC) kwa kufadhili kambi ya Stars 
kupitia mgodi wa Bulyanhulu.
================================================================ 
Shule za msingi za Rightway zaadhimishwa miaka 10 ya kuanzishwa kwake
Mgeni
 rasmi na Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando 
Mchechu akimpa mkono Barwany Mchechu kwa kufanya vizuri katika masomo 
yake wakati wa mahafali ya shule ya Msingi ya Rightway, Mbezi Beach 
Jijini Dar es Salaam.
Mgeni
 rasmi na Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando 
Mchechu akiwa katika picha ya pamoja na Blandina Kidda wakati wa 
mahafali ya shule ya Msingi ya Rightway, Mbezi Beach Jijini Dar es 
Salaam, Kushoto kwa Mkurugenzi ni Mzazi wa Blandina Fatma Chillo na 
kulia kwa Blandina ni Mercy Luhanga ambaye ni Mkurugenzi washule hizo na
 anayemfuatia ni Meneja wa Shule hiyo Moses Kyando.
================== ===================================
Tamasha la Tigo Welcome Pack Lapagawisha Mjini Kigoma
Msanii
 Alex Chalamila maarufu kama MCRegan akiburudisha katika tamasha la 
kuhamasisha matumizi ya mtandao wa simu ya mkononi ya Tigo lililofanyika
 kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. 
Msanii
 wa kundi la Origional Comedy Emanuel Mgaya (Masanja) akiburudisha 
kwenye tamasha la Tigo welcome pack lililofanyika kwenye uwanja wa Lake 
Tanganyika mjini Kigoma. 
Msanii
 wa kundi la Origional Comedy Isaya Mwakilasa (Wakuvanga) akiburudisha 
kwenye tamasha la Tigo welcome pack kwenye uwanja wa Lake Tanganyika 
mjini Kigoma. 
Msanii
 wa Bongo Flava Sunday Mjeda (Linex) akitumbuiza kwenye tamasha la Tigo 
welcome pack lililofanyika uwanja wa lake Tanganyika mjini Kigoma. 
Msanii
 nguli wa hiphop nchini Joseph Haule a.k.a Prof J akitumbuiza kwenye 
tamasha la Tigo welcome pack huku akisindikizwa na wasanii wa kundi la 
Origional Comedy kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. 
Msanii
 nguli wa hiphop nchini Joseph Haule a.k.a Prof J akitumbuiza kwenye 
tamasha la Tigo welcome pack huku akisindikizwa na wasanii wa kundi la 
Origional Comedy kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. 
 Baadhi ya wananchi wa manispaa ya kigoma ujiji wakipata huduma 
kuhusiana na bidhaa na huduma mbalimbali za mtandao wa simu ya mkononi 
ya tigo  kutoka kwenye vibanda mbalimbali vya kutoa huduma katika uwanja
 wa Lake Tanganyika wakati wa tamasha la Tigo welcome pack  
lililofanyika mjini Kigoma.
==================================================================== 
Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji yafanya Mahafali ya Sita
Naibu
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. 
Elisante Ole Gabriel (mwenye miwani) akiangalia na kupata maelezo kutoka
 kwa wahusika alipotembelea labaratori ya mitambo ya maji katika Taasisi
 ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) kabla ya kuudhuria maafali ya 
sita ya Taasisi hiyo hivi karibuni. 
Baadhi
 ya wahitimu kutoka Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) 
wakiwa katika maandamano ya kitaaluma wakati wa Maafali ya sita cha 
Taasisi hiyo hivi karibuni.
 Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) Dkt. Shija 
Kazumba (kushoto) akimkaribisha Mgeni rasmi katika maafali ya sita ya 
Taasisi hiyo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana 
Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel ambaye pia ni mgeni 
rasmi wa mahafali hayo.
Naibu
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. 
Elisante Ole Gabriel akiwahutubia wahitimu (hawapo pichani) wakati wa 
mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI). 
Kushoto ni Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) Dkt.
 Shija Kazumba na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi hiyo Prof. 
Gabriel Roderick Kassenga. 
Naibu
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. 
Elisante Ole Gabriel akipokea risala ya wahitimu iliyosomwa na 
kuwasilishwa kwa mgeni rasmi na Bw. Magembe Maduhu.
Naibu
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. 
Elisante Ole Gabriel akimpa tuzo mhitimu aliyeongoza katika kundi la 
wanawake na aliyekua na ufaulu mkukwa kuliko wahitimu wote Bi. Fatma 
Ngano, kulia ni Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI)
 Dkt. Shija na ushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi hiyo Prof. 
Gabriel Roderick Kassenga.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo ambaye 
pia ni mgeni rasmi katika mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo na 
Usimamizi wa Maji (WDMI) Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye miwani) 
katika picha ya pamoja na wakufunzi na wahitimu wa Taasisi hiyo.
 Kikundi cha ngoma kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania Mwenge wakitumbuiza
 wakati wa mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji
 (WDMI) yaliyofanyika hivi karibuni.
 Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo
====================================================================== 
BANDARI YA KASANGA KUANZA KUBORESHWA
Kiongozi
 wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya
 Mipango, Bibi Florence Mwanri (Watatu kushoto) akimsikiliza kwa makini 
Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) mara
 walipowasili katika bandari hiyo kujionea shughuli mbalimbali za 
maendeleo bandari hapo. 
Mkuu
 wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kushoto) 
akiwaongoza wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume 
ya Mipango kujionea moja ya meli za kigeni zinazotia nanga katika 
bandari hiyo. Meli hiyo ni MV Rwegura kutoka nchini Burundi. 
Mkuu
 wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) akitoa 
ufafanuzi juu ya namna bandari yake inavyohudumia meli kutoka nchi 
jirani. Wanaomsikiliza ni Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka 
Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiongozwa na Bibi Florence Mwanri 
(Kushoto aliyevaa fulana nyeusi). 
Timu
 ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango
 ikiwa katika picha ya pamoja katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato nchini 
(TRA) zilizopo kwenye Bandari ya Kasanga. 
Mkuu
 wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kushoto) 
akimfafanualia jambo Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo 
kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kulia) 
wakati akimkabidhi taarifa ya maendeleo ya bandari hiyo.
…………………………………………………………………….
Na Saidi Mkabakuli, Sumbawanga
Serikali imeazimia kuanza 
kuiboresha bandari ya kimkakati ya Kasanga inayohudumia nchi za Burundi,
 Rwanda na Kongo iliyopo katika Ziwa Tanganyika, mkoani Rukwa.
Ahadi hiyo imetolewa na Kiongozi 
wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya 
Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati walipofanya ziara ya kukagua 
maendeleo ya miundombinu katika Bandari ya Kasanga.
Bibi Mwanri alisema kuwa serikali 
kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania imepanga kuboresha bandari zote ili 
kuwa malango kuu la biashara kwa soko la ndani na kwa nchi jirani ili 
kuongeza uwezo wa kuhudumia shehena kwa ufanisi.
“Tumedhamiria kuendelea kuboresha 
miundombinu ya bandari hususan miradi iliyoibuliwa katika Programu ya 
Matokeo Makubwa Sasa ikiwemo Bandari ya Kasanga ili kuweza kukidhi 
mahitaji ya utoaji wa huduma katika eneo hili,” alisema.
Bibi Mwanri aliongeza kuwa 
serikali pia imejipanga kuendelea kuboresha miundombinu na ununuzi wa 
vifaa mbalimbali vya kuhudumia shehena katika bandari za Dar es Salaam, 
Tanga, Mtwara, Kasanga na Kigoma na kukamilisha maandalizi ya ujenzi wa 
bandari mpya za Mwambani (Tanga), Mbegani (Bagamoyo) na Bandari Kavu ya 
Kisarawe.
Akizungumza na ugeni huo, 
Msimamizi Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa 
alisema kuwa Bandari hiyo ina fursa nyingi katika kuhudumia shehena na 
abiria wanaopitia bandarini hapo.
“Bandari yetu ina fursa kubwa za 
kibiashara kwani tuna wateja wengi kutoka ndani na nje ya nchi 
wanaotumia bandari yetu kupitishia bidhaa zao, pamoja na abiria 
wanaosafiri kwenda nje na ndani ya Tanzania,” alisema.
Kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo 
kwa mwaka ujao wa fedha Serikali imedhamiria kuboresha mazingira 
yatakayowezesha sekta binafsi kuwekeza katika kujenga miuondombinu na 
kuboresha usafirishaji wa mizigo katika bandari zote nchini.
Pia, Mpango huo unaweka bayana kuendeleza na ukarabati na ununuzi wa vyombo vya usafiri na usafirishaji katika maziwa.
================================================================= 
PONGEZI KWA MSANII NASSIB ABDUL AKA DIAMOND KWA KUSHINDA TUZO TATU ZA CHOAMVA14
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kama msimamizi na mratibu wa sekta ya Sanaa nchini linapenda
 kutoa pongezi za dhati kwa Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nassib 
Abdul maarufu kama Diamond kwa kushinda tuzo tatu kwa mkupuo za CHOAMVA 
zinazoendeshwa na kituo maarufu cha luninga cha Channel 0 chenye makao 
makuu yake Afrika Kusini.
Tuzo alizoshinda Diamond ni pamoja na Most Gifted East African Artist, Most Gifted Afro Pop video na ile ya Most Gifted New Comer.
