TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, March 25, 2014

OPARASHENI TAFUTA TAFUTA NDEGE YA MALAYSIA MH370 YAFIKIA KIKOMO

Jamaa za abiria wa ndege hiyo wamekumbwa na majonzi makubwa.

Mamlaka ya usalama wa safari za baharini nchini Australia imesema kuwa operesheni ya kuitafuta ndege ya shirika la Malaysia iliyotoweka imesitishwa kutokana na hali mbaya ya hewa na mawimbi makali baharini.
Taarifa zinasema kuwa upepo mkali pamoja na mvua kubwa inayonyesha katika eneo hilo ina maana kuwa ndege hazitoweza kupaa kwa usalama. Mawimbi makali yameilazimisha meli ya jeshi la wanamaji wa Australia kuondoka katika eneo ambalo mabaki yanayodhaniwa kuwa ya ndege hiyo yalionekana hapo jana Jumatatu.

Dr Erik van Sebille, ambaye ni mtaalam wa maswala ya Baharini katika chuo kikuu cha New South Wales mjini Sydney, amefanya utafiti katika eneo hilo la kusini mwa Bahari Hindi kutambua ni wapi na vipi vifusi vinasafirishwa na mawimbi ya bahari. Anasema itakuwa vigumu sana kupata mabaki ya ndege hiyo.

Shughuli ya kuitafuta MH370 imesitishwa
" Ni eneo lisiloweza kukalika duniani, acha niseme. Upepo unaovuma ni mkali sana, mawimbi ni makubwa, ni mojawepo wa mawimbi makubwa zaidi baharini. Unapofika katika eneo hili la kusini, unaanza kuhisi athari za eneo la Antactica kwenye bahari. Hapa tunazungumzia dhoruba kali kali sana hususan wakati huu tunapoingia majira ya kupukutika," anasema Dr. Erik van Sebille.
Kadhalika amesema kuwa vifusi vilivyoenekana hapo jana tayari vimekwishaondolewa katika eneo hilo na mawimbi makali.
"Haitakuwa rahisi kabisa kupata kijisanduku cha kunasa habari. Mawimbi ya eneo hili ni makali na kwa hiyo vifusi ambavyo wametambua kwa sasa huenda vimehamishwa katika kipindi cha majuma mawili au matatu tangu ndege hiyo ianguka-na huenda vimesafiri kilomita alfu moja tayari. Na hii inaifanya vigumu kurejelea utafutaji kwa sababu bahari inabadilika sana hapa-ina vurugu ukipenda."
Hapo awali naibu waziri wa mashauri ya nchi za Kigeni wa China Xie Hangsheng, aliitaka serikali ya Malaysia kutoka ushahidi unaoelezea kuwa ndege hiyo ilianguka katika eneo la Kusini mwa bahari Hindi. Ndege hiyo ilitoweka kwenye mtambo wa Radar zaidi ya majuma mawili yaliyopita

RAIS UHURU KENYATTA NDANI YA TANZANIA JANA












Monday, March 24, 2014

Waziri mkuu wa Malaysia Najib Razak asema na jamaa na familia za abiria wa ndege iliyotoweka MH370 , kwamba hakuna manusura

 
Waziri mkuu wa Malaysia Najib Razak.
SHIRIKA la ndege la Malaysia limewaambia jamaa na familia za abiria waliokuwa wanasafiri kwa ndege iliyotoweka MH370 kwamba ndege hiyo imepotea na kwamba hakuna manusura. Tangazo hilo limetolewa kwa familia hizo kwa njia ya ujumbe wa simu ya mkononi , ambao BBC iliweza kuuona.

Ndege ya Malaysia MH320 ilitoweka ikiwa na abiria 239 baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur tarehe 8 mwezi huu.

