TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 4, 2014

WAHARIRI NA WAANDISHI WA HABARI WAPEWA SEMINA YA UHIFADHI WA MAZINGIRA.

unnamedMeneja  Uhifadhi wa Shirika la Utunzaji wa Mazingira WWF Tanzania, Dr. Amani Ngusaru ,akizungumza na wahariri na waandishi wa habari kutoka vyombo vya habari mbalimbali katika semina ilioandaliwa na (WWF) iliofanyika Disemba 2-3, 2014 mkoani Morogoro juu ya utunzaji wa mazingira ili kuleta uwiano sawa wa rasilimali zinazopatikana maeneo mbalimbali nchini. unnamed1Mkurugenzi wa  Shirika la Utunzaji wa Mazingira WWF Tanzania Bw. Bell’Aube Houinato akielezea malengo ya Shirika hilo, ambayo pamoja na mambo mengine ni kuhakikisha ulinzi wa viumbe hai na misitu izingatiwe ili kulinda mazingira na  kuinua uchumi wa taifa. unnamed2Kiongozi wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira WWF, CEA (Coastal East Africa Global Initiative Leader), Peter Scheren akifafanua jambo katika mkutano wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari katika utendaji wao kazi katika uhifadhi wa mazingira. Kwamba kuwepo na ushirikiano katika utunzaji wa mazingira ili kuleta uwiano sawa na rasilimali ambazo zinapatika katika maeneo husika. unnamed3Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Bw.Magese Bulayi akisisitiza jambo kuhusiana uvuvi haramu wakati wa semina hiyo. unnamed4Mtaalam wa Maendeleo ya Uhifadi kutoka Shirika la WWF Tanzania, Prof.Hussein Sosovele akiwakilisha mada yake wakati wa semina hiyo ambapo amesema kuwa kutoka na elimu inayotolewa na WWF katika maeneo mbalimbali hapa nchini, baadhi ya jamii zimeshatambua umuhimu wa hifadhi katika maeneoyao.  “Mapato hayo ni kiwango kikubwa mno, kwa kuwa yanasaidia kusukumamiradi ya maendeleo kakika kijiji husika. Ingawa kuna changamoto zahapa na pale lakini tunaamini haya ni mafanikio na kila mmoja wetuanapaswa kushiriki katika utunzaji wa mazingira,” alisema Profesa Sosovele.
unnamed5Waandishi wa habari wakichangia maada mbalimbali.
unnamed6 unnamed7Wahariri na waandishi wa habari wakiwa katika majadiliano ya namna ya kukabiliana uvuvi haramu katika mwambao wa bahari ya Hindi.

No comments:

Post a Comment