TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, March 24, 2014

PEAK PERFORMANCE INTERNATIONAL YATOA MAFUNZO YA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Training 1

Mkuu wa mafunzo kutoka Peak Performance International Tanzania Bi Claudine Muthama akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya utoaji bora wa huduma kwa wateja kwa wafanyakazi wa Quality Furniture Limited jana jijini Daressalaam katika hotel ya Accomondia.
Taking notes 1Baadhi ya wafanyakazi wa Quality Furniture Limited wakinuu maneno kutoka kwa mkuu wa mafunzo wa Peak Performance International Tanzania Bi Claudine Muthama ( hayupo pichani) jana katika hotel ya Accomondia jijini Daressalaam.Group photo2Wafanyakazi wa Quality Furniture limited wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mafunzo juu ya utoaji bora wa huduma kwa wateja jana katika Hoteli ya Accomondia. Mafunzo hayo yalitolea na kampuni ya Peak Performance International Tanzania yenye uzoefu wa karibu miaka kumi ya utoaji mafunzo mbalimbali kwa wafanyakazi na watu binafsi
……………………………………………………………..
Peak-Performance-Logo_0
Dar es Salaam, Wafanyakazi wa Quality Furniture Limited jana walipatiwa mafunzo juu ya utoaji bora wa huduma kwa wateja na kampuni ya Peak Performance International Tanzania, PPIT.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Accomondia  Hotel, mkuu wa mafunzo wa PPIT Bi Claudine Muthama alisema kuwa “ katika dunia ya sasa ya kibiashara ambapo ushindani ni suala la kila siku na wateja wana machaguo mengi ya bidhaa na huduma suala la huduma bora kwa wafanyakazi ni suala mtambuka.”
Aliendelea kusema maneno mazuri kwa mteja yanaweza kufanya huduma yako kusambaa kwa watu wengi zaidi maana watu wana tabia ya kusimuliana. Kwahiyo kama kampuni au mtu binafsi atakosea katika huduma kwa wateja watu hawatajikisikia kurudia biashara na wewe.
Zaidi ya hayo kazi ya huduma kwa wateja inahitaji mtu ambae ni msikivu, mwenye kusoma saikolojia ya mteja kwa haraka pia uvumilivu pale unapopata mteja mgumu kushika maelekezo.
Kwa upande wao wafanyakazi wa Quality Furniture walisifia mafunzo hayo wakisema yamewapa mwanga na kuongeza uelewa wao  katika huduma bora  kwa wateja ambao hawakuwa nayo hapo kabla.
“Mafunzo haya yalikuwa na lengo kubwa la kubadili mitazamo ya wafanyakazi. Tunaamini baada ya mafunzo haya leo kila mmoja wetu amepata nguvu mpya na anaenda kuhakikisha wateja wetu wanaendelea kupata huduma bora.” alisema bwana  Tonny Obura Meneja Mauzo na Masoko wa Quality Furniture.
Peak Performance International Tanzania,  PPIT ni kampuni inayoongoza Tanzania kwa kutoa mafunzo kwa makampuni na watu binafsi juu ya huduma bora kwa wateja, ufanisi kazini, umoja na mshikamano, kutambua uwezo ulioko ndani yako pamoja na mafunzo mengine mengi yenye lengo la kuboresha na kukuza ufanisi kazini na mafanikio kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment