TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, June 25, 2016

Rais Dkt MAGUFULI alitaka Jeshi la Polisi Nchini Kuwanyang'anya Silaha Majambazi

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA MPANGO WA KITAIFA WA KITUO CHA MAWASILIANO CHA JESHI LA POLISI (CALL CENTRE) JIJINI DAR LEO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua kituo cha mawasiliano ya polisi (Call centre) katika kituo cha Kati jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi. .Pamoja naye ni Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Ndani Meja Jenerali Projest Rwegasira, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine wa sekta ya umma na binfasi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akizindua Kituo kidogo cha Polisi kinachohamishika wakati wa uzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi (Call Centre) katika viwanja vya Biafra jijini Dar es salaam.. Pamoja naye ni Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu kiongozi Mhe. John Kijazi, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine wa sekta ya umma na binfasi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akizindua Kituo kidogo cha Polisi kinachohamishika wakati wa uuzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi (Call Centre) katika viwanja vya Biafra jijini Dar es salaam.. Pamoja naye ni Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu kiongozi Mhe. John Kijazi, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine wa sekta ya umma na binfasi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua kituo cha mawasiliano ya polisi (Call centre) katika kituo cha Kati jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi. .Pamoja naye ni Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Ndani Meja Jenerali Projest Rwegasira, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine wa sekta ya umma na binfasi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Maguguli akisimama wakati wa wimbo wa Taifa wakati wa uzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi katika viwanja vya Biafra jijini Dar es salaam leo. Pamoja naye ni Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu kiongozi Mhe. John Kijazi, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine wa sekta ya umma na binfasi.
Sehemu ya wananchi na wadau waliohudhuria uzinduzi wa Kitaifa wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi viwanja vya Biafra jijini Dar es salaam leo. Pamoja naye ni Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa mambo ya Ndani Mhe Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu kiongozi Mhe. John Kijazi, IGP Ernest manu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine wa sekta ya umma na binfasi.



Kituo hicho cha kwanza kuanzishwa na Jeshi la Polisi hapa nchini kipo katika kituo kikuu cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam na kinafanya kazi kwa kutumia teknolojia ya mawasiliano ya simu na mfumo wa utambuzi wa eneo (GPS) ambapo askari polisi waliopo katika kituo cha mawasiliano watakuwa wakipokea simu kutoka kwa wananchi wanaotoa taarifa za matukio ya uhalifu na kisha kuwaelekeza askari walio jirani ili wafike eneo la tukio na kukabiliana na wahalifu.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali (IGP) Ernest Mangu amemueleza Rais Magufuli kuwa kituo hicho kina uwezo wa kupokea simu 18 kwa mpigo kutoka kwa watu wanaopiga simu ya bure namba 111 au 112 kwa ajili ya kutoa taarifa za uhalifu na kwamba lengo la jeshi hilo ni kuhakikisha askari wanafika eneo la tukio ndani ya dakika 15.
IGP Mangu ameongeza kuwa kituo hicho kimeanzishwa kwa msaada kutoka benki ya CRDB iliyotoa shilingi milioni 320, kitaanza kutoa huduma tarehe 01 Julai, 2016 kikianzia katika mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni Kanda maalum ya Dar es salaam na polisi imejiwekea malengo ya kuwa na vituo kama hivyo nchi nzima ifikapo mwaka 2019.
Akizungumza katika uzinduzi wa kituo hicho, Rais Magufuli amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuanzisha mradi huo na ameahidi kuwa serikali itahakikisha inaunga mkono mpango huo ikiwa ni pamoja na kulifanyia kazi ombi la kununuliwa helkopta itakayorahisisha zaidi ufikaji eneo la tukio.
Aidha, Rais Magufuli amelitaka Jeshi la Polisi kuwanyang’anya silaha wahalifu kabla hawajawadhuru raia na kupora mali zao ama kusababisha mauaji, na amewataka viongozi wa jeshi hilo kuwazawadia askari wanaofanya kazi nzuri ya kupambana na wahalifu.
Dkt. Magufuli pia ametaka jeshi la polisi lisimame imara kuhakikisha serikali inatekeleza ahadi zake kwa wananchi zikiwemo upatikanaji wa maji na huduma nyingine za kijamii na kwamba hatarajii kuona mtu yeyote anafanya vitendo vitakavyosababisha ahadi hizo kutotekelezwa.
Katika hatua nyingine, Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi kubwa anazozifanya katika kuiongoza nchi.
Mufti Mkuu Sheikh Aboubakar Zubeir Ali ametoa pongezi hizo jana jioni tarehe 24 Juni, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam katika futari iliyoandaliwa na Rais Magufuli na akatumia nafasi hiyo kuwasihi Waislamu na watanzania wote kwa ujumla kukataa vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani.
“Niwahusie ndugu zangu watanzania wote, kwamba amani ni kitu muhimu tuitunze amani tuliyokuwa nayo, tuienzi amani tuliyonayo, na hapo tutakuwa tunaisadia serikali na tutakuwa tunamsadia Mhe. Rais katika kuilinda amani” Amesema Mufti Mkuu.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
25 Juni, 2016.

Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ashiriki kampeni ya Media Car Wash mjini Dodoma leo


TRA yazidi kuboresha timu ya kutoa elimu ya kodi, yazindua Jumuiya ya Wanafunzi wa Kodi IFM






MGAHAWA WA KIPEKEE WA PWEZA WAZINDULIWA JIJINI DAR








=====================================================

Baraza Kuu la kwanza la Wafanyakazi wa TAZARA lazinduliwa rasmi leo


=Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa. Makame Mbarawa (MB) amezindua rasmi Baraza Kuu la kwanza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) tukio lililofanyika mapema leo Juni  25.2016, Jijini Dar es Salaam.

Akisoma hutuba ya ufunguzi wa Baraza hilo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo upande wa Uchukuzi, Dk Leonard Chamuriho kwa niaba ya Waziri Profesa Mbarawa, Amelitaka Baraza hilo kufanya kazi kwa moyo mmoja katika hali ya kuifufua TAZARA kiutendaji na ufanisi kama ilivyokuwa zamani.

Akisoma hutuba hiyo, aliwapongeza viongizi wa wanaounda Mamlaka hiyo akiwemo Mhandisi Bruno Ching’andu kwa kuteuliwa kwake kuongoza Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia na viongozi wengine pamoja na wafanyakazi wote.

Ambapo alisema kuwa, ni dhahiri hatua ya leo imefikiwa baada ya jitihada kubwa na hasa tukitilia maanani hali ya kifedha ambayo TAZARA inapitia katika kipindi hiki. Hivyi kuwapongeza kwa uamuzi huo kwani Mabaraza yana umuhimu mkubwa katika maeneo ya kazi na yameonyesha mafanikio makubwa kila yalipoanzishwa kwani yameweza kuongeza uhusiano mwema kati ya Manejimenti, Vyama vya Wafanyakazi na wafanyakazi kwa upande mwingine.

“Mabaraza haya ni dhana ya ushirikishwaji ikiwa na maana kuwapatia wafanyakazi fursa ya kushauri juu ya masuala ya utendaji kazi, sera za taasisi, ufanisi wa kazi, mazingira ya kazi, ustawi wa wafanyakazi katika elimu, nidhamu, vyeo, pamoja na motisha kwa wafanyakazi. Pia dhana hii ya  ushirikishwaji ni kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 na kanuni zake za mwaka 2003 kifungu cha 108.

Pia ni kwa mujibu wa Sheria ya majadiliano katika Utumishi wa Umma Na. 19 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2005. Pia Sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2007 kifungu Na. 73 (1 - 3).