Mpaka sasa AUTRALIA ilikuwa ikiendelea na udadisi picha za Satelite kusaka mabaki ya ndege hiyo ya Malaysia.  

pamoja na ua ushirika wa Nchi za Norway, New Zealand na Marekani katika kutafuta mabaki hayo, tangazo hilo limekuja huku juhudi za kutafuta mabaki ya ndege hiyo Kusini mwa Bara la Hindi zikimalizika kwa siku na siku bila mafaniko.

Waziri mkuu wa Malaysia amesema kuwa ndege hiyo ilianguka Kusini mwa Bahari Hindi, bila ya manusura wowote.

Aliambia waandishi wa bahari kuwa udadisi uliofanyiwa data ya Satelite kutoka Uingereza ndio umewathibitishia kwamba ndege hiyo ilimalizia safari yake Magharibi mwa mji wa Perth mbali na eneo lolote la kutua.

Ameomba vyombo vya habari kuheshimu familia za watu waliokuwa ndani ya ndenge hiyo, akisema kuwa anasikitishwa sana kwani kipindi chote walichosubiri taarifa njema , mwishowe imekuja kuwa taarifa mbaya hata zaidi.

Ndege ya Malaysia MH-370, ilipoteza mawasiliano wiki mbili zilizopita. Ndege na meli za nchi mbali mbali zimekuwa zikitafuta angalau mabaki ya ndege hiyo bila ya kupata chochote.BBC

KINANA ASIMAMA KIDETE KUHAKIKISHA CCM INAIBUKA KIDEDEA JIMBO LA CHALINZE


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi na wanaCCM wa Kata ya Ubena Zomozi huku akishangilia kwa shangwe,leo Machi 24,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete akimwaga sera zake kwa Wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi na wanaCCM wa Kata ya Ubena Zomozi huku akishangilia kwa shangwe,leo Machi 24,2014.
Wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi wakifatilia kwa makini sera za Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete huku wakiwa wamejikinga kwa mvua kwa kutumia viti,wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.
Wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi wakiwa wamejikinga kwa mvua chini ya paa la moja ya Nyumba zilizopo kwenye Kata hiyo wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.

SIKU YA 17 KUPOTEA NDEGE YA MALAYSIA: NDEGE YA MALAYSIA ILIRUKA CHINI YA FUTI 12,000.

Malaysia-Airlines-Boeing-B777-200-Flight-MH370

Naibu Waziri Mkuu wa Malaysia, Warren Truss, kulia, akizungumza na ofisa wa juu ya kikosi cha uokoaji na mratibu wa operesheni ya kuitafuta ndege iliyopotea, John Rice. Wataalamu wa Rada wakiwa wamepigwa picha ndani ya ndege ya Kijeshi ya New Zealand wakiwa katika msako wa chombo hicho kilichopotea Kusini mwa bahari ya Hindi.
Mmoja wa wanajeshi wa kikosi cha maji cha China akiwa ndani ya meli Snow Dragon, wakiendelea na msako wa ndege iliyopotea kusini mwa bahari ya Hindi.
Mike Barton, mkuu wa kikosi cha uakoaji, kushoto, akiangalia ramani ya Bahari ya Hindi akiwa na Alan Lloyd, ofisa wa kitengo cha uokoaji katika Jeshi la Majini la Australia.
Ndugu wa abiria waliokuwemo ndani ya ndege hiyo, raia wa China wakilia na wengine kupatwa na mshangao baada ya kuendelea kuripotiwa habari za kutojulikana ilipo ndege hiyo, wakati wakiongea na waandishi wa habari mjini Beijing.
Naibu Waziri Mkuu wa Australia Warren Truss akizungumza na waandishi wa habari juu ya maendeleo ya utafutwaji wa ndege iliyopotea. 

NDEGE ya abiria ya Malaysia iliyopotea kiutatanishi wiki mbili zilizopita, inadaiwa iliruka chini ya futi 12,000 kutoka usawa wa bahari kutokana na matatizo katika chumba cha rubani kabla ya kupotea katika rada, ripoti mpya zimeeleza. 