Kushinda kwa Diamond katika tuzo hizo kubwa barani Afrika na kuwashinda wasanii wengine wenye ‘majina makubwa’ ni ishara kwamba muziki wetu unakubalika ndani na
Baraza linatoa wito kwa wasanii na wadau wote wa muziki kuzidisha ubunifu, bidii na weledi katika kazi wanazozifanya ili wasanii wengi zaidi waweze kuchomoza katika tuzo na majukwaa mbalimbali ya kimataifa kwa lengo la kujitangaza na kukuza soko la kazi zao kimataifa.
Aidha, Baraza linaendelea kuwakumbusha na kuwasisitiza wadau wa muziki na Sanaa kwa ujumla hususan wakuzaji Sanaa (mapromota) kuendelea kujenga mazingira rafiki kwa wasanii wetu kufanya kazi kwa ubora na weledi lakini pia kwa upendo na furaha ili kujenga daraja zuri kwa wasanii wengi zaidi kung’ara kwenye ngazi za kimataifa.
Ni imani ya Baraza kwamba, ushindi huu wa kihistoria wa Diamond utakuwa chachu kwa wadau wote wa Sanaa nchini hususan wasanii katika kujituma na kuhakikisha hawaridhiki na mafanikio waliyonayo.
Ni matumaini ya Baraza kwamba wasanii na wadau wote wa Sanaa wataendelea kutambua umuhimu wa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji sekta sambamba na kutambuliwa na Serikali.
Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini
Tuzo alizoshinda Diamond ni pamoja na Most Gifted East African Artist, Most Gifted Afro Pop video na ile ya Most Gifted New Comer.
Kushinda kwa Diamond katika tuzo hizo kubwa barani Afrika na kuwashinda wasanii wengine wenye ‘majina makubwa’ ni ishara kwamba muziki wetu unakubalika ndani na
Baraza linatoa wito kwa wasanii na wadau wote wa muziki kuzidisha ubunifu, bidii na weledi katika kazi wanazozifanya ili wasanii wengi zaidi waweze kuchomoza katika tuzo na majukwaa mbalimbali ya kimataifa kwa lengo la kujitangaza na kukuza soko la kazi zao kimataifa.
Aidha, Baraza linaendelea kuwakumbusha na kuwasisitiza wadau wa muziki na Sanaa kwa ujumla hususan wakuzaji Sanaa (mapromota) kuendelea kujenga mazingira rafiki kwa wasanii wetu kufanya kazi kwa ubora na weledi lakini pia kwa upendo na furaha ili kujenga daraja zuri kwa wasanii wengi zaidi kung’ara kwenye ngazi za kimataifa.
Ni imani ya Baraza kwamba, ushindi huu wa kihistoria wa Diamond utakuwa chachu kwa wadau wote wa Sanaa nchini hususan wasanii katika kujituma na kuhakikisha hawaridhiki na mafanikio waliyonayo.
Ni matumaini ya Baraza kwamba wasanii na wadau wote wa Sanaa wataendelea kutambua umuhimu wa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji sekta sambamba na kutambuliwa na Serikali.
Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini
==================================================================== 
Airtel yakabithi kisima cha maji kwa shule ya msingi Kumbukumbu Dar
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa pili kulia mbele) na 
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii,
 Jinsia na Watoto, Benedict Missani (wa tatu kushoto mbele), 
wakiwaongoza wafanyakazi wa Airtel Tanzania na wanafunzi kwenye 
matembezi ya hisani yenye lengo la kuchangisha pesa kiasi cha shilingi 
milioni 10, kwa ajili ya kuendelea kuboresha Shule ya Msingi Kumbukumbu ,
 yaliyoanzia katika Makao Makuu ya Airtel , Barabara ya Ali Hassan 
Mwinyi kupitia Bongoyo, Haile Selasie na kuishia shuleni hapo Block 41, 
jijini Dar es Salaam jana. 
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa pili kushoto) akimkabidhi
 Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto wa Wizara ya Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia na Watoto, Benedict Missani, funguo za kisima kipya cha 
maji safi kilichojengwa  kwa hisani ya Airtel kwa kushirikiana na 
Wafanyakazi wake,  katika Shule ya Msingi Kumbukumbu, wakati wa hafla 
iliyofanyika shuleni hapo eneo la Block 41 jijini Dar es Salaam jana. 
Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano 
Malya (kushoto), Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Priscilla Moshi (wa tatu 
kushoto), na Mwenyekiti wa Shule hiyo, Mwemba Mwilima. 
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso akifungulia maji ya bomba 
kama ishara ya uzinduzi rasmi wa  kisima kipya cha maji safi 
kilichojengwa  kwa hisani ya Airtel kwa kushirikiana na Wafanyakazi 
wake,  katika Shule ya Msingi Kumbukumbu, wakati wa hafla iliyofanyika 
shuleni hapo eneo la Block 41 jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia 
ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto wa Wizara ya Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia na Watoto, Benedict Missani (wa tatu kushoto) na Mwalimu 
Mkuu wa Shule hiyo, Priscilla Moshi (wa nne kushoto).
………………………………………………………………………….
 Yaendesha matembezi yahisani kuendelea kuboresha mazingira ya shule
- Zaidi ya shilingi milioni 10 kukusanywa
 
Dar es salaam Novemba 30, 2014 
Kampuni ya Airtel leo imeendesha matembezi ya hisani ili kuchangisha  
pesa kwajili ya kuendelea kuboresha shule ya msingi kumbukumbu iliyopo 
jijini Dar es salaam 
Matembezi yenye lengo la kupata 
pesa ili kufanya ukarabati wa darasa la watoto na kununua viti na meza 
za kukalia yameetimishwa kwa uzinduzi wa kisima cha maji kilichojengwa 
kwa hisani ya Airtel kwa kushirikiana na wafanyakazi wake ili 
kukabiliana na tatizo la maji shule hapo
Akiongea wakati wa kuzindua kisima
 hicho mgeni rasmi , Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto wa Wizara 
ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Benedict Missani kwa niaba ya 
Waziri wa Maendeleo ya jamii  jinsia na watoto Mh. Sophia Simba 
alisema”  naunga mkono juhudi zilizofanywa na Airtel katika kuendelea 
kuboresha mazingara ya utoaji elimu shuleni hapa. Nimefurai kuona kuwa 
Airtel haikuridhika na ujenzi wa kisima hii tu bali wameamua kuchua 
hatua nyingine ya kushirikisha wadau mbalimbali katika kutatua 
changamoto walizoziona shuleni hapa.
Leo tumetembe kwa pamoja ili 
kuweza kuchangisha kiasi cha shilingi milioni 10 zikazowesha kazi ya 
kuendelea kuboresha mazingara ya shule hii kuendelea. 
Serikali inaunga mkono dhamira hii
 na jitihada hizi zinazoenda sambamba na kauli mbili yetu ya Matokeo 
makubwa sasa  na kuhakikisha tunaboresha maeneo muhimu hususani elimu 
kwani vijana hao ndio nguvukazi na taifa la kesho. Natoa wito kwa 
mashirika mengine watu binafsi na taasisi mbalimbali kujitokeza na 
kuchangia katika shughuli za jamii ili kukubiliana na changamoto tulizo 
nazo sasa.
Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa
 Airtel Bwana Sunil Colaso alisema” nawashukuru wafanyakazi wa Airtel na
 kila moja aliyeshiriki hapa kwa kujitoa katika kusaidia jamii, sisi 
Airtel tumejipanga kutimiza dhamira yetu ya kuchangia katika kuhakiksha 
tunachangia katika sekta ya elimu kwa kuendelea kutoa vitabu na 
kuboresha mazingira ya shule. Kupitia mradi wa Airtel Shule yetu 
tumeweza kuzifika shule nyingi kwa kuwapatia nyenzo muhimu katika elimu 
na leo tumewafikia shule ya msingi kumbukumbu tukiwa na lengo na 
kuendelea kuboresha sekta ya elimu.
Mpango huu wa Airtel Tunakujali ni
 endelevu bado tutakuwa  shughuli nyingi zaidi na shule nyingi zikipokea
 misaada hivyo tunawaomba wadau mbalimbali kuendelea kushirikiana nasi.
Kwa upande wake mfanyakazi wa 
Airtel Bi Veneranda Boniface Alisema amejisikia furaha kutumia jumamosi 
yake kutembea kwaajili yakusaidia jamii, hii ni sehemu pia ya mazoezi 
lakini zaidi ni njia pekee ya kuniwezesha mimi kwa nafasi yangu katika 
jamii kushiriki kuchangia.
Matembezi hayo ya hisani yalianzia
 katika makao makuu ya Airtel yaliyoko Moroco Dar esaalam na kwenda njia
 ya Alihasan Mwinyi, kupitia Kaunda, Bongoyo , haileselaile , Ali 
hassani Mwinyi na kuishia katika shule ya msingi Kumbukumbu.
================================================================== 
AJALI ZA BARABARANI ZAONGEZEKA TABORA ZAUWA IDADI KUBWA YA WATU!!!