RIDHIWANI AKABIDHI MAGARI YA WAGONJWA KITUO CHA AFYA CHALINZE NA MIONO


MBUNGE wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akikabidhi gari la wagonjwa (ambulance)jana, kwa mganga mkuu wa halmashauri ya Mji wa Chalinze,dkt Hangai ,mbunge huyo alikabidhi magari ya wagonjwa mawili ikiwa ni pamoja na kituo cha afya Miono.
MBUNGE wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akiwasha gari la wagonjwa (ambulance) mara baada ya kulikabidhi katika kituo cha afya cha Chalinze, mbunge huyo alikabidhi magari ya wagonjwa mawili ikiwa ni pamoja na kituo cha afya Miono.(Picha na Mwamvua Mwinyi)

Na Mwamvua Mwinyi,Chalinze

MBUNGE wa jimbo la Chalinze mkoani Pwani,Ridhiwani Kikwete amekabidhi magari ya kubebea wagonjwa (ambulance)katika kituo cha afya cha Chalinze na Miono yote yakiwa yamegharimu zaidi ya sh.mil 200.

Ridhiwani ametoa magari hayo kwa lengo la kupunguza adha ya usafiri kwa wagonjwa hususan wanaotakiwa kwenda kupata matibabu zaidi katika hospital ya rufaa ya Tumbi na Muhimbili.

Akikabidhi magari hayo jana ,kwa mganga mkuu wa halmashauri ya Mji wa Chalinze, dkt Rahim Hangai, mbunge huyo alisema wakati huu sio wa longolongo bali ni wakati wa kutumikia wananchi na kutekeleza yale viongozi waliyoyaahidi ndani ya jamii.

Ridhiwani alisema hatotaka kuona gari hilo haliwatendei haki wananchi hivyo aliomba litumike kwa ajili ya wagonjwa na sio vinginevyo.
Alisema awali kituo cha afya cha Miono kilikuwa na gari la kubebea wagonjwa lakini kwasasa limeharibika hivyo kuamua kupeleka gari jingine lililokuwepo kituo cha afya cha Chalinze.

RAIS DKT. MAGUFULI AFUTURISHA MAKUNDI MBALIMBALI YA VIONGOZI, WALEMAVU WA NGOZI, WASIOJIWEZA PAMOJA NA WAFANYAKAZI WA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

Serikali yasitisha tamko la utoaji wa Chakula Muhimbili.

Na Ally Daud-Maelezo

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , imesitisha tamko la utoaji wa vyakula kwa wagonjwa watakaolazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili kupisha utafiti wa kina kuhusu huduma hiyo ili kuweza kutoa kilicho bora kwa watanzania.

Akizungumza hayo leo jijini Dar es salaam Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Ummy Mwalimu amesema kwamba wameamua kusitisha mpango mpaka watapotangaza tena ili kufanya utafiti kujua kama kuna faida au hasara kwa wananchi.

“Natoa tamko kwamba huduma hii iliyotarajiwa kuanza hivi karibuni isitishwe mara moja ili kupisha watafiti waweze kufanya uchunguzi kujua inawasaidia kwa kiasi gani wananchi” alisisitiza Bi. Mwalimu.

Aidha Bi. Mwalimu amesema kwamba huduma hiyo itatolewa kwa wagonjwa watakaolazwa hapo kwa kulipia shilingi elfu 50 ikiwemo shilingi elfu kumi ya kumuona daktari , elfu kumi ya kitanda na elfu 30 iliyobaki ni kwa malipo ya chakula kwa wiki.

“Huduma hii inalenga kuwasaidia wananchi katika kuwaandalia chakula stahiki kwa wagonjwa na kupunguza usumbufu kwa waangalizi wa wagonjwa wao kuleta vyakula hospitalini ili kuimalisha afya zao kwa ujumla” aliongeza Bi.Mwalimu.
=================================================

WATANZANIA WAASWA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA KWA HIARI BILA SHURUTI.

Na.Aron Msigwa- Dar es salaam.

