TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, September 26, 2013

WANAFUNZI WA DACICO WAPATA KATIBA YAO.

Rais wa Chuo Cha DACICO kISIZA AKIKABIDHI KATIKA KWA MKURUGENZI WA CHUO, Idrisa Mziray.
 Mmoja wa Waasisi wa chuo cha DACICO , Mr. Six akito neno kwa wanafunzi kabla ya Uzinduzi.
Wanafunzi wa Chuo Cha DACICO TANZANIA- Wakiwa katika Picha ya Pamoja muda mfupi baada ya kufanya Uzinduzi wa KATIBA yao waliyoipendekeza na kushiriki kwa asilimia 100 katika kuirekebesha na kuipigania kila kukisha kwa walimu wao, aidha katika Hafla hiyo ya Uzinduzi huo, wanafunzi wa masomo na fani zote walishiriki kufanya Uzinduz.(Picha kwa hissani ya Miiss Demokrasia Tanzania 2013/2015).

MAOMBOLEZO


  • RAIS KENYATTA ATANGAZA SIKU TATU ZA KUOMBOLEZA
  •  JESHI LA KENYA LAHITIMISHA KIBARUA KIGUMU
  •  AL SHABAAB WADAI MATEKA 137 WAMEUAWA,WAONYA

  •  Waandishi  Wetu  n a Mashirika ya Kimataifa


  
K
enya imeanza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kwa waathirika wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika katika jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi na kusababisha mapigano yaliyodumu kwa siku nne 
. Rais Uhuru Kenyatta amesema bendera zitapepea nusu mlingoti kuanzia jana kwa heshima ya waliopoteza maisha yao katika mashambulizi hayo. Katika hotuba yake kwa taifa juzi usiku, Rais Kenyatta alisema kuwa alihisi uchungu mkubwa na kuwa Kenya imejeruhiwa vibaya, lakini alielezea matumaini kwa kuwa shambulizi limeisha na kusema kwamba waliohusika watakiona cha mtemakuni. 
Juzi Rais Kenyatta ametangaza kuwa operesheni za kijeshi dhidi ya magaidi zimemalizika katika maduka ya kifahari ya Westgate.Alisema Kenya imewaaibisha washambuliaji hao, kwa kuua magaidi watano na kuwakamata wengine 11 ambao wamezuiliwa. Katika tukio hilo Watu 62 wameuawa ikiwemo wanajeshi watatu na wengine 8 wamejeruhiwa. Habari kutoka Kenya zinaeleza kuwa kuna hofu kuwa idadi ya watakaofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wa uchunguzi wa kimataifa wanaungana na wale wa Kenya kujaribu kuondoa miili ambayo imenaswa kwenye vifusi vya jengo hilo ambalo sehemu yake iliporomoka jana.Nia ni kujaribu pia kutambua uraia wa washambuliaji hao. Baraza la usalama wa kitaifa lilitarajiwa kukutana jana kudadisi yaliyotokea na kujiandaa kwa mkakati mpya wa kukabiliana na magaidi.

Magaidi watatu wa kundi la Al Shabaab lililokiri kutekeleza mashambulizi hayo,waliuawa katika shambulizi hilo lililodumu kwa siku nne na kuwa washukiwa we n g i n e 11 wa l i k ama twa wakijaribu kuondoka nchini.Wakati huo huo, ofisa mmoja mkuu wa serikali ya Somalia, amesema kuwa hakuna suluhu la kijeshi kwa kundi la wanamgambo wa Al Shabaab nchini humo. Wanamgambo hao wamekiri kuhusika na mashambulizi ya kigaidi nchini Kenya.

  Akizungumza na mjumbe wa nchi hiyo katika Umoja wa Mataifa, Yusuf Mohamed Ismail Bari Bari, alisema kuwa serikali yake na jamii ya kimataifa inapaswa, kuangazia zaidi mizizi ya tatizo la magaidi hao, upatikanaji wa rasilimali pamoja na uwakilishi wa kisiasa.Wakati huo huo, Wataalamu wa uchunguzi wa Kisayansi kutoka nchini Ufaransa na Israel wamewasili nchini Kenya kushirikiana na wazawa ili kujua silaha zilizotumika wakati wa shambulizi hilo la kigaidi.

  Wataalam hao wanalenga kubaini ni aina gani ya milipuko ilitumika kulipulia jengo hilo.Pia maofisa wa Serikali bado wapo eneo la tukio ili kuhakikisha usalama unakuwepo. Televisheni ya nchi hiyo ya Q TV imesema kuwa kazi ambayo ilikuwa nimeanza ni ya kuondoa vifusi ili kuweza kuondoa maiti zilizofukiwa baada ya sehemu ya jengo hilo kuanguka.
   Kwa mujibu wa matangazo hayo maiti hizo zitatambuliwa kwa kutumia kipimo cha DNA. Matangazo ya televisheni hiyo yalieleza kuwa ndani ya jengo hilo la kibiashara moshi mkubwa ulikuwa ukizidi kufuka lakini hakukuwa na taarifa zozote kwa waandishi wa habari kuhusu ni nini kilichokuwa kikiendelea.

   Katika hatua nyingine, Serikali ya Kenya imetangaza donge nono la dola milioni 25 kwa mtu yeyote atakayefanikisha kupatikana kwa magaidi sugu ulimwenguni. Tayari FBI imetoa orodha ya magaidi 23 wanaotafutwa.
   Wakati huo huo, wanamgambo wa Al-Shabaab kutoka Somalia jana walidai mateka 137 waliokuwa wakiwashakilia waliuawa katika jumba la kibiashara la Westgate jijini Nairobi.Kwa mujibu wa shirika la habari la Ufaransa, AFP, idadi kamili ya waliokufa imekuwa ngumu kujulikana na inaweza ikawa ni kubwa zaidi kuliko idadi ya walioorodheshwa kukosekana.

   Wapiganaji hao wenye uhusiano na al-Qaeda, katika ujumbe waliouweka kwenye mtandao wa Twitter, walisema "mateka 137 waliokuwa wakishikiliwa na mujahedeen" wamekufa."Wanamgambo hao pia waliwatuhumu wanajeshi wa Kenya kwa kupiga makombora yenye sumu kuhitimisha mapambano ya kuwasaka.


Matukio ya ubabe wa Al-Shabaab


   Haya ni miongoni mwa mashambulizi makubwa ya kigaidi ambayo yamewahi kutekelezwa katika Kanda ya Afrika Mashariki.


Taarifa zinazohusiana na Kenya

  Septemba 21, 2013: Magaidi walitumia guruneti na bunduki kushambulia jengo la kifahari la Westgate mjini Nairobi, Kenya lenye maduka na mikahawa 80 na kuwaua watu 62 huku zaidi ya 175 wakijeruhiwa.Kundi la kigaidi la Al-Shabaab lilikiri kufanya shambulio hilo.
    Oktoba 2011-Machi 2013: Al Shabaab na wapiganaji wake walifanya mashambulizi kadhaa nchini Kenya na kuwaua zaidi ya watu sitini wakilipiza kisasi kile walichosema ni hatua ya Kenya kupeleka majeshi yake nchini huo kupigana dhidi yao.Serikali ya Kenya ilituma vikosi vyake nchini Somalia baada ya al-Shabaab kufanya mashambulizi kadhaa katika maeneo ya mipakani pamoja na kuwateka nyara watalii wa kigeni.

    Julai 11 , mwaka 2010 : Wanamgambo wa Al Shabaab walilipua mabomu katika mji mkuu wa Uganda Kampala, katika mkahawa ambako mashabiki wa soka walikuwa wanatazama fainali ya michuano ya Kombe la Dunia, kwenye televisheni kubwa.
    Takriban watu 76 waliuawa. Kundi la Al-Shabaab lilisema kuwa mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Uganda kujihusisha na vita dhidi ya kundi hilo Somalia.Novemba 28, mwaka 2002: Kundi hilo la kigaidi lilishambulia hoteli ya kifahari iliyokuwa inamilikiwa na Waisraeli, katika eneo la Kikambala karibu na mji wa Mombasa na kuwaua watu 13.

   Dakika chache kabla ya shambulizi hilo, magaidi hao waliifyatulia makombora ndege ya Israel iliyokuwa inaruka katika Uwanja wa Kimataifa wa Mombasa, lakini waliikosa.Agosti 7, mwaka 1998: Kundi lingine la kigaidi la al-Qaeda lilishambulia balozi za Marekani mjini Nairobi na Dar es Salaam. Mashambulizi hayo yaliwaua watu 224 , wengi wakiwa Wakenya . Raia 123 wa Marekani pia waliuawa.

MWANAMKE AWATOKEA ‘PUANI’ WATU WATATU

  • MAHAKAMA KUU YAWAHUKUMU KUNYONGWA HADI KUFA


Na Moses Mabula, Nzega


Mahakama Kuu Kanda ya Tabora imewahukumu watu watatu kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi mkazi wa Kijiji cha Mbagwa wilayani Nzega mkoani Tabora,Mganga Mgisha, ili mmoja wa wauaji hao apate fursa ya kuoa mke wa marehemu huyo.Katika kesi hiyo, mmoja wa wauaji hao, Kulwa Makomelo alikuwa na njama za kutaka kumuoa mke wa marehemu huyo,Catherine John, ambapo ilidaiwa alimlipa kiasi cha sh. 20,000 muuaji mwenzake, Kisena Lutonja, ili amsaidie kufanikisha mauaji hayo.


Mke wa marehemu huyo ni miongoni mwa waliohukumiwa adhabu hiyo.Akitoa hukumu hiyo iliyochukua muda wa saa tatu, Jaji Amiri Mluma, alisema mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa kuwa washtakiwa hao walipanga mauaji hayo.  Alisema washtakiwa wamepatikana na shtaka hilo la kupanga kuua na kufanya mauaji."Walipanga makusudi kumuua Mugisa, hivyo mahakama inawahukumu kunyongwa hadi kufa ili iwe fundisho kwa watu wengine.


   Jaji huyu aliiambia mahakama hiyo kwamba; "Kutokana na kukithiri kwa vitendo vya watu kushambuliana kwa mapanga bila sababu na kujichukulia sheria mkononi natoa adhabu hii ili iwe fundisho kwa watu wa aina hiyo."
  Awali, mwanasheria wa Serikali, Iddforce Makandara, aliiambia mahakama hiyo kuwa watuhumiwa hao wote kwa pamoja walimuua, Mugisa kwa kumpiga kitu kizito kichwani na kisha kumshambulia kwa mapanga hadi kufa.Aliiambia mahakama hiyo kuwa mwaka 2005 watuhumiwa hao walikula njama za kumuua Mugisa ambaye ni mume wake na Catherine John.
  Alidai kuwa walifanya hivyo ili mjane wa marehemu aolewe na Makomelo, huku Lutonja akilipwa sh. 20,000 ili amsaidie kufanikisha mauaji hayo.Makandara aliomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa washtakiwa hao ili iwe fundisho kwa watu wanaojichukulia sheria mkononi


