TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 9, 2016

MVUA KUBWA ZINATARAJIWA KUNYESHA USIKU WA LEO MACHI 8 HADI 9 KWA UKANDA WOTE WA PWANI ADD SKILLS, SHOW YOUR POTENTIAL ON MARCH 21 - 25, 2016 - DAR ES SALAAM NINAWATAKIA WANAWAKE WENZANGU‎ ULIMWENGUNI KOTE, HERI YA SIKU YA MWANAMKE-MJ MFUMUKO WA BEI WA TAIFA WA MWEZI FEBRUARI, 2016 WAPUNGUA KWA ASILIMIA 5.6 WAFANYAKAZI WA MFUKO WA PENSHENI WA PPF WATOA MSAADA HOSPITALI YA MWANANYAMALA KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI. KICHUPA CHA LEO HARMONIZE FT DIAMOND - BADO NEW YORK SOCCER TEAM (NYATI) MAZOEZI YATAANZA MAPEMA HALI YA HEWA IMESHAANZA KUTULIA KUJIANDAA NA MECHI YA YANGA NA SIMBA PIA DC WAJE KULIPA. SERIKALI YATANGAZA BEI MPYA YA SUKARI NCHI NZIMA MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA KOREA NA INDIA LEO


Posted: 08 Mar 2016 10:27 AM PST

Posted: 08 Mar 2016 09:53 AM PST
Posted: 08 Mar 2016 09:51 AM PST
Monica Joseph
 Mmiliki wa  Kampuni ya Monfinance Investment
 Group na Muwakilishi  wa Philips Tanzania.
"Wanawake Tunapashwa Kuona Jinsia yetu kama rasilimali na sio Dhima". ( Women should view their gender as a resource rather than a liability) - MJ.

Ningependa kutumia fursa hii kama Dada, Mke, Mama, mfanyakazi, Mwanaharakati na mjasiliamali kuwapongeza wanawake wote kwa kuadhimisha siku hii muhimu ya kuwaenzi wanawake wote ulimwenguni. 

Historia ya Maisha yangu, ni kielelezo cha maisha ya wanawake wengi ulimwenguni wanaopitia changamoto mbalimbali.‎ Nililelewa katika mazingira kandamizi ya Jinsia ya kike-kwenye jamii ambayo mtoto wa kiume alipewa nafasi ya kipekee katika masuala mbalimbali dhidi ya mtoto wa kike...Kwa mfano kipaumbele cha kupata elimu walipewa watoto wa kiume wakati watoto wa kike wakitarajiwa kushughulika na kazi za nyumbani, kupika,kuchota maji na kusaidia shughuli za kilimo na hatimaye kuolewa. 

Bibi yangu (Apumzike kwa Amani) alikuwa mhanga wa mfumo huo kandamizi. Kwa taabu alizopita Bibi yangu alijiwekea nadhiri kwamba Mjuu wake, hatopitia shida alizopitia yeye...na hivyo siku zote alikuwa akiniasa kwamba "Niyu (jina langu la nyumbani),Unaweza kila kitu kinachofanywa na mtoto wa Kiume". Aliniimarisha kifikra na kiakili. 

Na siku zote alikuwa na msemo wake "Niyu Kasome, Ukasome umshinde Babu yako, Usije kuwa unanyanyasika kama sisi"- ushauri wake ndio ulikuwa dira yangu ya maisha ambapo nilisoma kwa bidii na kufanikiwa kuhitimu shahada ya uzamili katika masuala ya fedha kutoka Chuo Kikuu cha Strathclyde cha Uingereza. 


Hadi hivi leo, sauti ya Bibi haijakoma masikioni mwangu, sijaacha kutafuta elimu na maarifa ya masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo katika jamii...ni kwa sababu hiyo nilipata mafunzo ya muda mfupi ya uongozi na majadiliano kutoka Chuo kikuu cha Harvard cha nchini Marekani. Nitaendelea kuitafuta Elimu na pia kusaidia wenzangu, sababu naamini moja ya njia ya Mwanamke kujikomboa katika ukandamizaji wa kijinsia ni kuongeza kiwango cha elimu kwake mwenyewe na kwa wanawake wenzake. 

 Waswahili wana msemo usemao maisha ni shule.....msemo huu nimeuishi katika maisha yangu ya baada ya masomo. Nimefanya kazi katika mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali na sekta binafsi. nimefanya kazi na taasisi ya ISHI iliyokuwa inashughulikia masuala ya Ukimwi, baada ya hapo nimefanya pia katika kampuni‎ ya Philips Medical Systems ya Uholanzi na baadaye nimefanya kazi kampuni ya mawasiliano ya Maktech. Kwote nilipopita nimekumbana na changamoto mbalimbali zilizohusiana na jinsia yangu.

 Utekelezaji wa majukumu yangu ulinilazimu kuwa na mikutano na watu mbalimbali Serikalini na kwenye taasisi za fedha ambapo watu niliokuwa nakutana nao ni wanaume ambao baadhi yao wamekuwa na mawazo ya mfumo dume yaliyojaa dharau na manyanyaso. Wengine kwenye fikra zao wanadhani mwanamke yeyote mwenye mafanikio, iwe kwenye biashara, siasa, ajira, lazima anabebwa na wanaume.‎ Wakiona mwanamke amefanikiwa tu, utasikia..huyu 'hawala wa fulani'. hii ni dhana potofu na inayolenga kumdhalilisha na kumnyanyasa mwanamke. Mimi binafsi sikukubali kuyumbishwa na watu wenye mawazo ya aina hiyo. 

Kila nilipokumbana na changamoto za aina hiyo nilipata hamasa ya kufanya kazi kwa bidii zaidi na kuwadhihirishia kwamba NINAWEZA, ilee sauti ya bibi ndioa ilikuwa ikinitia hamasa zaidi na zaidi na hatimaye kuniwezesha kufanya vizuri hadi kufikia kuaminiwa kupewa majukumu makubwa zaidi kama vile Mkurugenzi Mkuu katika kampuni ya Mokasi Medical Systems ambayo ni wakala wa kampuni ya Philips ya Uholanzi. Hasama hiyo iliniwezesha pia kuanzisha kampuni yangu inayotoa Huduma za kifedha - Monfinance Investment Group Ltd. 

Mbali na shughuli hizo nimeweza pia kuchaguliwa kuwa mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya FINCA Microfinance Tanzania. Kwa ujumla siku zote za maisha yangu nimejihusisha na harakati za kupigania haki za wenye shida na mahitaji katika jamii kutokana na msingi niliojengewa na bibi yangu wa kukataa unyonge na kusaidia wanyonge. Hurka hiyo ndio ilipelekea ajira yangu ya kwanza kuwa kwenye taasisi ya uhamasishaji wa masuala ya ukimwi ya ISHI. Niliguswa kujihusisha na kampeni hizo kwasababu binafsi nimepoteza ndugu, jamaa na marafiki kutokana na ugonjwa huo. Mbali na ISHI,nimekuwa nikijihusisha na kampeni ya kuzuia mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) iitwayo IMETOSHA.

 Ni jambo la udhalilishaji uliopitiliza kuwakata binadamu wenzetu viongo vyao kwa imani za kishirikina. Pia nimeshiriki kwenye uhamasishaji wa magonjwa yasiyojulikana (Rare diseases).‎ Tunaposherehekea siku ya Mwanamke duniani rai yangu kwa wanawake wenzangu, tushirikiane, tusaidiane, tupeane moyo na tuwezeshana ili tufikie lengo letu la usawa 50/50 kufikia mwaka 2030. Kila mwanamke atimize wajibu wake kwa kujitambua na kuhakikisha haki yake hainyongwi. ‎‎

Mimi nimejitambua, ninasimamia haki yangu, na wala siipiganii, ni yangu, Jinsia yangu hainitofautishi kiutendaji na jinsia ya kiume. Ninachoangalia ni Mchango wangu katika maendeleo ya Uchumi, jamii na familia na sio Jinsia yangu. Ninachotambua katika jinsia yangu ni kuwa mimi ni Dada, Mama, rafiki, na Mke. Mengine yote,nipo sawa na wote, wanaume na wanawake.‎ Happy Women's Day 2016.
a7caeb96fbdcd21385508290de4f359f"Wanawake Tunapashwa Kuona Jinsia yetu kama rasilimali na sio Dhima".  Women should view their gender as a resource rather than a liability) - MJ. 