Wito umetolewa kwa Taasisi,mashirika, makampuni na watu binafsi kuanzia  ngazi ya familia kuendelea kuitumia Siku ya jumamosi ya kila mwisho wa mwezi kufanya usafi wa mazingira, kupanda miti na kutunza vyanzo vya maji kwa hiari bila kusubiri kushurutishwa na sheria kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wakiwemo wafanyabiashara na wafanyakazi wa taasisi na mashirika mbalimbali waliokuwa wakitekeleza wakifanya usafi katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam leo wamesema kuwa hatua ya Serikali kuirasimisha Siku ya jumamosi ya kila mwisho wa mwezi kuwa siku ya usafi wa mazingira kitaifa inaweka msisitizo kuhusu jukumu la kila mwananchi kuwa mlinzi na mwangalizi wa mazingira katika sehemu anayoishi.

Wamesema Suala la usafi wa mazingira linawahusu watu wote, hivyo kila mwananchi anao wajibu wa kushiriki kikamilifu kufanya Usafi wa Mazingira kwenye Makazi yake, Maeneo ya Biashara, maeneo ya Taasisi za Umma na maeneo yenye mikusanyiko ya watu mbalimbali kama masoko na minada.

Bi. Zaituni Musa mkazi wa Mwananyamala, Kinondoni jijini Dar es salaam aliyekuwa akisafisha mifereji eneo la mtaa anaoishi akishirikiana na wananchi wenzake amesema kuwa suala la usafi wa mazingira ni jukumu la kila mwananchi bila kuangalia cheo au nafasi yake katika jamii kwa kuwa kuishi katika mazingira machafu kuna athari kubwa kiafya hususan kuchangia milipuko ya magonjwa ikiwemo Kipindupindu.

" Suala la usafi wa mazingira linatuhusu sote, ni wakati wa kuchukua hatua na kuacha kuishi kwa mazoea,nawaomba watanzania wenzangu tufanye usafi bila kulazimishwa na Serikali kila mmoja atimize wajibu wake" Amesisitiza Bi.Zaituni.


Baadhi ya Wafanyakazi wa DAWASA waliokutwa wakifanya usafi wa mazingira kutii agizo la Kufanya Usafi kwa kila Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi ili kuyaweka maeneo ya Ofisi za Malamka hiyo katika hali ya usafi.

Baadhi ya Wakazi wa Mwananyamala wakipakia Taka walizozoa katika mitaa yao katika gari la kuzoa Taka la Manispaa ya Kinondoni.

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) Wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa zoezi la kufanya usafi wa Mazingira katika maeneo mbalimbali, Mwananyamala jijini Dar es salaam.

Baadhi ya Wafanyakazi wa DAWASA waliokutwa wakifanya usafi wa mazingira kutii agizo la Kufanya Usafi kwa kila Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi ili kuyaweka maeneo ya Ofisi za Malamka hiyo katika hali ya usafi.

Ugonjwa wa Sumukavu wagundulika Dodoma.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Ummy Mwalimu akiongea na waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam kuhusu mlipuko wa ugonjwa unaosababishwa na sumukavu uliotokea hivi karibuni mkoani Dodoma. Picha na Ally Daud-Maelezo.

Na Ally Daud-Maelezo

Ugonjwa unaosababishwa na Sumukavu kwenye Mahindi ya chakula umegundilika katika Wilaya za Chemba na Kondoa Mkoani Dodoma baada ya kupeleka jopo la Wataalam waliofanya utafiti na kugundua kuwepo kwa ugonjwa huo.

Akizungumza hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Ummy Mwalimu amesema kwamba matokeo ya awali ya watafiti hao imeonyesha kwamba ugonjwa huo umesababishwa na ulaji wa chakula kilichokuwa na sumukavu na kuleta madhara.

“Hayo ni matokeo ya awali ya watafiti wa wizara yangu hivyo basi nasubiri matokeo ya vipimo vya damu na haja ndogo vilivyopelekwa kwa uchunguzi zaidi katika Maabara ya CDC, Atlanta iliyopo nchini Marekani na matarajio yetu ni kupata majibu hayo katika kipindi kisichozidi wiki moja” aliongeza Bi Mwalimu.

Aidha Bi. Mwalimu amesema kwamba mpaka kufikia tarehe 24 Juni 2016, idadi ya wagonjwa imefikia 32, na idadi ya vifo imebakia 7. Hii ni baada ya kuongezeka kwa wagonjwa 11 katika kipindi cha wiki moja.