Katika kesi hiyo, mmoja wa wauaji hao, Kulwa Makomelo alikuwa na njama za kutaka kumuoa mke wa marehemu huyo,Catherine John, ambapo ilidaiwa alimlipa kiasi cha sh. 20,000 muuaji mwenzake, Kisena Lutonja, ili amsaidie kufanikisha mauaji hayo.Mke wa marehemu huyo ni miongoni mwa waliohukumiwa adhabu hiyo. Akitoa hukumu hiyo iliyochukua muda wa saa tatu, Jaji Amiri Mluma, alisema mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa kuwa washtakiwa hao walipanga mauaji hayo.  Alisema washtakiwa wamepatikana na shtaka hilo la kupanga kuua na kufanya mauaji."Walipanga makusudi kumuua Mugisa, hivyo mahakama inawahukumu kunyongwa hadi kufa ili iwe fundisho kwa watu wengine.



   Jaji huyu aliiambia mahakama hiyo kwamba; "Kutokana na kukithiri kwa vitendo vya watu kushambuliana kwa mapanga bila sababu na kujichukulia sheria mkononi natoa adhabu hii ili iwe fundisho kwa watu wa aina hiyo."  Awali, mwanasheria wa Serikali, Iddforce Makandara, aliiambia mahakama hiyo kuwa watuhumiwa hao wote kwa pamoja walimuua, Mugisa kwa kumpiga kitu kizito kichwani na kisha kumshambulia kwa mapanga hadi kufa.Aliiambia mahakama hiyo kuwa mwaka 2005 watuhumiwa hao walikula njama za kumuua Mugisa ambaye ni mume wake na Catherine John.  Alidai kuwa walifanya hivyo ili mjane wa marehemu aolewe na Makomelo, huku Lutonja akilipwa sh. 20,000 ili amsaidie kufanikisha mauaji hayo.Makandara aliomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa washtakiwa hao ili iwe fundisho kwa watu wanaojichukulia sheria mkononi


`BABU WA KIKOMBE LOLIONDO AIBUKA



 Na Mwandishi Wetu




Mchungaji Ambilikile Mwaisapila (Babu wa Kikombe) wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonesha kuwa Tanzania itakuwa kioo cha Afrika na dunia kwa ujumla.Alitoa kauli hiyo juzi mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia akiwa njiani kurejea mjini Arusha.Mchungaji Mstaafu Mwaisapila alisema kuna mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye Biblia, lakini hayakutokea Israeli na sasa yatafanyika hapa Samunge.“Mungu ametupenda sana, yanakuja mambo makubwa na wala hayako mbali. Kama mimi ni mzee na nitayaona, kwa hiyo mtarajie kuwa hayako mbali kutokea,” alisema huku akishangiliwa na wananchi.Alisema katika mafunuo aliyopewa na Mungu ameoneshwa kwamba watu wengi zaidi watafurika kijijini Samunge kuliko ilivyokuwa hapo awali. Alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kwa misaada iliyotoa wakati wa kugawa kikombe ikiwemo mahema, maji na ulinzi.


Waziri Mkuu, Pinda ambaye yuko mkoani Arusha kwa ziara maalum ya kusikiliza matatizo na migogoro ya ardhi yanayowakabili wakazi wa wilaya ya Ngorongoro, katika tarafa za Ngorongoro, Loliondo na Sale alisema anakubaliana na utabiri wa Mch. Mwaisapila kwani Tanzania imejaliwa gesi nyingi na mafuta mengi ambavyo vitabadili sura ya Taifa hili."Mungu ametupa gesi nyingi sana, katika miaka miwili tutakuwa na umeme kila mahali. Tuna makaa ya mawe ambayo ni nishati kubwa na sasa tuna fursa ya kupata nishati ya umeme kutoka ardhini (Geo-thermal) katika Ziwa Natron," alisema.Alisema Tanzania imekuwa kimbilio la kila mwekezaji na sababu kubwa ni amani na utulivu uliopo nchini. Aliwaeleza wakazi wa Samunge kwamba mapema mwakani mkandarasi wa barabara atakuwa katika eneo lao kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya lami ambapo awamu ya kwanza itaanzia Wasso hadi Mto wa Mbu kupitia Samunge.


  Akitoa ombi maalum kwa niaba ya vijana mbele ya Waziri Mkuu, Elias Kalumbwa, alisema wanaomba kuchimbiwa bwawa ili waweze kujiajiri kupitia kilimo cha mboga na matunda.Kalumbwa ambaye amesomea masuala ya wanyamapori alisema eneo la kuchimba bwawa lipo katika mto wa msimu unaopita kijijini hapo.  Naye MarthaSereri (70) alimweleza Waziri Mkuu kwamba wanaomba jimbo la Ngorongoro ligawanywe kwa sababu ni kubwa sana kiasi kwamba inamuwia vigumu mbunge wao kufika maeneo yote. Aliomba pia wapatiwe walimu wa sayansi na hisabati kwa ajili ya shule 10 za sekondari zilizopo kwenye tarafa yao.  Aliomba wapatiwe mikopo ya matreka ili waweze kuongeza ukubwa wa mashamba yao. “Tunaomba mikopo ya matrekta na plau, haya mashamba umeyaona njiani yamelimwa na Wakenya. Ukikodisha trekta kila ekari unatozwa sh. 100,000/-. Je tutafika wapi? Mkitukopesha matrekta mtakuwa mmetusaidia zaidi,” alisema.


