TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 9, 2016

CHAMA CHA WAGONJWA WA KISUKARI WAANDAA KAMBI YA UPIMAJI BILA MALIPO.


Mwathirika wa ugonjwa wa Kisukari, Ramadhan Mongi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na kufuata sheria za ulaji ili kuepukana na ugonjwa wa kisukari ambao ni ugonjwa usaosababishwa na ulaji mbaya wa chakula pamoja na kutokufanya mazoezi.
Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ugonjwa wa Kisukari(Tanzania Diabets Association), Profesa Andrea Swai katikati, kulia ni Mwathirika wa ugonjwa wa Kisukari, Ramadhan Mongi na Mratibu wa Mpango wa kitaifa wa kisukari Tanzania, John Gadna wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na ugonjwa wa Kisukari.

CHAMA cha wagonjwa wa Kisukari Tanzania kushirikiana na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto 


kuandaa kambi ya upimaji wa ugonjwa wa kisukari bila malipo




Machi 13 katika viwanja vya shule ya msingi Kibugumu Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ugonjwa wa Kisukari(Tanzania Diabets Association), Profesa Andrea Swai jijini Dar es Salaam leo amesema kuwa ugonjwa wa kisukari ni ugonjwa ambao hauambukizwi ambao husababishwa na ulaji mbaya.

 Swai amesema kuwa madaktari na matabibu watakuwepo kwaajili ya kupima afya ya kinywa, kupima uzito naushauri wa lishe siku hiyo na 


watakaogundulika matatizo maalumu watapewa rufaa.

Swai amesema kuwa ugonjwa wa kisukari husababishwa na ulaji mbovu (kula vyakula vilivyokobolewa), kutokufanya mazoezi na kutokula matunda.

Amesema kila watu 100 wakikusanyika kwa kupima ugonjwa wa kisukari hapo utawapata watu 9 wenye kisukari na 2 wanakuwa wanajua na wengine 7 hawajui kama wanaugonjwa huo.

Aidha ametoa wito kwa jamii kufuata kanuni bora za ulaji wa chakula ili kuepukana na ugonjwa huo usio wa kuambukizwa.

No comments:

Post a Comment