TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, March 11, 2016

ZEC yawanoa mawakala wa uchaguzi

Na Ali Issa, MAELEZO-ZANZIBAR 

WILAYA YA KASKAZINI A

MAWAKALA 1,500 kutoka vyama mbalimbali vya siasa kutoka majimbo manne ya Mkoa wa Kaskazini Unguja, wamepatiwa mafunzo ya usimamizi wa uchaguzi wa marudio wa Zanzibar, unaotarajiwa kufanyika Machi 20, mwaka huu.

Mafunzo hayo yametolewa leo katika skuli ya msingi Mahonda, yakishirikisha mawakala kutoka majimbo ya Donge, Mahonda, Bumbwini na Kiwengwa.Akifungua mafunzo hayo, Msimamizi Mkuu wa uchaguzi Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Makame Khamis Pandu, amesema lengo la Tume ya Uchaguzi Zanzibar kutoa mafunzo hayo, ni kuwawezesha kutekeleza majukumu yao katika kufanikisha uchaguzi huo.

Aidha alifahamisha kuwa, uwakilishi mzuri wa vyama vyao ndio utakaosaidia kuendesha uchaguzi usiokuwa na mivutano na hivyo kuendeleza amani na utulivu nchini.“Mafunzo haya ni muhimu kwenu kwani nyinyi ndio mnaotegemewa na vyama vyenu katika kuviwakilisha na kuhakikisha zoezi la kusebu kura linafanyika kwa uwazi pasi na matatizo yoyote,” alieleza Pandu.

Msimamizi huyo alisema wakala wa vyama vya siasa hapa Zanzibar wapo kwa mujibu wa sheria ya Tume ya Uchaguzi na ushiriki wao ni muhimu katika kufanikisha zoezi hilo na kuondoa kasoro zinazoweza kujitokeza.

Mafunzo hayo ya siku moja ni miongoni mwa hatua za tume kuwapa elimu wadau wote wa uchaguzi wakiwemo makarani wataobahatika kuteuliwa kwa ajili ya shughuli hiyo muhimu ya kutafuta Rais na viongozi wa majimbo.

Kwa hivyo, aliwataka mawakala hao kuyapokea vyema mafunzo hayo na kasha wakayafanyie kazi kwa manufaa ya taifa.Washiriki wa mafunzo hayo walihakikisha kwamba watayafanyia kazi maelekezo yote na kuwajibika kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi.

IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR-

SPIKA AKUTANA NA WABUNGE KUTOKA UJERUMANI

Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akimkabidhi zawadi Kiongozi wa Msafara wa Wabunge kutoka Bunge la Ujerumani Mhe. Jens Koeppen. Anayeshuhudia kulia ni Naibu Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson.Wabunge hao walimtembelea Spika ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam

Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akipokea zawadi Kutoka kwa Kiongozi wa Msafara wa Wabunge kutoka Bunge la Ujerumani Mhe. Jens Koeppen. Wabunge hao walimtembelea Spika ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akimsikiliza Kiongozi wa Kiongozi wa Msafara wa Wabunge kutoka Bunge la Ujerumani Mhe. Jens Koeppen (wa pili kushoto) waliomtembelea Spika ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Naibu Spika Dkt Tulia Ackson na wa Kwanza kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini Bw. Egon Kochake.
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akiagana na Kiongozi wa Msafara wa Wabunge kutoka Bunge la Ujerumani Mhe. Jens Koeppen waliomtembelea Spika ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia wa kwanza kulia ni Naibu Spika Dkt Tulia Ackson na wa Kwanza kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini Bw. Egon Kochake.
Spika wa Bunge (wa pili kutoka kulia kwa walio kaa) akiwa katika picha ya Pamoja na Wabunge la Ujerumani waliomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha kutoka kulia ni Naibu Spika Dkt Tulia Ackson, Kiongozi wa Msafara wa Wabunge kutoka Bunge la Ujerumani Mhe. Jens Koeppen na Balozi wa Ujerumani nchini Bw. Egon Kochake.(Picha na Ofisi ya Bunge)

MWIGULU NCHEMBA AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA VIETNAM HII LEO,FURSA ZA KILIMO,MIFUGO NA UVUVI ZAFUNGULIWA RASMI

Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh.Mwigulu Nchemba akisalimiana na Rais wa Vietnam NdgTruong Tan Sang mapema hii leo walipokutana kwaajili ya mazungumzo kuhusu fursa zilizopo katika kilimo,mifugo na uvuvi katika nchi mbili hizi rafiki
Katika mazungumzo ya pamoja kati ya Rais wa Vietnam na Mh.Mwigulu Nchemba na ujumbe wake,Pande hizi mbili zimekubaliana kushirikiana kwenye uzalishaji wa mbegu bora za mazao na uzalishaji wa samaki hapa nchini,Mbali zaidi wamekubaliana kufungua fursa zaidi kwa wafanyabiashara wa nchi hizi mbili kuwekeza kwenye kilimo,mifugo na uvuvi.
Mauzungumzo yakiendelea kati ya ujumbe kutoka Vietnam na wadau wa kilimo hapa nchini.
Mh.Mwigulu Nchemba akiagana na Rais wa Vietnam mara baada ya mazungumzo ya pamoja kumalizika.Picha/Maelezo na Festo Sanga Jr.

NAIBU WAZIRI ANASTAZIA WAMBURA AFUNGUA MAONYESHO YA SABA YA BIDHAA ZA HARUSI

Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akimkabidhi Cheti cha ushiriki Bw.Erasto Mike wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya saba ya bidhaa za harusi leo jijini Dar es Salaam.
Mhe. Anastazia Wambura Naibu waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akiangalia bidhaa kutoka kwa mjasiriamali Bi Helen-Lukundo Chonjo( Kulia) wakati alipokuwa akifungua maonyesho ya saba ya bidhaa za Harusi.Katikati ni mbunifu wa mavazi Bw. Mustafa Asanali.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura akipokea maelekezo kuhusu jarida la Bidhaa za Harusi kutoka kwa mbunifu Mustafa Asanali kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Sanaa Bi Leah Kihimbi.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe Anastazia Wambura akisikiliza ufafanuzi kuhusu bidhaa za harusi zinazotengenezwa hapa nchini kutoka kwa Bi Dianna Kaijage wakati alipofungua maonyesho ya saba ya bidhaa hizo leo jijini Dar es Salaam.
Bi Sakina Kubino akimuonyesha Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura baadhi ya urembo unaovaliwa katika Sherehe za harusi wakati alipofungua maonyesho ya bidhaa hizo leo jijini Dar es Salaam.
Mbunifu wa mavazi Bw. Mustafa Asanali akimkaribisha Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo katika maonyesho ya saba ya bidhaa za harusi yanayofanika katika ukumbi wa St Peters jijini Dar es Salaam

TAASISI YA DORIS MOLLEL KWA KUSHIRIKIANA NA CBA WASAIDIA HOSPITALI YA MWANANYAMALA.


 Meneja Mahusiano wa Benki ya CBA, Caroline Makatu (wa pili kushoto)  akikabidhi msaada wa vitanda na mashine kumsaidia mtoto anayezaliwa kabla ya muda, kwa Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk. Delilah Moshi, katika hafla fupi iliyofanyika hospitalini hapo, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Maafisa kutoka Benki ya CBA wakiwa katika picha ya pamoja wadau waliofanikisha msaada huo katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
TAASISI ya Doris Mollel Foundation (DMF) kwa kushirikiana na Benki ya  CBA wametoa msaada vitanda viwili na mashine tatu za kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati vyenye wa vitu vyenye thamani ya Sh.milioni  mbili  katika Hospitali ya  Rufaa ya Mwananyamala  jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jana Jijini Dar es Salaam  Mkurugenzi wa DMF,  Doris Mollel, alisema  kwa kutambua umuhimu kwa sababu wanawakumbuka  wanawake wanaojifungua kabla ya wakati na kutoa msaada huo ni kutaka  kuokoa uhai wa watoto hao .
“Kutambua thamani ya watoto njiti tumeona katika kuokoa uhai na kuweza kufikia malengo tumeona ..mashine za kuwasaidia kufikia malengo yao kama walivyo watoto wengine…taasisi itaendelea kutoa mchango kwa jamii,” alisema Doris.
Naye Meneja Mahusiano wa Benki ya CBA ,Caroline Makatu amesema  kuna changamoto nyingi  hospitali ikiwemo na uhaba wa vifaa kwa kutambua hilo wametoa msaada huo  ili kusaidia mama na mtoto.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dk. Delilah Moshi amesema wanashukuru kwa msaada huo uliotolewa na taasisi hizo kwa kutambua uwepo wa wanawake na kuziwezesha hospitali.
Amesema kwa sasa shida kubwa iliyopo kwa sasa ni uhaba wa majengo kutokana na nafasi chache za kuhifadhia watoto njiti kwa sababu idadi ya watoto inaongezeka.
“Kutokana na kuwapo kwa mashine za kuhifadhia watoto njiti idadi ya vifo vya watoto hao imepungua hivyo naiomba serikali kuongeza madaktari wa watoto kwani hadi sasa wapo wawili tu,” amesema Mushi.