  Akijibu hoja hizo, Waziri Mkuu alisema hoja zao ni za msingi na kwamba suala la vijana kupatiwa bwawa ni jambo linalowezekana kupitia mipango ya maendeleo ya kilimo ya wilaya (DADPS)."Andaeni andiko lenu, inabidi litoke kwa wananchi na si Serikalini. Mkituletea ni jambo linalowezekana kwani liko ndani ya mipango ya wilaya," alisema.  Akijibu hoja kuhusu ukubwa wa jimbo, Waziri Mkuu aliwaambia wakazi hao kwamba inawezekana kuongeza jimbo isiwe suluhisho la matatizo yao kwa sababu ya jiografia ya eneo lao."Kuongeza jimbo inaweza isiwe jibu la kila kitu kwani matatizo mnayopata yanatokana na jiografia ya eneo lenu, kutoka Ngorongoro, Loliondo hadi huku Sale.Mimi nadhani tuangalie pia uwezekano wa kuwapa Halmashauri ili kusogeza huduma kwa wananchi. Tutaangalia njia zote mbili na kuona ipi italeta majibu ya haraka kwenu," alisema.


WATANZANIA WATAKIWA KUWEKEZA ANJOUAN


  Na Mwandishi Wetu

Watanzania wametakiwa kuchangamkia fursa za uwekezaji zinazopatikana katika kisiwa cha Anjouan nchini Comoro ili kukuza na kuendeleza ushirikiano uliopo kwa maslahi ya kijamii na kiuchumi kati ya pande hizo mbili. Gavana wa Anjouan, Anissi Chamsidine,al ielezah ayoalipotembel eaKituo cha Uwe kezaji Ta nz ania(TIC) janajijini Dar es Salaam."Tuna fursa nyingi za uwekezaji katika kisiwa cha Anjouan na tunaamini Watanzania wako katika nafasi nzuri ya kuzitumia," alisema na kuongeza kuwa ushirikiano kati ya pande hizo mbili ni wadamu na wa kihistoria.

   Alisema kuna umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika eneo la uwekezaji na kutaja maeneo ambayo yan ahitaji uwekezaji kuwa ni elimu,utalii,nishati na katika sekta ya afya."Tuna hospitali kubwa zinajengwa lakini tatizo ni kukosekana kwa wataalamu wa afya ikiwemo wauguzi na madaktari hivyo tunaomba Watanzania waje kutusaidia katika eneo hilo," alisema.

   Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Juliet Kairuki amesema kuwa ujio wa Gavana huyo na ujumbe wa wawekezaji utasaidia kufungua fursa za uwekezaji na ushirikiano mzuri kiuchumi kati ya nchi hizo.  "TIC na Serikali inathamini ziara ya Gavana na ujumbe wake, uhusiano wetu ni wa siku nyingi na tungependa kuimarisha," alisema na kuongeza kuwa ziara hiyo itasaidia kuvutia uwekezaji kutoka katika kisiwa hicho.

WATANZANIA WATAKIWA KUWEKEZA ANJOUAN

  Na Mwandishi Wetu  


Watanzania wametakiwa kuchangamkia fursa za uwekezaji zinazopatikana katika kisiwa cha Anjouan nchini Comoro ili kukuza na kuendeleza ushirikiano uliopo kwa maslahi ya kijamii na kiuchumi kati ya pande hizo mbili.


   Gavana wa Anjouan, Anissi Chamsidine,al ielezah ayoalipotembel eaKituo cha Uwe kezaji Ta nz ania(TIC) janajijini Dar es Salaam."Tuna fursa nyingi za uwekezaji katika kisiwa cha Anjouan na tunaamini Watanzania wako katika nafasi nzuri ya kuzitumia," alisema na kuongeza kuwa ushirikiano kati ya pande hizo mbili ni wadamu na wa kihistoria.  

 Alisema kuna umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika eneo la uwekezaji na kutaja maeneo ambayo yan ahitaji uwekezaji kuwa ni elimu,utalii,nishati na katika sekta ya afya."Tuna hospitali kubwa zinajengwa lakini tatizo ni kukosekana kwa wataalamu wa afya ikiwemo wauguzi na madaktari hivyo tunaomba Watanzania waje kutusaidia 

katika eneo hilo," alisema.   Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Juliet Kairuki amesema kuwa ujio wa Gavana huyo na ujumbe wa wawekezaji utasaidia kufungua fursa za uwekezaji na ushirikiano mzuri kiuchumi kati ya nchi hizo.  "TIC na Serikali inathamini ziara ya Gavana na ujumbe wake, uhusiano wetu ni wa siku nyingi na tungependa kuimarisha," alisema na kuongeza kuwa ziara hiyo itasaidia kuvutia uwekezaji kutoka katika kisiwa hicho.

BALOZI WA HISPANIA KUWASHAWISHI WAFANYABIASHARA KUWEKEZA NCHINI


Na Gladness Mboma



 
Balozi wa Hispania nchini,Bw.Luis Cuesta amesema kuwa atawashawishi wafanyabias hara wa nchini mwake kuja kushirikiana na Watanzania kuwekeza katika sekta mbalimbali kwa kuwa ina fursa nyingi za kiuchumi.  Bw.Cuesta aliyasema hayo juzi wakati alipomtembelea Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya IPP, Bw.Reginald Mengi,ambapo alisema Tanzania ikitumia vizuri fursa mbalimbali z ilizopo wana nafasi kubwa ya kupiga hatua za kiuchumi.