![]()  | 
| Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akipata maelezo kutoka kwa Dr.Anna Kichambati wa Redcross Tabora wakati wa sherehe za wiki ya usalama barabarani mkoani Tabora | 
![]()  | 
| Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila akisalimiana na Afisa mfawidhi wa Sumatra mkoa wa Tabora Bw.Joseph Michael wakati wa wiki ya usalama barabarani mkoa wa Tabora | 
![]()  | 
| Kikosi cha zimamoto mkoa wa Tabora kikionesha vifaa vinavyotumika wakati wa uokoaji ajali zinapojitokeza. | 
![]()  | 
| Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila akimpatia cheti cha pongezi Mwenyekiti mstaafu wa Kamati ya Usalama barabarani mkoa wa Tabora Bw.Moshi Abrahamu maarufu Nkonkota. | 
![]()  | 
| Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akikabidhi cheti cha pongezi kwa mmiliki wa kampuni ya mabasi ya NBS kwa usafirishaji salama bila kusababisha ajali kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja. | 
 ==============================================================
UNESCO WAANZISHA PROGRAM YA UTAMADUNI KUKABILI UKIMWI
Afisa
 Ardhi na Mazingira wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala (Kahama), Zablon
 Donge, akifungua rasmi warsha ya siku tatu ya wadau wa mapambano dhidi 
ya UKIMWI kwa niaba ya Mkurugenzi wa wilaya hiyo, iliyofanyika Kata ya 
Segese wilayani Kahama mkoani Shinyanga. Kushoto kwake ni Mkurugenzi 
Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na
 Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues pamoja na Afisa Mradi wa
 Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias.
Na Mwandishi Wetu, Kahama
MKURUGENZI
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues ametaka jamii 
kujumuisha suala la utamaduni katika kupambana na maambukizi mapya ya 
Ukimwi.
Alisema
 hayo kwenye warsha ya siku tatu ya wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI 
inayofanyika Kata ya Segese wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Alisema
 katika ufunguzi huo kwamba kwa miaka mingi pamoja na kuwepo kwa elimu 
ya UKIMWI, kumekosekana mabadiliko yanayotakiwa kukabili maambukizi 
mapya.
Alisema
 UNESCO iliangalia tatizo hili na kubaini kwamba kutobadilika kwa hali 
kumetokana na kutounganishwa kwa kipengele cha mila ambacho ndicho 
kinachofanya kuwepo na mazingira rafiki ya kupashana habari.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza na 
washiriki wakati wa uzinduzi wa program ya utamaduni kukabili UKIMWI 
itakayoendeshwa na shirika lake.
Warsha
 hiyo ya Siku tatu imelenga katika kuhamasisha jamii, Shule, Asasi, 
Taasii za Dini na Serikali katika utoaji wa Elimu sahihi ya huduma 
rafiki za Afya ya Uzazi, VVU/UKIMWI, ujinsia na maadili ya Afya kwa 
vijana balehe na vijana.
Amesema
 mpaka sasa utoaji wa elimu ya afya, ueleweshaji wa ugonjwa haujafanya 
mabadilikoya kutosha kutokana na ukweli kuwa katika utekelezaji wa 
kampeni masuala ya utamaduni na uwasilishaji wa taarifa haukuwa 
umezingatiwa.
Alisema
 wakati Kahama (Msalala) kwa sasa kiwango cha maambukizi ni asilimia 
5.9, Juhudi zinatakiwa kufanywa katika kuhakikisha kwamba elimu 
inayotolewa inahusishwa na masuala ya kitamaduni ili kubadilisha maisha 
ya wakazi.
Alisema katika mapambano ya maambukizi mapya mila na utamaduni zinaweza kabisa kusaidia kukabiliana na maambukizi ya UKIMWI.
Afisa
 Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias 
akielezea madhumuni ya warsha hiyo ya siku tatu iliyojumuisha makundi 
mbalimbali ikiwemo Waganga wa jadi, wakunga wa jadi, viongozi wa dini, 
viongozi wa vijiji na kata, walimu, wataalamu wa afya na elimu na Asasi 
zisizokuwa za kiserikali.
Alisema
 program inayoangaliwa sasa ni ile iliyoleta mafanikio katika nchi 
kadhaa za Afrika ikiwamo Msumbiji na hivyo wanaona waijaribu Tanzania 
katika wilaya sita ikiwemo Kahama na hasa halmashauri ya wilaya ya 
Msalala.
Alisema
 pamoja na watu wengi kutibiwa na waganga wa kienyeji ni vyema 
watengeneza sera na watu wengine kutambua umuhimu wao ili kwa kupitia 
mila waweze kuwafunua watu akili na kujikinga na maambukizi ya UKIMWI.
Alisema
 anaamini kuwa mila na tamaduni zikitumika vyema na hata matibabu 
zitasaidia kuokoa maisha ya wengi na pia kuzuia maambukizi mapya.
Alisema
 maambukizi mapya ni tatizo kwa sasa hasa ikizingatiwa kwamba wananchi 
wengi wanajua uwapo wa UKIMWI lakini ufahamu ni mdogo kwa kuwa katika 
kufundisha watu hawakupewa elimu ya kutosha inayoambatana na kuangalia 
mila na desturi njema za afya zilizopo.
Afisa
 afya mkuu kitengo cha elimu ya afya kwa umma-programu ya afya mashuleni
 kutoka Wizara ya afya na ustawi wa jamii, Avit Maro akielezea jambo kwa
 washiriki kuhusiana na masuala ya afya ya uzazi wakati wa warsha ya 
siku tatu ya wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI iliyofanyika Kata ya 
Segese wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Alisema ni vyema wananchi wakatumia mali asili waliyonayo kufundishana juu ya kukabiliana na maambukizi mapya ya UKIMWI.
Alisema
 UNESCO imeamua kuanzisha programu maalumu ya kutumia mila na desturi 
kukabili UKIMWI kama njia nyingine ya kuoanisha nguvu katika mapambano 
dhidi ya maambukizi mapya.
Naye 
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala (Kahama), 
Zablon Donge alishukuru UNESCO kwa kuanzisha program ya kujifunza namna 
ya kukabiliana na maambukizi mapya ya UKIMWI.
Alisema
 ukiwa na halmashauri ya wagonjwa huwezi kuwa na halmashauri kwa kuwa 
shughuli za kiuchumi na kijamii kushindikana kutekelezwa, na kusema kuja
 kwa UNESCO ni msaada mkubwa.
Warsha
 hiyo imejumisha makundi mbalimbali ikiwemo Waganga wa jadi, wakunga wa 
jadi, viongozi wa dini, viongozi wa vijiji na kata, walimu, wataalamu wa
 afya na elimu na Asasi zisizokuwa za kiserikali.
Mkurugenzi
 msaidizi masuala mtambuka kutoka Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi, 
Dkt. Laetitia Sayi akifafanua jambo jinsi wizara yake inavyoshirikisha 
jamii katika utoaji wa elimu mashuleni hususani afya ya uzazi, 
VVU/UKIMWI huku ikishirikiana na wadau wao wa karibu UNESCO.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues, akiendesha warsha 
hiyo kwa njia ya majadiliano na washiriki juu ya dhana na maana ya 
balehe, vijana balehe na vijana sambamba na maana ya mimba na ndoa za 
utotoni.
Pichani
 juu na chini ni sehemu ya washiriki hao wakifuatilia majadiliano kwenye
 warsha hiyo ya siku tatu iliyofanyika Kata ya Segese wilayani Kahama 
mkoani Shinyanga.
Pichani
 juu na chini ni baadhi ya washiriki wakichangia maoni wakati 
majadiliano ya kutafuta suluhu ya kupunguza maambukizi mapya ya 
VVU/UKIMWI, mimba na ndoa za utotoni kwenye jamii zao.SUNDERLAND 0 CHELSEA 0 AND TANZANIA 1
 
By Ayoub Mzee-London
Tanzania Tourist Board was in the UK to launch a series of events related to the promotion of Tourism In Tanzania at Sunderland FC .The day also saw the launch of ‘a holiday of a lifetime’ campaign to visit Tanzania .
Tanzania Tourist Board was in the UK to launch a series of events related to the promotion of Tourism In Tanzania at Sunderland FC .The day also saw the launch of ‘a holiday of a lifetime’ campaign to visit Tanzania .
The day saw Sunderland players 
wearing special t-shirts ahead of the home draw with Chelsea as part of 
the club’s partnership with Tanzanian Tourist Board.
The Black Cats took to the field in the pre-game warm up 
sporting shirts emblazoned with the ‘Visit Tanzania’ logo as part of the
 partnership.SAFC has already developed close links with Tanzania, through providing technical and practical support to the development of the football academy project, the first of its kind in the country.
The project will see thousands of youngsters benefit from a joined up approach combining football, education and community engagement, harnessing the knowledge and expertise of Sunderland AFC and its own successful Academy.