“Hadi jana kulikuwa na jumla ya wagonjwa 9 ambao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Dodoma, na 14 wako katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa. Wagonjwa watatu waliolazwa Hospitali ya Mkoa Dodoma, na wawili waliolazwa Kondoa, bado hali zao ni tete” aliongeza Bi. Mwalimu.

Pamoja na hayo Bi. Mwalimu alisema kwamba Serikali itaendelea kuimarisha mikakati ya kitaifa ya kupunguza uchafuzi wa sumukuvu katika vyakula, ikiwa ni pamoja na kujenga uwezo wa kupima vimelea hivyo katika damu na mkojo miongoni mwa taasisi za ndani ya nchi.

“ Tutaendelea kutoa matibabu kwa wananchi walioathirika na Ugonjwa huo, kwenye Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na Hospitali ya Wilaya ya Kondoa ili kudhibiti na kurudisha afya za wananchi katika kiwango kinachohitajika” aliongeza Bi. Mwalimu

Aidha Bi. Mwalimu ametoa rai kwa wananchi na wakazi wa Dodoma kwamba wanapaswa kuchambua nafaka zilizoharibika (zilizooza, kuvunjika, zilizobadilika rangi), kukoboa mahindi kabla ya kusaga au kuacha kutumia nafaka zitakazoonekana kuharibika sana ili kuepukana na kiasi kilichozidi sumukavu kwenye nafaka.
=================================================

JUMUIYA YA MUZDALIFAT YATOA MSAADA WA VIFAA MBALIMBALI KATIKA HOSPITALI YA MNAZI MMOJA ZANZIBAR.


Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Muzdalifat Farouk Hamadi katikati akiwa na Muakilishi wa Shirika la Halping Hand Muhammad Irfan Bashir kushoto wakimkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Dk,Msafiri Marijani moja kati ya Vifaa vilivyotolewa Msaada na Jumuiya ya Muzdalifat wakishirikiana na Shirika la Halping Hand kutoka marekani,katika Hospitali ya Mnazi mmoja Mjini Unguja.
Baadhi ya Vifaa mbalimbali vya Hospitali ambavyo vimetolewa Msaada na Jumuiya ya Muzdalifat wakishirikiana na Shirika la Halping Hand kutoka marekani vikiteremshwa katika Hospitali ya Mnazi mmoja Mjini Unguja.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Muzdalifat Farouk Hamadi akitoa nasaha kwa mgeni rasmi na Waalikwa katika hafla ya kukabidhi msaada wa Vifaa mbalimbali vya Hospitali vilivyotolewa msaada na Jumuiya ya Muzdalifat wakishirikiana na Shirika la Halping Hand kutoka marekani,katika katika Hospitali ya Mnazi mmoja Mjini Unguja. Muakilishi wa Shirika la Halping Hand Muhammad Irfan Bashir akitoa hotuba katika hafla ya kukabidhi msaada wa Vifaa mbalimbali vya Hospitali vilivyotolewa msaada na Jumuiya ya Muzdalifat wakishirikiana na Shirika la Halping Hand kutoka marekani,katika Hospitali ya Mnazi mmoja Mjini Unguja.
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Dk,Msafiri Marijani akitoa nasaha kwa niaba ya Naibu Waziri wa Afya Baada ya kupokea Msaada wa Vifaa mbalimbali vya Hospitali vilivyotolewa Msaada na Jumuiya ya Muzdalifat wakishirikiana na Shirika la Halping Hand kutoka marekani,katika Hospitali ya Mnazi mmoja Mjini Unguja.PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.
==================================================

MAGUFULI AWATAKA POLISI KUDHIBITI MAJAMBAZI NCHINI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kwenye uzinduzi wa kituo cha Mawasiliano cha Polisi Call Centre Biafra Kinondoni.

Jonas Kamaleki, MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amelitaka jeshi la polisi nchini kuwadhibiti majambazi ipasavyo kwa kuwanyanganya silaha kwenye matukio ya kiuharifu ili kukomesha vitendo viovu katika Taifa.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii.