  Alitaja fursa zilizopo nchini ni sekta ya gesi,utalii, mafuta na bahari na kusisitiza kwamba ikiwa maeneo hayo yataendelezwa yanaweza kusaidia nchi kupiga hatua kubwa.“Hispania ina watu wapatao milioni 43 ambayo inakaribiana idadi ya Watanzania, lakini sisi tumeweza kupiga hatua katika uchumi kutokana na kujikita katika sekta za nishati na utalii,”alisema.


Alisema kuwa Tanzania ina mazingira mazuri ya kibiashara ikiwemo amani,hali ya hewa, rasilimali, upatikanaji wa gesi na fursa nzuri ambayo inaweza kuwanufaisha Watanzania wote.Naye Dkt . Mengi alisema mazingira mazuri ya uwekezaji yatafanikiwa iwapo wawekezaji kutoka Hispania watakaokuja nchini wataungana na Watanzania katika ushirikiano.

“Kamakutakuw anaushirikiano wa dhatika tika sektambalimbali kati ya wawe kezaji wanjenaWatanz anianc hiinaweza kupigahat uaku bwa zakiuchumi.Dkt.Mengi alisema kuwa kunahaj a yaWatanzania kujifu nzamazu ri kutoka kwaHispaniahusu sanna mnailivyopiga hatuakati kasekta ya nishati na utalii. 

MFUMO WA ELIMU UBORESHWE NCHINI'



 Na Allan Ntana, Tabora

Serikali  kupitia watendaji wake imeshauriwa kuboresha mfumo wa utoaji elimu hapa nchini ili elimu hiyo iweze kumpa msingi mzuri na mwanga utakaomsaidia mwanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yake.Sambamba na hatua za kumuwezesha kufanya vizuri katika kujiendeleza kielimu.

Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na Askofu Mkuu wa Kanisa la FPCT hapa nchini, Mchungaji David Batenzi katika sherehe za mahafali ya 23 ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Umoja iliyoko wilayani Igunga mkoani Tabora.Sherehe iliyoambatana na maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa shule hiyo inayomilikwa na kanisa hilo.Alisema, serikali inaweza kupitia upya mfumo wake wa elimu na ikiwezekana ikaufanyia marekebisho kwa lengo la kuboresha mtaala unaotumika kwa sasa ili mfumo huo uweze kumsaidia mwanafunzi kupata msingi mzuri kielimu." Hatujisik i vizuri tunapoona matokeo mabaya kwa wanafunzi wetu hasa yanaposababishwa na dosari kadhaa za kimfumo kutokana na kubadilishwa mara kwa mara pasipo kufanya utafiti, katika hili viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia elimu hiyo hapa nchini wanapaswa kulaumiwa, mfano matokeo ya kidato cha nne mwaka jana hali ilikuwa tete," alisema askofu

VODACOM YAIPIGA 'JEKI' WIZARA YA MICHEZO

.Ibrahim Mussa na Theophan Ng'itu

 
Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, imekabidhi vifaa vya michezo kwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamduni na Michezo vyenye thamani ya sh.milioni 11,000,000 jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Kelvin Twissa alisema Vodacom ina furaha kushiriki katika mpango unaolenga kutambua na kuendeleza vipaji vya michezo kwa ngazi ya shule nchini. "tunahitimisha ahadi tuliyoitoa kwako, kwamba tutakuunga mkono katika kufanikisha jambo hili pia Vodacom, tunatambua juhudi kubwa zinazofanywa na serikali kupitia wizara yako, hivyo nasi tunajisikia furaha kuwa sehemu ya mikakati ya serikali," alisema Twissa.

Aliongeza kuwa Vodacom, inatambua kuwa michezo ni sehemu ya kuzalisha ajira na kwa sababu hiyo hawaoni ugumu wa kuwekeza kwenye michezo, ili kutengeneza fursa za ajira kwa vijana wa kitanzania. Vodacom ilikabidhi jezi seti 12, mipira 40 na kombe moja kwa Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Fenella Mukangara pia watatoa posho kwa ajili ya waamuzi na wasimamizi watakaoendesha mashindano hayo.

Naye Waziri Mukangara aliishukuru kampuni hiyo kwa kujitolea kushiriki katika kudhamini michezo mbalimbali nchini ikiwemo Ligi Kuu ya Tanzania Bara. " Vifaa hivi ambavyo tumevipokea leo(jana) , tutavitumia katika mashindano ya soka yatakayoshirikisha timu 12 kutoka shule za sekondari za Manispaa zote tatu za Mkoa wa Dar es Salaam, Temeke, Ilala na Kinondoni," alisema. Aliongeza kuwa wamechukua Mkoa wa Dar es Salaam kama mahali pa kuanzia, lakini wizara ingependa mpango huo uendelee katika mikoa yote Tanzania Bara.

MTIBWA SUGAR: SARE SASA BASI

 Na Fatuma Rashid 


 Timu ya Mtibwa Sugar imedhamiria kuondoa mdudu wa sare anayeiandama timu hiyo mara kwa mara.Akizungumza kwa simu akiwa Morogoro Katibu Mkuu wa timu hiyo, Salum Kijazi alisema hivi sasa wanajipanga ili waweze kufanya vizuri katika mechi dhidi ya Ashanti United.