WAKALA WA MAJENGO TANZANIA YAIPA MKATABA YONO AUCTION MART WA KUKUSANYA MADENI NCHINI


Na Dotto Mwaibale

WAKALA  wa Majengo Tanzania (TBA), umecharuka kwa kuingia mkataba na Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd ili kusaidia kukusanya madeni ya wadaiwa sugu ambao walikopa nyumba.

Wakati huo huo mwakilishi wa kampuni hiyo ya udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela ametoa siku tatu kwa wadaiwa wote wa TBA kuhakikisha wanalipa fedha hizo kabla ya kufikiwa na kampuni hiyo ambayo Jumatano ya Machi 16 mwaka huu itaanza rasmi kazi ya kuwaondoa katika nyumba za wakala huo watumishi wote wanaodaiwa kwa kufuata sheria kama inavyoelekeza.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wa kutiliana saini na kampuni hiyo ya udalali kwa ajili ya kukusanya fedha kutoka kwa wadeni wa wakala huo  Mtendaji Mkuu wa TBA ,  Elius Mwakalinga alisema wamefia hatua hiyo baada ya kuona wadaiwa wao ambao wengi wao ni kutoka sekta za serikali kushindwa kulipa fedha hizo.

"Tumeingia mkataba na Kampuni ya Yono Auction Mart baada ya kushinda zabuni ambayo tulitangaza Februari 23,2016 na sasa kazi yote ya ukusanyaji wa fedha hizo itafanywa na kampuni hiyo" alisema Mwakalinga.

Mwakalinga alisema fedha nyingi za wakala huo zipo mikononi mwa wadaiwa wao ambapo kwa mkoa wa Dar es Salaam na Dodoma ni shilingi.Bilioni 6 na kwa waliokopa ni sh.milioni 800 huku fedha zinazodaiwa kwa ajili ya kutoa ushauri mbalimbali wa ujenzi ni sh.bilioni 6.95.

Mwakilishi wa kampuni  ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela alisema wametoa siku tatu kwa wadaiwa wote kuhakikisha wanalipa fedha hizo vinginevyo watafikiwa na kampuni hiyo ambayo imepanga rasmi kupita kila nyumba inayodaiwa na kuwa kila muhusika atatakiwa kuilipa kampuni hiyo asilimia tano ya fedha anazodaiwa na TBA.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ,  Arch. Elius Mwakalinga (kushoto), akikabidhiana hati ya mkataba na Mwakilishi wa Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela Dar es Salaam leo asubuhi, baada ya kampuni hiyo kushinda zabuni ya kukusanya madeni ya TBA kuanzia leo.
 Taswira meza kuu katika mkutano huo.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) , Arch Elius Mwakalinga (katikati), akizungumza katika mkutano huo kabla ya kutiliana saini na kampuni ya Yono. Kushoto Ofisa wa Idara ya Manunuzi, Mariam Kazoba.