Present at the event was the Tanzania High Commissioner HE Peter Kallaghe ,the Chairperson of the board of Governors of TTB ,TTB’s Marketing Manager Devota Mdachi and other members of TTB team
For more details visit www.safc.com/tanzaniaholiday
========================================================================
MAKAMU WA RAIS AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI (EAC) KUHUSU MIUNDOMBINU JIJINI NAIROBI
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wa tatu kutoka (kushoto) Makamu wa Rais wa
 Kenya, William Ruto, (kushoto kwake) Makamu wa Rais kwanza wa Burundi, 
(kulia kwake) wakijumuika kwa pamoja na viongozi  wengine wakionyesha 
Taarifa ya pamoja waliyoisaini kuhusu majadiliano ya kuimarisha 
Miundombinu kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika 
mkutano wa 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) kuhusu 
Miundombinu, uliofanyika kwenye Ukumbi wa KICC, jijini Nairobi jana 
Novemba 29, 2014. Picha na OMR
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akizungumza katika mkutano wa 3 tatu wa wakuu wa Nchi za Afrika 
Mashariki (EAC) kuhusu miundombinu, uliofanyika katika ukumbi wa KICC 
jijini Nairobi jana Novemba 29, 2014. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wakati wakitoka
 kwenye Ukumbi wa mikutano wa KICC, baada ya kushiriki katika mkutano wa
 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Miundombinu 
uliofanyika jijini Nairobu, Kenya jana Novemba 29, 2014. Picha na OMR
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine walioshiriki katika 
mkutano huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia jambo na Makamu wa Rais wa Kenya
 William Ruto na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, wakati 
wakiondoka katika viwanja vya Ukumbi wa mikutano wa KICC, baada ya 
kushiriki kwenye mkutano wa 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC)
 kuhusu Miundombinu, uliofanyika jijini Nairobi, Kenya jana Novemba 29, 
2014. Picha na OMR
………………………………………………………………………………
Mheshimiwa Makamu wa Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal jana Novemba 
29, 2014 aliiwakilisha Tanzania katika mkutano wa siku moja wa Wakuu wa 
Nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Nairobi, Kenya. 
Mkutano huo, kwa mujibu wa utaratibu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, 
unafanyika kila baada ya miaka miwili na lengo lake kuu ni kufanya 
tathmini juu ya miradi ya miundombinu inayoshirikisha nchi washirika, 
sambamba na kutazama fursa ya kutanua miundombinu mipya katika nchi hizi
 kwa lengo la kukuza uchumi wa pamoja kwa nchi za Afrika Mashariki.
Tathmini hii ya Miundombinu 
inafanyika kwa kuwa mataifa ya Afrika Mashariki yanatambua umuhimu wa 
kuwa na miundombinu bora katika nchi hizi ili kuharakisha ukuaji wa 
uchumi, sambamba na kutanua mtengamano wa nchi hizi na hivyo kuwafanya 
wananchi wanaoishi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuzidi kuwa 
wamoja.
Mkutano wa jana uliongozwa na 
Kaimu Rais wa Kenya Mheshimiwa William Ruto na kuhudhuriwa na Mheshimiwa
 Makamu wa Rais Dkt. Bilal, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi, Waziri 
Mkuu wa Rwanda pamoja na Waziri wa Afrika Mashariki wa Uganda. Viongozi 
wengine waliopata nafasi ya kuhudhuria mkutano huo ni pamoja na 
Mheshimiwa Balozi Richard Sezibera, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika 
Mashariki, Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika 
Mashariki na Waziri wa Wizara hiyo kutoka Tanzania, Mheshimkiwa Samwel 
Sitta, Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Dkt. Donald Kaberuka, 
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Ukanda wa Afrika, Bwana Makhtar Diop, 
Katibu Mtendaji wa UNCTAD, Dkt. Mukhisa Kituyi na Baalozi wa Umoja wa 
Ulaya nchini Tanzania Balozi Filiberto Sebregondi. Pia mkutano huo 
ulihudhuriwa na wawakilishi wa nchi za China, Marekani, Japan na 
nyinginezo ambazo ni wadau wakubwa wa ujenzi wa miundombinu katika nchi 
za Afrika Mashariki.
Akizungumza wakati wa ufunguzi 
wa mkutano huo, Kaimu Rais wa Kenya, William Ruto alifafanua juu ya 
umuhimu wa kuhakikisha Afrika Mashariki inaunganishwa kwa miundombinu 
imara ili kukuza uchumi na akapongeza jitihada mbalimbali zinazofanyika 
katika kufanikisha azma hiyo huku pia akiomba nchi wanachama wa Afrika 
Mashariki kuendelea kuungana katika kutekeleza miradi ya miundombinu na 
kujitahidi kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo.
Mkutano huu pia uliambatana na 
kupokea ripoti ya utekelezaji wa maagizo ya Wakuu wa Nchi za EAC kuhusu 
Miundombinu kutoka kwa Mawaziri wa Nchi za Jumuiya.  Wakuu wa Nchi 
katika Mkutano huu walipokea taarifa ya utekelezaji wa maagizo 
waliyoyatoa katika mkutano wa pili uliofanyika mwezi Novemba, 2012 na 
kuidhinisha miradi 72 ya miundombinu ya kipaumbele ya Barabara, Reli, 
Nishati na Bandari.
Kwa upande wa utekelezaji; 
miradi 16 imekamilika, 39 inaendelea kutekelezwa na 17 ipo katika hatua 
za awali za kutafutiwa fedha kwa ajili ya utekelezaji wake.
Kwa upande wa Tanzania miradi 
minne imekamilika ambayo ni Umeme katika mji wa Kibondo, mradi wa 
barabara ya Mbezi-Shule-Tangibovu-Makutano ya Nelson Mandela na barabara
 ya Tabata. Barabara nyingine iliyokamilika ni Nyangunge – Musoma – 
Sirari na sehemu ya Simiyu – Musoma inayounganisha Kenya na Tanzania 
huko ujenzi unaendelea.
Akizungumza katika Mkutano huo 
Makamu wa Rais amezitaka nchi wanachama kuharakisha utekelezaji wa 
miradi ya Miundombinu ili kusaidia utekelezaji wa Itifaki ya Soko la 
Pamoja, ambayo inalenga kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na abiria. 
“Tusiishie kubakiza mipango hii katika karatasi, tusiishie kuzungumza tu
 bali huu ni wakati wa kuhakikisha tunarahisisha ufanyaji biashara 
katika nchi zetu na kupunguza vikwazo visivyo vya lazima,” alisema 
Mheshimiwa Makamu wa Rais.
Katika mkutano huo, Mheshimiwa 
Makamu wa Rais pia aliambatana na Mheshimiwa Dkt. Mahadhi J. Maalim, 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na 
Waziri wa Viwanda na Biashara wa Zanzibar, Mheshimiwa Nassor Ahmed 
Mazrui. Mheshimiwa Makamu wa Rais na msafara wake tayari wamerejea 
nyumbani Tanzania ambapo kesho anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika 
Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, maadhimisho 
yanayofanyika Kitaifa Mkoani Njombe.
 =======================================================================TRA ARUSHA YAVUKA MALENGO
MAMLAKA ya mapato Tanzania( TRA) mkoani arusha imevuka kiwango cha
makusanyo ya kodi kutoka bilioni 205.1 kwa mwaka 2012 /2013 hadi
kufikia bilioni 244.2 kwa mwaka 2013 /2014 huku wakitarajia kukusanya
bilioni 293.3 kwa mwaka 2014 /2015.
makusanyo ya kodi kutoka bilioni 205.1 kwa mwaka 2012 /2013 hadi
kufikia bilioni 244.2 kwa mwaka 2013 /2014 huku wakitarajia kukusanya
bilioni 293.3 kwa mwaka 2014 /2015.
Hayo yalisemwa jana na meneja wa mamlaka ya TRA mkoani hapa Evarest
Kileva alipokuwa akizungumza katika maadhimisho ya siku ya mlipa kodi
yaliyofanyika katika viwanja vya makumbusho vilivyopo jijini hapa.
Kileva alipokuwa akizungumza katika maadhimisho ya siku ya mlipa kodi
yaliyofanyika katika viwanja vya makumbusho vilivyopo jijini hapa.
Kileva alisema kuwa mafanikio hayo yalitokana na jitihada za mamlaka
hiyo kuwahimiza wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kulipa kodi katika
kukuza pato la taifa .
hiyo kuwahimiza wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kulipa kodi katika
kukuza pato la taifa .
Alisema kuwa mamlaka hiyo imekuwa ikitambua umuhimu wa walipa kodi na
hivyo kuamua kuwazawadia wale wote waliofanya vizur katika kutimiza
wajibu wao kulipa kodi kwa kupeana mkono ili kuhamasisha na wengine
waweze kujua umuhimu wa ulipaji kodi.
hivyo kuamua kuwazawadia wale wote waliofanya vizur katika kutimiza
wajibu wao kulipa kodi kwa kupeana mkono ili kuhamasisha na wengine
waweze kujua umuhimu wa ulipaji kodi.
Aliongeza kuwa mamlaka hiyo kwa sasa Imejipanga kuongeza jitihada kwa
kufanya kazi kwa bidii ili kuvuka malengo waliyokusudiwa katika
kuhakikisha wafanyabiashara wadogo na wakati wanalipa kodi kwa wakati
ili kuwezesha pato la taifa lizidi kuongezeka
kufanya kazi kwa bidii ili kuvuka malengo waliyokusudiwa katika
kuhakikisha wafanyabiashara wadogo na wakati wanalipa kodi kwa wakati
ili kuwezesha pato la taifa lizidi kuongezeka
Akizungumza katika maadhimisho hayo kwa niaba ya mkuu wa mkoa,mkuu wa
wilaya ya monduli Jowika Kasunga alitaka mamalaka kuhakikisha
inathibiti wafanyabiashara ambao hawalipi kodi kwa wakati kwani swala
hilo ni la kisheria .
wilaya ya monduli Jowika Kasunga alitaka mamalaka kuhakikisha
inathibiti wafanyabiashara ambao hawalipi kodi kwa wakati kwani swala
hilo ni la kisheria .
