TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, September 26, 2013

WAKULIMA RUFIKI KUFAIDIKA NA MATREKTA KUTOKA KWA MWEKEZAJI.

Mratibu wa mradi wa kilimo cha miwa wa Kampuni ya Agro Foresty Plantation Ltd, Bw. Kiondo Mahanyu, akikabidhi funguo za Trekta kwa Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji cha Chumbi B, Wilayani Rufiji, Bw. Abdulrahiman Ngongwe, kusaidia wakulima wa kijiji hicho kwa gharama nafuu. Kulia ni Afisa kilimo, Bi. Rose Mbezi na Bi. Mwanaidi Singano
Mratibu wa mradi wa kilimo cha miwa wa Kampuni ya Agro Foresty Plantation Ltd, Bw. Kiondo Mahanyu, akikabidhi funguo za Trekta kwa Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji cha Chumbi B, Wilayani Rufiji, Bw. Abdulrahiman Ngongwe, kusaidia wakulima wa kijiji hicho kwa gharama nafuu. Kulia ni Afisa kilimo, Bi. Rose Mbezi na Bi. Mwanaidi Singano
Baadhi ya Matrekta ambayo wakulima hao watafaidika nayo
 WENYEVITI wa vijiji vya kata ya Chumbi Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani wamemuomba muwekezaji ambaye amepewa aridhi kwa ridha yao kuwekeza haraka katika mashamba ya miwa ili wananchi waanze kufaidi matunda ya uwekezaji.

Matunda wanayotarajia kufaidika nayo ni pamoja na ajira kwa vijana wao kwa vile ya kulimwa miwa muwekezaji atafugua kiwanda kikubwa cha sukari na kuwa mkombozi mkubwa kwa ajira katika kata hiyo hasa kwa vijana wengi wanaomaliza darasa la saba na kulanda mitaani bila ya shghuli ya kufanya.

Wakiongea juzi mbele ya mratibu wa mradi anaesimamia shughuli zote za Agro plantation wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani, Kiondo Mahanyu ,walisema ukimia wa kuanza mradi unawatia wasiwasi wakazi wa eneo hilo kutokana na maamuzi yao ya kutoa aridhi ili baadae waje wafaidi matunda.

Wakiongea kwa pamoja katika maongenzi yaliofanyika katika ofisi za serikali Chumbi, juzi ambako wenyeviti wote wa vijiji nane katika kata hiyo walikusanyika kwa lengo la kuchukua matrekta toka kwa muwekezaji kama sehemu ya kusaidiwa kulimiwa mashamba kupitia kaya ya vijiji.

Mwaka jana muwekezaji alitoa matrekta katika kila kijiji na kufanya baadhi ya kaya kuogeza nafaka maradufu pamoja na kuwepo kwa mvua zisozoridhisha. Pamoja na kutoa matrekta pia muwekezaji anatoa misaada ya kijamii katika vijiji hivyo kitu ambacho kimefanya wanavijiji wavutiwe zaidi na muwekezaji huyo.

Wenyeviti waliokuwepo katika makabidhiano ya matrekta juzi ni pamoja na kijiji cha Nyamwage, Ibrahimi Mboweto,Said Makangu mwenyekiti wa kijiji cha Muhoro Magharibi,Rashid kisomo, mwenyekiti wa Muhoro Mashariki,Ali Nguyu mwenyekiti wa Chumbi A.

Wengine ni pamoja na Abdalahamani Ngongwe kaimu mwenyekiti wa kijiji cha Chumbi B na mwenyekiti wa kijiji cha Chumbi C. Salum Mtimbuko, wwenyeviti wa vijiji vya Roma , Tawi,Roma na Muyuyu hawakuweza kufika kutokana na udhuru, lakini trekta zao zipo kwa ajili ya kuchukua na kukodisha wananchi katika vijiji hivyo.

Akiongea wakati wa kukabidhi matrekta kwa niaba ya muwekezaji,Mratibu wa kampuni Mahanyu,alisema sehemu kubwa ya uwekezaji katika kata hiyo ni kuakikisha wananchi wananufaika na mradi huyo ikiwemo ajira kwa vijana na kwenye taaluma mbalimbali za elimu.

Amesema kuchelewa kwa kuanza mradi kumetokana na mchakato wa kupimiwa aridhi kama unavyoelekezwa na Serikali na si Muwekezaji, hatahivyo amesema hatua iliofikiwa inaridhisha na wakatai wowote wanakijiji watatagaziwa kupatikana kwa hati rasmi ya umilikaji halali wa mashamba hayo.

"Nawataka wanavijiji watulie na kutafakari masuala ya mbele kutokana na mchakato kuelekea mwisho wa kufanikiwa kupata hati ili shughuli ziianze rasmi",alisema Mahanyu na kuongeza kuwa faida nyingine watakazopata wanakijiji hao ni pamoja na kushilikishwa katika kilimo cha miwa ambapo kila mwanakijiji atalima miwa na kuuzia kiwanda.

Faida zingine ni pamoja na kupewa ushauri toka kwa mabwanashamba watakaotoa elimu juu ya mashamba ya miwa na nafaka zingine zitakazolimwa katika kata hiyo.Tayari

Akiongea kwa niaba ya wenyeviti wezake nane wa vijiji hivyo katika kata hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa kijiji cha Chumbi A, Ali Nguyu,alisema kusuasua kwa mradi huo kumewatia wasiwasi wanavijiji wa maeneo hayo ambapo waliwakilisha suala hilo kwa Mkurungenzi wa Wilaya ambaye pia aliwasiliana na mwakilishi wa na kwa pamoja waliwekena sawa kwa ajili ya kuendelea na mradi huo.

Hatahivyo wenyeviti  walimtaka muwekezaji kupuguza ghrama za kulima kwa kutumia matrekta hayo ambapo wametaka heka moja kulimiwa kwa shilingi 35,000 badala ya 45,000/= kama ilivyokuwa mwaka jana ambapo kutokana na maombi hayo mwakilishi wa Kampuni ya Agro Forest plantation alikubali ombi hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani mama Mwantumu Mahiza alimpogeza muwekezaji huyo kwa kujitolea na kuwawezesha wakulima katika kata hiyo kulimiwa mashamba ili kuondoa hali ya njaa katika kata hiyo kutakokoenda sambamba na ukulima wa kisasa.

Akiongea kwa njia ya simu , Mahiza alisema muwekezaji huyo anatarajia kuleta mabadiliko makubwa ya kilimo na kiuchumi kwa jumla pindi atakapoaanza shughuli zake za kutayarisha mashamba ya miwa na hatimaye kufugua kiwanda cha sukari Wilayani humo.
Mwishoooo

No comments:

Post a Comment