Mwenyekiti
 wa wa chama cha wamiliki wa malori Tanzania (TATOA), Angelina Ngalula 
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na
 ujenzi wa madarasa 12 katika manispaa ya Temeke.
Sehemu ya Bodi ya TATOA  na watendaji wa ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki akizungumza na bodi ya TATOA jijini Dar es Salaam leo.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
CHAMA 
cha Wamiliki wa Malori nchini (TATOA) kinatarajia kujenga madarasa 12 
katika shule msingi maji matitu ikiwa ni jitihada za kumuunga mkono Rais
 Dk.John Pombe Magufuli ya kuhakikisha shule zinaboreshwa.
Akizungumza
 na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Mkuu wa Mkoa wa Dar es 
Salaam, Said Meck Sadiki amesema kuwa wanatambua mchango wao na kuwa 
watakuwa wamesaidia jitihada za serikali katika kupunguza changamoto za 
madarasa.
Amesema
 kuwa Mkoa wa Dar es Salaam unakabiliwa na changamoto ya madarasa na 
madawati hivyo kunahitaji wadau kujitokeza kusaidia maeneo hayo.
Mwenyekiti
 wa TATOA, Angelina Ngalula amesema kuwa wameunga mkono jitihada za 
serikali kwa upande wa elimu hivyo wanawajibu wa kufanya hivyo katika 
kutatua changamoto ya vyumba vya madarasa.
Amesema
 kwa kuanzia wanaanza na madarasa 12 lakini wataendelea kuwasiliana na 
wanachama zaidi katika kuongeza au kujenga shule nzima ili watoto wasome
 shule na kuja kuweza kutumikia sekta ya usafirishaji.
Angelina
 amesema kuwa bodi yao iko imara katika kwenda na suala la shule za 
msingi ili watoto wapate elimu bora kutokana na mkakati wa Rais kutoa 
kipaumbele ya elimu ya nchini.



No comments:
Post a Comment