TAWLA YAENDESHA SEMINA KWA WANAHABARI KUHUSU AFYA YA UZAZI NA CHANGAMOTO ZAKE

1
Afisa Uchechemuzi wa Shirika la Wanasheria wanawake la TAWLA Bi. Sime Bateyunga akifungua mafunzo kwa wanahabari hawapo pichani yanayolenga kujenga uelewa kwa waandishi wa habari kuhusiana na masuala ya haki ya afya ya uzazi Changamoto wanazokutana nazo na namna ambavyo matumizi ya sheria za kimataifa kama Maputo Protocal yataweza kupunguza Chanagamoto hizo, Semina hiyo ya siku mbili ilikuwa ikifanyika Luther House Azania Front jijini Dar es salaam na imemalizika leo
2
Wanahabari wakimsikiliza Afisa Uchechemuzi wa Shirika la Wanasheria wanawake la TAWLA Bi. Sime Bateyunga wakati akifungua semina hiyo jana.
4
Dk. Ali Said kutoka muhimbi akiwasilisha mada katika mafunzo hayo kuhusu utoaji miba usio salama na madhara yake.
5
Goodness Mrema Afisa habari na mawasiliano TAWLA akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa semina hiyo leo.
6
Afisa Mipango wa TAWLA Bi. Sara Kinyaga kulia akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuendesha mafunzo hayo kwa waandishi wa habari leo.
7
Maofisa wa TAWLA pamoja na waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja nmara baada ya kumalizika kwa semina hiyo leo jijini Dar es salaam.

Waziri Ummy akutana na mabalozi Ujerumani na Ireland leo



Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu (kulia kwa waziri) akimsikiliza Balozi wa Ujerumani nchini ,Egon Kochanke (Katikati) wakati alipomtembelea ofisini kwake leo.
Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akimsikiliza Balozi wa Ireland nchini Fionnuala Gilsen Nan(kulia kwa waziri wakati alipomtembelea ofisini kwake leo.Wengine ni baadhi ya maofisa wa ubalozi huo.

RAIS Dkt. MAGUFULI KUZINDUA KINYEREZI II


  Na Zuena Msuya, Dar Es Salaam

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ataweka jiwe la msingi katika ujenzi wa  kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi II chenye uwezo wa kuzalisha megawati 240 unaotokana na gesi asilia iliyogundulika nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo,Rais Dkt Magufuli anatarajiwa kuweka jiwe la msingi wiki ijayo  machi 16, na ujenzi wa mradi huo umeanza  mwezi Machi mwaka huu na unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 28.

Prof. Muhongo alifafanua kuwa mwanzoni mwaka 2018 ,kituo cha Kinyerezi II kitaanza kuzalisha umeme wa megawati 240 ambapo kati ya hizo megawati 180 zitatokana na Gesi asilia na megawati 60 zitatokana umeme utakaozalishwa kutokana na joto litakalotokana na kuendesha mitambo ya kituo hicho.

" Mtambo huu ni wa kisasa zaidi kwani hakuna kitakachopotea lile joto litakalokuwa linatoka kutokana na kuendehsa mashine litazalisha umeme , tofauti na ilivyokuwa kwa Kinyerezi I ambapo joto hupotea bure," alisema  Profesa Muhongo.

Alisema kuwa kituo hicho kitagharimu Dolla za Kimarekani milioni 344 hadi kukamilika kwake na tayari Mkandarasi  atakayejenga kituo hicho amekwisha lipwa fedha zake ambazo ni fedha kutoka Serikali ya Tanzania na mkopo  wa bei nafuu kutoa Serikali ya Japan.Pia Profesa Muhongo alitumia ziara hiyo kuuleza umma kuwa  kwa sasa Serikali inaondokana na miktaba ya malipo ya ziada ya mtaji  kwa kampuni zinazoiuzia umeme (TANESCO) ( Capercity charge) kwa mikataba mipaya .

Sambamba na hilo alisema kuwa kinachofanyika sasa ni kupitia upya mikataba iliyopo na kufanya mazungumzo na kampuni husika ili kuondoa gharama zisizo za lazima.
Katika ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la umeme nchini (TANESCO) Mhandisi Felchesim Mramba alisema mwishoni mwa mwezi huu kituo cha umeme cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi I kitaongeza uzalishaji wa umeme wa megawati 80 na hivyo kufanya kituo hicho kuzalisha jumla ya megawati 150 kama inavyokusudiwa.

Mramba aliongeza kuwa  mwanzoni mwa mwezi April, Mkoa wa Dar es salaam , utakuwa unapata umeme moja kwa moja kutoka Kinyerezi I tofauti na ilivyokuwa hapo awali ilikuwa ikitegemea kupata umeme kutoka kituo cha ubungo pekee.

Mramba alisema kukamilika kwa kiasi hicho cha umeme kutapunguza kabisa tatizo la kukakatika umeme mara kwa mara nchini.Katika ziara hiyo Profesa Muhongo alitembelea Kituo cha umeme cha City Center pamoja na cha Mikocheni ambavyo vitaliwezesha jiji la Dar es salaam kuondokana na nyaya za umeme zinazopita juu.

Akimfafanua waziri Mhongo meneja mwandamizi wa miradi ya usafirishaji na usambazaji Mhandisi Gregory Chegere, alisema miundombinu ya umeme ya katika kituo hicho itapita chini ya ardhi na hivyo kuondoa adha ya kukata miti pamoja na kuangushwa kwa nguzo kutokana na mvua zitakazokuwa zinanyesha kwa jiji la Dar Es Salaam.

Mhandisi Chegere alisema kituo hicho kitaanza kazi mwezi April na kuuwezesha Mkoa wa Dar es salaam kuwa na umeme wa uhakika na usiokatika. 

DK.KIGWANGALLA AFUNGA MOCHWARI YA HOSPITALI YA TUMBI, AIPA MASAA 72


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ametoa siku tatu kwa uongozi wa Hospitali y teule ya rufaa ya Mkoa wa Pwani-Tumbi kufunga chumba cha kuhifadhi maiti (Mochwari) baada ya kubaini matatizo mbalimbali baada ya kufanya ziara katika hospitali hiyo.

Katika ziara hiyo, Dk. Kigwangalla alibaini mambo mbalimbali kutoenda sawa ikiwemo suala la utendaji mbovu ambapo alitoa agizo la kumtaka Mkurugenzi wa Shirika la Elimu Kibaha wanaosimamia Hospitali hiyo kutoa maelezo ndani ya masaa 24 kama anafaa kubaki ama la!.

Aidha, Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, hali aliyoikuta katika chumba cha kuhifadhia maiti ni mbaya hivyo ilikuondoa matatizo amelazimika kuifunga kwa muda huo wa siku tatu ilikufanyia marekebisho kwa baadhi ya mambo ndani ya chumba hicho cha mochwari hospitalini hapo.

Awali vyombo vya habari vilitoa taarifa mbalimbali juu ya Mochwari hiyo ikiwemo badhi ya maiti kuhifadhiwa nje na kuatarisha afya za wananchi.
tumbi99
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla (katikati) akiwa na uongozi wa Hospitali hiyo akiwemo Mganga Mkuu wa Hospitali, Dk. Peter Datani (kulia) akitembelea katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Pwani-Tumbi wakati wa ziara hiyo mapema jana Machi 10.2016.
tumbi hjjh
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akikagua Mochwari ya Hospitali ya Rufaa ya Tumbi.

LOWASSA AMJULIA HALI MAALIM SEIF LEO


Waziri Mkuu Mstaafu na Aliekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akisalimiana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati alipokwenda kumjulia hali katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo Machi 11, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu na Aliekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akifanya mazungumzo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati alipokwenda kumjulia hali katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo Machi 11, 2015.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya hali ya afya yake.
Waziri Mkuu Mstaafu na Aliekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akiagana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, mara bade ya kumjulia hali katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo Machi 11, 2015.

TATOA KUJENGA VYUMBA VYA MADARASA 12 MANISPAA YA TEMEKE.

Mwenyekiti wa wa chama cha wamiliki wa malori Tanzania (TATOA), Angelina Ngalula akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na ujenzi wa madarasa 12 katika manispaa ya Temeke.
Sehemu ya Bodi ya TATOA  na watendaji wa ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki akizungumza na bodi ya TATOA jijini Dar es Salaam leo.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
CHAMA cha Wamiliki wa Malori nchini (TATOA) kinatarajia kujenga madarasa 12 katika shule msingi maji matitu ikiwa ni jitihada za kumuunga mkono Rais Dk.John Pombe Magufuli ya kuhakikisha shule zinaboreshwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki amesema kuwa wanatambua mchango wao na kuwa watakuwa wamesaidia jitihada za serikali katika kupunguza changamoto za madarasa.

Amesema kuwa Mkoa wa Dar es Salaam unakabiliwa na changamoto ya madarasa na madawati hivyo kunahitaji wadau kujitokeza kusaidia maeneo hayo.

Mwenyekiti wa TATOA, Angelina Ngalula amesema kuwa wameunga mkono jitihada za serikali kwa upande wa elimu hivyo wanawajibu wa kufanya hivyo katika kutatua changamoto ya vyumba vya madarasa.