Wakati ndege hiyo Boeing 777-200 ikiwa bado inatafutwa katika bahari ya Hindi, habari zinasema chombo hicho kilibadili uelekeo ikiwa juu ya bahari ya Kusini ya China.

Mara ya mwisho ndege hiyo ilionekana katika rada ya jeshi la Malaysia saa 2.15 asubuhi kwa saa za nchi hiyo, Machi 7 mwaka huu, ikiwa katika kisiwa cha Penang kilicho kusini mashariki mwa taifa hilo, muda kama saa moja baada ya kuwa imeruka kutoka Kuala Lumpur kwenda Beijing nchini China.

Mapitio ya Rada yalionyesha ndege hiyo ikibadili mwelekeo baada ya kugeuka ghafla na kwa kasi upande wake wa kushoto kuelekea Malacca.

Ofisa mmoja aliyekataa kutajwa jina kwa vile siyo msemaji, aliiambia CNN kwamba kuruka chini ya futi 12,000 katika anga yenye ndege nyingi kama ilipokuwa ikipita kungeifanya ndege hiyo kutoonekana na ndege zingine.
CHANZO: DAILYMAILY

MWANAFUNZI MAKONGO AFARIKI KATIKA AJALI YA BAJAJ NA LORI JIJINI DAR ES SALAAM


Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Makongo, Priscus Mallya, baada ya kufariki katika ajali ya lori na Bajaj.
Mwili wa  Priscus Mallya ukiwa katikati ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi baada ya ajali.
Bajaji ambayo mwanafunzi alikuwa amepanda akielekea shuleni Makongo ikiwa eneo la ajali.

MWANAFUNZI wa kidato cha nne, Shule ya Sekondari Makongo, Priscus Mallya, amefariki dunia katika ajali iliyolihusisha lori na Bajaj katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi eneo la Bamaga, Dar.
Kwa mujibu wa watu waliokuwa eneo la tukio wakati ajali hiyo ikitokea, wamesema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ndani ya Bajaj pamoja na wenzake wawili wakielekea shuleni Makongo ambapo walikutana uso kwa uso na lori kisha kumrusha na kutokea upande wa pili marehemu.
(PICHA/STORI: ANDREW CARLOS, DENIS MTIMA/GPL)

TAZAMA SIMBA ILIVYOVUTWA SHARUBU UWANJA WA TAIFA NA COASTAL UNION!!

Wachezaji wa Simba wakiingia uwanjani wakati wa mchezo wao na Coastal Union ya Tanga.
Wachezaji wakisalimiana.
 Benchi la ufundi la Simba.
 Kikosi cha Coastal Union ya Tanga.
 Kikosi cha Simba.
 Mashabiki wa Simba wakishangilia timu yao.
Mashabiki wa Simba wakichagiza ushindi.
 Mshambuliaji wa Simba, Ramadhani Singano akimiliki mpira huku akizongwa na beki wa Coastal Union ya Tanga, Hamadi Juma katika mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Coastal ilishinda 1-0.

ASHABIKI SIMBA WATULIZWA JAZIBA, LOGA KUSUKA KIKOSI KAZI KUWAVAA AZAM , KAGERA SUGAR, ASHANTI, YANGA MECHI ZILIZOSALIA!!