   Kijazi alisema katika mechi, lazima kunakuwa na upungufu mbalimbali ambao husababisha wapinzani kutumia kama faida, hivyo timu yake inaendelea kurekebisha makosa yaliyojitokeza."Unajua katika kila mechi kuna upungufu wake na mpinzani wako hutumia kama faida, ila kwa kipindi hiki timu imejipanga vizuri na imefuta makosa yote ambayo kama tusingeyarekebisha tungekuwa katika nafasi mbaya," alisema.  Alisema msimu huu kila timu ipo vizuri, hivyo inasababisha kila mechi wawe wanajiandaa vizuri na kutumia kila mbinu katika mechi."Katika mpira unapoingia uwanjani hautakiwi kukurupuka, 

wachezaji wanatakiwa kujipanga na kujua ni mbinu gani wanazotumia timu pinzani, ili waweze kupambana nao, hivyo vijana wanajipanga ipasavyo kwani ligi inazidi kupamba moto kutokana na kila timu kujiandaa vizuri," alisema.  Akizungumzia waamuzi wanaochezesha Ligi Kuu msimu huu, Kijazi alisema katika mechi iliyopita dhidi ya Prisons mwamuzi alikuwa akifanya makosa hivyo walichukulia kama makosa ya kawaida."Waamuzi wote wanachezesha vizuri, ila kuna makosa y a k i b i n a d amu amb a y o huwa yanatokea kwani huyo anayechezesha ni binadamu pia hivyo kuna haja ya kukaa na kuongea naye," alisema.   Alisema katika mechi dhidi ya Ashanti wamejipanga kufanya vizuri, licha ya kuwa na majeruhi ambao ni Mussa Hassan 'Mgosi' na Masudi Ally, walioumia wakati wa mazoezi lakini wanaamini katika mechi hiyo wataweza kucheza kutokana na hali zao kuwa nzuri.

MANJI AWATULIZA WACHEZAJI YANGA


 Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amewatuliza wachezaji wa timu hiyo na kuwataka wakaze buti katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zinazokuja  Manji aliwatuliza wachezaji hao juzi alipokutana nao katika hoteli ya Serena, Dar es Salaam kwa ajili ya kula chakula cha usiku pamoja na viongozi wengine wa Yanga.Katika mechi za ligi hiyo, ambazo Jumamosi itafikia mzunguko wake wa sita, Yanga ina pointi sita ikiwa imeachwa na watani wao wa jadi Simba yenye pointi 11 kileleni.

Manji aliwataka wachezaji hao, wasimlaumu mtu kwa matokeo waliyoyapata na badala yake kuelekeza nguvu katika mechi zilizobaki.Akizungumzia suala la baadhi ya wachezaji kudai fedha za usajili, Manji alisema tatizo hilo litashughulikiwa haraka iwezekanavyo ili kila mmoja apate chake.   Katika hatua nyingine, mchezaji aliyesajiliwa kutoka Simba Mrisho Ngassa ametakiwa kulipa deni la faini sh.milioni 45 kwa Simba kwa kosa la kusaini katika timu mbili. Habari kutoka ndani ya Yanga, zimeeleza kuwa mchezaji huyo anatakiwa kulipa fedha hizo kwa kuwa tayari walishamalizana na kama klabu ikilipa atalazimika kuongeza mkataba wa kuichezea timu hiyo miaka mitatu. 

  Chanzo hicho kimeeleza kwamba Yanga inamtaka Ngassa, kulipa fedha hizo kwa kuwa hazikuisaidia klabu bali zilimfaidisha yeye binafsi.
Ngassa alipotafutwa jana kuzungumzia suala hilo simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita bila kupokelewa.

