TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, December 3, 2014

SIRI YA MTUNGI SEHEMU YA PILI YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

1 
Muongozaji wa Tamthilia ya Siri ya Mtungi, Jordan Riber akizungumza katika uzinduzi wa tamthilia hiyo Sehemu ya pili  kwenye ukumbi wa Cinemax Century jijini Dar es salaam.
3 
MC wa shughuli ya uzinduzi wa Siri ya Mtungi 2, Ambi Lusekelo akimtambulisha muigizaji nyota wa tamthilia hiyo, Cheche4Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Nchini, Joyce Fisoo Katikati na wadau wa Filamu Tanzania waliohudhuria katika uzinduzi huo  wakifuatikia hotuba bali mbali zilizotolewa wakati wa uzinduzi wa Tamthilia ya Siri ya Mtungi awamu ya pili.
6Maofisa kutoka kampuni ya John Hopkins University For Communication Programs (JHU CCP) ambao moja wa wadhamini wa tamthilia hiyo katika picha ya pamoja.7Le Mutuz akiwa na mmoja wa waigizaji wa Tamthilia ya Siri ya Mtungi awamu ya pili Richa Adhia, Msemaji wa Umoja wa Vijana wa CCM, Paul Makonda na Muigizaji mkongwe nchini, Mwita nao walikuwepo katika uzinduzi huo
8
Le Mutuz akiwa na Msemaji wa Umoja wa Vijana wa CCM, Paul Makonda9 
Waigizaji wa Tamthilia ya Siri ya Mtungi wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya uzinduzi rasmi kwenye ukumbi wa Cinemax Century
…………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu
Bodi ya Filamu Tanzania imewataka waandaaji wengine wa fani hiyo kuiga mfano wa waandaaji wa tamthilia ya Siri ya Mtungi, Shirika Lisilo la Kiserikali (NGO ya Media for Development International Tanzania (MFDI-TZ) kwa kutoa filamu yenye mafundisho mbali ya kuburudisha.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Joyce Fissoo kupitia kwa mwakilishi wake, Beatrice Sumari kwenye ukumbi wa Cinemax Century wakati wa uzinduzi rasmi uliowashirikisha wadau wa fani hiyo, wadhamini na waandaaji.
Sumari alisema kuwa Tamthilia ya Siri ya Mtungi Msimu wa Pili mbali ya kuburudisha, pia imetoa ajira kwa Watanzania wengi, pia imeleta changamoto kuhusiana na mabadiliko ya tabia kwa jamii.
“Filamu imetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu, hii ni fursa kwa wadau wa fani hiyo kuiga MFDI-Tanzania kwa kuleta katika jamii filamu yenye ubora huu, naomba wengine wafuate nyayo zao,” alisema  Sumari.
“Filamu hiyo ina ubora  wa picha, sauti, maudhui na mfuatano wa matukio wa kipekee na kuleta burudani ya aina yake.. ni tamthilia ambayo ukianza kuangalia, hauta kinai na kuwa na hamu ya kufuatilia kile kinachofuata,” alisema.
Afisa kutoka Taasisi ya Misaada ya Wamarekani kupitia (Usaid), Ana Bodipo alisema kuwa wanajisikia furaha kudhamini tamthilia hiyo ambayo imezungumzia maisha halisi ya Mtanzania.
Bodipo alisema kuwa alisema kuwa tamthilia hiyo inaelekeza jamii kuhusiana na ugonjwa hatari wa Ukimwi na kwa wao ni moja ya nyenzo ya kushiriki katika masuala ya afya katika maeneo mbalimbali nchini.
“Matukio mengi katika tamthilia hii yana akisi taswira ya kweli katika jamii na na kuwafanya wafuatiliaji kupata somo halisi kutokana na changamoto mbalimbali,” alisema Bodipo.
Mtayarishaji wa tamthilia hiyo, Louise Kamin kutoka taasisi ya Media for Development International Tanzania (MFDI-TZ) alisema kuwa wamefuraishwa na mapokeo ya tamthilia hiyo pamoja na kuhitimisha na kufichua kilichopo katika mtungini.
 
alisema kuwa sehemu ya pili ya tamthilia hii inakamilisha Siri ya Mtungi kufuatia msisimko mkubwa wa msimu wa kwanza.
Kamin alisema kuwa kukamilika kwa hatua ya pili kunatokana na udhamini mnono wa the John Hopkins University Centre for Communication Programs (JHU CCP) ambao walitoa uongozi wa elimu na mkakati katika tamthilia, taasisi ya Misaada ya Wamarekani kupitia (Usaid), Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii na MFDI.
Mwisho….
.

No comments:

Post a Comment