Na Baraka Mpenja 

IMG_2166
KIPIGO cha bao 1-0 walichopokea Simba sc kutoka kwa Wagosi wa Kaya, Coastal Union ya Tanga  jana  uwanja wa Taifa  katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara kimezidi kuwavuruga  na kuwafanya wawe wanyonge  ngwe hii ya lala salama.
Wagosi wa Kaya wakiwa katika morali ya ushindi , waliandika bao la ushindi dakika ya 45 kipindi cha kwanza kupitia kwa mlinzi wake wa pembeni, Hamadi Juma kufuatia mabeki wa Simba kujikoroga.
Matokeo hayo yamepokewa kwa hisia tofauti na mashabiki wa klabu hiyo ambao wanaona kama ligi kuu inawaonea msimu huu.
Hata hivyo Uongozi wa Simba sc kupitia kwa Afisa habari wake, Asha Muhaji umewataka mashabiki na wanachama wao kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu kwao.
“Matokeo ya jana hatukuyatarajia hata kidogo. Tumeshitushwa mno na kipigo hicho. Lakini hayo ndio mambo ya uwanjani. Mpira umechezwa vizuri na tumepoteza. Hatuna budi kuukubali ukweli japo unauma”. Alisema Asha.
Mwamuzi vipi?: Kocha wa Simba sc, Dravko Logarusic (wa kwanza kulia) akiwa hailewi cha kufanya na kuonesha kuwa muda bado wakati mwamuzi anapuliza kipenga cha mwishoIMG_2041Shughuli ilikuwa pevu mno jana uwanja wa Taifa
Afisa habari huyo aliongeza kuwa kutokana na matokeo wanayozidi kuyapata, yanawapa watu cha kusema, lakini soka huwa lina tabia ya kupanda na kushuka.
“Siku za nyuma mashabiki wetu walikuwa wanatoka na furaha uwanjani. Kwa sasa mambo yamebadilika. Huo ndio Mpira, ukiupenda lazima uwe  na moyo wa kukubaliana na kile kinachotokeo”. Alisema Asha.
Asha alisisitiza kuwa bado wamebakiwa na mechi nne, hivyo mashabiki waendelee kuiunga mkono klabu yao ili iweze kufanya vizuri.

IDDI BONGE BAADA YA KUMPIGA MWAKASANGA SASA AMTAKA MCHUMIATUMBO!!

Bondia Amani Bariki ‘Manny chuga’ kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Selemani Moto wakati wa mpambano wao Many chuga alishinda kwa TKO ya raundi ya nne 

Bondia Kasimu Gamboo kulia akipambana na mohamed babeshi wakati wa mpambano wao Ganmboo alishinda kwa k,o ya raundi ya tatu ya mpambano huo.
REFARII OMARI YAZIDU AKIMWINUA MKONO JUU BONDIA KASSIMU GAMBOO

BONDIA aLi Bugingo kushoto akioneshabna umwamba wa kutupiana makonde na Hassani Mandula mandula alishinda kwa pointi
Bondia Fadhili Majia kulia akimtupia konde Juma Selemani wakati wa mpambano waio uliofanyika manzese majia alishinda kwa k,o ya raundi ya tatu
Bondia iddi bonge akiwa ulingoni
Refarii Pembe Ndava akiwapatia maelezo mabondia Idd Bonge na Bernard Mwakasanga kabla ya mpambano wao uliofanyika Manzese
 Bondia Iddi Bonge kushoto akimtwika Bernard Mwakasanga ngumi wakati wa mpambano wao uliofanyika manzese Dar es salaam Bonge alishinda kwa k,o ya raundi ya kwanza katika mpambanio huo.

Bondia Iddi Kipandu .Iddi Bonge’ mwishoni mwa wiki iliyopita alikata ngebe za Bernard Mwakasanga ‘Shoka ya Bucha; baada ya kumtwanga kwa K,O ya raundi ya kwanza katika mpambano wao wa uzito wa juu uliofanyika Manzese Dar es salaam

