TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, March 23, 2014

Barcelona wapeleka vilio kwa mashabiki wa Real Madrid katika Uwanja wa Santiago Bernabéu, Madrid nchini Hispania.

BARCELONA VS REAL MADRID, IONEL MESSI APACHIKA 3 - NA CHRISTIANO RONALDO 1.

Lionel Messi (kushoto) akishangilia bao lake la tatu na wachezaji wenzake Gerard Pique (katikati) na Alexis Sanchez.

Karim Benzema akishangilia na wachezaji wenzake wa Madrid Angel Di Maria na Marcelo baada ya kufunga bao la pili.
Iniesta baada ya kufunga bao la kwanza akipongezwa na Jordi Alba (kushoto) na Dani Alves (katikati). Pembeni ni Neymar na Messi.
Pepe juu akishangilia pamoja na wenzake wa Madrid baada ya bao la tatu lililofungwa na Ronaldo.
Mashabiki wa Real Madrid na mabango yao.
Inakuwaje! Pepe akimshika tai Fabregas wakati wa mtanange huo. Pembeni ni Neymar.
Sergio Ramos akionyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Neymar.
MSHAMBULIAJI mahiri wa Barcelona, Lionel Messi, usiku huu
 amepeleka vilio kwa mashabiki na wapenzi wa Real Madrid 
baada ya kufunga 'hat-trick' wakati timu yake ikishinda 
bao 4-3 dhidi ya mahasimu wao Real Madrid.
Mechi hiyo kali ya La Liga imechezwa katika Uwanja wa 
Santiago Bernabéu, Madrid nchini Hispania.
Mshambuliaji huyo amefunga mabao mawili kwa penalti dakika 
ya 65 na 84 wakati lingine akilifunga dakika ya 42 baada 
ya Andres Iniesta kufunga mapema dakika ya 7. 
Mabao ya Madrid yamewekwa kimiani na Karim Benzema 
aliyetupia
 mawili dakika ya 20 na 24 la tatu likifungwa na Mchezaji 
Bora wa Dunia mwaka 2013/14, Cristiano Ronaldo kwa mkwaju 
wa penalti dakika ya 55

No comments:

Post a Comment