Amesema kwa kuanzia wanaanza na madarasa 12 lakini wataendelea kuwasiliana na wanachama zaidi katika kuongeza au kujenga shule nzima ili watoto wasome shule na kuja kuweza kutumikia sekta ya usafirishaji.


Angelina amesema kuwa bodi yao iko imara katika kwenda na suala la shule za msingi ili watoto wapate elimu bora kutokana na mkakati wa Rais kutoa kipaumbele ya elimu ya nchini.

DUKA LA KAMERA LA KAMPUNI YA JUMBO LAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

 Meneja mauzo kampuni ya Jumbo Camera House Ltd, Mathias Luoga akizungumza na wadau mbalimbali wa Kamera pamoja na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa duka la kampuni ya Jumbo Camera House Ltd linalouza kamera za picha za mnato, picha za mjongeo, mabegi na vitu mbalimbali vya kamera, duka lililopo jengo la Benjamini Mkapa Tower Posta jijini Dar es Salaam.
 Muonekano wa duka la kampuni ya Jumbo Camera House Ltd linalouza
linalouza kamera za picha za mnato, picha za mjongeo, mabegi na vitu mbalimbali vya kamera.
Mkurugenzi Mtendaji, Paul Buckendahl akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka la kampuni ya Jumbo Camera House Ltd linalouza kamera za picha za mnato, picha za mjongeo, mabegi na vitu mbalimbali vya kamera duka lililopo katika jengo la Benjamini Mkapa Tower Posta jijini Dar es Salaam.Kushoto ni  Meneja mauzo kampuni ya Jumbo Camera House Ltd, Mathias Luoga.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Jumbo Camera House Ltd, Sara Filikunjombe(wa kwanza kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali leo katika uzinduzi wa Duka la Kamera katika jengo la Benjamin Mkapa Tower jijini Dar es Salaam leo.

WAZIRI WA MAJI AIAGIZA BODI YA DAWASCO KUWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI WAKE KWA TUHUMA MBALIMBALI

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge (katikati) akiongozana na Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Maji taka na Maji safi Dar es Salaam (DAWASCO) , Meja General (mstaafu), Samuel Kitundu (kushoto) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Cyprian Luhemeja , wakati Waziri huyo alipoitembelea Dawasco leo na na kisha kutangaza watumishi tisa ambao ameiagiza bodi kuwasimamisha kazi kupisha uchunguzi dhidi yao kufuatia tuhuma mbalimbali. Mhandisi Lwenge alitembelea leo. 

WATUMISHI AMBAO WAZIRI AMEAGIZA BODI IWASIMAMISHE KAZI NI:-
Meneja Rasilimali Watu, Mvano Mandawa, Meneja Ufuatiliaji na Tathmini, Reinary Kapera, Teresia Mlengu, Emmanuel Guluba, Peter Chacha, Fred Mapunda, Reginald Kessy, Jumanne Ngelela na Bernard Nkenda. 

Aidha Waziri Lwenge aliagiza pia kuchunguzwa kwa CEO wa zamani Jackson Midala.

Miongoni mwa tuhuma zao ni pamoja na kufanya maunganisho ya maji yasiyofuata utaratibu kwa kampuni ya STRABAG inayotekeleza mradi wa mabasi yaendayo kasi na kusababisha kulikosesha shirika mapato yenye thamani ya sh Bilioni 2.8 (2,887,577,134/=). 
Mameneja wa Dawasco wakiwa katika mkutano huo.Baadhi yao walisimamisha kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazo wakabili.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge (kulia) akizungumza na bodi pamoja na menejimenti ya Shirika la Maji taka na Maji safi Dar es Salaam (DAWASCO) wakati Waziri huyo alipotembelea makao makuu ya shirika hilo Dar es Salaam jana na kuiagiza bodi kusimamisha kazi watumishi tisa. 
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge (aliyesimama) akizungumza na bodi pamoja na menejimenti ya Shirika la Maji taka na Maji safi Dar es Salaam (DAWASCO) wakati Waziri huyo alipotembelea makao makuu ya shirika hilo Dar es Salaam jana na kuiagiza bodi kusimamisha kazi watumishi tisa.