Kasunga alidai kuwa ngezeko hili ni kubwa sana tofauti na ongezeko la
mwaka lililopita hivyo kuitaka mamlaka hiyo kuzidi kuongeza jitihada
za kutoa elimu zaidi kwa walipa kodi pamoja na wafanyabaishara ili
kuweza kuvuka hata malengo waliyojiweka ya ukusanyaji mapato kwa mwaka
huu.
mwaka lililopita hivyo kuitaka mamlaka hiyo kuzidi kuongeza jitihada
za kutoa elimu zaidi kwa walipa kodi pamoja na wafanyabaishara ili
kuweza kuvuka hata malengo waliyojiweka ya ukusanyaji mapato kwa mwaka
huu.
NHIF WAZINDUA KAMPENI YA MFUKO WA AFYA YA JAMII VIJIJI VYA NZEGA
![]()  | 
KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AMPA MWAKYEMBE MWEZI MMOJA KUTOA MAJIBU KWA NINI MAZAO YA KOROSHO NA UFUTA HAYASAFIRISHWI NJE KUPITIA BANDARI YA MTWARA
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman
 Kinana akiwahutubia wananchi wa mjini Mtwara katika mkutano wa hadhara 
uliofanyika kwenye  viwanja vya Mashujaa mjini humo akihitimisha ziara 
yake ya siku 16 aliyoifanya katika mikoa ya Lindi na Mtwara akikagua 
utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na 
serikali kwa kushirikiana na wananchi wenyewe na kuhimiza uhai wa chama 
cha Mapinduzi CCM, Katika ziara hiyo Katibu mkuu huyo aliongozana na 
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi, Katika kutano huo 
Kinana amempa wiki mbili Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe kutoa
 maelezo kwanini bidhaa mbalimbali hazisafirishwi kwenda nje kupitia 
bandari ya Mtwara, Lakini pia Kinana amewaagiza Waziri wa Nishati na 
Madini kutoa maelezo ni kwanini wawekezaji wenye kampuni zinazofanya 
shughuli zao mtwara wanalipia kodi zao jijini Dar es salaam badala ya 
kulipia mkoani Mtwara ambako wanafanya shughuli zao, Pia waziri wa Ofisi
 ya Mkamu wa Rais Mazingira amepewa mwezi mmoja kuhakikisha dampo la 
taka za sumu zinazotupwa na wachimbaji wa gesi na viwanda kuacha mara 
moja kwa sababu zinahatarisha maisha ya wakazi wa Mtwara, Mwisho 
akaagiza Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa kibali cha kugawa viwanja katika 
manispaa ya Mtwara kwani viwanja vimeshapimwa, Fedha za kulipa fidia 
zipo ila kibali kutoka ofisi ya Waziri mkuu ndiyo kimkwama kwa muda wa 
mwaka mmoja sasa.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu 
Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati alipokuwa akiwahutubia 
wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya 
Mashujaa mjini Mtwara.
 Wananchi wakinyoosha mikono yao juu 
kufurahia hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati 
alipokuwa akiwahutubia.
 Mbunge wa jimbo la Mtwara mjini Mh. 
Hasnein Murji akiwahutubia wapiga kura wake ambao walifurahia sana 
hotuba yake kwenye viwanja vya Mashujaa mjini Mtwara.
 Umati wa wananchi ukiwa umefurika katika mkutano huo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa na viongozi mbalimbali katika meza kuu wakati wa mkutano huo.
 Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akiwahutubia wananchi katika mkutano huo.
 Ndugu Abdulrahman Kinana na Nape nnauye wakiingia katika uwanja wa mkutano.
![]()  | 
| Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangali vikundi vya ngoma mara baada ya kuwasili katika mkutano wa hadhara. | 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman 
Kinana wa tatu kutoka kulia Nape Nnauye na viongozi wa mkoa wa Mtwara 
wakiwasili katika mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Mashujaa mjini 
Mtwara leo.
=============================================================== 
KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA ATOA HESHIMA KWA SHUJAA ALIYETUNGUA NDEGE MBILI ZA KIRENO WAKATI WA VITA YA UKOMBOZI WA NCHI YA MSUMBIJI
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa heshima zake katika mnara 
wa Shujaa wa vita vya ukombozi wapigania uhuru wa nchi ya Msumbiji 
mwanajeshi wa Tanzania Marehemu Ahmad Mzee aliyeuwawa na wanajeshi 
wakoloni wa  Kireno waliokuwa wakitawala nchi ya Msumbiji mwaka 1972 
wakati akilinda mipaka ya Tanzania na kifaru kandokando ya mto Ruvuma 
katika kata ya Kitaya Mtwara vijijini, Mwanajeshi huyo alifanikiwa 
kuangusha ndege mbili za mreno aina ya Jet Fighters zikitokea Msumbiji 
katika kijiji cha Kitaya, ambapo na yeye alijeruhiwa baada ya kupigwa na
 wareno hao na kukimbizwa katika hospitali ya Mtwara ambapo baadaye 
alifariki dunia, Katibu Mkuu Kinana yuko katika ziara ya kikazi mkoani 
Mtwara akikagua ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na
 serikali, Huku akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa 
na Uenezi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma ujumbe uliopo katika mnara huo ukimuelezea shujaa Ahmad Mzee. 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akielekea kwenye eneo la mkutano wa hadhara. 
Nape
 Nnauye Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi akiwahutubia wananchi 
katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Kitaya. 
Baadhi
 ya wageni  kutoka nchi jirani ya Msumbiji wakiwa katika mkutano wa 
hadhara wananchi wa Kitaya waliwaalika majirani zao wa Msumbiji 
kuhudhuria katika mkutano huo. 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika kata ya Kitaya Mtwara vijijini. 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza wakati  akiwahutubia wananchi katika kata ya Kitaya Mtwara vijijini. 
Mkuu wa wilaya ya Wilman Ndile akiwahutubia wananchi. 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikaguamajengo ya kituo cha afya cha Nanguruwe Mtwara vijijini. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi katika kituo cha afya cha Nanguruwe Mtwara vijijini. 
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdlrahman Kinana hayupo pichani katika kijiji cha Naguruwe 
Baadhi ya mabango yakionyesha Mabango yanayoonyesha ujumbe wa kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Huu ndiyo mnara wa Shujaa Ahmad Mzee katika kijiji cha Kitaya. Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Kitaya Mtwara vijijini leo.
===================================================================== 
SHULE YA SOUTHERN HIHGHLANDS MAFINDA YAOMBA WADAU KUCHANGIA SEKONDARI MPYA YA MUFINDI HIGHLANDS SCHOOLS
WAZAZI   na  wadau  wa  shule ya  
kimataifa ya Southern Highlands Mafinga  mkoani Iringa  wanataraji 
kukutana  kesho  kwa ajili ya  kutathimini ufaulu  mzuri wa wanafunzi 
shuleni hapo na kuichangia  shule   hiyo ili  kuendeleza  ujenzi wa  
shule mpya ya  sekondari  inayofahamika kama  Mufindi Highlands Schools 
ambayo inataraji  kuanza rasmi mwakani 2015
 Hatua  ya  shule   hiyo  kukutanisha  wadau na wazazi 
imekuwa  ikifanyika  kila mwaka ila kwa  mwaka   huu wanataraji 
kuitumia   siku hiyo ya  wazazi wa  wanafunzi wanaosoma na  waliosoma  
shuleni hapo kufanya harambee  kama  njia ya kuunga mkono   jitihada za 
 elimu  zinazofanywa na uongozi  wa  shule  hiyo.
Akizungumza na mtandao huu wa 
matukiodaima Mkuu  wa  shule  hiyo Joson Nyabuto alisema  kuwa  zoezi 
hilo  litafanyika mapema  kesho na hivyo kuwaomba  wadau kujitokeza  
kushiriki harambee  hiyo yenye lengo la kuinua kiwango cha  elimu ya  
sekondari wilaya ya Mufindi.
Kwani  alisema kuwa  kuanzishwa 
kwa  shule  hiyo mpya ya  sekondari  katika  wilaya ya  Mufindi ni 
mafanikio makubwa katika  sekta ya  elimu na ni jambo la kujivunia kwa  
kila mdau wa  elimu ndani ya  wilaya hiyo ni nje ya  wilaya ya Mufindi.
Kwani  alisema  kwa mwaka huu 
katika  wilaya ya Mufindi wazazi  wawe na  imani ya  wanafunzi  wote  
watakaofanya  vizuri mtihani wa darasa la saba ambao watateuliwa  
kujiunga na sekondari  nafasi  zipo pia katika  shule  ya sekondari ya 
Southern  Mafinga ambayo ni ujio mpya wa shule za sekondari katika  
wilaya ya Mufindi huku moto  wake  ukiwa ni kufaulisha kwa  kiwango  cha
 juu.