Posted: 08 Mar 2016 08:57 AM PST
 Mkurugenzi wa Takwimu za Sensa na Jamii Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana, kuhusu mfumuko wa bei wa taifa wa mwezi Februari, 2016. Kulia ni Meneja Idara ya Ajira na Bei, Ruth Minja.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Wapiga picha wakiwa kazini.

Na Dotto Mwaibale

OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema mfumuko wa bei katika Februari mwaka huu umepungua  mpaka kufikia asilimia 5.6  kutoka asilimia 6.5 ya  mwezi Januari.

Akizungumza  katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana, Mkurugezi wa Sensa za Jamii, Ephraim Kwesigabo alisema kasi ya upunguaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka huu kumechangiwa na kupungua kwa bei za baadhi za vyakula na bidhaa zisiyakula kwa kipindi kilichoishia  cha Februlia, 20 ikilinganishwa na bei za Februari mwaka 2015.


Alisema kuwa mfumuko wa bidhaa za vyakula na vinjwaji baridi kwa Februari mwaka huu umepungua kwa  asilimia 10.3, mafuta ya dezeli kwa asilimia 4.5  na matunda kwa asilimia 7.2.


Kwesigabo alisema pamoja na kupungua kwa  kasi  ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kuna baadhi ya bidhaa zinaonyesha  kuongezeka  katika hicho  ni pamoja na Sukari kwa asilimia 7.1, Mkaa asilimia 4.3, Mchele kwa asilimia 22.9 na viazi 16.3.



Aidha alisema hali ya mfumuko wa bei katika nchi za jilani unaelekea kufanana na nchi za afrika  mashariki ambapo Kenya umepungua hadi asilimia 6.84 kutoka  asilimi7.78 mwaka huu, Uganda umeongezeka kwa asilimia 7.7 kutoka  asilimia  7.6 kwa mwezi  Januari mwaka huu.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com)
Posted: 08 Mar 2016 08:42 AM PST
  Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni, Zahra Kayugwa (katikati) akimkabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali Caroline Hanne Van, Raia wa Denmark kwa niaba ya watoto wawili (kitandani) waliodaiwa kuokotwa jana maeneo ya Mbezi Beach na kufikishwa hospitalini hapo leo asubuhi, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo Machi 8, 2016. Kushoto ni Emel Kudahl Christensen na wa tatu (kulia aliyekaa) ni Emma Nikoline Wennberg, wauguzi wa kujitolea kutoka nchini Denmark.
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya Watoto wachanga/Njiti, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya Watoto wachanga/Njiti, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya Watoto wachanga/Njiti, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni, Zahra Kayugwa (kulia) akimkabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali mzazi aliyejifungua mtoto wa Kiume, Hospitali ya Mwananyama, Joyce Lucas, mkazi wa Magomeni jijini Dar es Salaam, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni, Zahra Kayugwa (kushoto) akikabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali kwa wazazi waliokuwa wamelazwa kweye Wodi ya Watoto wachanga/Njiti  katika  Hospitali ya Mwananyama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni, Zahra Kayugwa (kulia) akimkabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali mgonjwa mzazi aliyelazwa kwenye Wodi ya kina mama waliofanyiwa upasuaji Hospitali ya Mwananyama, jijini Dar es Salaam, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya Kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni, Zahra Kayugwa (wa pili kulia) na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Janet Ezekiel, wakiwaangalia watoto wawili waliodaiwa kuokotwa maeneo ya Mbezi Beach, waliofikishwa Hospitali ya Mwananyamala.
 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Picha ya pozi ......
 Picha ya pozi na mtoto.....
Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo

 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akigawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa wazazi waliolazwa kwenye Wodi ya kinamama, wakati Wafanyakazi wa Mfuko huo walipofika Hospitalini hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa Wazazi na watoto ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa leo
 Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakisubiri kuingia wodi ya wazazi wa upasuaji kugawa msaada wa vitu mbalimbali leo.
 Wafanyakazi hao wakipozi na baadhi ya vitu walivyoshusha kwenye magari yao kabla ya kuanza zoezi la kugawa.
 Wafanyakazi hao wakiendelea kushusha vitu hivyo kutoka kwenye magari...
 Wafanyakazi hao wakiendelea kushusha vitu hivyo kutoka kwenye magari...
Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni, Zahra Kayugwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mfuko huo baada ya zoezi la kugawa vitu hivyo leo kwenye Hospitali ya Mwananyamala.
Posted: 08 Mar 2016 07:52 AM PST
Mazoezi  yataanza sooner kujiandaa na  mechi ya Yanga na Simba  Memorial Weekend hapa hapa New york. Hiyo ni nafasi ya wapenzi wa Yanga na Simba kutoana jasho na Kombe uwanjani siku hiyo mtoto hatumwi dukani kwani akitumwa dukani change mali yake au itapotelea njiani kabisa kabla kufika nyumbani. Tafadhani tafadhali ukisoma hii habari mwambie mnazi mwenzio kuwa awile mwana siku hiyo.