UGAIDI KENYA : NGOMA NZITO


  • ESHI LASISITIZA HAKUNA KURUDI NYUMA HADI MWISHO

  • MAGAIDI SITA WAUAWA,10 WAKAMATWA AIRPORT
NAIROBI, Kenya
  Hali si shwari, unaweza kusema hivyo kutokana na mapambano yanayoendelea ndani ya Jengo la Westgate, nchini Kenya, kati ya majeshi ya Serikali nchini humo na magaidi wenye silaha tangu Septemba 21 mwaka huu .  Jengo hilo lilivamiwa na wapiganaji wa Al Shabaab ambao wanadaiwa kufikia 10 hadi 15, kusababisha mauaji ya watu 62, wengine 175 kujeruhiwa na kuwateka baadhi ya watu ambao hadi sasa wanawashikilia ndani ya jengo hilo.  
Taarifa iliyotolewa na Kituo cha Televisheni cha Citizen nchini humo, kilisema magaidi sita wameuawa katika mapambano hayo na wengine waliobaki ndani ya jengo hilo, wanaweza kujisalimisha baada ya kuwazidi nguvu.  Kituo hicho kimeongeza kuwa, wanajeshi watatu wa Kenya kati ya 11 waliojeruhiwa katika mashambulizi yanayoendelea ndani ya jengo hilo, wamefariki dunia na kubaki wanane.Mkuu wa Majeshi nchini humo, Jenerali Julius Karangi, alisema katika mapambano hayo hakuna kurudi nyuma hadi magaidi hao wajisalimishe wenyewe.
Raia wa nchi nyingine wahusishwa
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje nchini Kenya, Bi. Amina Mohamed, amesema mwanamke mmoja raia wa Uingereza anadhaniwa kuhusika na tulio hilo.Bi. Mohamed alisema, mbali ya mwanamke huyo pia kuna raia wawili au watatu Wamarekani ambao inasemekana ni miongoni mwa magaidi hao wa mtandao wa Al Shabaab.   Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), lilisema raia sita wa Uingereza wamethibitishwa kufa katika shambulio hilo.Ofisi inayohusika na Mambo ya Nje nchini Uingereza, ilisema ndugu wa karibu wa raia hao ambao wamepoteza maisha katika shambulio hilo, tayari wamepewa taarifa.
  Pia ofisi hiyo ilifafanua kuwa, haina taarifa zozote juu ya raia wao kuhusika na shambulio hilo, lakini bado wanaendelea kushirikiana na mamlaka za Kenya ili kuwasaidia katika uchunguzi kutokana na shambulio hilo la kinyama.   Akizungumza na waandishi wa habari nchini Pakistan, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uingereza, Theresa May, alisema "Nimepata taarifa kuwa mwanamke raia wa Uingereza amehusishwa na tukio hili."Tutathibitisha taarifa hizi kama uchunguzi utakamilika, si rahisi kukubali au kukanusha kwa sasa," alisema May. 
Jeshi la Kenya
   Hadi jana mchana, Jeshi la Kenya lilikuwa katika hatua za mwisho kukamilisha msako wa kulikomboa jengo hilo mikononi mwa magaidi.Shirika la Habari nchini Ufaransa (AFP), lilisema majeshi ya Kenya yalikuwa yakikabiliana na upinzani mkali kutoka kwa magaidi wawili walioosalia ndani ya jengo hilo kila mmoja akiwa amejificha eneo lake.    Milio ya risasi na milipuko ilisikika jana asubuhi katika jengo hilo, lakini Serikali ya Kenya, haijatoa idadi kamili ya mateka waliookolewa katika shambulio hilo.Kwa mujibu wa Kituo cha Televisheni cha K24 nchini Kenya, jana kilitangaza majina sita ambayo ni miongoni mwa magaidi wanaodaiwa kuhusika na shambulizi hilo. 
   Washukiwa hao ni Sayd Nuh (25), anayetoka Kismayu, Isamil Galed (23), Finland, Mustafa Noordiin (24) na Abdifatah Osman (24) wote raia wa Marekani, Kassim Musa (22), Garissa na Mohammed Badr (24), ambaye ni raia wa Syria.
Al Shabaab ni nani?
   Jina Al-Shabab linamaanisha kijana kwa lugha ya Kiarabu. Kundi hilo liliibuka kama tawi la vijana la muungano wa mahakama za Kiislamu ambao baadaye ulivunjika mwaka 2006 baada ya kupigana na wanajeshi wa Ethiopia waliokuwa wameingia nchini Somalia kuyaunga mkono majeshi ya Serikali. Kundi hilo limeweka sheria kali za Kiislamu katika maeneo wanayoyadhibiti ikiwemo ya kupigwa mawe hadi kufa wanawake wanaodaiwa kufanya uasherati na kuwakata wezi mikono.Ingawa kundi hilo limepoteza udhibiti katika baadhi ya miji mikubwa nchini Somalia, liliondoka Mji Mkuu Mogadishu Agosti 2011 na Mji wa Kismayo Septemba mwaka 2012.
    Kismayo ulikuwa mji muhimu wa kundi hilo na uliwawezesha kufikiwa na bidhaa pamoja na kuwatoza watu ushuru kwa shughuli zao.Kundi hilo lilianza kufanya mashambulizi ya kuvizia baada ya kushindwa na Majeshi ya Muungano wa Afrika wanaotumia nguvu dhidi yao ambapo Kenya ilianza harakati za kulimaliza kundi hilo mwaaka 2011 Kenyailiwatuhumu wapiganaji wa Al Shabaab kwa kuwateka nyara wanajeshi wake pamoja na watalii.
Nani kiongozi wa Al-Shabaab?
   Ahmed Abdi Godane ndiye kiongozi wa kundi hilo ambaye anajulikana kama Mukhtar Abu Zubair, akitokea katika Jimbo la Somaliland. Kumekuwa na taarifa za mgawanyiko katika kundi hilo, ambazo hata hivyo, zinapingwa vikali na kundi lenyewe.    Kiongozi wa kundi hilo Godane huwa haonekani hadharani, ambapo mtangulizi wake, Moalim Aden Hashi Ayro, aliuawa katika shambulizi lililofanywa na Marekani mwaka 2008.Al Shabaab walijiunga na al Qaeda, Februari mwaka 2012, ambapo kiongozi wa Al Shabaab (Godane), aliahidi kumuunga mkono kingozi wa al Qaeda, Ayman al-Zawahiri. Makundi hayo mawili yamekuwa yakifanya kazi kwa pamoja na baadhi ya raia wa kigeni wamekuwa wakiweaunga mkono na kuwasaidia katika harakati zao za mapigano 



MAAJABU YA MAITI DAR,, YAKUTWA NA DAWA ZA KULEVYA PIPI 33


  •  Na Frank Monyo


   Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewashikilia watu wawili wakazi wa Tabata, kwa tuhuma za kukutwa na maiti ambayo tumboni ilikuwa na dawa za kulevya aina ya heroine.Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema maiti hiyo ilikuwa na dawa hizo pipi 33 na kuwataja watuhumiwa kuwa ni Nasri Omari 'Roboti' (36) na Mwanaisha Salim (36), wote wakazi wa Kigogo Luhanga, wakiwa na mwili wa marehemu Rajabu Kadunda. "Tulipata taarifa kuwa kuna mtu amefariki ghafla muda mfupi baada ya kutoka bafuni kuoga... tulikwenda eneo la tukio nyumbani kwa Omari na kuhoji hatimaye tuligundua uwepo wa maiti sebuleni ikiwa imelazwa chali katika godoro sakafuni. 


"Omari ambaye ndiye mmiliki wa chumba kilichokutwa maiti, alisema marehemu ambaye kwa jina lingine anafahamika kama Mashaka Mabruki (43) ni mfanyabiashara," alisema.