Hata   hivyo  mkuu  huyo alisema 
kuwa  shule  hiyo kwa mwaka  huu   2014 ilikuwa na  wanafunzi 48 na 
wote  walifaulu kujiuga na  sekondari na kuifanya  shule  hiyo katika 
matokeo ya mtihani  huo  kitaifa kwa wilaya kushika nafasi ya kwanza 
kati ya  shule 167  kimkoa nafasi ya nane kati ya shule 458  na kitaifa 
kuwa  shule ya 353 kati ya  shule zaidi ya 15,867 hivyo kwa matokeo  
hayo shule  hiyo imeweza kupanda kwa wastani wa pointi tano  zaidi ya 
mwaka jana .
  Alisema kwa mwaka jana shule  
hiyo ilifaulisha  pia  wanafunzi wote  47  na kushika nafasi ya pili  
kiwilaya  nafasi ya  9 kimkoa na kitaifa  kuwa shule ya  288.
Pia alisema ni muda umefika wa  
ndoto ya  shule  hiyo kuanza  kufanya  kazi  kuendesha  shule  yake ya  
sekondari kuanzia mwakani.
Akielezea  mikakati ya mbeleni 
katika kuwawezesha  watoto  wanaosoma  katika  shule hiyo mkurugenzi 
mtendaji Bi Mary Mungai  alisema  kuwa  tayari ujio wa  shule ya  
sekondari  inayofahamika kwa jina la Mufindi Highalnds Schools ambayo  
kuanzia  mwakani inaanza  kupokea  wanafunzi wa kidato  cha kwanza .
Alisema  kuwa ombi la  
kuanzisha  shule ya  sekondari  lilitolewa na  wazazi wa  wanafunzi  
wanaosoma katika  shule  hiyo ili kuepuka watoto  wao kwenda kupata  
elimu ya  sekondari  mbali na mikono ya shule  hiyo ya  Southern 
Highlands Mafinga na  kuwa  tofauti ya  shule  hiyo  ya  sekondari na 
shule  nyingine ni unafuu wa ada na ubora  wa elimu itakayotolewa lengo 
 likiwa ni  kuifanya  wilaya ya Mufindi kuendelea  kuwa  kisima cha 
elimu  bora nchini.
==================================================================== 
DR. SHEIN AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA NA MAKATIBU ZANZIBAR LEO
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein 
akimuapisha  Bw.Khamis Jabir Makame  kuwa  Mkuu  wa Wilaya ya Kusini 
Unguja  katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo kabla alikuwa
 Mkuu wa Wilaya Kaskazini B Unguja.[Picha na Ikulu.]
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein 
akimuapisha  Bw.Haji Makungu Mgongo  kuwa  Mkuu  wa Wilaya ya Kaskazini B
 Unguja  katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo kabla 
alikuwa Mkuu wa Wilaya Kusini Unguja.[Picha na Ikulu.]
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein 
akimuapisha  Bw.Hassan Khatib Hassan kuwa  Mkuu wa Wilaya ya Wete Pemba 
 katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.[Picha na Ikulu.]
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed 
Shein akimuapisha Bi Madina  Mjaka Mwinyi kuwa Naibu  Katibu Mkuu Wizara
 ya Elimu na Mafunzo ya Amali katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini 
Zanzibar leo.[Picha na Ikulu.]
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein 
akimuapisha Dkt. Said Seif Mzee kuwa Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya 
Biashara,Viwanda na Masoko katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini 
Zanzibar leo.[Picha na Ikulu.]
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein 
akimuapisha Dkt. Juma Yakout Juma kuwa Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya 
Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini
 Zanzibar leo.[Picha na Ikulu.]
Rais
 wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein 
akimuapisha Bibi Khadija Bakari Juma kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na
 Mafunzo ya Amali katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar 
leo.[Picha na Ikulu.]
Mufti
 Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (katikati)akiwa na Waziri wa 
Habari,Utamaduni,Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk na Mkuu wa Mkoa wa 
Kaskazini Pemba Meja Mstaafu Juma Kassim Tindwa wakifuatilia kwa makini 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed 
Shein alipokuwa akiwwapisha Manaibu Katibu Wakuu Wizara mbali mbali za 
Serikali na Wakuu wa Wilaya mbali mbali za Unguja na Pemba  katika 
ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo, [Picha na Ikulu.] 
Mawaziri
 waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Wakuu wa Wilaya mbali mbali za 
Unguja na Pemba pamoja na Manaibu Katibu Wakuu Wizara mbali mbali za 
Serikali wakifuatilia kwa makini walipokuwa wakiapishwa na Rais wa 
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein leo 
katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar, [Picha na Ikulu.] 
 Mwanasheria Mkuu wa Serkali ya Mapinduzi ya Zanzibar Said Hassan 
Said(kulia) akiwa na Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman 
Ngwali ni miongoni mwa Viongozi waliohudhuria  katika Viapo mbali mbali 
vya Wakuu wa Wilaya za Zanzibar na Katibu Mkuu na Manaibu Katibu wakuu 
wa Serikali waliapishwa leo na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
 la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, [Picha na Ikulu.] 
Mawaziri
 waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Wakuu wa Wilaya mbali mbali za 
Unguja na Pemba pamoja na Manaibu Katibu Wakuu Wizara mbali mbali za 
Serikali wakifuatilia kwa makini walipokuwa wakiapishwa na Rais wa 
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein leo 
katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar, [Picha na Ikulu.]
================================================================= 
Lamudi Tanzania kutangaza huduma za madalali bure

Meneja
 Huduma kwa Wateja wa Lamudi Tanzania, Godwin Lemma akizungumza na 
waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam.

 Meneja
 Huduma kwa Wateja wa Lamudi Tanzania, Godwin Lemma akizungumza na 
waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
KAMPUNI ya Lamudi Tanzania, 
imetambulisha huduma yake ya kuwawezesha madalali mbalimbali wanaofanya 
kazi ya kuwatafutia nyumba, viwanja na magari wateja wao ili kuweza 
kutangaza huduma wanazotoa.
Akizungumza na mwandishi wa habari
 hizi leo jijini Dar es Salaam, Meneja Huduma kwa Wateja wa Lamudi 
Tanzania, Godwin Lemma amesema kwa sasa madalali wanaweza kutangaza 
nyumba, viwanja na magari yaliyoko sokoni kupitia mtandao wa kampuni 
hiyo bila malipo yoyote.
Akifafanua zaidi Lemma alisema 
dalali anayependa kupata huduma hiyo anatakiwa kufika katika ofisi za 
Lamudi Tanzania zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam (Garden Road) na
 kujaza fomu ambayo itaelezea huduma yake na kuanza kuitangaza kwenye 
tovuti www.lamudi.co.tz bila malipo yoyote.
“…Kimsingi huduma hii inawasaidia 
sana madalali kutangaza kazi walizonazo, bei zao na hata eneo ilipo. 
Mfano kama ni nyumba au kiwanja baada ya dalali kutoa taarifa za kutosha
 sisi tunamtangazia bure kazi hiyo kupitia tovuti yetu 
(www.lamudi.co.tz),” alisema Lemma.
Alisema mbali ya kuwasaidia 
madalali kutangaza bidhaa zao wameanza kutoa pia mafunzo ya kuwajengea 
uwezo madalali kuweza kufanya kazi zao kiuaminifu zaidi ili kujenga 
heshima ya kazi zao.
“Wakati mwingine tumekuwa 
tukifanya kazi ya kuchukua baadhi ya madalali na kuwajengea uwezo, 
kuwapa mafunzo ya namna ya kufanya kazi zao kiuaminifu zaidi na masuala 
mengine ya msingi katika shughuli zao,” alifafanua Meneja huyo wa Huduma
 kwa Wateja.
Pamoja na hao alisema kwa sasa 
kampuni ya Lamudi Tanzania imezinduwa huduma mpya ya kumwezesha mteja 
kupata taarifa za uuzaji au ukodishaji nyumba ama viwanja kupitia simu 
za mkononi hivyo kumrahisishia kupata taarifa kwa wakati.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
================================================================= 
MAXCOM AFRIKA YATIMIZA MIAKA MITANO, YABADILI MUONEKANO WA HUDUMA YAO YA MAX MALIPO
 Mkurugnezi
 Mtendaji wa Kampuni ya Kitanzania ya  MaxCom Africa, inayotoa huduma za
 Max Malipo,  Juma Rajabu  na Mwakilishi wa Manispaa ya Kinondoni, 
Richard Chagula wakikata utepe kuzindua muonekano mpya wa huduma ya Max 
Malipo, katika hafla iliyokutanisha uongozi wa kampuni hiyo ya Jukwaa la
 Wahariri, leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugnezi
 Mtendaji wa MaxCom Africa, watoaji wa huduma za Max Malipo, Juma Rajabu
 akizindua muonekano mpya wa huduma ya Max Malipo itakavyokuwa sasa 
kwenye ofisi za mawaakala wake.