Posted: 08 Mar 2016 05:08 AM PST
Siku chache baada ya Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutangaza zuio la uingizwaji wa bidhaa ya sukari kutoka nje ya nchi, leo March 8 2016 Serikali kupitia bodi ya sukari Tanzania, imetangaza viwango vipya vya bei ya sukari nchini vitakavyoanza kutumika hivi karibuni, akiongea na waandishi wa habari Mkurugenzi wa bodi ya sukari Tanzania Henry Semwanza amesema.

Serikali, kupitia bodi ya Sukari Tanzania, inawaarifu wananchi wote kuwa bei ya rejareja ya sukari sasa itakuwa sh. 1,800 kwa kilo moja‘

‘wafanyabiashara wote wanapaswa kuzingatia agizo hili, pamoja na kuhakikisha kuwa sukari inaendelea kusambazwa na kuuzwa kwa wananchi bila kuihodhi‘

‘Maafisa biashara wa mikoa na wilaya watafuatilia na kusimamia utekelezaji wa agizo kuhusu bei elekezi ya sukari, na hawatasita kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wale watakaobainika kupandisha bei ya bidhaa hiyo‘

Posted: 08 Mar 2016 04:42 AM PST
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Profesa Choi Oe Chool Rais wa GLOBAL SAEMAUL DEVOLOPMENT NETWORK ya Jamhuri ya Korea, Wakati Rais huyo na Ujumbe wake alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwenye mazungumzo yao Viongozi hao wamezungumzia juu ya kukuza na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea ratiba ya mpango wa maendeleo wa Jumuiya ya GLOBAL SAEMAUL UNDONG kutoka kwa Profesa Choi Oe Chool Rais wa GLOBAL SAEMAUL DEVOLOPMENT NETWORK ya Jamhuri ya Korea, Wakati Rais huyo na Ujumbe wake walipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwenye mazungumzo yao Viongozi hao wamezungumzia juu ya kukuza na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Jumuiya ya GLOBAL SAEMAUL DEVOLOPMENT NETWORK ya Jamhuri ya Korea, Wakati Ujumbe huo ulipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Ujumbe wa Uwekezaji katika Nyanja wa Viwanda vya Sukari kutoka Kampuni ya RAK INTERNATIONAL LTD ya India, Wakati Ujumbe huo ulipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwa lengo la kutaka kuwekeza Viwanda vya Sukari hapa Nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia mpango wa maendeleo wa Viwanda ulioandaliwa na Kampuni ya RAK INTERNATIONAL LTD ya India, Wakati Ujumbe wa Kampuni hiyo ulipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwa lengo la kutaka kuwekeza Viwanda vya Sukari hapa Nchini. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya RAK INTERNATIONAL LTD Bw. Sundeep Patil. (Picha na OMR)
Posted: 08 Mar 2016 03:24 AM PST
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premieum Lager, Charles Boniface Mkwasa leo ametangza kikosi cha wachezaji 25 kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa Afrika (AFCON) dhidi ya Chad, Machi 23, 2016 mjini Djamena.

Akiongea na waandishi wa habari wakati akitangaza kikosi hicho, Mkwasa amewaomba wachezaji aliowaita katika kikosi hicho, kujiweka fit katika mazoezi wanayoyafanya katika vilabu vyao, kwani hakutakua na muda wa kufanya mazoezi kwa ajili ya mchezo huo wa ugenini.

