TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, September 23, 2013

SHAMBULIO LAUA WATU 22 NCHINI KENYA Posted: 22 Sep 2013 11:05 PM PDT



 NAIROBI, Kenya
  Watu 22 wanahofiwa kufariki baada ya watu wenye silaha kufyatua risasi mjini Nairobi, Kenya, kwenye eneo la maduka katika mtaa wa Westlands.Walioshuhudia tukio hilo, wanasema kuwa maguruneti pia yalitumika katika shambulio hilo.

  Kwa mujibu wa Mwandishi wa BBC mjini Nairobi washambuliaji inaarifiwa walivaa vilemba kama vya al-Shabaab, lakini haikuthibitishwa kama wapiganaji hao wamehusika. Taarifa za awali za BBC zilieleza kuwa watu sita waliuawa kwenye shambulio hilo.

  Polisi waliokuwa na silaha walizingira jengo la maduka liitwalo Westgate, katika mtaa wa Westlands na kuna taarifa ya watu waliojeruhiwa walikuwa wakitolewa hapo kwa machela.Ilielezwa kuwa watu wengi walikuwa wamenasa ndani ya jengo.

  Magari yaliyoegeshwa nje ya maduka yaliharibika. Shirika la Habari la Reuters liliarifu kuwa mpiga picha mmoja aliona watu wamelala chini.Hadi sasa hakuna taarifa rasmi kama kuna watu waliokamatwa kwa kuhusishwa na tukio hilo

No comments:

Post a Comment