“Inashangaza jambazi anavamia kituo cha polisi anaua na anaondoka wakati polisi wapo na wana silaha na risasi wanazo lakini wanashindwa kumnyang’anya silaha,”alishangaa Rais Magufuli.Ameongeza kuwa ujambazi na vitendo vya uharifu nchini inabidi vikomeshwe mara moja ili watanzania waishi kwa amani na kufanya maendeleo kwani wananchi wanataka maendeleo.Akiongelea kuhusu maslahi na vitendea kazi kwa jeshi la polisi, Rais Magufuli amesema kuwa serikali yake itafanya kila iwezalo kuliwezesha jeshi hilo ili liweze kufanya kazi kwa ubora zaidi.

Rais Magufuli ameonyesha kuwa na imani na jeshi la polisi licha ya kuwa na kasoro ndogo ndogo kwa baadhi ya polisi ambao wanalichafua jeshi hilo. Aidha ametoa agizo kwa TCRA kushirikiana na jeshi la polisi nchini ili kuweza kurekodi simu na kutoa print out mara moja tofauti na ilivyo sasa.

Kuhusu kundi la wafanyakazi wanaofanyakazi kwenye Dawati la Taarifa la polisi, Mhe. Rais amemtaka Mkuu wa Jeshi hilo, IGP Ernest Mangu kuwafikiria na kuwapatia posho ya kazi kwani kazi wanayoifanya ni ngumu mno na inahitaji umakini zaidi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amemwomba Mhe. Rais kuliongezea fedha jeshi hilo ili liweze kufanya kazi kwa ustadi zaidi na kukomesha vitendo vya uharifu nchini. Makonda amelipongeza jeshi la polisi kwa kudhibiti matukio ya ujambazi hapa nchini hususan kwenye mabenki.

Mpango huu wa Usalama wa Jamii umezinduliwa leo na utadumu hadi 2019 na unatarajiwa kutoa matokeo makubwa ya kudhibiti uharifu nchini.
===============================================

=============================================

Wizara ya Fedha na Mipango yatoa elimu ya ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi kwa wabunge

MPALULEBLOGS:
Mgeni Rasmi, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson akifungua Semina iliyoandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango kuhusu Ubia kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma ilifofanyika leo Mjini Dodoma katika ukumbi wa Pius Mswekwa ikiwa na Lengo la kuwajengea uwezo wabunge kuhusu umuhimu wa kushirikisha Sekta Binafsi katika miradi ya maendeleo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Uratibu Bunge Vijana Kazi Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama(wa kwanza kushoto) akifuatilia Semina iliyoandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango ikilenga kuwajengea uwezo wabunge kuhusu umuhimu wa kushirikiana kati ya Sekta Binafsi na ile ya Umma (PPP) Katika miradi ya maendeleo. Kulia ni Spika wa Bunge Mhe. Tulia Ackson ambaye alikuwa mgeni rasmi katika semina hiyo.
Mbunge wa Ileje Mhe. Janet Mbene akitoa maoni yake wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wabunge kuhusu umuhimu wa kushirikisha Sekta Binafsi katika miradi ya maendeleo.
Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Sophia Simba akitoa maelezo jinsi miradi itakayotekelezwa kwa ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi inavyoweza kuchangia kukuza maendeleo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (katikati) ambaye alikuwa mgeni rasmi wa semina ya kuwajengea uwezo Wabunge kuhusu umuhimu wa Ubia kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma (PPP) akifurahia jambo mapema leo Bungeni Mjini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bajeti Mhe. Josephat Kandege.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Mhe. Josephat Kandege akiwakaribisha wajumbe kutoa maoni katika Semina iliyoandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa lengo la kuwajengea uwezo Wabunge kuhusu umuhimu wa ubia kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma. Kulia ni Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson ambaye alikuwa Mgeni Rasmi kwenye semina hiyo.( Picha na Frank Mvungi-Dodoma )