MultiChoice Africa, kampuni 
inayoongoza katika kutoa burudani ya kulipiwa ya dijitali pamoja na IPP 
Media wamesaini makubaliano yatakayoleta chaneli maarufu zaidi Tanzania,
 ITV, kuwa sehemu ya jukwaa la DStv.
Ushirikiano huu wa kusisimua utawapa watazamaji wa Tanzania kote
 nchini fursa ya kuangalia vipindi vilivyotengenezwa hapa hapa nchini 
vikiwa na ubora mkubwa kidijitali. Chaneli hii itapatikana kwenye 
vifurushi vyote vya DStv ikiwemo kifurushi kilichozinduliwa hivi 
karibuni cha Bomba, Family, Compact, Compact Plus na Premium. 
Akizungumzia ushirikiano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa ITV Bi 
Joyce Mhaville alisema: “Tunajivunia sana ushirikiano huu ambao tumekuwa
 tukiufanyia kazi kwa muda mrefu. Fursa zinazojitokeza kutokana na 
makubaliano haya yatanufaisha kampuni zote mbili pamoja na kuwanufaisha 
watazamaji wetu, hasa kwa wakati huu ambao tumehama kutoka katika mfumo 
wa analojia kuingia dijitali. ITV ina vipindi vyenye ubora 
vilivyotengenezwa hapa hapa nchini na ambavyo vinawafaa watanzania 
wakati DStv itatuwezesha kupanua wigo wetu.”
Akizungumza juu ya hili, Mkurugenzi wa MultiChoice Africa kanda 
ya Afrika Mashariki Bwn Stephen Isaboke alisema: “MultiChoice 
imejizatiti kuwapa watazamaji wake chaneli nyingi mbalimbali zikiwepo 
zinazoonyesha vipindi vya hapa hapa na vile vya nje. Kwa kuwa ITV 
inakuwa kwa kasi na ina watazamaji wengi, ushirikiano huu utatufaa kwa 
vile unaongeza vipindi vilivyotengenezwa hapa nchini. Tutaendelea 
kuwekeza katika kuwaletea vipindi vyenye utofauti. Kwa kupitia vifurushi
 vyetu mbalimbali, tunawapa wateja wetu chaneli nyingi kwa bei tofauti 
ili wawe na uwanja mpana wa kuchagua.”
Bw Isaboke na Bi Mhavile walionyesha kufurahishwa sana na 
kujitoa kwao kwa ushirikiano huu. Waliwahamasisha watanzania kununua 
DStv ili waweze kufurahia ITV na chaneli zingine nzuri.

No comments:
Post a Comment