TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, August 28, 2014

Atlanta Falcons Edition

Castle lite yataja washindi sita wa wiki ya kwanza kwenye shindano la Casttlelite Yachy Party.

Meneja msaidizi  wa bia ya castle lite Victoria Kimaro kushoto akizungungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam alipokuwa akiwatangaza washindi sita wa wiki ya kwanza katika shindano la promosheni ya Castle lite Yacht Party ambapo baadae watapatikana washindi watakaojishindia zawadi kubwa ya kushiriki katika burudani itakayofanyika katika kisiwa kwenye Bahari ya Hindi na kulia kwake ni meneja wa bia hiyo Geoffray Makau.
Sehemu ya waandishi mbalimbali wa vyombo vya habari wakiwa katika mkutano wa waandishi wa habari kwenye kutangazwa kwa washindi sita wawiki ya kwanza ambao walishiriki katika shindano kubwa la promosheni ya Castle lite Yachy Party jijini Dar Es Salaam.

RAIS KIKWETE KATIKA SHEREHE ZA UZINDUZI WA PROGRAMU YA UIMARISHAJI WA MIPAKA YA KIMATAIFA MKOANI KAGERA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipokea nyimbo za Taifa za nchi zao eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi wa Tanzania na Burundi katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizindua kwa pamoja eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.

JUKATA WAMBEBESHA LAWAMA SITTA, WASEMA KATIBA MPYA NI NDOTO KUPATIKANA

 Kaimu mwenyekiti wa Uukwaa la Katiba Tanzania Hebron Mwakagenda akizungumza na wanandishi wa habari leo Agosti 27, 2014 juu ya mwenendo wa bunge la katiba.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Wakati mchakato wa katiba Tanzania ukiwa ni kama kitendawili kisicho na majibu sahihi kutokana na mchakato huo kuvurugika na kukosa mwelekeo, nao Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) wazidi kumtupia lawama zote za kuvurugika bunge hilo mwenyekiti wa bunge hilo mheshimiwa Samweli Sitta na kudai kuwa ndiye aneyeuvuruga mchakato huo baada ya kugeuza Bunge hilo kama kikao cha Chama cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza na wanahabari muda huu jijini Dar es salaam kaimu mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania Hebron Mwakagenda amesema kuwa JUKATA wamekuwa wakifuatilia mchakato huu wa bunge ka katiba kwa wiki mbili hizi na kubaini mapungufu makubwa sana ambayo yanatokea jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa mwenyeikiti wa bunge hilo hana nia wala dhamira ya kulipatia taifa katiba mpya ya watanzania.
Wanahabari mbalimbali wakiwa wanamsikiliza kiongozi huyo wakati wa mkutano Bw Mwakadenga amesema kuwa swala la mahudhurio ya wabunge wanaoshiriki katika kamati mbalimbali za bunge hilo yamekuwa madogo sana na yasiyo ya kuridhisha ikiwa ni pamoja na wabunge wengi kutokuhudhuria katika kamati hizo pamoja na kusaini kulipwa posho za siku jambo ambalo amesema kuwa ni wizi mpya kwa
watanzania,
 “Kwanza bunge la katiba linaonyesha kuwa wajumbe 441 wamehidhuria lakini uchunguzi wetu unaonyesha kuwa hawa ni wale wote ambao wamewahi kufika na kusaini kwenye kitabu cha mahudhurio wengine wao takribani 100 tuligundua kuwa hawapo bungeni wakiwemo mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na serikali ya mapinduzi Zanzibar pamoja na baadhi ya viongozi wa kamati”amesema Mwakagenda.
Ameongeza kuwa mambo mengine ambayo yanalifanya bunge hilo kuvurugika ni pamoja na kukosekana kwa muafaka na maridhiano ya kitaifa, matumizi mabaya fedha ikiwa ni pamoja na Wajumbe kulipwa bila kuhudhuria bungeni, kukosekana kwa theluthi mbili toka Zanzibar ili kupitisha katiba,pamoja na uondoaji wa vifungu muhimu kwenye rasimu mambo ambayo amesema kuwa mwenyekiti Samweli Sitta ameyafumbia macho na kijifanya kama hayaoni huku akiwa anajua wazi kuwa anauzika mchakato huo.
“Huyu mzee hatujamwelewa kabisa, sisi tumekaa tumezungumza naye tukamuuliza atueleze swala la theluthi mbili hawa wajumbe watapatikana wapi hajatupa jibu la kuridhisha na ukimwona ni kama mtu ambayeameshachanganyikiwa, anapambana na kila anayekuja mbele yake, iwe mwandishi, mwanaharakati, mbunge, yeye amekaa kujihami tu, sasa hali hii sio nzuri kwa mchakato muhimu kama huu”alisema kiongozi huyo wa JUKATA.
Katika hatua nyingine JUKATA wamemwomba raisi Kikwete kiusimamisha mchakato huu wa katiba hadi kipindi kingine kutokana na kuonekana wazi kuwa hauwezekani na kusema Tanzania imekuwa na michakato mingi ambayo sisi kama taifa hatuwezi kuiendesha kwa wakati mmoja na kupata katiba bora, 
“Kusema ukweli taifa sasa lina michakati mingi sana mfano mchakato wa vitambulisho vya taifa, uchaguzi wa serikali za mitaa, daftari la kudumu la kupiga kura na michakato mingine mikubwa, hii haitaki usome sana ndo uelewe ni kutumia busara tu kwamba huu mchakato wa katiba hautawezekana tena, sisi tunamwomba mheshimiwa Rais Kikwete awasikilize watanzania na kuusimamisha mchakato huu wa katiba ili tujipange upya kuanza
tena.
Mchakato wa katiba umekuwa ukiendelea jijini Dodoma bila ya mariano na wajumbe waliotoka wa UKAWA huku kukiwa na taarifa kuwa rais amekubali kukutana nao wiki hii kwa ajili ya mazungumzo ya kuunasua mchakato huu.

