Waziri
 wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge (katikati) akiongozana na 
Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la Maji taka na Maji safi Dar es Salaam 
(DAWASCO) , Meja General (mstaafu), Samuel Kitundu (kushoto) na Afisa 
Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Cyprian Luhemeja , wakati Waziri huyo 
alipoitembelea Dawasco leo na na kisha kutangaza watumishi tisa ambao 
ameiagiza bodi kuwasimamisha kazi kupisha uchunguzi dhidi yao kufuatia 
tuhuma mbalimbali. Mhandisi Lwenge alitembelea leo. 
WATUMISHI AMBAO WAZIRI AMEAGIZA BODI IWASIMAMISHE KAZI NI:-
Meneja
 Rasilimali Watu, Mvano Mandawa, Meneja Ufuatiliaji na Tathmini, Reinary
 Kapera, Teresia Mlengu, Emmanuel Guluba, Peter Chacha, Fred Mapunda, 
Reginald Kessy, Jumanne Ngelela na Bernard  Nkenda. 
Aidha Waziri Lwenge aliagiza pia kuchunguzwa kwa CEO wa zamani Jackson Midala.
Miongoni
 mwa tuhuma zao ni pamoja na kufanya maunganisho ya maji yasiyofuata 
utaratibu kwa kampuni ya STRABAG inayotekeleza mradi wa mabasi yaendayo 
kasi na kusababisha kulikosesha shirika mapato yenye thamani ya sh 
Bilioni 2.8 (2,887,577,134/=). 
Mameneja wa Dawasco wakiwa katika mkutano huo.Baadhi yao  walisimamisha kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazo wakabili.
Waziri
 wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge (kulia) akizungumza na bodi 
pamoja na menejimenti ya Shirika la Maji taka na Maji safi Dar es Salaam
 (DAWASCO) wakati Waziri huyo alipotembelea makao makuu ya shirika hilo 
Dar es Salaam jana na kuiagiza bodi kusimamisha kazi watumishi tisa. 
Waziri
 wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge (aliyesimama) akizungumza na
 bodi pamoja na menejimenti ya Shirika la Maji taka na Maji safi Dar es 
Salaam (DAWASCO) wakati Waziri huyo alipotembelea makao makuu ya shirika
 hilo Dar es Salaam jana na kuiagiza bodi kusimamisha kazi watumishi 
tisa.
No comments:
Post a Comment