mpambano huo uliokuwa na mashabiki wengi wa kike na kiume ulivuta hisia za watu mbalimbali ambapo baadhi ya mashabiki walikuwa wakisema hapa K,O tu ata hivyo mashabiki wengi walikuwa upande wa Bonge ambao walikuja kumshangilia na ngoma pamoja na filimbi
Bonge alipiga ngumi ya kwanza na kumfanya ‘Shoka ya Bucha ‘ kwenda chini kama pakacha alipo hesabiwa na kusimama aijapita mda akapigwa ngumi nyingine na kudondoka kama mnazi hapo hapo refarii pembe ndava akakatiza mpambano na kumpatia ushindi bonge akimwacha mwakasanga anagalagala kwa ngumi nzito ngumi ya kushiba ya uzito wa juu
mara baada ya mpambano huo bondia Iddi Bonge alijigamba kwa sasa ana mpinzani ila anasikia tu jina la bondia Alphonce Mchumiatumbo ambapo amemtahadhalisha ole wake akutane na mikono ya mwanaume mchumiatumbo anacheza na wachovu ndio mana anawakaslisha mapema tu raundi ya kwanza na ya pili mimi nikikutana nae nitakuwa sina msalie mtume nae nitahakikisha namsambalatisha raundi za awari tu
 
katika mpambano huo uliosindikizwa na mabondia mbalimbali ambapo bondia Salum Kombe alimpiga kwa pointi Ally Jagalaga uku Amani Bariki ‘ Manny Chuga’ akimsambaratisha kwa TKO ya raundi ya nne Selemani Motto na Kassimu Gamboo akimpiga bila huruma bondia  Mohamed Babeshi kwa K,O ya raundi ya tatu na Ally Ramadhani akitoa droo na Ashrafu Selemani katika mpambano wea uzito wa juu bondia halidi manjee alishindwa kufurukuta kwa Shabani Mtengera baada ya kupigwa kwa point na Hassani Mandula alimtwanga Ally Bugingo kwa point wakati Fadhili Majia akimpiga bila huruma Juma Selemani kwa K,O ya raundi ya nne
 
Mchezo huo wa masumbwi uliokuwa ukisimamiwa na chama cha ngumi za kulipwa nchini PST chini ya Emanuel Mlundwa

WASHIRIKI 29 WA SHINDANO LA MAISHA PLUS 2014 WAINGIA RASMI KIJIJINI

Afisa mtendaji wa Kampuni ya DMB ambao ni wamiliki wa Maisha Plus Masoud Ally (Masoud kipanya) akiongea katka uzinduzi wa kijiji cha Maisha Plus, ambapo jana washiriki wapatao 29 waliingia kijijini kuanza kukabiliana na changamoto za kuweza kupata shilingi milioni 25 za kitanzania. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Wageni waalikwa waliofika kijijini cha Maisha Plus kuangalia uzinduzi… Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Washiriki wa shindano la Mshindi wa Maisha Plus wakipewa maelekezo machache mara baada ya kuwasili kijijini kwao. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Mmoja ya wawakilishi toka Oxfam ambao ni wadhamnini wa Maisha Plus 2014 akizungumza machache. Pembeni yake ni Afisa mtendaji wa Kampuni ya DMB ambao ni wamiliki wa Maisha Plus Masoud Ally (Masoud kipanya). Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog
Mkuu wa Kijiji… Mwite babu wa kaya akiwepo kuhakikisha wanakijiji wanakaribishwa kwa shangwe. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog
Wageni waalikwa. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog
Kazi ya kujenga nyumba za kuishi washirki wa maisha plus ikiendelea… ambapo washiriki hao walitakiwa kujenga nyumba zao za kuishi ndani ya masaa 48. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog
Kila mmoja anawajibika kuhakikisha kazi ya kujenga nyumba inafanikiwa. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Wadau kutoka Oxfam wakibadilisha mawazo mara baada ya kufika katika tukio la uzinduzi wa wawashiriki kuingia kijijini. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Safari ya kuelekea kijiji cha Maisha Plus imeanza rasmi… washiriki wakiwa wamebeba mabegi yao ambapo kila mmoja alibeba mzigo wake mwenyewe kwa kutembea kwa miguu umbali wa kilometa 1.5. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Safari ikiendelea huku washiriki wakiwa wameshachoka… wengine walitamani kughairi kuendelea na safari. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Wengine ilibidi wasaidiane kupeba mizigo. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Hakuna kuchoka, kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe… Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Wengine waliamua kulala ili waweze kunyoosha mgongo. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.