WANAWAKE ZAIDI YA 600 KUNUFAISHWA NA ELIMU YA UJASILIAMALI MKOANI MWANZA

Afisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile akielezea jukumu la TBS katika kuwaelimisha wanawake wajasiriamali wa Kitanzania watakaoshiriki katika kampeni ya Mwanamke na Uchumi juu ya ubora na viwango katika bidhaa wanazoandaa.
 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Angels Moment, Naima Malima akizungumza na na waandishi wa habari kuhusu Kampeni ya Mwanamke na Akiba inayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza kuanzia Septemba 4-5, ambapo zaidi ya wanawake wajasiriamali 600 wanatarajiwa kufaidika na mafunzo hayo. 
Afisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile pamoja na Meneja wa Kanda ya ziwa wa PPF Bwana Meshach Bandawe wakifuatilia mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika ukumbi wa Gold Crest kuwahabarisha kuhusu kampeni ya Mwanamke ya Uchumi itakayofanyika jijini Mwanza tarehe 4-5 Septemba, 2014 katika viwanja vya Mwaloni Kirumba Jijini Mwanza.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Angels Moment, Naima Malima akizungumza na na waandishi wa habari kuhusu Kampeni ya Mwanamke na Akiba inayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza kuanzia Septemba 4-5, ambapo zaidi ya wanawake wajasiriamali 600 wanatarajiwa kufaidika na mafunzo hayo. 
Afisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile akielezea jukumu la TBS katika kuwaelimisha wanawake wajasiriamali wa Kitanzania watakaoshiriki katika kampeni ya Mwanamke na Uchumi juu ya ubora na viwango katika bidhaa wanazoandaa.

Wednesday, August 27, 2014

Umoja wa Machifu Tanzania (UMT) wawasilisha mapendekezo yao kuhusiana na Rasimu ya Katiba Mpya.

 Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu akiwaeleza jambo Wawakilishi wa Umoja wa Machifu Tanzania (UMT) kuhusu mapendekezo yao waliyoyawasilisha kwake kwaajili ya Katiba Mpya.
 Chifu John Nyanza (aliyekaa katikati) wa kutoka Magu akimueleza jambo Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu (kulia) juu ya uwasilishaji wa mapendekezo yao kwa ajili ya Katiba Mpya alipokutana naye leo kwenye Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
 Chifu Agnes Ndaturu (kushoto) wa kutoka Ntuzu, Bariadi akimueleza jambo Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu (kulia) juu ya uwasilishaji wa mapendekezo yao kwa ajili ya Katiba Mpya alipokutana naye leo kwenye Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
 Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu (kulia) akipokea mapendekezo ya maoni toka kwa Chifu John Nyanza alieuwakilisha Umoja wa Machifu wa Tanzania (UMT) leo kwenye Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
Baadhi ya Waandishi wa Habari walikifuatilia uwasilishwaji wa mapendekezo toka kwa Machifu waliouwakilisha Umoja wa Machifu wa Tanzania (UMT) leo kwenye Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
 

 
 
Na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma.
26/08/2014.
UMOJA wa Machifu wa Tanzania (UMT) kupitia wawakilishi wake, leo umewasilisha nyongeza ya mapendekezo yake kuhusu Katiba Mpya kwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Akiuwakilisha Umoja wa Machifu Tanzani (UMT), Chifu kutoka Magu John Nyanza amemueleza Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba kuwa wanaishauri Serikali kutayarisha mkakati wa Kitaifa wa Utamaduni kwa kuwashirikisha wadau wakuu wa masuala ya Utamaduni ili mpango mkakati huo uwe na Dira ya Utamaduni itakayobainisha cha kufanya ili kujenga, kuhamasisha na kuendeleza Utamduni katika maeneo yote nchini.