“Ligi Kuu ya Vodacom, michuano ya CAF (CL, CC) inachezwa wikiendi ya tarehe 18-20 Machi, hivyo wachezaji wote watakua na majukumu katiak timu zao, muda wa kufanya mazoezi kwa pamoja kwa ajili ya mchezo huo hautakuwepo, ndio maana nasisitiza wachezaji niliowachagua wahakikishe wanajilinda wenyewe kwa kuwa fit wanapokuja kwenye safari ya mchezo huo wa machi 23, 2016” alisema Mkwasa

Wachezaji walioitwa Taifa Stars ni magolikipa Aishi Manula (Azam FC), Ally Mustapha (Young Africans) na Shaban Kado (Mwadui FC), walinzi ni Juma Abdul, Haji Mwinyi, Kelvin Yondani (Young Africans), Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, David Mwantika (Azam FC) na Mohamed Hussein (Simba SC).

Viungo Himdi Mao (Azam FC), Ismail Juma (JKU), Jonas Mkude, Said Ndemla, Mwinyi Kazimoto (Simba SC), Mohamed Ibrahim, Shiza Kichuya (Mtibwa Sugar), Farid Mussa (Azam FC), Deus Kaseke (Young Africans).

Washambuliaji ni Nahodha Mbwana Samatta (KRC Genk), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe), John Bocco (Azam FC), Elias Maguri (Stand United), Jeremia Mgunda (Tanzania Prisons) na Ibrahim Hajibu (Simba SC).
Posted: 08 Mar 2016 03:14 AM PST
Baada ya kudumu Ikulu kwa takribani siku 127zikiwamo 67 tangu aongezewe muda wa mwaka moja akiwa na Serikali ya Awamu ya Tano, Balozi Ombeni Sefue ameshukuru heshima aliyopewa na Rais John Magufuli kwa muda wote aliomsaidia kutekeleza majukumu yake ya ukatibu mkuu kiongozi na kueleza kuwa Serikali ya sasa ni ya mabadiliko.
Wakati Sefue akiondoka, mhandisi John Kijazi amepokea kijiti cha ukuu wa utumishi serikalini na kuahidi kuwa atafuatilia mazingira ya watumishi wote pamoja na mazingira yao, ili kurekebisha panapohitajika kwa lengo la kuongeza uwajibikaji na tija kwa wananchi.
Akizungumza muda mfupi baada ya kuapishwa kwa mrithi wake, licha ya kumshukuru Rais, Balozi Sefue aliwataka watendaji wote serikalini kumpa ushirikiano wa kutosha Balozi Kijazi ili kuleta ufanisi kwenye huduma za umma.
“Namshukuru Rais kwa kuniamini kwa kipindi chote nilichodumu naye. Ni heshima kubwa kuwatumikia Watanzania pamoja naye. Nitampa ushirikiano wowote atakaouhitaji katibu mkuu kiongozi mpya kwenye utekelezaji wa majukumu yake,” alisema Sefue.
Rais Magufuli, ameahidi na mara zote amekuwa akisisitiza adhma yake ya kutumbua majipu kwa watumishi wote ambao hawaendani na kasi yake. Tangu taarifa za mabadilio hayo zilipotangazwa jana, kumekuwepo na tetesi nyingi kuwa huenda Sefue naye ni jipu lilikuwepo ikulu, suala ambalo halikupata maelezo ya kutosha kutoka kwa balozi huyo.
Alipoulizwa juu ya tetesi hizo alijibu kwa ufupi: “Hii ni Serikali ya mabadiliko.”
Kwa upande wake Kijazi, alisema atafanya kazi kwa kuzingatia vipaumbele vya Rais huku akimshauri namna sahihi za kuboresha mazingira ya utumishi serikalini.
Akieleza juu ya majukumu yake mapya, alionyesha kuyatambua ipasavyo na kubainisha kuwa atashirikiana na Baraza la Mawaziri kwenye vikao vyao, bila kusahau kuzifuatilia wizara husika na kuona endapo kila kitu kinaenda kama inavyotakiwa.
“Nitakutana na mawaziri kwenye vikao vyao nitakavyoviandaa. Nitawasiliana na kuwafuatilia watendaji wa wizara husika juu ya masuala yatakayokuwa yamejitokeza ndani ya maeneo yao ya uwajibikaji. Kila mmoja atimize wajibu wake ili Taifa lisonge mbele,” alisema Kijazi.
Ili kuitendea haki hadhi ya utumishi wa umma, Kijazi ameahidi kuhakikisha kila kitu kinasimamiwa kwa ukaribu huku akitoa msisitizo kwenye vipaumbele vya Rais. “Kwenye suala la mapato na rushwa, nitafuatilia kwa nguvu ili kuongeza uwajibikaji kwa watumishi wa Serikali,” alisisitiza Kijazi.
Balozi Kijazi aliteuliwa juzi kushika nafasi inayoachwa na Balozi Sefue. Kabla ya uteuzi huo, Kijazi alikuwa mwakilishi wa Tanzania kwa nchi za India, Singapore, Sri Lanka, Bangladesh na Nepal huku makazi yake yakiwa jijini New Delhi, India kuanzia mwaka 2007.
Katika wadhifa huo, alikuwa mkuu wa mabalozi wote wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi pamoja na mkuu wa mabalozi wa Afrika nchini India. Kabla hajateuliwa kuwa mwakilishi wa nchi, Kijazi amekuwa mtumishi serikalini kwa nafasi mbalimbali ikiwamo Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi kuanzia mwaka 2002 mpaka 2006.
Kabla ya hapo alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu kati ya mwaka 1996 hadi 2002.
Ndani ya Wizara ya Ujenzi, kabla hajawa katibu mkuu, alikuwa mhandisi mwandamizi wa ujenzi wa barabara kisha kupandishwa cheo na kuwa mkurugenzi wa barabara za mikoa.
Kumbukumbu za taaluma yake zinaonyesha kuwa alipata Shahada yake ya kwanza ya Sayansi ya Uhandisi wa Umma mwaka 1982 kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na baadaye Shahada ya Uzamili katika Uhandisi wa Barabara kutoka Chuo Kikuu cha Birmingham, Uingereza mwaka 1992.
Jana wakati anaapishwa, saa 4:15 asubuhi, Kijazi alikuwa sambamba na mke wake, Fransiscar Kijazi na kwa pamoja wamejaliwa watoto watatu, David, Emmanuel na Richard. Kwa heshima ya familia hiyo, baada ya kukamilisha protokali, Rais Magufuli alipiga picha ya pamoja na familia ya mteule huyo mpya atakayehudumu ikulu kuanzia sasa.
Hata hivyo kwa mara ya mwisho, Sefue aliendelea na kazi yake mpaka jana asubuhi na ndiye aliyemkabidhi Kijazi kitabu kitakatifu cha Biblia, Katiba na kiapo cha uongozi ambacho alisaini.
Wadau wazungumza
Balozi Abdul Faraji alisema mabadiliko yaliyofanyika ya katibu mkuu kiongozi ni ya kawaida katika nchi mbalimbali ulimwenguni, hasa pale Serikali mpya inavyoingia madarakani. Alisema kila Rais mpya mara nyingi hupenda kuingia ofisini akiwa na timu ya watu wake, ambao anaona watafanikisha utelekelezaji wa malengo aliyojiwekea katika Serikali yake.
Faraji ambaye aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania katika nchi mbalimbali duniani ikiwamo Ufaransa (1972-1973), alisema balozi Sefue emeondoka Ikulu akiwa amefanya kazi kubwa ambayo anatakiwa kupongezwa na kila Mtanzania. “Tunamsifu kwa kazi yake hasa kwa kipindi hiki cha miezi mitatu ya utawala wa Rais Magufuli. Alijitahidi kwenda na kasi ya mabadiliko kwa uwezo wake ukizingatia alikuwa kwenye awamu ya Serikali ya awamu ya nne ambayo siasa yake haikuwa na kasi kama ya sasa,” alisema.
Wakati mijadala katika mitandao ya kijamii ikiendelea juu ya muda mfupi aliokaa balozi Sefue, Mhadhiri wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Shumbusho Damian alisema muda huo huenda ulikuwa ni maalumu kumpatia uzoefu Rais Magufuli katika masuala mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea Serikalini.
“Jambo ambalo sikutegemea ni kumteua Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi kwa sababu nadharia iliyokuwepo ni kwamba Rais Magufuli anataka kufanya kazi na watu wapya ambao hajawahi kufanya nao kazi”, alisema.
Katibu Mkuu wa chama cha CCK, Renatus Muabhi alimpongeza Rais Magufuli kwa uteuzi huo na kueleza kuwa ni wakati mwafaka kwa Serikali yake kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wenye kashfa.
“Kila utawala ni lazima uwe na safu yake ya uongozi ili kuondoa viraka vitakavyokwamisha utekelezaji wa baadhi ya mambo yanayoletwa na mfumo mpya. Rais alitwambia kuwa ameikuta nchi katika hali mbaya, hivyo ni wakati muafaka wa kuwaondoa wote wenye tuhuma,” alisema Muabhi.
Akizungumzia ahadi ya balozi Sefue kupangiwa kazi nyingine, Mhadhiri wa Chuo cha Diplomasia, Dk Ahmed Kiwanuka alisema kauli hiyo ni ya kawaida na humaanisha dhamira ya kweli ya Rais kutafuta nafasi mpya ya kumpeleka mhusika hata kama itachukua muda mrefu. “Kuna kazi nyingine kama za ubalozi ni lazima zipitie mchakato mrefu siyo rahisi kama watu wanavyofikiri. Hivyo Rais hawezi ghafla akasema ‘namteua fulani kuwa balozi wa nchi fulani’ kama jina la huyo mtu halijakubaliwa upande wa pili,” alisema Dk Kiwanuka.
Posted: 08 Mar 2016 01:58 AM PST
UKAGUZI wa hesabu za fedha za Halmashauri ya Jiji la Arusha uliofanywa na Mkaguzi wa Ndani (Internal Auditor) umeibua ‘madudu’ ya baadhi ya watendaji wa Jiji hilo, ikibainika kuchotwa kwa mamilioni miezi minne tu kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.
Ukaguzi huo umefanyika kwa mujibu wa sheria na kanuni za fedha za serikali za mitaa (LAFM) ya mwaka 2009 na (LAAM) ya mwaka 2009 na kanuni za ununuzi za mwaka 2013, sambamba na maelekezo ya kamati ya fedha.
Kwa mujibu wa taarifa za ukaguzi huo ambao Raia Mwema imeona nakala yake, fedha zilizopotea ni zaidi ya milioni 500, kati ya mwezi Julai 2014 na Juni 2015, ikiwa ni miezi minne kabla ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba, mwaka jana.
Hali hiyo inatokana kinachoelezwa kuwa ni udhaifu mkubwa wa wakala wa kukusanya mapato ya halmashauri ambaye ni kampuni maarufu ya Max-Malipo inayojishughulisha na biashara fedha kwa njia ya mtandao.
Kampuni hiyo ya Max-Malipo iliingia mkataba unaodaiwa kuwa na utata mkubwa na Halmashauri ya Jiji la Arusha Julai mwaka jana, kwa shinikizo kubwa la Mkurugenzi wa Jiji, Idd Juma, pamoja na baadhi ya madiwani wakiwamo cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa wakati huo.
Mapato yalivyopotea
Taarifa hiyo inaonyesha kuwa katika kipindi hicho cha miezi mitatu, imegundulika kuwa mapato yanayokusanywa na mashine za maxcom yalishuka badala ya kuongezeka.
“Wakati wa ukaguzi na ukusanyaji wa mapato kwa vyanzo vinavyokusanywa na mashine za maxcom, masoko, vituo vya mabasi, vyoo na machinjio mapato yamepungua kwa asilimia 40 tofauti na kipindi cha awali makusanyo yalipokuwa yanafanywa na mawakala,” inasomeka sehemu ya taarifa ya ukaguzi huo.
Inaendelea zaidi: “Mapato yanashuka kutokana na wakusanya mapato kutotoa stakabadhi za mashine kwa wateja na kusababisha makato hayo yasiyokatiwa stakabadhi kutoingia halmashauri, kinyume cha kanuni za fedha za serikali za mitaa”.
Pamoja na taarifa hiyo ya ukaguzi, habari kutoka ndani ya Jiji zinadai kuwa halmashauri imeingia hasara kubwa ya kupoteza mapato yake kutokana na mfumo huo na mkataba ambao unadaiwa kuwa umejaa utapeli.
Akitoa mfano wa hasara hiyo, mmoja wa watumishi wa halmashauri aliyeomba jina lake lihifadhiwe, alieleza kuwa kabla ya kuingia mkataba na Max-Malipo wakala aliyekuwa akisimamia choo cha Soko la Kilombero alikuwa anawasilisha kiasi cha shilingi milioni 1.5 kwa mwezi.
“Kwa Max-Malipo mapato yameshuka na pia halmashauri inalazimika kulipa gharama za uendeshaji kama maji na umeme kila mwezi kati ya shilingi 500,000 na 800,000 pamoja na mshahara wa msimamizi, hivyo kukosa mapato kwa asilimia 50,” alidai mtoa taarifa huyo.
Takwimu za ukaguzi zinaonyesha kuwa katika kipindi cha miezi mitatu ya Machi ,Aprili na Mei mwaka 2015 kabla ya kuingia mkataba na Max-Malipo Halmashauri ya Jiji la Arusha ilikuwa inakusanya wastani wa shilingi 95,225,018 kwa mwezi.
Fedha hizo ni kutoka vyanzo vya mapato vya vituo vyote vya mabasi, vyoo vya umma, machinjio na masoko yote ya Jiji.
Taarifa hiyo inabainisha kuwa katika kipindi hicho cha miezi mitatu kampuni ya Max-Malipo ilikusanya wastani wa shilingi 56,768,104 na 83,296072, hivyo halmashauri kupoteza zaidi ya shilingi milioni 100.
Ufisadi Arusha Meat
Aidha ufisadi mkubwa umebainika katika ukaguzi huo, katika kampuni tanzu ya Arusha Meat inayomilikiwa na Jiji ambayo inasimamia machinjio ya Jiji na kiwanda cha kusindika nyama cha Arusha Meat.
Ukaguzi huo unaonyesha kuwa kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria na kanuni za matumizi ya fedha za serikali kutokana na usimamizi mbovu wa Mkurugenzi wa Jiji, mweka hazina na watumishi wa kiwanda hicho.
Miongoni mwa mfano wa matumizi mabaya ya kanuni za fedha ni kukosekana kwa hati za malipo (Invoice) yenye thamani ya shilingi 178,164,308 kati ya Julai 2014 na Juni 2015.
Ukaguzi unaonyeha kuwa katika kipindi hicho malipo yenye thamani ya shilingi 64,604,574 pia yalikosa uthibitisho na viambatanisho halali kinyume cha sheria namba 10 ya kifungu cha 2 (d) cha mwaka 2010, kinachohusiana na usimamizi wa fedha za serikali za mitaa.
Pia ilibainika kuwa fedha za mauzo ya duka la nyama la kampuni hiyo lililopo eneo la Nanenane katika Jiji la Arusha kiasi cha shilingi 9,614,000 hazikuwasilishwa benki kinyume cha sheria ya fedha za serikali za mitaa ya mwaka 2010, namba 37 kifungu cha tatu.
Mkaguzi huyo anafafanua kuwa hatua ya kutopelekwa kwa fedha hizo benki kumesababisha kampuni hiyo kukosa uwazi na kuzua upotevu wa fedha za umma.
Ukaguzi huo umeendelea kubainisha kuwa kampuni hiyo ya nyama pia imepoteza kiasi cha shilingi 16,635,320 kati ya Julai 2014 na Juni 2015, kabla ya kuwasilishwa benki na hakukuwa na vielelezo vyovyote vya matumizi ya fedha hizo.
Aidha pia imebainika kuwa kati ya siku 4 hadi 54 daktari msimamizi wa ukaguzi wa nyama katika kiwanda hicho hakuwasilisha benki malipo ya shilingi milioni 15,770,000, kinyume cha sheria ya fedha za serikali za mitaa namba tano na 50 ya mwaka 2009.
Katika idara nyingine za halmashauri, ukaguzi unaonyesha kuwa katika kipindi cha Julai 2015 na Septemba 2015 kiasi cha shilingi 12,280,750 zimelipwa kwa wadai mbalimbali (creditors) ambao hawako katika orodha ya wadai wa Jiji.
Taarifa hiyo inaendelea: “Pia hati za malipo zenye thamani ya shilingi 339,044,587,22 katika idara mbalimbali za halmashauri zilikosekana kati ya Julai 2015 na Septemba 2015”
Pia watumishi 49 wa Jiji walishindwa kurejesha masurufu wala kuingizwa katika rejista yenye thamani ya shilingi 144,777,100.45, wakiwamo maofisa wa ngazi za juu katika

No comments:

Post a Comment