TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, March 23, 2014

MPUNGUZENI GHARAMA YA KUCHIMBA VISIMA – WAZIRI MKUU

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameitaka Wizara ya Maji itafute njia mbadala zitazosaidia kupunguza gharama za kuchimba visima ili wananchi waweze kupata maji safi na salama.
“Wizara ya Maji angalieni uwezekano wa kupunguza gharama za uchimbaji wa visima ili wananchi waweze kumudu kuchimba visima na wapate uhakika wa maji safi na salama,” alisema.
 
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Machi 23, 2014), wakati akifunga Maadhimisho ya Wiki ya Maji Kitaifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.
 
“Hivi sasa nimeambiwa gharama ya kuchimba kisima mita moja ni sh. 150,000/. Je kama mtu anataka kuchimba kisima chenye urefu wa mita 180 au 200 itakuwaje? Ni dhahiri kuwa watu hawataweza kumudu hizo gharama. Angalieni namna ya kuzipunguza,” alisisitiza.
Habari zaidi soma hapa.

www.missdemokrasia.blogspot.com

No comments:

Post a Comment