“Chifu kutoka Magu, John Nyanza amesema kuwa lengo la kuwasilisha mapendekezo hayo kwaajili ya kusisitiza masuala mazuri ya Utamduni kuendelea ili kuweza kudumisha madili kwa nia nzuri ya kudumisha amni na ushirikiano”. Alisema Chifu Nyanza.

Naye Chifu kutoka Ntuzu, Bariadi Chifu Agnes Ndaturu ameeleza kuwa mapendekezo yao yatasaidia kuweza kuwatambua waganga wa Jadi ambapo hapo zamani , mganga wa Jadi alikuwa anatambulika na kufanya kazi katika eneo husika analotoka, lakini hivi sasa waganga wengi wa jadi wamekuwa na tabia ya kufanya kazi zao bila mipaka.

 ”Mapendekezo haya yatasaidia viongozi wa waganga wa jadi nchini kuwatambua wale waganga wanaokiuka maadili ya shughuli zao mfano mauaji ya Albino, kwakuwa kila kiongozi atakuwa anawatambua waganga wa eneo lake husika”. Alisema Chifu Ndaturu.

Aidha, Machifu hao wameongeza kuwa, Wajumbe wenzao waliowatuma kuwawakilisha wanasisitiza juu ya umuhimu wa Utamaduni kupewa nafasi rasmi katika Katiba mpya na Serikali ili pawepo na kipaumbele katika utekelezaji wake nchini.

Wakizungumza kwa kauli moja Umoja wa Machifu wa Tanzania wamesema kuwa suala la Utamaduni katika Rasimu ya Pili ya Katiba lifanyiwe marekebisho kwa kuzingatia mapendekezo yaliyoibainishwa huku msisitizo wao ukiwa katika Katiba kueleza wazi kuwa sera na Sheria mpya zitakazotungwa  zihakikishe kuwa Tume ya Taifa ya Utamaduni inaanzishwa kisheria ili kusimamia masuala ya Utamaduni.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewatotoa wasiwasi wawakilishi wa Umoja wa Machifu hao wa Tanzania aliokutana nao kwa kuwaeleza kuwa atayawasilisha katika Uongozi wa Kamati ya Bunge ambapo Kamati Ndogo ya Uongozi inatarajiwa kukutana leo jioni ili kuweza kuyajadili.

“Nimeyapokea mapendekezo yenu, kwakuwa Kamati zinaendelea na kazi ambapo wiki hii kamati zitakuwa zimemaliza kazi zake na hakutakuwa na nafasi tena ya kuyapokea mapendekezo na maoni mengine”. Alisema Samia.

Hivi karibuni, makundi mbalimbali yaliwasilisha mapendekezo yao ambapo baadhi ya makundi hayo yakiwemo Wafugaji, Wasanii na Wanahabari yaliwasilisha.

Miami Dolphins Edition

Preseason Division-by-Division Predictions Preseason Division-by-Division Predictions
BleacherReport.com
Dolphins Cut WR Binns Among Moves to 75 Dolphins Cut WR Binns Among Moves to 75
ProFootballTalk.com
Quinn Confirms He Was Cut: 'Enjoyed Every Second' Quinn Confirms He Was Cut: 'Enjoyed Every Second'
Sun-Sentinel.com
Report: Team 'Strongly Considering' Activating Pouncey Report: Team 'Strongly Considering' Activating Pouncey
BleacherReport.com
Lamar Miller Still Leader to Be Fins' Lead Back Lamar Miller Still Leader to Be Fins' Lead Back
MiamiHerald.com
Tougher Cuts Loom for Dolphins Tougher Cuts Loom for Dolphins
Sun-Sentinel.com
Clay Determined to Become Household Name Clay Determined to Become Household Name
Sun-Sentinel.com
Jones: Suspension Won't Derail My Season Jones: Suspension Won't Derail My Season
MiamiHerald.com
Bucs Don't Sign Incognito After 5-Hour Meeting Bucs Don't Sign Incognito After 5-Hour Meeting
BleacherReport.com
DL Mitchell Already Proving He's a Free Agent Gem DL Mitchell Already Proving He's a Free Agent Gem
MiamiHerald.com
Caleb Sturgis Returns to Practice Caleb Sturgis Returns to Practice
ESPN.com
James Making Every Snap Count This Preseason James Making Every Snap Count This Preseason
MiamiDolphins.com
Grades for NFL's Biggest Offseason Moves Grades for NFL's Biggest Offseason Moves
BleacherReport.com

Miami Dolphins Visit BleacherReport.com for more Dolphins Coverage »

Carolina Panthers Edition