Mkoa wa Arusha Umetekeleza agizo 
la raisi la ujenzi wa maabara kwa asilimia 80% hadi Novemba 30 mwaka huu
 ambapo hadi kufikia desemba,10 watakuwa wamekamilisha kwa asilimia 90% 
ya ujenzi huo.
 Hayo yalibainishwa na Katibu tawala msaidizi wa mipango na 
uratibu Anza Amen Ndossa ofisini kwake wakati akiongea na waandishi wa 
habari na kusema kuwa wilaya ya Karatu ilikuwa nyuma katika uhamasishaji
 kutokana na malumbano ya kisiasa.
 Ndosa alisema kuwa mkoa wa Arusha unajumla ya shule 138 za 
sekondari za serikali ambapo mahitaji ya vyumba vya maabara ni 414 
ambapo vilivyokamilika ni 105 sawa na asilimia 25% huku ambavyo vipo 
katika hatua mbalimbali ya ukamilishaji ujenzi na uwekaji wa vifaa ni 
309 .
 Alibainisha kuwa Halmashauri ya jiji la Arusha ndio inaongoza 
ikiwa na shule 24 huku mahitaji ya vyumba vya maabara ni 72 ambapo 
vilivyokamilika ni 15 huku 57 vipo katika hatua mbali mbali za 
ukamilishaji.
 Ndossa,alisema kuwa wilaya ya Ngorongoro ina jumla ya shule 10 
huku mahitaji ni vyumba 30 vilivyokamilika 12 huku 18 vipo kwenye hatua 
mbali mbali za ukamilishaji.
 Alisema kuwa wilaya ya Longido inajumla ya sekondari 7 mahitaji
 ni vyumba 21 vilivyokamilika ni 3 huku 18 vipo kwenye hatua mbali mbali
 za ukamilishaji
Aliendelea kusema kuwa Halmashauri
 ya Arusha DC, ina Sekondari 26 mahitaji ni vyumba 78 vilivyokamilka 23 
huku 55 vipo katika hatua mbali mbali,wilaya ya Monduli ina sekondari 13
 mahitaji ni vyumba 39 vilivyokamilika ni 15 huku bado24 vipo katika 
hatua mbalimbali.
Karatu sekondari 29 mahitaji 87 
vilivyokamilika11 huku 76 vikiwa katika hatua mbali mbali za 
ukamilishaji,akamalizia na halmashauri ya Meru ina sekondari 29 mahitaji
 ni 87 huku 26 vikiwa vimekamilika na vilivyo kwenye hatua ya 
ukamilishaji ni 61.
 Ndossa,alisema kuwa ziara aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Arusha, 
Magesa Mulongo, aliyoifanya Oktoba 15 mwaka huu imesaidia kubadilisha 
mitizamo ya wananchi wa Karatu na kuamua kuitikia wito wa kuchangia 
ujenzi wa maabara ambao awali walikuwa wakisuasua kutokana na siasa .
Katika ziara hiyo mkuu wa mkoa 
alikutana na baraza la madiwani pia wananchi na kuwaeleza kuwa swala la 
ujenzi wa maabara sio swala la chama bali ni swala la maendeleo na hivyo
 watoto watakaoshindwa kufanya mazoezi na mitihani ya sayansi kutokana 
na ukosefu wa maabara ni wao hivyo ni jukumu lao kuchangamkia ujenzi huo
 wa maabara.
“Ujenzi wa maabara umeathiriwa na 
ratiba ya uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo wahamasishaji wakubwa wa 
maendeleo ambao ni wenyeviti wameingia kwenye kampeni za uchanguzi hivyo
 ushiriki wao kwenye kuhamsisha ujenzi wa maabara unakuwa ni 
mgumu’’alisema Ndossa..
Ndossa,alisema kuwa wananchi 
wamepata mwamko wa uchangiaji baada ya ziara hiyo ya mkuu wa mkoa,japo 
zoezi hilo limegongana na uchaguzi wa serikali za mitaa,vitongoji na 
vijiji ambapo wenyeviti wa vijiji ndio wasimamizi wa uhamasishaji na 
ukusanyaji wa michango ya ujenzi huo.
Alisema kuwa wananchi wamepata 
mwamko wa uchangiaji japo zoezi hilo liligongana na uchaguzi wa serikali
 za mitaa,vitongoji na vijiji ambapo wenyeviti wa vijiji ndio wasimamizi
 wa uhamasishaji na ukusanyaji wa michango ya ujenzi huo.
Aliongeza kuwa ifakapo Desemba 9 
mwaka huu wakati wa maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru mikoa na wilaya 
zitatakiwa kutoa taarifa ya utekelezaji wa agizo la rais kuhusu ujenzi 
wa maabara katika shule zote za sekondari nchini

No comments:
Post a Comment