 Mkurugnezi
 Mtendaji wa Kampuni ya Max Com Africa, watoaji huduma za Max Malipo, 
Juma Rajabu akimkabidhi mfano wa hundi ya sh. milioni 10, kwa Mwakilishi
 wa Manispaa ya Kinondoni, Richard Chagula, kuashiria kampuni hiyo kutoa
 kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara katika shule 
zilizomo katika Manispaa hiyo, wakati wa hafla ya kampuni hiyo kutimiza 
miaka mitano ambapo uongozi ulikutana na wadau wakiwemo Jukwaa la 
Wahariri katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, 
 Mkurugnezi Mtendaji wa Kampuni ya Max Com Africa, watoaji huduma za Max
Malipo, Juma Rajabu akimkabidhi mfano wa hundi ya sh. milioni 10, kwa
Mwakilishi wa Manispaa ya Ilala Mashauri Saidii, kuashiria kampuni
hiyo kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara katika
shule zilizomo katika Manispaa hiyo, wakati wa hafla ya kampuni hiyo
kutimiza miaka mitano ambapo uongozi ulikutana na wadau wakiwemo Jukwaa
la Wahariri katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, leo
Malipo, Juma Rajabu akimkabidhi mfano wa hundi ya sh. milioni 10, kwa
Mwakilishi wa Manispaa ya Ilala Mashauri Saidii, kuashiria kampuni
hiyo kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara katika
shule zilizomo katika Manispaa hiyo, wakati wa hafla ya kampuni hiyo
kutimiza miaka mitano ambapo uongozi ulikutana na wadau wakiwemo Jukwaa
la Wahariri katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, leo
 Mkurugnezi
 Mtendaji wa Kampuni ya MaxCom Africa, Juma Rajabu akishikana mkono na 
Katibu wa Jukwaa la Wahariri Nevile Meena baada ya kutangaza kulichangia
 Jukwaa hilo sh. milioni 5
 Mkurugnezi
 Mtendaji wa Kampuni ya  MaxCom Africa, Juma Rajabu (wapili kushoto) 
akiwa katika picha ya pamoja na wadau mwishoni mwa mazungumzo 
yaliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, leo. Watatu 
kushoto ni Katibu wa Jukwaa la Wahariri Nevile Meena
 Mkurugnezi Mtendaji wa MaxCom Africa, Juma Rajabu akizungumza na wahariri Serena hotel  
 Ofisa
 Mkuu wa Operesheni, wa Maxcom Africa, Ahmed Rusasi akieleza huduma za 
Max Malipo zitolewazo na kampuni hiyo, wakati wa kikao hicho na wadau 
katika hoteli ya Serena jijini DSar es Salaam, leo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa MaxCom Afrika akiwa ameketi meza kuu na wadau
 Baadhi ya viongozi wa Maxcom Afrika katika hafla hiyo
 Wadau kutoka Jukwaa la Wahariri
 Wadau kutoka Jukwaa la Wahariri 
 Wadau kutoika jukwaa la wahariri
Baadhi
 ya waalikwa kutoka Jukwaa la wahariri wakipata chakula cha mchana 
ambacho kilitoplewa kwa wote katika hotelo ya Serena jijini Dar es 
Salaam, baada ya uongozi wa MaxCom Afrika kumaliza mazungumzo yao na 
wadau katika kuadhimisha miaka mitano ya kampuni hiyo. Picha zote na 
Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog
=================================================== 
CLARIFICATION ON 2014 CECAFA CHALLENGE CUP EDITION
The New Vision [Uganda] of this 
Friday November 28, 2014 has run a news story on Page 49 titled ‘CECAFA 
SHOW OFF’ under which the author indicated that this year’s CECAFA 
edition won’t take place. 
As much as the author doesn’t clearly indicate the source of his information for the alleged call-off of the regional event, he somewhere claims to have spoken to me yesterday [Thursday] which never happened.
I therefore wish to clarify as follows:
1. It’s true, this year’s CECAFA challenge Cup had been scheduled for Ethiopia but the intended Member Association later showed inability to host the event.
2. The CECAFA Executive Committee headed by Eng. Leodgar Tenga and the Secretary General Mr. Nicholas Musonye are still working out the possible measures to ensure that a late championship is at least organized.
3. CECAFA will later officially communicate its position on this matter.
4. CECAFA therefore wishes to ask all journalists and Media Houses to consult the relevant authorities before running personal opinions attributed to CECAFA officials.
Anticipating your continued cooperation as we jointly work together for the development of our game.
Yours
ROGERS MULINDWA
CECAFA MEDIA MANAGER
+256 772 751 829/ +256 701 520 115
As much as the author doesn’t clearly indicate the source of his information for the alleged call-off of the regional event, he somewhere claims to have spoken to me yesterday [Thursday] which never happened.
I therefore wish to clarify as follows:
1. It’s true, this year’s CECAFA challenge Cup had been scheduled for Ethiopia but the intended Member Association later showed inability to host the event.
2. The CECAFA Executive Committee headed by Eng. Leodgar Tenga and the Secretary General Mr. Nicholas Musonye are still working out the possible measures to ensure that a late championship is at least organized.
3. CECAFA will later officially communicate its position on this matter.
4. CECAFA therefore wishes to ask all journalists and Media Houses to consult the relevant authorities before running personal opinions attributed to CECAFA officials.
Anticipating your continued cooperation as we jointly work together for the development of our game.
Yours
ROGERS MULINDWA
CECAFA MEDIA MANAGER
+256 772 751 829/ +256 701 520 115
============================================================= 
WIZARA YA AFYA YAKABIDHIWA MAGARI MAPYA
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Donald Mmbando 
(kushoto)akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari   leo  baada ya 
kupokea msaada  wa magari manne na vifaa vya afya  kutoka kwa Mwakilishi
 wa Shirika la Afya  la Dunia(WHO),Dk. Rufaro Chotaro(kulia). 
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Donald Mmbando 
(kushoto)akipokea mojaya funguo kati  ya magari manne kutoka kwa 
Mwakilishi wa Shirika la Afya  la Dunia(WHO),Dk. Rufaro Chotaro(kulia)Serikali imesema inatambua VICOBA kama mkombozi wa wanyonge nchini.
=========================================
Na Eleuteri Mangi- Dodoma
Serikali imesema kuwa VICOBA ni 
taasisi binafsi inayomilikiwa na wananchi wenyewe vikiwa ni miongoni mwa
 tasisi ndogo za kifedha ambazo ni za kibinafsi na huanzishwa, 
kuendeshwa na kusimamiwa ama kijijini, kitongojini na hata kwenye kata.
Hayo yamebainishwa leo Bungeni 
mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba alipokuwa akijibu 
swali la Mbunge wa Rungwe Magharibi Prof. David Mwakyusa (CCM) ambaye 
alitaka kujua kama Serikali inatambua VICOBA  kama mkombozi wa wanyonge.
Mwigulu amefafanua kuwa taasisi hizo zimo kwenye sekta ya fedha isiyorasmi na zinatoa huduma za kifedha mijini na vijijini.
 “Uwepo wa taasisi hizi, 
umewezesha kufikisha huduma za kifedha kwa wananchi waliombali na huduma
 za sekta rasmi ya fedha na hivyo kuwa mkombozi wa wanyonge” alisema 
mwigulu.
Aidha, kwa kutambua suala hilo, 
ili kusaidia na kuimarisha taasisi hizo, Mwigulu amesema kuwa Serikali 
baada ya kupata ushauri kutoka kwa Mshauri Mwelekezi wa masuala ya 
uchumi na tafiti za kijamii, inafanya mapitio ya Sera ya Taifa ya 
Taasisi ndogo za huduma ya fedha ya mwaka 2000 ili kuihuisha iweze 
kukabili na kuzingatia mabadiliko na maendeleo yanayojitokeza katika 
sekta hiyo. 
Vilevile Mwigulu amesema kuwa 
Serikali inakamilisha uhuishaji wa sera ya taasisi ndogo ndogo za 
kifedha ambapo hatua inayofuata ni kuandaa mapendekezo ya muswada ambayo
 yatapelekwa Baraza la Mawaziri mara baada ya kupata idhini na maelekezo
 ya Baraza hilo na muswada huo utafikishwa bungeni.
Taasisi ya VICOBA ilianzishwa 
nchini mwanzoni mwa miaka ya 2000, ambapo imekuwa na manufaa kwa 
wananchi wengi wenye kipato cha chini hususan wanawake waishio vijijini 
wamefanikiwa kuboresha kipato chao na maisha yao kwa ujumla kwa kujiunga
 na taasisi hiyo.
================================================================= 
WAWEKEZAJI WA MAKAMPUNI YA UBELGIJI WAFANYA ZIARA ZANZIBAR.
 Balozi wa Tanzania Nchini Ubelgiji Dkt. Diodorus B. Kamala akielezea 
lengo la ujio wa wawekezaji kutoka Ubelgiji kuja kuwekeza nchini 
Tanzania alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kufuatia ujio wa 
wawekezaji wa nchi hiyo Zanzibar. Picha na Makame Mshenga-Maelezo 
Zanzibar 
Waziri
 wa Miundombinu na Mawasilino Juma Duni Haji akiwa na watendaji wake 
wakuu wakimsikiliza Meneja mauzo  wa Kampuni ya ujenzi ya Anglo Belgian 
Corporation ya Ubelgiji walipofanya mazungumzo Ofisini kwake Kisauni.
Wamiliki
 wa makampuni  toka Ubelgiji wakimsikiliza Mkurugenzi Uenezi wa Mamlaka 
ya Uendelezaji  Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) Bi. Nasria Mohd Nassor 
(hayupo pichani)  walipofika ofisini kwake Maruhubi Mjini Zanzibar. 
Afisa
 Mipango wa Shirika la Bandari Zanzibar   Ali Haji akizungumza na 
wamiliki wa makampuni  kutoka Ubelgiji walipotembelea bandari ya Malindi
 mjini Zanzibar . 
 Waziri wa Fedha Omar Yussuf Mzee akizungumza na ujumbe wa 
Wafanyabiashara  wa Makamupuni ya uwekezaji kutoka Ubelgiji 
walipomtembelea Ofisini kwake  Vuga Mjini Zanzibar. 
 
 
Picha
 ya pamoja ya wawekezaji kutoka nchini Ubelgiji na viongozi  wa Mamlaka 
ya Uendelezaji Vitega Uchumi Zanzibar  (ZIPA).(Picha na Makame 
Mshenga-Maelezo Zanzibar).
======================================================================= 
Msanii wa Komedy wa Nigeria awasifu wasanii wa Tanzania
Na  Mwandishi Wetu
MSANII wa vichekesho (komedy) 
kutoka Nigeria,Okopcha Bright Onyekere maarufu kama Basket Mouth 
amewasifu wasanii wa Tanzania kwa juhudi wanazofanya kuelimisha jamii 
kutumia vipaji vyao.
Akizungumza Dar es Salaam jana 
baada ya kuwasili kutoka Nigeria kwa ajili ya onesho maalum kushirikiana
 na wasanii wa Tanzania juzi Dar es Salaam alisema kutoka aanze sanaa ya
 vichekesho miaka 16 iliyopita amekuwa akipata sifa za wasanii wa 
Tanzania wakiwika katika fani za muziki, sanaa za filamu, michezo ya 
kuigiza na vichekesho.
Onyekere aliyetamba nchini Nigeria
 na Bara la Afrika katika fani hiyo amekuja kufanya onesho moja 
lililopangwa kufanyika jana hoteli ya Golden Tulip, aliongeza kuwa sanaa
 ni utajiri mkubwa kama vipaji walivyopewa vitatumika ipasavyo na 
kutawala jukwaa .
Mkurugenzi wa Kampuni ya Vuvuzela,
 Evans Bukuku alisema lengo la kumleta msanii huyo wa komedy ni 
kuimarisha sanaa ya vichekesho kwa wasanii chipukizi wa Tanzania ambao 
wanahitaji kuandaliwa kwa soko hilo nchini na nje ya nchi.
Alisema Kampuni ya Vuvuzela 
imejitolea kusaidia wasanii wa vichekesho nchini na kuwafundisha namna 
watakavyoweza kuendeleza fani hiyo kazi iliyoanza miaka minne iliyopita 
kampuni ilipoanzishwa.
Bukuku alisema kila mwisho wa 
mwezi kuna onesho maalum ambalo hutumika kuonesha vipaji vya wasanii wa 
vichekesho na jinsi msanii anavyoweza kutawala jukwaa kuwaburudisha 
watazamaji.
Alisema kampuni yake inatarajia 
kufanya maonesho kama hayo mikoa mbalimbali ya Tanzania kuibua wasanii 
wengine wenye uwezio katika fani hiyo.
Mkurugenzi Bukuku alisema katika 
onesho la karibuni Watanzania walikongwa nyoyo zao pale wasanii wa 
Tanzania washirikiana na wasanii wa vichekesho kutoka Kenya ambaye ni 
Mdomo Baggy na Dick Omondi kutoka Uganda anayejulikana kama Uncle Bob 
kufanya onesho kali nchini.
Bukuku aliwashukuru wadhamini 
waliojitokeza kusaidia kufanyika kwa onesho hilo ambao ni Shirika la 
Ndege la Afrika Kusini (SAA),Hoteli ya  Golden Tulip, Gazeti la 
Mwananchi Communications, Clouds Media Group, Ultimate security, Simu 
TV, Prime Advertising, Dar insites, Advertising Dar, Bongo 5, 
Eventlites, Hugo Domingo na Michuzi Blog.
=============================================================== 
MBUNGE MGIMWA APIGANIA UMEME KALENGA ,WANANCHI WAKE WAMPONGEZA
| Mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa akiwa katika usafiri wa Baiskeli kutembelea wananchi wake | 
………………………………………………………………………………………. 
Na Kikosi kazi  cha   matukiodaimablog Dodoma na Iringa  
MBUNGE
wa Kalenga Godfrey Mgimwa (CCM) ameiomba Serikali kupeleka umeme katika
vijiji vilivyopitiwa na umeme huku vyenyewe vikikosa Nishati hiyo.
wa Kalenga Godfrey Mgimwa (CCM) ameiomba Serikali kupeleka umeme katika
vijiji vilivyopitiwa na umeme huku vyenyewe vikikosa Nishati hiyo.
Alitoa ombi hilo wakati akiuliza swali la nyongeza Bungeni ,Mgimwa alivitaja
vijiji vilivyopitiwa na umeme ni Kipela kata ya Nzihi,Wenda kata ya Mseke , Tagamenda kata ya Luhota,Stand ya Mbuzi na Migori kata ya Maguliwa.
vijiji vilivyopitiwa na umeme ni Kipela kata ya Nzihi,Wenda kata ya Mseke , Tagamenda kata ya Luhota,Stand ya Mbuzi na Migori kata ya Maguliwa.
Pia Mbunge huyo alitaka kujua Serikali inawaambia nini wananchi wa Vitongoji vya Majengo Mapya   ,Ilala ,godown A na B kata ya Magulilwa ambayo havina nguzo za kutosha.
Akijibu Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga aliwataka wananchi
hao kutokuwa na wasiwasi na kusema nguzo zitasambazwa katika maeneo yote.
hao kutokuwa na wasiwasi na kusema nguzo zitasambazwa katika maeneo yote.
Vile vile alisema,Serikali inachukua takwimu ya vijiji vyote ambavyo vimepitiwa na  umeme wakati vyenyewe havina ili navyo vipate Nishati hiyo.
Katika swali la msingi Mbunge huyo alitaka kujua ni lini Serikali itapeleka
umeme katika jimbo la Kalenga kata za Lumuli,Kiwelo ( Kiwele),Ulanda na
Magulilwa ili wananchi wa maeneo hayo waweze kuongeza kasi ya maendeleo.
umeme katika jimbo la Kalenga kata za Lumuli,Kiwelo ( Kiwele),Ulanda na
Magulilwa ili wananchi wa maeneo hayo waweze kuongeza kasi ya maendeleo.
 Nguzo  za umeme zikiwa tayari  kata ya Mgama
Akijibu Kitwanga alisema,kata hizo zimewekwa kwenye utekelezaji wa Mradi
Kabambe wa Umeme vijijini awamu ya pili wa kusambaza umeme vijijini
kupitia ufadhili wa mfuko wa Nishati Vijijini ( REF).
Kabambe wa Umeme vijijini awamu ya pili wa kusambaza umeme vijijini
kupitia ufadhili wa mfuko wa Nishati Vijijini ( REF).
Alisema kazi za mradi huo zinajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa
kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 37 .7 ,ujenzi wa njia ya umeme
msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 26.
kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 37 .7 ,ujenzi wa njia ya umeme
msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 26.
Kazi zingine ni ufungaji we Transfoma 12 ,transfoma moja ya kVA 25 ,Transfoma nane za kVA 50 ,Transfoma kVA 100 na mbili za kVA 200 ambapo jumla ya wateja wa awali wapatao 829 wataunganishiwa umeme.
Alisema mradi huo utagharimu kiasi cha sh.bilioni 2.0 na utekelezaji wa mradi
unatarajiwa kukamilika kabla ya Juni 2015 huku mkandarasi wa kazi hiyo akiwa ni kampuni ya M/S. Sengerema Engineering Group ya Tanzania.
unatarajiwa kukamilika kabla ya Juni 2015 huku mkandarasi wa kazi hiyo akiwa ni kampuni ya M/S. Sengerema Engineering Group ya Tanzania.
Kwa
 upande wao  wakazi wa  Magulilwa na  Kiwere na Ulanda  wamempongeza  
mbunge   huyo  kwa  jitihada  zake za  kupigania maendeleo ya  jimbo la 
Kalenga  likiwemo suala la umeme katika maeneo yao.
Akizungumza
 na mtandao  huu John Kibiki  kutoka kata ya  Magulilwa  alisema  kuwa 
wananchi  wa  eneo  hilo  wamefarijika  zaidi na kasi ya  mbunge  wao 
katika kupigania kata  hiyo  kuwa na umeme na kuwa kwa  kufanya hivyo  
kutaongeza kasi ya maendeleo kwa wananchi wa kata  hiyo.
Huku
 Anna Sanga mkazi  wa  Kiwere  alisema  kuwa  uwajibikaji wa mbunge  wao
 ndio ambao  umeendelea  kuwafanya  wana Kalenga   kutoka kimaendeleo 
na  kuwa  wao  walikuwa hawanajiona kama bado hawajapata  uhuru  
kutokana na kukosa  umeme  toka nchi ipate  uhuru wake mwaka 1961.





































+akiwa+katika+picha+ya+pamoja+na+wadau+.jpg)













No comments:
Post a Comment