Mkuu
 wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro akizungumza na wanafunzi wa 
Makete Girls Sekondari (hawapo Pichani) na pia kutoa maagizo kwa uongozi
 wa shule.
Shule
 ya sekondari ya wasichana (Makete Girl's) imetii agizo la mkuu wa 
wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro la kutaka wanafunzi hao wapewe uji
 mara baada ya vipindi viwili vya asubuhi badala ya saa nne agizo 
alilolitoa Agosti 8 mwaka huu
Hali
 kadhalika mkuu huyo aliagiza wapewe chakula cha mchana saa saba ili 
kuweka uwiano mzuri wa muda wanaokula wanafunzi hao wawapo shuleni hapo
 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi na walimu wa shule hiyo.
Mwandishi
 wetu aliyefika shuleni hapo ijumaa ya Agosti 22, ameshuhudia maagizo 
hayo yakitekelezwa jambo ambalo limepongezwa kwa kiasi kikubwa na 
wanafunzi hao
"Ni
 kweli tumeshuhudia ratiba ya chakula ikibadilika kama alivyoagiza mkuu 
wa wilaya aliyokuja hapa shuleni, na kweli tunaona ni afadhali na 
tutajisomea vizuri na limetekelezwa mara tu alivyoagiza hivyo naupongeza
 uongozi wa shule kwa kutekeleza hilo" alisikika akisema mwanafunzi 
mmoja
Katika
 hatua nyingine shirika la sumasesu limetoa elimu ya ujinsia kwa 
wanafunzi hao na kuwataka kujiepusha na vitendo vya ngono ilihali wao ni
 wanafunzi ili waweze kufikia malengo yao
Rai
 hiyo imetolewa na Bi Anifa Mwakitalima na kusema kuwa wao ni wanafunzi 
wa kwanza katika shule hiyo na wanategemewa kufaulu na kuweka sifa nzuri
 kwa wilaya, hivyo itakuwa nia aibu kubwa kwa mwanafunzi kuweka historia
 ya kuwa mwanafunzi wa kwanza kusoma katika shule hiyo na pia akawa wa 
kwanza kupata mimba na kufukuzwa shule
"Ninani
 anayependa awe wa kwanza kupata mimba na kuandika historia mbaya kwa 
shule? bila shaka hakuna, wadogo zangu nawaomba mzingatie masomo 
achaneni na ngono kabisa muda wenu bado, huu ni muda wa kusoma" alisema 
Mwakitalima
Kwa
 upande wake Faustine Mwenda amewataka wanafunzi hao kujitambua kuwa 
wamepelekwa shuleni kwa ajili ya kusoma hivyo wajisomee na watafaulu 
vizuri hivyo kujijenge amsingi mzuri wa maisha pasipo kupata shida
Amesema
 mafanikio yao yanajengwa na wao wenyewe hivyo endapo wataonesha uzembe 
wa kupuuzia masomo ni dhahiri kwamba wataharibu malengo yao, hivyo 
wanatakiwa kushika elimu na si mambo mengine yanayoweza kuwasababisha 
wasifikie malengo yao ikiwemo kupata ujauzito.
Makete
 girls ni sekondari pekee na ni mpya ya wasichana iliyoanzishwa mapema 
mwaka huu wilayani hapo ambapo kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 36.Na Edwin Moshi, Makete. 
No comments:
Post a Comment