   Aliongeza kuwa, uchunguzi unaonesha kuwa marehemu alifika Dar es Salaam akitokea mkoani Mtwara Septemba 21 mwaka huu, kwa maelezo kuwa ni mgonjwa na alikwenda kuchukuliwa na watuhumiwa hao ambapo muda mfupi kabla ya kifo chake, alikwenda bafuni kuoga na hatimaye kufariki dunia.



   Kamishna Kova aliongeza kuwa, mazingira ya kifo hicho yalisababisha polisi kufika eneo la tukio, kuchukua maiti na kuipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi. "Uchunguzi uliofanywa na jopo la madaktari wawili pamoja na Maofisa wa Juu wa Polisi na ndugu wa karibu wa marehemu, zilikutwa pipi 33 za dawa za kulevya tumboni kwake.



"Pia marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambazo hazikuonesha anasafiri kwenda nchi gani hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kubaini mtandao mzima wa usafirishaji dawa hizi uliomhusisha marehemu," alisema.



     Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).



      Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa mtuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili "Tulipata taarifa kuwa kuna mtu amefariki ghafla muda mfupi baada ya kutoka bafuni kuoga... tulikwenda eneo la tukio nyumbani kwa Omari na kuhoji hatimaye tuligundua uwepo wa maiti sebuleni ikiwa imelazwa chali katika godoro sakafuni."Omari ambaye ndiye mmiliki wa chumba kilichokutwa maiti, alisema marehemu ambaye kwa jina lingine anafahamika kama Mashaka Mabruki (43) ni mfanyabiashara," alisema.

   Aliongeza kuwa, uchunguzi unaonesha kuwa marehemu alifika Dar es Salaam akitokea mkoani Mtwara Septemba 21 mwaka huu, kwa maelezo kuwa ni mgonjwa na alikwenda kuchukuliwa na watuhumiwa hao ambapo muda mfupi kabla ya kifo chake, alikwenda bafuni kuoga na hatimaye kufariki dunia.

   Kamishna Kova aliongeza kuwa, mazingira ya kifo hicho yalisababisha polisi kufika eneo la tukio, kuchukua maiti na kuipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi. "Uchunguzi uliofanywa na jopo la madaktari wawili pamoja na Maofisa wa Juu wa Polisi na ndugu wa karibu wa marehemu, zilikutwa pipi 33 za dawa za kulevya tumboni kwake.

"Pia marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambazo hazikuonesha anasafiri kwenda nchi gani hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kubaini mtandao mzima wa usafirishaji dawa hizi uliomhusisha marehemu," alisema.

     Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).

      Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa  tuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili "Omari ambaye ndiye mmiliki wa chumba kilichokutwa maiti, alisema marehemu ambaye kwa jina lingine anafahamika kama Mashaka Mabruki (43) ni  mfanyabiashara," alisema.

   Aliongeza kuwa, uchunguzi unaonesha kuwa marehemu alifika Dar es Salaam akitokea mkoani Mtwara Septemba 21 mwaka huu, kwa maelezo kuwa ni mgonjwa na alikwenda kuchukuliwa na watuhumiwa hao ambapo muda mfupi kabla ya kifo chake, alikwenda bafuni kuoga na hatimaye kufariki dunia.    Kamishna Kova aliongeza kuwa, mazingira ya kifo hicho yalisababisha polisi kufika eneo la tukio, kuchukua maiti na kuipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi. "Uchunguzi uliofanywa na jopo la madaktari wawili pamoja na Maofisa wa Juu wa Polisi na ndugu wa karibu wa marehemu, zilikutwa pipi 33 za dawa za kulevya tumboni kwake.

"Pia marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambazo hazikuonesha anasafiri kwenda nchi gani hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kubaini mtandao mzima wa usafirishaji dawa hizi uliomhusisha marehemu," alisema.  Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).

      Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa  tuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili    Aliongeza kuwa, uchunguzi unaonesha kuwa marehemu alifika Dar es Salaam akitokea mkoani Mtwara Septemba 21 mwaka huu, kwa maelezo kuwa ni mgonjwa na alikwenda kuchukuliwa na watuhumiwa hao ambapo muda mfupi kabla ya kifo chake, alikwenda bafuni kuoga na hatimaye kufariki dunia.    Kamishna Kova aliongeza kuwa, mazingira ya kifo hicho yalisababisha polisi kufika eneo la tukio, kuchukua maiti na kuipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi. "Uchunguzi uliofanywa na jopo la madaktari wawili pamoja na Maofisa wa Juu wa Polisi na ndugu wa karibu wa marehemu, zilikutwa pipi 33 za dawa za kulevya tumboni kwake.

"Pia marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambazo hazikuonesha anasafiri kwenda nchi gani hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kubaini mtandao mzima wa usafirishaji dawa hizi uliomhusisha marehemu," alisema.       Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).

      Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa  tuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili    Kamishna Kova aliongeza kuwa, mazingira ya kifo hicho  yalisababisha polisi kufika eneo la tukio, kuchukua maiti na kuipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi. "Uchunguzi uliofanywa na jopo la madaktari wawili pamoja na Maofisa wa Juu wa Polisi na ndugu wa karibu wa marehemu, zilikutwa pipi 33 za dawa za kulevya tumboni kwake. "Pia marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambazo hazikuonesha anasafiri kwenda nchi gani hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kubaini mtandao mzima wa usafirishaji dawa hizi uliomhusisha marehemu," alisema.

     Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).       Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa mtuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili "Pia marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambazo hazikuonesha anasafiri kwenda nchi gani hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kubaini mtandao mzima wa usafirishaji dawa hizi uliomhusisha marehemu," alisema.

     Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).   Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa mtuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili

     Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).  Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa mtuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili

      Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa  tuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili